Mchungaji Msigwa agoma kupanda gari za CCM, alakiwa na wana-CHADEMA

Mchungaji Msigwa agoma kupanda gari za CCM, alakiwa na wana-CHADEMA

Yote ya yote Mimi na familia yangu nafaidika na serikali ya ccm kwa kuwa inanilipa mshahara, na Kuna wengine humu wanafaidika na chadema kwa kuwa inawalipa mshahara, sifungamani na upande wowote, na Kura yangu itabaki kuwa siri. Japo CCM hawajawah kupata Kura yangu since 95.

Hii michezo ya kisiasa ninayoiona Ni ya KIJINGA SANA KUPATA KUTOKEA
 
Sio tatizo kikubwa kalipiwa faini Na mh. Rais Na katoka.
Mchango wa Rais umesaidia sana kutoka kwa msigwa leo Na kujumuika Na familia yake.
 
CCM nahisi wamelogwa. Mbaya zaidi yule hakimu aliyewaloga juzi hajui hata dawa ya kuagua alipoiweka. Matokeo yake wanahangaika kukamata kila kitu. Hata Nzi akikatiza mbele yao wanampiga risasi na kumdai dawa.
 
Ushahidi Mwingine kwamba ccm haina tena viongozi sasa inataka kila mpinzani awe mwana ccm.

planing zao na mikakati yao ni yakizamani sana wameacha kuwekeza kwenye kutengeneza viongozi wamebaki kuwawaza viongozi wa upinzani what shame!
 
Hongera sana Mhe. P. Msigwa! Hongera Sana CHADEMA! Hongera Sana Watanzania!
Message sent, delivered, seen and read by Kayafa!!
Shame on you #ccm! Mnaoperate kishamba sana! But siwezi kushangaa zaidi make mmejaza washamba wengi sana kuanzia kayafa, polepole na bashite!!
 
Mchango wa mh Rais umesaidia sana,
Chadema iliomba msaada wa michango Kwa wananchi wote Na Rais JPM kaitikia ombi lkn pia familia ya mchungaji msigwa imeomba msaada kutoka Kwa Rais Na Rais kakubali ombi, tatizo linatoka wapi?
Hongera sana Kwa Rais
 
Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa amekataa kupanda gari la serikali lililopelekwa gerezani Segerea ili kumchukua baada ya kulipiwa faini.

Awali kulitokea mzozo kati ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na Ndugu Humphrey Polepole ambao walitaka Msigwa apande gari ya serikali kwa madai kuwa amelipiwa faini yake na Rais JPM, lakini wafuasi wa Chadema wakamtaka apande gari aliloandaliwa na Chadema kwa kuwa chama hicho ndicho kimemlipia faini kupitia michango ya watanzania.

Wafuasi hao walidai kwamba wakati Rais JPM anapeleka fedha tayari Chadema ilikua imeshamlipia Msigwa na hivyo fedha hiyo irudishwe kwa Rais ili ikafanye shughuli nyingine za maendeleo.

Kufuatia mzozo huo wafuasi wa Chadema walizuiwa kuingia gerezani humo na wafuasi wa CCM wakiongozwa na Polepole waliingia wakiwa kwenye magari ya serikali tayari kumlaki Msigwa.

Lakini Msigwa alikataa kupanda gari ya serikali aliyoandaliwa na kutembea kwa mguu hadi nje ya gereza walikokuwa wafuasi wa Chadema ambao wamemlaki kwa shangwe na sasa anaelekea makao makuu ya Chadema, eneo la Kinondoni ili kufanya mkutano na wanahabari.!

Msigwa nae ana deko sana 😅
Anaringa sbb anajua Mh. Rais ni ndugu yake, basi anafanya atakalo deko tupu. Mh. Rais wetu ana roho nzuri sana ya kibinadamu, ingekuwa mm hiiiiiiiii silipi wala simletei gari tena namuacha jela akae kae nikiona hakuna wa kumtoa ndio natoa mchango..😅😅
 
Mchango wa mh Rais umesaidia sana,
Chadema iliomba msaada wa michango Kwa wananchi wote Na Rais JPM kaitikia ombi lkn pia familia ya mchungaji msigwa imeomba msaada kutoka Kwa Rais Na Rais kakubali ombi, tatizo linatoka wapi?
Hongera sana Kwa Rais
Oya tutolee matapishi yako hapa.
 
Back
Top Bottom