Mchungaji Msigwa agoma kupanda gari za CCM, alakiwa na wana-CHADEMA

Mchungaji Msigwa agoma kupanda gari za CCM, alakiwa na wana-CHADEMA

Mh. Rais na Msigwa ni ndugu na pia ndugu wa Msigwa waliomba mchango kwa mh. Rais baada ya kujichanga na kupata 2 mil, ikabakia mil 38, Mh. Rais akatoa kwa huruma kama ndugu yake baada ya kuombwa. Sasa hapo kuna ubaya gani? Sema Msigwa ana deko sana ila atapata shida siku moja na atakosa msaada kabisa, shauri yake


Na Huyo Polepole naye Ana udugu na Msigwa?

Au Msigwa alishafika Bei na kwamba waende kumchukua wampeleke lumumba kutangaza kuhamia ccm?

Msigwa, sema ukweli Kama na wewe ni pandikizi la ccm.
 
Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa amekataa kupanda gari la serikali lililopelekwa gerezani Segerea ili kumchukua baada ya kulipiwa faini.

Awali kulitokea mzozo kati ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na Ndugu Humphrey Polepole ambao walitaka Msigwa apande gari ya serikali kwa madai kuwa amelipiwa faini yake na Rais JPM, lakini wafuasi wa Chadema wakamtaka apande gari aliloandaliwa na Chadema kwa kuwa chama hicho ndicho kimemlipia faini kupitia michango ya watanzania.

Wafuasi hao walidai kwamba wakati Rais JPM anapeleka fedha tayari Chadema ilikua imeshamlipia Msigwa na hivyo fedha hiyo irudishwe kwa Rais ili ikafanye shughuli nyingine za maendeleo.

Kufuatia mzozo huo wafuasi wa Chadema walizuiwa kuingia gerezani humo na wafuasi wa CCM wakiongozwa na Polepole waliingia wakiwa kwenye magari ya serikali tayari kumlaki Msigwa.

Lakini Msigwa alikataa kupanda gari ya serikali aliyoandaliwa na kutembea kwa mguu hadi nje ya gereza walikokuwa wafuasi wa Chadema ambao wamemlaki kwa shangwe na sasa anaelekea makao makuu ya Chadema, eneo la Kinondoni ili kufanya mkutano na wanahabari.!
View attachment 1385889
Vijana wa CCM WALISEMA HAWALIPII WAHALIFU MBONA BABA YAO ALITAKA KULIPIA MHALIFU ..
 
Sasa Msigwa akiongea hovyo, tunamrudisha mahakamani, achunge ulimi wake, si anaringa tumejaribu kumsaidia hataki, sasa akienda mahakamani tena hakuna msaada tena hata akiita Magufuliiiiiii njooooooo baba njooooo Mh. Rais njoooooooo hakuna tena kumsaidia.. Shauri yake [emoji28][emoji28][emoji28]
Acha vitisho vyako, labda mumhukumu kifungo bila faini. Kwa faini, tutachanga, hata mkimpiga faini ya kuleta mchanga kutoka mwezini, tutaufuata na utapatikana. Usicheze na nguvu ya Umma weye.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa mtoa mil. 38 simwaminigi anaweza kuiagiza mahakama imrudishiwe hiyo elayake
 
Kwa jinsi polepole alivyoenda kumchukua Msigwa ili hali Msigwa hana taarifa na wala hawajakubaliana naye, ni kama jaribio la kuuuutekwaa (kumchukua mtu bila ridhaa) vile.

Kwenda kumchukua mtu sehemu bila ridhaa yake ni mbaya sana hususani kwa jinsi ushindani wa vyama hivi viwili ulivyo; Alitumwa na nani na Kwa nini aende na Kamera? na Msigwa wa Ikulu naye ni msemaji wa ikulu sio familia as per Msigwa Mbunge, vipi aliingia kwenye TV kwa maswala ya kifamilia?

Yametokea na tunashukuru Mungu yanaisha bila madhara, kujaribu kumchua Msigwa kwa style ile kungeweza kuleta hatari kama ile ya Akwilina na pengine tungeweza kupata matatizo tena kama taifa.

Naomba vile msigwa kakana hadharani basi taasisi zitowe tamko la kuonya mambo kama hayo. Wanasiasa wanajaribu kila jambo wapate umaarufu lakn hawaangalii madhara yanayoweza kutokea. Changa la Akwilina na Kifungo cha kina Mbowe kiwa fundisho kwa kila upande, wale waliosababisha tafurani kwa kutotoa viapo mapema na hawa waliodai haki hiyo hadi kusasabisha yote yaliyotokea.

Ni maoni yangu.
 
Nimekusikiliza kwa makini sana ukizungumzia kitu uonevu mliofanyiwa na mahakama ,nimestaajabu sana ikiwa mlipata muda wa kuweka wakili na kujitetea,

hilo niwaachie wajuzi wa mambo ya sheria .

Ninachokupa kongole la ukomavu wako kisiasa ni baada ya wewe kukwepa kuzungumzia juu ya ukweli kuhusu nani hasa aliekulipia faini ukatoka jela,ni Magufuli na ndugu zako au Chadema?

Nasema kwa sababu ilitegemewa na baadhi ya watanzania hasa wanachama wa chama chako uliweke wazi kuondoa malumbano yalioshamiri jana mitandaoni ,baadhi wakidai umelipiwa na Magufuli na wengine wakisema chama kimekulipia.

Matokeo yake umecheza sarakasi kali ukinukuu hukumu za hayati baba wa taifa ,
pia ukisema ni kweli unamahusiano na Magufuli na yanabaki kuwa ya kwenu na hayawezi kuzungumziwa hadharani,
ukatumia podium kumshambulia Humphrey Polepole na Gerson Msigwa.

Swali linabaki ,Je ni risiti zipi zilizokutoa gerezani ?,ni zile za Gerson Msigwa au za chama chako?( chadema).kwani inaonyesha umelipiwa mara mbili
 
Hii fursa ya bongo movie kutoa filamu ya hii habari...
 
Kwa jinsi polepole alivyoenda kumchukua Msigwa ili hali Msigwa hana taarifa na wala hawajakubaliana naye, ni kama jaribio la kuuuutekwaa (kumchukua mtu bila ridhaa) vile.

Kwenda kumchukua mtu sehemu bila ridhaa yake ni mbaya sana hususani kwa jinsi ushindani wa vyama hivi viwili ulivyo; Alitumwa na nani na Kwa nini aende na Kamera? na Msigwa wa Ikulu naye ni msemaji wa ikulu sio familia as per Msigwa Mbunge, vipi aliingia kwenye TV kwa maswala ya kifamilia?

Yametokea na tunashukuru Mungu yanaisha bila madhara, kujaribu kumchua Msigwa kwa style ile kungeweza kuleta hatari kama ile ya Akwilina na pengine tungeweza kupata matatizo tena kama taifa.

Naomba vile msigwa kakana hadharani basi taasisi zitowe tamko la kuonya mambo kama hayo. Wanasiasa wanajaribu kila jambo wapate umaarufu lakn hawaangalii madhara yanayoweza kutokea. Changa la Akwilina na Kifungo cha kina Mbowe kiwa fundisho kwa kila upande, wale waliosababisha tafurani kwa kutotoa viapo mapema na hawa waliodai haki hiyo hadi kusasabisha yote yaliyotokea.

Ni maoni yangu.
Nachukia mambo ya msingi yanapowekewa sura ya siasa [emoji22][emoji22]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa amekataa kupanda gari la serikali lililopelekwa gerezani Segerea ili kumchukua baada ya kulipiwa faini.

Awali kulitokea mzozo kati ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na Ndugu Humphrey Polepole ambao walitaka Msigwa apande gari ya serikali kwa madai kuwa amelipiwa faini yake na Rais JPM, lakini wafuasi wa Chadema wakamtaka apande gari aliloandaliwa na Chadema kwa kuwa chama hicho ndicho kimemlipia faini kupitia michango ya watanzania.

Wafuasi hao walidai kwamba wakati Rais JPM anapeleka fedha tayari Chadema ilikua imeshamlipia Msigwa na hivyo fedha hiyo irudishwe kwa Rais ili ikafanye shughuli nyingine za maendeleo.

Kufuatia mzozo huo wafuasi wa Chadema walizuiwa kuingia gerezani humo na wafuasi wa CCM wakiongozwa na Polepole waliingia wakiwa kwenye magari ya serikali tayari kumlaki Msigwa.

Lakini Msigwa alikataa kupanda gari ya serikali aliyoandaliwa na kutembea kwa mguu hadi nje ya gereza walikokuwa wafuasi wa Chadema ambao wamemlaki kwa shangwe na sasa anaelekea makao makuu ya Chadema, eneo la Kinondoni ili kufanya mkutano na wanahabari.!
View attachment 1385889
Hivi siku hizi majeshi nayo Ni sehemu ya siasa?nakumbuka wakati tuko jeshini tulikuwa tunakatazwa kujihusisha na siasa Ni nn kimejiri kwa majeshi yetu kuwa Ni sehemu ya siasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha sinema limebuma vibaya. Asante Msigwa kwa kuwaaibisha mashetani mchana kweupe.
Tena wanajuta,kwa nini walienda na vwanahabari?aibu wamejikaanga kwa mafuta yao wenyewe
 
Hapa ndipo Tanzania tajiri tulipofikia. sijui nisemeje!!!!! '

Tutafika kweli?
 
Kwa nini vijana wa CHADEMA hawajakakamata haka kakondefu wakaue? Siasa za awamu hii za kipumbavu kabisa!
 
Back
Top Bottom