Mdada usikubali hizi swaga za kwamba tutafute maisha pamoja. Mpaka mkayapate maisha utakuwa umechakaa, mwanaume ataoa kabinti ka darasa la saba

Mdada usikubali hizi swaga za kwamba tutafute maisha pamoja. Mpaka mkayapate maisha utakuwa umechakaa, mwanaume ataoa kabinti ka darasa la saba

wewe ndio una maisha magumu unategemea kuuza K humu JF, unasumbua wanaume inbox kuomba omba hela na wakutoe out...
Ungejua nachangia hata kukufanya wewe uvae na kula usingesema hilo
 
Mwanamke ni kama ua, lisipotunzwa linapoteza mvuto kabisa. Hivyo usidanganyike kuolewa na mchovu akaanza kukulaza chini kwenye mkeka, mnakaa sakafuni, mnapikia kuni au jiko la mkaa mpk kucha zinajaa masizi.

Saloon unakuwa unazipita tu kama kituo cha polisi maana wewe nywele husuki bali unakata kama shamba boy. Na hukumbuki mara ya mwisho ulienda shopping mwaka gani.

Mafuta unajipaka ya kupikia mpk ukipita mtaani unafuatwa na mbwa wakidhani wewe ni kitoweo.

Ukicheza miaka yako 5 tu ktk mzunguko huu wa umaskini uliomaliza nao shule watakupiga shikamoo, maana utakuwa umefubaa, umechakaa na kuchoka. Sasa mpk mkayapate maisha miaka 10 au 15 utakuwaje??

Mkishayapata maisha mumeo lazima jicho lake litahamia kwa ving'asti ambao kucha zao hazijaathiriwa na mkaa. Sura zao zimetunzwa vema na lotion za Uturuki.

Hebu tafuteni wanaume wenye nazo ufikie kwenye maisha fulani ambayo hayatakufubaza. Achana na wenye subwoofer moja chumba kimoja cha kupanga halafu anataka ndoa na wewe.

Ni ushauri tu. Kama hutaki acha
Hili nalo ni tatizo la akili unahamasisha kutaka wanawake waanzishe mahusiano na wanaume wenye pesa kana kwamba matajiri wanagawa bure pesa kwa kila mwanamke mzuri
 
Hili nalo ni tatizo la akili unahamasisha kutaka wanawake waanzishe mahusiano na wanaume wenye pesa kana kwamba matajiri wanagawa bure pesa kwa kila mwanamke mzuri
Mm nawaonya wanawake waepuke kuingia kwenye ndoa na mwanaume maskini. Watapata taabu na watazeeka mapema.
 
jina lako tuu linasadifu kilichopo kichwani mwako
 
Ni Ajabu sana, Wanawake wanataka Wanaume wakiwa na Hela wawathamini...

Na wakati Wanaume walipokuwa hawana Hela hawakuthaminiwa na Wanawake...

Mwanaume ambae hakuthaminiwa alipokuwa Fukara akipata Pesa ni ngumu kumthamini Mwanamke...
5d850f1493ed4ceb98d14955981b346a.jpg
 
Na wenye maisha tayari labda upore mme wa mtu.
Vumilia tu dada anza upya kama ulibugi simama imara wekeza kwa Mungu ndie uponya yote.
Mapenzi yanauma potepote
 
Alichokisema mtoa mada xaxa ni ukweli mtupu kwa wanaume hufanya hivo.
Kama mwanaume sio mpambanaji ni tatizo sana wakuu.
Wanaume tupambane tuongeze vipato vyetu ili mwanamke naye awe na unafuu wa maisha, sasa umeacha mke nyumba za mbavu na barabarani unakodoa mimacho kama komba.

Gesi sh.50,000 kila mwezi 23,000.
Kitanda na godoro sh.300,000 vyote 5x6 size.
Kodi ya nyumba sh.60,000
Hakikisha mwanaume mwezi usipite hujapata angalau laki 3 kwa hali ngumu ili kuondoa aliyo sema mtoa mada.
 
Mtoa mada hajakosea kitu wanaume tuache kuishi maisha mabovu.
 
Back
Top Bottom