Mdude CHADEMA: Hii katiba haifai, Wazanzibari wanakuwa wakuu wa wilaya Tanzania bara huku Watanganyika hawaruhusiwi kuwa wakuu wa wilaya Zanzibar

Mdude CHADEMA: Hii katiba haifai, Wazanzibari wanakuwa wakuu wa wilaya Tanzania bara huku Watanganyika hawaruhusiwi kuwa wakuu wa wilaya Zanzibar

Kiongozi atakae kuja kuifanya zanzibar kama mkoa.Tanzania ikawa moja atakua kalifanyia taifa hili jambo la kukumbukwa daima.

Tanganyika ilikufa baada ya kuzaliwa Tanzania, kwann zanzibar iwe hai [emoji2357].Tanzania ndo cha kuzingatiwa hakuna cha Tanzania zanzibar au Tanzania bara,hii inachochea huu ubaguzi.

Nyerere na karume walileta muungano si kosa kuboresha walichokifanya ,Rais awe na cheo cha President of Republic of Tanzania.

Kama ilivo kwa mtu wa mwanza kufany chochote arusha bas iwe ivo ivo kwa mtu wa kigoma kufanya chochote zanzibar kuanzia kumilik ardhi na mambo meng.

Nchi ndan ya nchi ni jibu la kwann mpka leo Ajenda za madara zinashika chart.

#MABORESHO
#KWENYE
#MUUNGANO
Kamwe tena wasahau Zanzibar kuwa mkoa !! Zanzibar ni Nchi kamili iliyoungana na Tanganyika hapo juzi juzi mwaka 1964 !! Zanzibar ilikuwepo kwa karne na karne kama Nchi ! Someni history yake !!
 
Asante sana mkuu. Na mimi nilifikiri kuwa kuna masharti ya ukaazi yanayoweza kumpa mtu wa bara Uzanzibari, lakini nikatukanwa kwamba sijui kitu hapa.

Zanzibar haina uraia, kwa sababu si nchi kamili. Uraia ni jambo la Muungano, kuna uraia wa Tanzania tu. Uraia wa Zanzibar ulikufa baada ya Muungano, kama uraia wa Tanganyika.

Kule kuna ukaazi tu.

Nafikiri ukaazi huu, angalau kinadharia tu, unafanya hii distinction ya "Mzanzibari" isiwe na maana kubwa.

Kwa sababu, in theory, kila Mtanzania anaweza kuwa Mzanzibari, sema kuna wengine wamezaliwa Zanzibar hawana masharti ya kukaa miaka hiyo inayotakiwa kabla ya kupata ukazi, na wengine wanatoka bara inawabidi wakae miaka hiyo.

Na hiyo miaka imewekwa hivyo, kwa sababu Zanzibar hawataki watu wa bara waende kwa wingi kupiga kura Zanzibar na kubadili matokeo ya uchaguzi bila kuwa wakazi, pamoja na kudhibiti watu wengi wa bara wasije kununua ardhi kwa sana na kuibadilisha Zanzibar.

Sasa, tukimkatalia Shaka kuwa Mkuu wa Wilaya bara, na Mndengereko atakayehamia Zanzibar naye akataliwe kuwa Mkuu wa Wilaya bara?

Wale kina Sepetu kina Wema baba yao alikuwa Zanzibar sana, kina Adam Mwakanjuki wamekaa sana Zanzibar mpaka SMZ walikuwepo.

Hawa nao wapigwe marufuku vyeo vya serikali ya Muungano kama vya ukuu wa Wilaya bara?

Ukianza siasa hizo maana yake nini? Utasema wakuu wa wilaya za Dar wote wawe Wazaramo? Wasije Wabondei kuwa wakuu wa Mkoa wala wilaya Dar?

Hapo hamuoni mnaanza dhambi ya ubaguzi aliyoisema Nyerere (probably akirejea mfano wa Simba walawatu wa Tsavo kutoka kitabu cha "The Man Eaters of Tsavo" cha John Henry Patterson) kuwa ni sawa na kula nyama ya mtu, ukianza huachi utabagua watu mpaka kwenye koo na familia?
Ubaguzi ni Unyama !!
 
Natoa ushauri kwa CHADEMA watu kama mdude CHADEMA na wengine wenye aina yake ya siasa hawaisaidii CHADEMA Bali wanaiharibia kabisa.

Kwa mujibu wa katiba ,uteuzi wa wakuu wa wilaya unafanywa na Rais kama ulivyo kwa uteuzi mwingine wowote wa kikatiba.

Mfano, aliyekuwa katibu mkuu wizara ya nishati Tanzania bara mhandi Zena, Rais Dkt. Mwinyi alipoingia tu madarakani alimteua kuwa katibu mkuu kiongozi na katibu wa mabaraza la Mapinduzi la Zanzibar, cheo cha juu kwa utumishi wa umma Zanzibar.

Sasa Kama mtanganyika amepewa cheo Cha juu kabisa Cha utumishi wa umma, ni kweli
Mkuu wa wilaya hawezi kuteuliwa?

Acheni upotoshaji CHADEMA mtapoteana mtafute mchawi
Kwa hiyo nchi imeamua kuajiri raia wa kigeni kwenye nafas za utawala? Usije kushangaa siku moja kuna mtendaji wa kata kutoka china!
 
..kuwa mkweli.

..Watanganyika hawawezi kuingia Zanzibar wakauwa wananchi bila msaada wa wenyeji Wazanzibari.

..hata ukisema kuwa mapinduzi ni uvamizi, jiulize walioshika madaraka baada ya uvamizi huo ni nani kama sio Wazanzibari?

..Vifaru mnavyoletewa kila baada ya miaka 5 si kwa ajili ya kusimika Wazanzibar wenzenu madarakani?

..Mimi nashauri kauli zako uzilenge kwa wahusika wanaofanya uovu dhidi yenu, usizielekeze kwa Watanganyika wote.
Wenyeji na hawa Watanganyika waliokaribishwa vizuri wakaona Sasa ni wakati wa kuichukuwa nyumba. Wazanzibara
 
Huyu n mjinga wa kupuuzwa. Mkuu wa wilqya magharibi A susaz kunambi, mkuu wa wilaya ya kati Medina Joel Thomas, Meneja mkurugenzi PBZ, Mkurugenzi ZBS na ZRA( ZRB) hao wote ni Watanganyika na hawana wazee znz. Zena katibu mkuu kiongozi. Babu yake ndiyo.alikimbia Pemba lakini yeye kazaliwa tanga na hajawahi kutumikia Seriki ya znz. Ali Hassan Mwinyi amekuja znz ana miaka 10 na amechauliwa kuwa raising wa Zanzibar, Aboud Kumbe Mwinyi kwao ni.mji mwema na amekuwa rais wa znz. Sasa huyo.mdude mpuuzi. Na ako wakurugenzi wa wa wizara wengi sana baba zao wana asili ya Tanganyika na hivi sasa viongozi. Kwani mnasema Zena siyo.mtanganyika kwa sababu babu zake wana asili ya kizanzibar. . Hayo.madai yenu yq katiba mpya yataonekana ni upuuzi wa sabau mnazozitoa. Eti chakuna kimepanda bei na suluhisho lake katoba mpya!!
Tulia uandike vizuri basi, unapanic nini au Shaka!!?
 
dah kumbe ana mume? niliwahi sikia mengi mabaya kwa kweli
Hata mimi nilishasikia mabaya mengi sana kuhusu wewe lakini niliona hayana maana yoyote. Vivyo hivyo na ya Zena mwachie Zena mumewe.

Uzuri wa Zena aujua mume wake
 
Hakuna mtanzania Nusu. Kwanini watanganyika wanajimilikisha Tanzania?
Chako changu changu changu. A 20 years assimilation policy would have cleared this mess.

Nyerere alitupoteza hapa wadanganyika.
 
Hilo swala la identity, utamaduni wangeufany na bara kama ni muhim. Si sawa kupoteza utamaduni wa wachaga kwa kuruhus wahaya kuhamia uchagan huku unalinda utamaduni wa wazanzibar kwa kumminya mtanganyika huko zanzibar.

Mtanzania yoyote lazima awe na haki sawa sehem yoyote nchi.Watafute jina lingine watoe ilo muungano.

Zanzibar ni mkoa haipaswi kuwa na rais.[emoji41]
Aya ya kwanza hauko sawa hali hiyo ingeua utaifa ndiyo maana watu hawataki kusikia habari za machifu

Bila shaka kama tungelazimisha kuwa na serikali moja ili rais awe na mamlaka kamili na visiwa vya Zanzibar kwa sasa hali hii isingekuwepo.

Kuna ongezeko la manunguniko kwa Watanzania bara kuona Zanzibar ikichotewa pesa za misaada lukuki ilihali haichangii chochote kwenye kulipa, wazanzibar kuteuliwa hata kwenye wizara zisizohusu masuala ya Muungano, rais wa sasa ameenda beyond wizara anateua hata kwenye ofisi zingine za umma ambazo siyo sehemu ya masuala ya Muungano ilihali Zanzibar watanzania wanachukuliwa kama foreigners.

Zamani tuliona Nationalism ikikua Zanzibar katika mrengo wa secession lakini sasa kwa sababu wananufaika direct na Muungano ni kama wametulia hali hiyo imeibuka tena kwa watanzania bara ambao ni wazi tofauti na mambo ya kisiasa ni kama Muungano hauna maana kabisa kwao.
 
Mlaumu Nyerere ambaye aliingiza Tanganyika kwenye Muungano huu na Zanzibar bila hata kupata baraka za bunge.

Nimemsoma Profesa Issa Shivji na wenzake hapa wakieleza maisha ya Nyerere kwenye vitabu vyao vitatu vile, nimegundua kwamba Nyerere aliiburuza Tanganyika na Tanzania kuliko nilivyofikiri.

Ubaya au uzuri Watanzania wengi hawasomi tu, wangesoma Nyerere angeonekana mtu tofauti sana kulinganisha na Watanzania wengi wanavyomchukulia.

Yani kuna sehemu hata sera zake za Ujamaa zilipoanza kunawiri kwa nguvu za watu bila kupitia TANU Nyerere alipiga marufuku vijiji vya Ujamaa hivyo kwa sababu tu havikuwa chini ya TANU.

Tuliwekwa kwenye bonge la political experiment na mtu mmoja bila hata ridhaa.
Ile one man show ya Nyerere ilikuwa kubwa sana kiasi kwamba iliharibu mengi kuliko kutengeneza.
 
Kamwe tena wasahau Zanzibar kuwa mkoa !! Zanzibar ni Nchi kamili iliyoungana na Tanganyika hapo juzi juzi mwaka 1964 !! Zanzibar ilikuwepo kwa karne na karne kama Nchi ! Someni history yake !!
Historia ni mkusanyiko wa matukio hivyo inaweza kutengenezwa tu.

South Sudan never existed before lakini sasa ni taifa linalojitegemea.
 
Historia ni mkusanyiko wa matukio hivyo inaweza kutengenezwa tu.

South Sudan never existed before lakini sasa ni taifa linalojitegemea.
Ni kweli kabisa historia inaweza ikatengenezwa ya uongo na ikapigiwa debe sana ili ionekane ni ya kweli ! Lakini kwa Zanzibar it’s another case !! Zanzibar ilikuwepo kama Nchi na baadaye ikaungana na Tanganyika !!
 
Ni kweli kabisa historia inaweza ikatengenezwa ya uongo na ikapigiwa debe sana ili ionekane ni ya kweli ! Lakini kwa Zanzibar it’s another case !! Zanzibar ilikuwepo kama Nchi na baadaye ikaungana na Tanganyika !!
Basi waiondoe kama haiwez kuwa mkoa.
 
Alichondika Mdude kwenye ukurasa wa twitter.
"Moja ya mapungufu ya katiba iliyopo ni kwamba, mtu kutokea Bara-Tanganyika hawezi kuwa mkuu wa wilaya Zanzibar lakini mtu kutokea Zanzibar anaweza kuwa mkuu wa wilaya Bara. Sasa huu ni muungano wa namna gani? Ndio maana tunahitaji #KatibaMpya kuondoa ubaguzi wa namna hii."
View attachment 2496334
Kiukweli sioni maana ya muungano kwa hili
 
Back
Top Bottom