Mei Mosi Mwanza: Rais Samia ahutubia, aahidi kuongeza mishahara kuanzia mwakani, agusia mafao ya wastaafu

Sikuwahi kuwaza kuwa binadamu anaweza kuwa "mjinga" kiasi hiki.
 
Mkuu, swala la kuongeza mishahara sio jepesi kama watu wanavyofikiri lina impact kubwa sana kwenye uchumi na sio kila nchi huwa inaongeza mishahara mara kwa mara.

Tatizo la jamii yetu sio kila mtu ni mwajiriwa na anafahamu ongezeko la mshahara ni kiasi gani, mfanyabiashara ambaye hajawahi ajiriwa akisikia tu tangazo kuwa mshahara umeongezeka basi naye atapandisha bei ya bidhaa na huduma, hajui kwamba mshahara umeongezeka kiasi gani, mradi kasikia tu umeongezeka naye atapandisha bei.

Sasa hii inamadhara kwani kipato hicho hakijaongezeka kwa watu wote bali kwa watu wachache tu, hii itaathiri mno wale ambao hawana ajira ambao ni wengi,

Ongezeko la mishahara pia inamaana kwamba tupunguze kufanya baadhi ya mambo tuliyokua tunayafanya ili fedha ziende huko

Kupanga ni kuchagua, tuamue kulipana mahela tu tusifanye lolote au tubebane hivyo hivyo kwa manufaa ya wote.

Rais ataamua.
 
Aliyasema haya maghufuli kwamba tutaongezewa mishahara ila hakuna kitu nawe unaleta hizi habari
 
Hahah...

NN umeukumbuka ule uzi wako wa askari mmoja tu!
Wala hakuwa mmoja, to be fair! So you’re being very disingenuous.

Na nilisema kuwa mazingira ndo huwa yana dictate aina ya ulinzi ulio appropriate.

Lakini kama ilivyo kawaida ya walio wengi humu JF, walio na akili ya kuweza ku reason, ni wachache sana. Hata 10 hawafiki.

Hata leo si ajabu akaja akatokea mtu mwingine na kudai askari aliyekuwa na bunduki ni mmoja tu, ilhali picha inaonyesha dhahiri…
 
Tupia kapicha kama umezinasa mkuu..
 
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Madame Samia Suluhu Hassan
Ameondoka Asubuhi Dodoma ~ Mwanza
Jioni Atakuwa Dodoma

Wote Macho 🙄🙄🙄Kwa Mama
 
Hotuba ya leo.. itasikilizwa na wananchi wengi.. kwa sababu wengi wanataka kusikia habari za....

Mimi alipo nipo kumsikiliza Rais wetu
Wewe msikilize Makonda ndiyo saizi yako.
 
Hii sherehe inaendeshwa kama vile ni sherehe ya chama tawala. Naona Mkuu wa mkoa anatambulisha viongozi wa CCM sambamba na wale wa serikali...... Vyama vya upinzani anadai anayambua uwepo wa wawakilishi wa Vyama vya upinzani.......!!

By the way hii ni sherehe ya vyama vya wafanyakazi au ya kiserikali.... Vyama vya ushirika vimefunikwa kabisa. Hawana Chao hapo. CCM wako kwenye kampeni.
 
Watanzania msilalamike sana... Mungu aliona awape miaka mitano ya kujifunza ukakamavu. Mlikuwe legelege sana kuanzia ndani ya CCM hadi mwananchi wa kawaida. Baada ya miaka mitano ya kuvurugwa hatutarudia tena makosa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…