Uchaguzi 2020 Membe ahsante sana, karibu rasmi CHADEMA. Karibu utuvushe

Uchaguzi 2020 Membe ahsante sana, karibu rasmi CHADEMA. Karibu utuvushe

Hayo hayo makapi yenu yanawatosha hata Nyerere alishasema hayo.
Si CCM anayatema CHADEMA mnayaokota. Sijui kwanini CHADEMA inashindwa kuamini vijana wake na viongozi wanaopigana usiku na mchana inaamini makapi
 
Ile kiu ya wapinzani(wapinzani halisi) wa Tanzania kupata mkombozi wa kutuvusha hatimaye imefikia pazuri baada ya Membe kukaribishwa ndani ya chadema na hatimaye kusubiri kuwa mgombea wa urais.

Chadema katika siku ambayo mmefanya jambo la maana na umuhimu sana basi ni hii ya kumpa Membe nafasi ya kutuvusha 2020.

Membe ni mwanamkakati na mbobezi kwenye masuala yote ya intelijensia, hivyo ni mtu sahihi kabisa na muhimu kwa wakati huu kuliko wakati wowote ule.

Membe sio Lissu, Membe ana ushawishi, ana mtaji wa watu wengi sana kitu ambacho Lissu hana na kamati kuu imeona hili suala.
Karibu Membe chadema, karibu utupiganie, karibu utuvushe.

#2020 upinzani tunaenda na Membe#
Membe for president via chadema.
 
Sema ndio itakuwa mwanzo wa mwisho wako wewe. Alafu watu kama nyie hatuwahitaji huku
Membe 2020 for presidency
Membe anataka urais tu basi. akiukosa October, atai-Lowasa kambi ya upinzani immediately!

Chadema wakimpokea ndiyo mwanzo wa mwisho wa chama!
 
Lissu ndio nani?? Kwa hiyo kwa sababu kapigwa risasi 16 basi ndio tumpe nafasi ya kugombea?? Ingekuwa hivyo 50 cent angekuwa raisi wa marekani
Lissu aendelee kula zake bata huko alipo, tunaenda na membe jasusi mbobezi
Daah Tundu lissu ashatoka kwenye utukufu Tena Ila kwakwel inahitaji nguvu nyingi chadema kuwaelewa wanapenda Nini na hawapendi Nini ?

Na nilichogundua Watanzania huwa hatujifunzi kutokana na makosa tuliyoyafanya nyuma.

Yani mtu alipigwa risasi Zaid ya 16 akikipigania chama leo hii mmemuona Hana umuhimu tena kisa kachero mmoja aliefukuzwa uanachama ndani ya chama chake.

Dhambi ya usaliti itaendelea kuwatafuna Sana CHADEMA.
 
We sio mpinzani na hujui chochote zaidi ya kucomment utumbo. Kama unampenda sana lissu naenda kanywe nae chai
Upinzani 2020 tunaenda na membe, jasusi mbobezi
Huu utopolo washirikishe wapumbavu wenzako hapo Lumumba
 
Hongera Chadema,hongera B.Membe.
ahsanteni sana viongozi wakuu wa Cdm kwa uwamuzi wenye tija na afya kwa nchi yetu na taifa kwa ujumla.
Wembe ni uleule.
 
Suala hili linafahamika kwa uwazi bila chenga," MPANGA MAFAILI CCM ANAUSHAWISHI NA UELEWA MPANA KULIKO MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA ". Nenda Membe ukawavunje nyonga kabisa. Kazi aliyo ianzisha Lowassa haijaisha bado. Nenda Membe kaimalize. Tafadhali Membe usituangushe. Peopleeeeeeeees Powerrrrrrrrrr.
 
Wewe ni mpiga deki tu, tulia Membe atuvushe tunaojielewa.
Naona watu wa propaganda wa CCM mpo kazini. Kwa taarifa yako mmeshafeli na pandikizi lenu Membe.
Wapinzani na watanzania saivi wameelevuka sana na wanajua mipango yenu yote ovu dhidi ya Upinzani wa kweli.

CCM jiandaeni, Mwaka huu ni Lissu tu. Andaeni hoja za kujibizana nae maana mwaka huu hata kura hamtaweza kuiba.
 
Back
Top Bottom