Tetesi: Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba

Tetesi: Membe awakatalia Kardinali Pengo na Askofu Malasusa kumsamehe Musiba

Mm mkatoliki ila huyo Pengo ni mnafiki sana kipindi Cha Magufuri alikuwa anarambishwa asali na alikuwa kimya tu Leo anataka kumuokoa mtu waliyekuwa wanaramba asali wote.

Membe shikilia hapo hapo mpaka nyani ateme bungo.
 
Askofu Pengo na Malasusa walikuwa karibu sana na JPM hivyo kujiingiza kwao kumuombea msamaha huyu mhalifu Musiba kunadhihirisha dhahiri kuwa Musiba alikuwa anatumwa na rafiki yao JPM na walikuwa wanajua.
Hii ni aibu kubwa kwao na wanaliaibisha kanisa kwa kushirikiana na uovu
 
Musiba ni mtu mwenye kiburi kupindukia.

Kupigwa mbada mali zake zote ni jambo jema kabisa kwa nia ya kuwafunza watu wengine wenye tabua kama zake au wale ambao wangekuja kuwa na tabia kama za kwake.

Madam adhabu haijahusisha kuundoa uhai wake, ni jambo jema.

Viongozi wa dini, nao wasitumie nafasi zao kuulinda uovu. Wakati Musiba akitukana watu na kuhamasisha baadhi ya watu wauawe, Askofu Mkuu Pengo na Askofu Malasusa walikuwa wapi? Walitoa kauli gani?

Wakati watu wanauawa, wanapotezwa, wanatekwa na kudhulumiwa mali zao, Maaskofu wa Kanisa Katoliki waliandika waraka kulaani matukio hayo, lakini jambo la ajabu Kadinali Pengo aliukana waraka ule na kudai yeye si sehemu ya azimio lile, na wala sahihi kwenye waraka ule siyo ya kwake. Yote hayo ilikuwa kwaajili ya kutomkera mtawala aliyekuwa akiufadhili uovu.

Hayo ya nyuma yaliishapita, tuliishayasamehe. Kadili Pengo ni vema akapumzika, asijiingize katika mambo haya. Nchi hii inahitajika kujengwa upya, japo ujenzi wake unaenda taratibu mno. Upatikanaji wa Katiba ulkohitajika kuwa kipaumbele cha kwanza, unapelekwa kwa danadana na hadithi nyingi bila vitendo.
 
Membe itakua kafulia anataka hela hakuna kingine hapo nimemshtukia.
Hizo mali ziwekwe wazi mahali zilipo. Hilo shamba kama lipo maeneo ya karibu na mjini, ninalihitaji. Nikilinunua nitaligawa kwa kwa taasisi za dini wajenge sehemu ya kuabudia, au kwa wanaotaka kujenga kituo cha kulelea watoto yatima, au eneo la wazi kwa vijana wasio na ajira wafanyie shughuli zao hapo.
 
Hahaaa..... wapambe mmeshindwa kumchangua shujaa wenu msiba?

Yuko mwingine alisingizia watu madawa ya kulevya.

Kesi zake zitafunguliwa hata baada ya miak 30 mbele. Ajiandae tu.
Kila siku watu wanarekebisha miandiko kwenye documents tu. Siku miandiko ikikaa sawa hatoboi
 
Kwa nini haku appeal mpaka case ifike mahama za EAC, yaani yeye angeenda na mwendo wa ku apeal tu!
Sidhani kama hii case ilifika kwenye Mahakama ya Rufaa!
Well I’m just curious [emoji3166]
Hakuwa na sababu ya ku-appeal akiamini wale maafisa wa TISS ambao marehemu aliwapa ujaji wangetoa hukumu ya kumlinda kama ilivyokuwa inafanyika wakati marehemu akiwa hai.
 
Ku-deal na mtu kariba ya Membe ujipange hasa. Huyu ni jasusi si wa kitoto. Ni diplomat maarufu sana huko duniani. Bila Membe Jakaya asingepata Urais na hata baada ya kupata Kuna baadhi ya viongozi duniani asingewafikia. Huyo ni mwandamizi wa Jesuits mbali na kuwa Mwalimu wa ukachero wa M16 ya Uingereza. Niishie hapo maana kwanza ujue Membe anawakilisha wangapi kwenye kesi hiyo?
Umeandika utumbo tu.
 
Huyo mzee kafulia mpaka anasikitisha.

Sasa kuuza mali za musiba ndio kutamtoa kwenye ukata.
Kamchangie Musiba. Kumsema vibaya mwenye haki hakuzuii haki yake. Njia mojawapo ya kumchangia, wakati wanapiga mnada apartments zake, unanunua mojawapo. Halafu unamrudishia Musiba ila ibakie kwenye jina lako, la sivyo pesa isupokamilika, ndani ya miaka 10 kunaweza kufanyika mnada mwingine wa vitu vingine alivyo chuma tena.
 
Wakati dalali wa Mahakama kampuni ya Yono (vijana wa kazi) ikihesabu siku zilizobaki katika 14 (siku za kazi) alizolewa mtukanaji Cyprian Majura Musiba kumlipa fidia Kachero Bernard Membe jumla ya shilingi 9.2 Bilioni, Bwana Musiba amewaangukia viongozi wa dini Askofu Alex Malasusa (KKKT Diyosisi ya Pwani) na Kardinali Porlycarp Pengo kumwombea msamaha kwa Membe asipige mnada mali zake.

Taarifa kutoka ndani ya familia ya Membe nyumbani kwake Mikocheni zinaeleza kwamba Jumatatu ya tarehe 24/4/2023 majira ya saa 10 alasiri mjumbe kutoka kwa Pengo alifika kwa Membe kumpa ujumbe wa Pengo kumsihi amsamehe Musiba.

"Alikuja hapa padre wa moja ya makanisa yetu kuleta ujumbe huo lakini naona Mzee alimkatalia na kumwambia 'namheshimu sana baba Askofu Pengo lakini kwenye hili anisamehe yeye (Pengo) huyu kijana lazima alipe gharama ya matusi yake' " anasema mwanafamilia aliyetajwa kwa jina la Colleta na kuongeza:

"Lakini jioni yake ya saa moja Askofu Malasusa naye alimpigia simu Mzee kuongelea suala hilo hilo lakini naye Mzee alimpa majibu yale yale aliyompa mjumbe wa Pengo." Hata hivyo kwa maelezo ya Colleta ni kwamba si tu ni msimamo wa Mwanadiplomasia huyo Bali ni msimamo pia wa familia.

Hii inakuja baada ya jitihada za Askofu Mwamakula pia kugonga mwamba baada ya kumwandikia barua Membe ya msamaha kwa Musiba.

Wakati hayo yakijiri hapa Mikocheni, tayari kampuni ya Yono imeshatua jijini Dodoma itakapoanzia kazi ya mnada kwa kuanza na apartments za Musiba zilizoko Ihumwa, nyumba yake ya Chamwino, guest house yake ya Msalato na shamba la hekari 10 njia ya Singida.

Baada ya hapo Yono atatimba apartment ya Kigamboni, shamba la hekari 5 Bagamoyo kabla ya kugeukia mitambo yake ya uchapaji iliyoko jengo la Exim ghorofa ya 8 jirani na Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es salaam.

Ikumbukwe kwamba huko nyuma Musiba alichapa magazeti yake kampuni ya Malindi Printing huko Mbweni ambayo ni mali ya TISS. Jambo hili lilileta ukakasi wa kisheria kwani sheria ya vyombo vya habari (2016) inamtaka mlalamikaji kumshitaki Mwandishi, mhariri, mchapaji na msambazaji. Kwa mantiki hiyo DG wa TISS angetakiwa kusimama kortini. Ili kuokoa jahazi Musiba "alinunuliwa" mitambo mingine Mpya kutoka Ujerumani na kwa "huruma" mwana TISS Membe aliridhia. Nayo itanadiwa baada ya siku 14 kutamatika pamoja na nyumba na mashamba yake ya kijijini nakadhalika.

My take: Vijana tujifunze kitu katika sakata hili la Musiba na Membe kwamba tuwe na akiba ya maneno. Lakini pia akili ya kupewa changanya na zako. Waliokuwa wakimpa akili karibia wote wamemkimbia tena ndio wamekuwa jirani na Membe. Amtegemeae mwanadamu mwisho huwa kama hivi. Musiba kwishney!
Kuuliza Sio ujinga, hizo mali zote zinazotangazwa kupigwa mnada zina hati? Kama zina hati je zote zimeandika Majina yake au kuna zenye Majina ya mke na Watoto?
 
Back
Top Bottom