Uchaguzi 2020 Membe: Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala, nitajitosa na nitashinda

Uchaguzi 2020 Membe: Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala, nitajitosa na nitashinda

Duh!
JF ya siku hizi hata kujibu comment za wachangiaji inahitaji moyo sana!

Wewe kwa uzoefu wako hapa ulipaswa angalau ujitofautishe na kundi la instagram lililovamia JF lakini umeshindwa!

Samahani kama nimekukwaza!
Concept yake ni kwamba kama Magufuli kafanya mazuri mengi kwanini anaogopa kushindana na wengine ndani ya chama.
 
Bernard Kamillius Membe waziri wa zamani wa Mambo ya nchi za Nje na uhusiano wa kimataifa, anazidi kukoleza mbio za kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa 2020 ndani ya chama cha Mapinduzi CCM. Anaripoti Yusufu Katimba.

Taarifa za hivi karibuni zinasema Membe ambaye alikuwa waziri kwa miaka minane ya utawala wa Jakaya Kikwete, ameapa kujitosa katika kinyang'anyiro cha kumpinga rais wa sasa John Pombe Magufuli.

"Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala tuombe Mungu niwe mzima. Nitajitosa na nitashinda." Amenukuliwa mwanasiasa huyo akiwaeleza baadhi ya wafuasi wake wa karibu ndani ya chama hicho.

Amesema, "Katika hili siwezi kurudi nyuma na hayupo anayeweza kunishawishi kurudi nyuma. Nitagombea, nitajitosa katika kinyang'anyiro hicho kwa kuwa nina kila sababu ya kufanya hivyo."

Kupatikana kwa taarifa kuwa Membe amepanga kujitosa katika mbio za urais 2020, kutaweza kumaliza mining'ono kuwa kwa muda mrefu kiongozi huyo amekuwa akiendesha mikakati yake kimya kimya ya kumkabili Magufuli ifikapo 2020.


Sawa...kujitosa kwake ni sawa kabisa...ila jina lake litaishia kwenye kamati ya maadili...Kamati Kuu itabariki uamuzi wa kamati hiyo na kuamua jina moja tu nalo ni la JPM liende kwenye NEC...Nayo NEC itakubaliana na maamuzi ya Kamati KUU na kuamua kulipeleka kjina moja tu kwenye Mkutano Mkuu..huo ndio utamaduni wa CCM...
 
IMG_5906.JPG
 
Sawa...kujitosa kwake ni sawa kabisa...ila jina lake litaishia kwenye kamati ya maadili...Kamati Kuu itabariki uamuzi wa kamati hiyo na kuamua jina moja tu nalo ni la JPM liende kwenye NEC...Nayo NEC itakubaliana na maamuzi ya Kamati KUU na kuamua kulipeleka kjina moja tu kwenye Mkutano Mkuu..huo ndio utamaduni wa CCM...
Kwahiyo maamuzi ya vikao vyote vya chama tayari yanajulikana, kumbe CCM ni predictable.
 
Kuna la ajabu hapo mpaka usiamini, huoni juzi kakiri kuwa sauti iliyodukuliwa ni ya kwake? Kama ameweza kukiri yale atashindwa kuzungumza hayo? Ukweli ni kuwa kuna wanaccm wengi hawaridhishwi na namna Magufuli anavyoongoza chama chao na nchi kwa pamoja kwani kajigeuza kuwa mkubwa kuliko chama na nchi. Sasa huyo Membe anachofanya ni kumuonyesha kwamba yeye sio mkubwa kuliko chama au nchi, hivyo yuko tayari kupambana naye ili kumuonyesha hana madaraka zaidi ya hayo anayopaswa kuwa nayo.

Mimi ninaamini Membe hawezi kuwa rais mzuri, lakini huyu wa sasa sio mzuri pia. Na pia tulishatoka kwenye kuongozwa kwa vitisho na kusujudia viongozi. Sasa hivi tunataka kiongozi anayeheshimu wananchi sio anayeogopwa na wananchi kisa anapandikiza hofu. Kama ni maendeleo tungeweza kuyapata hata chini ya wakoloni, lakini uhuru wetu ulikuwa na maana kuliko maendeleo ya wakoloni.
Umeandika poa na kila kitu lakini sioni mantiki ya yeye kusema hivyo halafu Mwanahalisi ndiyo liwe lenye stori husika.
 
Membe kwa urais hapana. Ila nasema hivi . kwa vile hata Magu ameonesha kuto faa . wakipambanishwa tu Magu atakaa . ni bora Membe azuiwe kwa namna yoyote kumuepushia aibu the incumbent
 
Na atafukuzwa tu hakuna namna hata akisema anagombea Urais hawezi kunusurika na kufukuzwa. Atafukuzwa yeye na wenzake wote kama vipi akaanzishe Chama chake ama aungane na vyama vingine
Atafukuzwa kwa kosa gani.
 
Amesema, "Katika hili siwezi kurudi nyuma na hayupo anayeweza kunishawishi kurudi nyuma. Nitagombea, nitajitosa katika kinyang'anyiro hicho kwa kuwa nina kila sababu ya kufanya hivyo."
Labda urais wa YANGA
Kams alishindwa lowassa,alikua na NEC yote,na asilimia 90 ya wajumbe wa mkutano mkuu itakua kikaragosi membe?
Membe ni sawa na joka la mdimuni
 
Ninachokiona ni Membe kupewa sifa ambazo hana. Hata hivyo sishangai kwa sababu wapinzani wa Rais Magufuli wana ombwe la mtu ambaye atapambana naye katika kiti cha Urais.

Kinachofanyika kwa sasa ni kumshabikia mtu yeyote anayesema au kuonekana atapambana na Rais Magufuli hata kama hana sifa ili tu kujaza ombwe.
Ombwe lililopo magogoni ni dhahiri lahitaji kuzibwa. Kinyago tulichokichonga tukiogope vipi? Akalime nyanya chato na kwa vile uwanja wa ndege kajijengea kama maandalizi awe mjasilia mali tu.Nchi hii si sehemu ya Gitarama!
 
Kamilius Membe...! ananikumbusha miaka ya elf 2 kuelekea uchaguzi mkuu wa 2005 kuna Mbunge alikuwa wa jimbo fulani mkoa wa Lindi akiwa mbuge mfululizo zaidi ya miaka 30 na waziri mwandamizi ktk serikali ya Benjamin. Akajitokeza mshindani ktk jimbo hilo ambaye alikuwa timu Membe. Mbunge aliyekuwepo hakukubali kusalenda kwa huyo ndugu ingawa alijua promo ya huyo mshindani wake mtaani. Timu Membe ikamwambia Mbunge Waziri lazima 'tukung'oe tu'. Mbunge akapanic kwamba hawezi kung'olewa km muhogo, alijitahidi kututumia mbinu zake zote abaki lkn wapi mwisho wa siku ilipokaribia mchakato wa kumpata mgombea ndani ya chama akatangaza kutogombea. Wakati wa mchakato ndani ya chama akaja na mbinu ya kumbemba X-DC mmoja ili mshindani wake timu Membe naye akose ubunge lkn alishindwa. Mgombea timu Membe akapeta ndani ya chama na uchaguzi wa 2005 akshinda ubunge na Jakaya akampa uwaziri. Huyo ndo Membe.
 
Bernard Kamillius Membe waziri wa zamani wa Mambo ya nchi za Nje na uhusiano wa kimataifa, anazidi kukoleza mbio za kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa 2020 ndani ya chama cha Mapinduzi CCM. Anaripoti Yusufu Katimba.

Taarifa za hivi karibuni zinasema Membe ambaye alikuwa waziri kwa miaka minane ya utawala wa Jakaya Kikwete, ameapa kujitosa katika kinyang'anyiro cha kumpinga rais wa sasa John Pombe Magufuli.

"Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala tuombe Mungu niwe mzima. Nitajitosa na nitashinda." Amenukuliwa mwanasiasa huyo akiwaeleza baadhi ya wafuasi wake wa karibu ndani ya chama hicho.

Amesema, "Katika hili siwezi kurudi nyuma na hayupo anayeweza kunishawishi kurudi nyuma. Nitagombea, nitajitosa katika kinyang'anyiro hicho kwa kuwa nina kila sababu ya kufanya hivyo."

Kupatikana kwa taarifa kuwa Membe amepanga kujitosa katika mbio za urais 2020, kutaweza kumaliza mining'ono kuwa kwa muda mrefu kiongozi huyo amekuwa akiendesha mikakati yake kimya kimya ya kumkabili Magufuli ifikapo 2020.

Ahhhh wapi , fisiem wajinga sana! Hapa wanataka kutuaminisha wagombea Urais 2020 ni kati ya Jiwe Vs Membe , mwisho wa siku Membe anajitoa Jiwe anapita bila kupingwa.

Na msitegemee Membe kufukuzwa Uanachama wa Ccm kwa kumpinga Jiwe , haya ni maigizo. Membe akifukuzwa uanachama wa ccm hapo kweli nitaamini kweli alikuwa anampinga jiwe siyo vinginevyo.


Mark my words.
 
Na atafukuzwa tu hakuna namna hata akisema anagombea Urais hawezi kunusurika na kufukuzwa. Atafukuzwa yeye na wenzake wote kama vipi akaanzishe Chama chake ama aungane na vyama vingine

Wakimfukuza ndio itakuwa vizuri ili mkose pa kujifichia pale mnaposema ccm kuna demokrasia, na mkimuacha mmemuogopa.
 
November 2020 baada ya uchaguzi utuletee feedback please.

Ashinde yeye,asishinde ila moto atakua ameupata na aameungua mpaka matak0!

Atakua ametambua demokrasia ni demokrasia na wananchi ndio maboss wa everything!
 
Back
Top Bottom