Uchaguzi 2020 Membe: Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala, nitajitosa na nitashinda

Uchaguzi 2020 Membe: Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala, nitajitosa na nitashinda

Miundombinu inajengwa kwa kodi za wananchi na sio hisani au mshahara wa rais. Hivyo miundombinu itajengwa na yoyote hata kama nchi itakuwa haina rais kwani mipango ya nchi ipo tayari.
Duh mkuu, uko sawasawa kweli. Huo ndo upeo wako wa kufikiria au kuna kitu kime hack ubongo wako
 
CCM kuna demokrasia ambapo wanachama wanajadili mambo yao kwa uwazi kwenye vikao halali vya Chama. Hiyo demokrasia ya kujificha na kuanza kufanya mipango ya uhaini si demokrasia bali domogasia
Makatibu wamekuja na waraka kwa nia njema tu, tumeona walivyoshambuliwa kwa matusi sijui ndiyo demokrasia unayoisema.
 
Umetoa mchango wa mawazo mzuri sana. Wewe ni great thinker
Kuna la ajabu hapo mpaka usiamini, huoni juzi kakiri kuwa sauti iliyodukuliwa ni ya kwake? Kama ameweza kukiri yale atashindwa kuzungumza hayo? Ukweli ni kuwa kuna wanaccm wengi hawaridhishwi na namna Magufuli anavyoongoza chama chao na nchi kwa pamoja kwani kajigeuza kuwa mkubwa kuliko chama na nchi. Sasa huyo Membe anachofanya ni kumuonyesha kwamba yeye sio mkubwa kuliko chama au nchi, hivyo yuko tayari kupambana naye ili kumuonyesha hana madaraka zaidi ya hayo anayopaswa kuwa nayo.

Mimi ninaamini Membe hawezi kuwa rais mzuri, lakini huyu wa sasa sio mzuri pia. Na pia tulishatoka kwenye kuongozwa kwa vitisho na kusujudia viongozi. Sasa hivi tunataka kiongozi anayeheshimu wananchi sio anayeogopwa na wananchi kisa anapandikiza hofu. Kama ni maendeleo tungeweza kuyapata hata chini ya wakoloni, lakini uhuru wetu ulikuwa na maana kuliko maendeleo ya wakoloni.
 
Kwani katiba ya CCM inasemaje kuhusu hilo?
 
Ukweli ni kwamba JPM ni kiongozi mzuri sana,kama angeheahimu katiba na chama chake pia,angeshughulika na matatizo ya nchi pasipo kiburi na jeuri,angeacha kufanya upendeleo wa wazi wazi kama afanyavyo sasa,angeimarisha taasisi zaidi na sio kwa kiburi cha kujiona yeye ni booora kuliko wengine wote!

Amekuta nchi hii inaendelea kujengwa,(barabara,viwanja vya ndege,madaraja,na miradi mingine mingi) ila ajabu sasa akisimama yeye anazungumza kana kwamba nchi ameikuta ikiwa jangwa na ameanza yeye kuijenga (hii si sawa hata kidogo)

Tazama mfano mdogo tu huu,alipokuwa anazindua terminal 3 ya uwanja wa mwl.Nyerere,amesahau kuwa terminal 1 na two tayari zilikuwa zimejengwa na watangulizi wake,na yeye kwa sehemu yake amesimamia ujenzi wa hiyo terminal 3,lakini namna anavyozungumza utadhani yeye ndo wa kwanza kuijenga hiyo airport!

Ameenda mbali zaidi kwa kiburi na jeuri kwamba "ikitokea siku Mungu amenichukua sina hakika kama anayekuja ataweza kazi hii..." Khaaa! Yaani amefika mahali anaona hakuna mtu mwingine anayeweza kufanya kazi ya urais isipokuwa yeye? Na anadiriki kusema hadharani eti Mungu akimchukua, kwani watanzania wamesema wanataka awe rais mpaka Mungu amchukue?

Katiba aliyoapa kuilinda na kuitetea inamwambia kuwa atakuwa hapo mpaka Mungu atakapomchukua? Au ni jeuri na kiburi cha madaraka? Ni kiongozi wa kawaida sana tu,na kama ingekuwa mtu wa kukaa madarakani mpaka kufa alikuwa baba wa taifa hili,kwa sababu watu walimpenda pamoja na mapungufu machache aliyokuwa nayo!

Hawa wengine ni wadanganyifu tu,wanaitumia Ikulu yetu kujinufaisha,tena huyu anafanya wazi wazi,tazama CHATO inavyofanywa bila aibu tunahamisha mpaka hifadhi!

Kama kila mtu angetaka kufanya kama afanyavyo huyu,basi kuna maeneo yangekuwa masikini kabisaaa kwa sababu tu,hayakutoa mtu mwenye wadhifa wa rais!

TUJIREKEBISHE,TUHESHIMU KATIBA YETU ,TUJENGE NCHI KWA ZAMU!
 
Kwa wanasiasa ni jambo la kawaida
Hata wewe zipo nyuzi zako humu unawsshabikia slaa,zitto na kitila,nina uhakika ukikutana nao leo unaweza hata kuwatemea mate
Labda Slaa, lkn Zitto na Kitila tangu mwanzo nilikuwa na wasiwasi wao.
 
Akili za wana CCM wasio kuwa na maono ndio hutoa michango kama yako. Mbona hamja mshughulikia au mnasubiri wakati wa kura za maoni? Shame!!!
Kwanza anatakiwa kuchukuliwa hatua na Chama chake baadae ile sauti yake iliyodukuliwa kusambaa. Hii ya kugombea anasema ili wakimfukuza apate agenda ya kisiasa eti baada ya kuonesha nia ya kugombea urais 2020 ndo amefukuzwa chamani.

Membe anatakiwa kufukuzwa fasta CCM ili akastaafie siasa akiwa opposition.
 
Miundombinu inajengwa kwa kodi za wananchi na sio hisani au mshahara wa rais. Hivyo miundombinu itajengwa na yoyote hata kama nchi itakuwa haina rais kwani mipango ya nchi ipo tayari.
Tatizo hapq siyo kujenga swala kubwa hapa ni usimamizi na nidhamu kwa pesa zetu wananchi.
 
Labda Slaa, lkn Zitto na Kitila tangu mwanzo nilikuwa na wasiwasi wao.
Nassary kauza mechi upo kimyaa,Mbowe kapitiliza muda madarakani hataki uchaguzi upo bize na ccm na membe
Akili yako inakuambia kabisa,membe atachukua fomu,atarudisha,atapitishwa na sekretarieti,atapitishwa na kamati kuu,ataputishwa na NEC,halafu atapita kwa kishindo kwenye mkutano mkuu?lazima ukapimwe
Membe na January wameshakosa sifa za kugombea urais,kwa sababu walishafunguliwa ma file na mangula ya kucheza rafu 2015 kwa kuanza mapema kampeni
Zama hizi ni za magufuli ni bora tu wakae nyumbani
 
Bernard Kamillius Membe waziri wa zamani wa Mambo ya nchi za Nje na uhusiano wa kimataifa, anazidi kukoleza mbio za kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa 2020 ndani ya chama cha Mapinduzi CCM. Anaripoti Yusufu Katimba.

Taarifa za hivi karibuni zinasema Membe ambaye alikuwa waziri kwa miaka minane ya utawala wa Jakaya Kikwete, ameapa kujitosa katika kinyang'anyiro cha kumpinga rais wa sasa John Pombe Magufuli.

"Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala tuombe Mungu niwe mzima. Nitajitosa na nitashinda." Amenukuliwa mwanasiasa huyo akiwaeleza baadhi ya wafuasi wake wa karibu ndani ya chama hicho.

Amesema, "Katika hili siwezi kurudi nyuma na hayupo anayeweza kunishawishi kurudi nyuma. Nitagombea, nitajitosa katika kinyang'anyiro hicho kwa kuwa nina kila sababu ya kufanya hivyo."

Kupatikana kwa taarifa kuwa Membe amepanga kujitosa katika mbio za urais 2020, kutaweza kumaliza mining'ono kuwa kwa muda mrefu kiongozi huyo amekuwa akiendesha mikakati yake kimya kimya ya kumkabili Magufuli ifikapo 2020.

Huyu Mzee anaota ndoto za mchana. Hivi kwani lazima kila mtu afanye siasa?.
 
Wakati mwingine unaweza usielewe watanzania wanataka nn. Hata kama ni kuchanganyikiwa sio kwa kiwango hicho. Hatujafikia hatua ya kuona membe anaweza kuwa rais mzuri kuliko magufuli.

Mi naona ni mbinu tu za kisiasa baada ya kuona hana mwelekeo yeye na kundi lake so wanajaribu kutafuta umaarufu. Lakin kwa akili y kawaida hawana tena future kwenye siasa za nchi hii. Wamepoteza wakubali either kustaafu au kushirikiana na serikali iliyopo otherwise wanajitengenezea future mbaya tu bila sababu za msingi.

Hakuna mtu alikuwa na nguvu ndan ya CCM kuliko Lowasa. Lakin unavotangaza kupambana na mtu alie madarakan hadharan sidhan kama unaelewa maana yake. Marekan tu wameshindwa kumchomoa Trump sembuse nchi zetu hizi changa kidemocrasia. Wanaomshauri wanamdanganya.

Membe habari yake ishaisha kwenye siasa za Tanzania. Ni kama Lowasa habari yake ilivoisha baada ya kuondolewa kwenye uwaziri mkuu. Its over. Kwanza mtu mwenyewe hana mvuto kama aliokuwa nao Lowasa. Lakin pia hana ubavu wa kupambana na kundi jipya la akina Magufuli ambao ni majasiri kuliko ujasiri wenyewe. Subirin mtaona.

Kama obama alivopambana kumuondoa Trump akashindwa ndivo wanaomshauri Membe wanavojiharibia.

Kama kuna kosa walifanya ni pale walipompa Nchi magu. Hawawezi kumnyang'anya tena. Wasubiri tu muda wake uishe. Lakin as i know story ya Membe kuwa Rais ishafungwa. Asahau kabisa
 
Nassary kauza mechi upo kimyaa,Mbowe kapitiliza muda madarakani hataki uchaguzi upo bize na ccm na membe
Akili yako inakuambia kabisa,membe atachukua fomu,atarudisha,atapitishwa na sekretarieti,atapitishwa na kamati kuu,ataputishwa na NEC,halafu atapita kwa kishindo kwenye mkutano mkuu?lazima ukapimwe
Membe na January wameshakosa sifa za kugombea urais,kwa sababu walishafunguliwa ma file na mangula ya kucheza rafu 2015 kwa kuanza mapema kampeni
Zama hizi ni za magufuli ni bora tu wakae nyumbani
Kati ya wanasiasa Nassary naye unamhesabu, kuhusu Mbowe kasome katiba ya Chadema. Kama matokeo ya vikao vyote vya CCM unayajua yanajulikana kwa wanachama kama wewe kuna haja tena ya CCM kufanya vikao.

Ni kweli kwa sasa Magufuli ni kila kitu, amekuwa mkubwa kuliko chama, yeye ndio katiba, neno lake halipingwi wala kukosolewa.
 
Back
Top Bottom