Uchaguzi 2020 Mfa maji haachi kutapatapa! CHADEMA maji shingoni

Uchaguzi 2020 Mfa maji haachi kutapatapa! CHADEMA maji shingoni

Ndugu zangu,

Sisi waswahili huwa tuna msemo ''ukiona kenge anatoa damu masikioni ujue anakufa''..hali ipo hivi, yawapasa muelewe. Hakuna mtu anayeweza kusema ''nimeshindwa'' au ''tumeshindwa'' hasa ikiwa alishajigamba na kujimwambafai kuwa anashinda saa mbili asubuhi.

Kauli za ''kiutu uzima'' ni kama ''hatuna pesa za kampeni'', ''mguu wangu haukunjuki'' ''habaru zangu hazirushwi'',''mshindani wangu anahela sana''.

Kwa wale tunaojua hesabu za ''cross multiplications'' tunasema ''ikiwa Tundu kafanya mikutano 10 ndani ya siku 10 basi ndani ya siku 60 anatafanya mikutano 60''

Ukweli ni kuwa angalau ya watanzania asilimia 70 wanaishi vijijini sasa kama kishagundua kuwa hawezi kukutana na kushawishi wanachi walio wengi wampigie kura, ni dhahiri kishaanguka.

Wakati umefika ambao Robert Amsterdam amejichokea na kutokomea bila kuandika ''vijibarua vyake uchwara''.

Uraisi sio Urahisi.
 
Huu uchaguzi una uhaba mkubwa wa mabango na bendera za kampeni hata za mwaka 1995 nyingi. Nadhani ni mambo ya funds. Just thinking aloud.
 
Naona kilaza wa Lumumba umekuja kujidhalilisha humu!

Kwanza nani kakwambia mgombea wa Chadema kalalamika hawana hela? Aliulizwa swali juu ya bajeti na akaelezea kuwa wanategemea michango, shida iko wapi?

Kwani ni uongo kuwa mmempitisha mgombea ambae mlidai ni fisadi na anashirikiana na mabeberu kugombea Ubunge njombe????? Hapa hamna lolote lile la kujisafisha.

Kuhusu raisi kutoa kufanya utekelezaji kipindi cha kampeni hivi hujui kuwa kuna maadili ya uchaguzi??? Hujui kuwa kuna kitu kinaitwa rushwa kwenye uchaguzi!? Mtu kuwa raisi haiondoi ukweli kuwa na yeye ni mgombea ivyo lazima aheshimu miiko na taratibu a uchaguzi!

Ni dhahili kuwa sasa CCM mmeshindwa kuja na majibu ya hoja za Lissu hivyo mmeamua kufanya upotoshaji ila ukweli ni kuwa watanzania tumemuelewa sana Lissu.
 
Are you insane? Barabara ilishafanyiwa upembuzi yakinifu. Alafu rais anasema ataijenga ni rushwa? Kuwashauri watu wa Bunda wasikosee kuchagua ni kuwatisha.
Walikuwa wapi siku zote kuanza ujenzi hadi wasubiri kipindi cha kampeni tena Maji ya shingo???
 
Hakuna msimu chadema wamekosa mgombea uraisi kama awamuu hiiii.

Maana ukiangalia mgombea walie mpisha, kwenye kujenga hoja na kuleta heshima ya mgombea uraisi, kiukweli anapwaya saana. Tungu lisu mda wote wa kampeni anautumia kama mwanaharakatii. Sasa hiii imesha mgarimu, vinginevyo abadili namna ya kuendesha kampeniii. Au viongozi wenzake wamshauliiii.
Mwaka huu kuna mgombea mzuri na anayetosha Kama Tundu Lissu?
 
Walikuwa wapi siku zote kuanza ujenzi hadi wasubiri kipindi cha kampeni tena Maji ya shingo???
Ujenzi umeanza mkuu? Mtendaji mkuu Tanroads ameambiwa atangaze tenda. Alafu kila jambo na wakati wake.
 
Chama chochote kushinda uchaguzi sio tu inategemea uongozi wake umefanya vitu vingapi! bali ni lazima kwenda mbali zaidi kujiuliza hivyo vitu vimefanyika kwa njia zipi na wakati gani alafu visingefanyika je,chama kingine kingefanya kwa njia gani na ubora gani kulinganisha na lasirimali watu na vitu vilivyopo.

Kwaufupi nilazima tutambue sera mbadala na namna gani ya kufanya vitu na manufaa yake kwa watu na kwa wakati kuliko kujivuna kufanya tu ,wakati labda kuna wengine wanaweza kufanya zaidi ya hapo bila kuumiza wananchi wake.
 
Uchaguzi wa mwaka huu ulionyesha mapema kabisa kuwa CCM itashinda kwa urahisi sana. Hii ni kwa sababu kazi nzuri iliyofanyika ndani ya miaka minne ilikuwa ni kete tosha kwa CCM kutusua bila matatizo

Zimebaki siku 49 watanzania waende kupiga kura ili kuchagua wabunge, madiwani na rais wa JMT kakini mpaka siku ya leo inafika tayari Chadema wameshaonyesha kushindwa. Na hii ni kwa sababu wamenza kulialia kama watoto wadogo.

Kitendo cha mgombea urais wa CHADEMA kuanza kutoa sababu ambazo hazina msingi,hizi ni Dalili kuwa sasa jahazi linazama. Mfano kulialia kwa waandishi wa habari kuwa sasa hana pesa na inalazimu kutembeza bakuli hii ni dalili kuwa hali ni mbaya. Lakini kwa nini hakufanya tahimini kuwa Chama chake hakina fedha hivyo akakaa kando na kuacha kuingia kwenye mtanange ambao ni gharama kubwa kuuendesha? Lissu hakufanya tathimini kuwa kuna michango ya wabunge iliyokuwa itumike kwenye uchaguzi ilikwapuliwa na wamiliki wa Chadema? Maana hii ni aibu kutembeza bakuli wakati wananchi tuna hali ngumu.

Kusema kuwa CHADEMA wanachota pesa za serikali pia ni dalili kuwa huyu jamaa amekosa hoja za msingi. Hivi hajui kuwa Ccm wana asset ambazo zinawaingizia pesa lukuki ambazo wakizikusanya kwa miaka mitano zinaweza kuendesha kampeni kwa ufanisi mkubwa? Kutoa sababu eti Hayati Benjamin Mkapa alisema kuna watu walimdanganya na kukwapua pesa za Epa sio justification kuwa Ccm inachota pesa serikalini. Maana CCM ya mwaka 2005 sio hii ya leo.

Kuleta hoja eti CCM imepitisha mgombea ubunge wa Njombe ambae alikuwa na mashitaka ya ufisadi. Kwa hiyo Ccm haipambani na ufisadi huku nako ni kukosa hoja zenye mashiko na zisizo na msaada kwa CHADEMA . Mimi nafikili kama chama makini wangetuambia namna gani watamshinda huyu mgombea ubunge aliyekuwa na makosa ya ufisadi ili wachukue jimbo la Njombe kuliko kuanza kulalama juu ya kuteuliwa kwake kugombea. Pia ifahamike huyu mgombea baada ya kubainika amefanya makosa ya kusaidia Acaccia wasilipe kodi alikamatwa nakufunguliwa mashitaka na kisha kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria. Na hukumu yake haijamuondolea sifa ya kuwa mgombea ubunge. Kwa hiyo ni wazi kuwa serikali ya CCM ilichukua hatua stahiki, kusema kwamba haipambani na ufisadi ni uongo na kukosa hoja.

Kujibu hoja ya kuwa anatumiwa na mabeberu kizembe hivyo pia imeonyesha ni wazi kuwa anapata misaada toka kwa mabeberu. Maana huwezi kusema kuwa kisa Usaid au JICA wakitoa misaada tayari tumepata msaada toka kwa mabeberu. Maana dhana nzima ya ubeberu huwa inakamilika pale misada ya taifa lenye uwezo linapotoa msaada ambao una lengo la kuinyonya nchi yetu kiuchumi,kisiasa na kiutamaduni. Hili hajajibu vuzuri maana anakiri kuwa impliedly kuwa anapata misaada. Je hiyo misaada anaipata kwa mashariti gani huyu ndugu Lissu? Ili aje alinde faragha za watu wanaovunja sheria za nchi!

Kusingizia media za Tanzania hazifanyi coverage ya mikutano yake ni aibu na hii ndio imeonyesha sasa ameishiwa nguvu. Amesahau kilichotokea pale Zakheim? Lakini pamoja na hayo mimi naona vyombo vya habari karibu vyote vinaripoti mikutano yake.

Kusema rais anatumia madaraka yake kujipatia kura. Hili nalo linachanganya. Kwani Tundu Lissu hajui kuwa ukomo wa rais wa JMT ni mpaka aapishwe mwingine? Maana pale Nyehunge rais Magufuli alikuwa anatumia kofia yake ya urais kutekeleza majukumu yake,na kwa katiba ya JMT lipo wazi. Ila dalili zinaonyesha sasa maji yamefika shingoni na baada ya siku kumi itakuwa aibu kwa Chadema.
Naona mkuu CHADEMA imekunata akilini. Kutaja kuwa CHADEMA inakwapua hela ya Serikali badala ya CCM, inadhihirisha hoja hiyo. Pili n kwamba CCM bila msaada wa tume ya uchaguzi na vyombo vya dola na habari ni wepesi sana. Kama CCM inapendwa na wananchi kwa nini itumie tume kuengua wagombea wa upinzani na kutisha vyombo vya habari visitangaze kampeni za wapinzani? "The entire media through CCM influence is biased against the opposition. Shame on CCM!"
 
Mwaka huu kuna mgombea mzuri na anayetosha Kama Tundu Lissu???
Kwa kujifariji mnawezaa. Yaani anatia huruma, alidhani kwa zile kiki alizozifanya halafu akatimkia ugaibuni, alidhani akirudi atapindua meza fasta kwa kutumia kiki ya miujizaaa, sasa zote zimebumaaa.
 
Back
Top Bottom