Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Fanya hivyo mzee may be I can change my view cause a critical thinker always changes his view when presented with better argument
Nmeshindwa kuilocate kwa sasa ila kuna clip moja fupi hapa inaelezea kiufupi theory hii ambayo bado inafanyiwa utafiti zaidi kila cku ili kuja na conclusion moja nzito kwa ufupi tu inasema gharika lilikuja baada ya water canopy kuanguka duniani na kujaza maji dunia nzima na inadai baada ya mabonge hayo ya barafu kuanguka ndio ilisababisha pia ice age at some point!!



 
Kwanza kuna kitu hakileti ukweli katika Biblia maana hapa katika maandiko ya mwanzo kuna mkanganyiko inaonyesha WANEFILI WALIKUWEPO KABLA YA BINADAMU

1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo 6 :1

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.
Mwanzo 6 :2

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
Wana wa Mungu agano la kale walikuwa malaika
 
Nmeshindwa kuilocate kwa sasa ila kuna clip moja fupi hapa inaelezea kiufupi theory hii ambayo bado inafanyiwa utafiti zaidi kila cku ili kuja na conclusion moja nzito kwa ufupi tu inasema gharika lilikuja baada ya water canopy kuanguka duniani na kujaza maji dunia nzima na inadai baada ya mabonge hayo ya barafu kuanguka ndio ilisababisha pia ice age at some point!!



Mkuu soma Post [HASHTAG]#279[/HASHTAG]
 
Zote hizo ni myths, na ndo maana same stories zimepatikana mabara tofauti na kwa namna tofauti zikielezea matukio hayo hayo kwa namna na tamaduni zao.
Mbona mfalme Ogu nmekuwekea hapo mpaka kasri lake liliotajwa kwenye biblia lipo mpaka leo na eneo ambalo alifia kuna kaburi limekutwa lenye vipimo kma ambavyo vipo kwenye biblia au ushahidi gani zaidi unataka kuhusu uwepo wa mfalme ogu???

Hoja yangu hapa ni kwamba kuna ushahidi hta kma ni mdogo wa uwepo wa gharika kuanzia canopu theory inayosuggest kuwa katika muda flani dunia ilikuwa imemezwa na maji (gharika) haijalishi ni gharika la Nuhu au utnapishtim au Unju bin unuku wa mtwara!!! Ila gharika lilikuwepo sasa watu wanatohoa simulizi kutoka hapo na kwa kuwa wengine hawakuwa na contact na maeneo mengine ya dunia hivo wanaeleza story kwa mifano ya jamii zao

Mfano quran inamuita Yesu ni nabii Issa , biblia inamuita nabii issa kuwa ni Yesu..... Talmud inamuita Yesu ni yashua ila story zote zinafanana ssa je itakuwa uongo kisa tu kila kitabu cha dini kinamuita tofauti?? Story ni moja ila kila mtu anaandika kuendana na muktadha wake

So gharika lilikuwepo moja tu ila kila mtu anaelezea kwa muktadha wake!!
 
mkuu, wana wa Mungu ambao wanachukua hadhi flani ya malaika angalau ni wale wa kwenye kitabu cha ayubu ambao shetani alijihudhulishaamoja nae.
lkn pia panaacha vimaswali kidogo, kwa nini malaika wajihudhulishe mbele ya Mungu wakati yuko nao kila siku huko. CC Isaya 6.

Kuhusu Nebukadneza.
Alianza kwa kusema "Naona watu wanne"
Kisha akasema " mmoja wao ni mfano wa mwana wa Miungu"
Kisha akasema " Mungu katuma malaika kuja kuwaokoa"
Nebukadneza alikuwa mpagani, mwenye uelewa finyu wa mambo ya Mungunwa waebrania.
utajiuliza alijuaje kuwa yule ni mwana wa Miungu? lakini kwa nini aone watu wa nne, badala ya watatu na malaika mmoja.
Sisi tunayemjifunza Yesu, Tunaamini huyo alikuwa ni Yesu. Na yawezekana kwa kukaa na wale madogo nebukadneza alikuwa na mwangwi wa uelewa wa uwepo wa mwana wa Mungu (Mwana katika GodHead). Ndio maana yesu aliwashangaa mafarisayo kwa nini wanasoma maandiko hayo likiwemo na hilo lakini hawaelewi?

uelewa mdogo wa nebukadneza sidhani kama ni sahihi kuutumia kama kigezo ha kuhalalisha uwana wa malaika.

maoni mkuu.
Hoja yangu sio nebukadneza nasema neno lilitomuka kwenye biblia ya kiebrania ni MOJA yaani bene elohim? Ila limeelezwa kama mwana wa Mungu kwenye mstari wa 23 na baadae ikaelezwa kama malaika kwenye 28 hoja hapa ni kwamba LINA MAANA MOJA kwa muktadha wa kitabu cha daniel na ndio maana limeelezwa kma substitute ya malaika na mwana wa Mungu

Hivyo usiangalie alichosema nebukadneza ila angalia muandishi wa kitabu ambaye alikuwa na ufaham wa dini na alijua tofauti ya mwanadamu na malaika ila bado alitumia NENO moja tu kwenye verse 23 na 28
 
Huyo ogu naye alikua mhutu kama Ww?
Hapana alikuwa kabila la Waamori huko kanani na alikuwa ni mweusi kama mimi ila aliongea lugha ya kisemiti kma ya watu wa mashariki ya kati ya sasa (waarabu) na alitawala TERRITORY inaitwa bashani iliokuwa na majiji 68 ambayo sidhani kma Rwanda yenu itaweza fikisha maana ina jiji moja tu!!!

Ila kwa kuwa umeuliza je alikuwa mhutu ?? Naweza sema ameshare one thing in common na wahutu kwamba wayahudi hawapendi kutawaliwa na makabila mengine ndio maana kila nchi wanayoenda wanataka kutawala wao tu kila nyanja ya nchi na waliwaua hawa waamori sababu waliwaona ni tishio kma tu watutsi mlivyowafanyia wahutu so hilo pekee ndio linaweka relation kati ya mfalme ogu na wahutu 😀😀😀
 
Mbona Yesu alizaliwa bila mwanaume kulala na Maria??? Ina maana Roho mtakatifu alikuwa na jinsia hadi apandikize mtoto kwenye kizazi cha maria??

Kama hoja ni sex Majini wanaolala na wanawake wanawezaje?? Hata kma wakiwa ndotoni ila huwa wanaamka asbuhi na kukuta wametumika!!

Kwa ufahamu wangu malaika hawana jinsia ni wakiwa katika mfumo wa kiroho ila wakija hapa duniani huwa lazima wavae mwili ukisoma biblia utaona malaika waliomtembelea Abraham walikuwa wanaonekana ni wanaume!!! Hata waliomtembelea Lutu walionekana ni wanaume na walikula walilala walioga walicheka n.k kma walifanya yote hayo kwanni huamini wanaweza pia kumlala mwanamke/mwanaume???

Tuanzie hapo
Umejibu vizuri sana mkuu
 
Vipi kuhusu Goliath na ndugu zake nao si walikuwa Nephilium?
Yes walikuwa wana damu ya wanefili sababu joshua hakuua wanefili wote wengine walikimbilia gaza waliachwa na ndio baadae tunaona wanaoana na baadhi ya familia za mizraim (misri ya sasa) na wanapata uzao mwingine huko ugiriki ambako ndipo goliath alitokea hivyo basi conclusion ni kwamba NDIO goliath alikua uzao wa wanefili
 
Sasa kwa ukubwa huo wa wanefili wa kike ilikuwa lazima wajamiiane na wanefili wenzao wa kiume. Sababu mwanaume wa kawaida ungeweza kuzama na kupotelea kwenye kiungo cha uzazi cha jitu la kike. Vivyo hivyo mwanamke wa kawaida angewekewa dhakari ya jitu la kiume ingekuwa kama kabebeshwa nguzo ya umeme angekufa papo hapo.

Swali linakuja wanefili(majitu) walizaana vipu na binadamu?

Labda tujenge nadharia kwamba baba wa wanefili wa kwanza walikuwa malaika waovu ambao kwa uwezo wao walichukua maumbo madogo ya miili sawa na binadamu.
Lakini walipowapa mimba binadamu ndipo wakazaliwa watoto majitu yaani wanefili wanaume kwa wanawake. Nao wanefili wakapata kuoana wenyewe kwa wenyewe.
Mkuu wanefili naona walikuwa wanaoana wenyewe kwa wenyewe na ndio maana hatukuti kwenye uzao wa shem au japhet kuwa kuna uzao wa wanefili ila kwenye kizazi cha HAM pekee ikimaanisha walioana wao kwa wao tu na ndio maana kizazi kikaendelea ona kuanzia canaan mpaka kwa wanawe walikuwa wakubwa na wajukuu mpaka vitukuu kina goliath bado wakubwa hivo kma ulivosema kwamba ni lazima walioana wao kwa wao ila sidhani kma wangeweza kuoana na wanawake wa kawaida fikiria mtu wa futi 16 alale na mwanamke wa kawaida tu si kutafuta kifo tu
 
Mkuu zitto junior ukitaka uyasome vizuri haya mambo watafute wasomi wa Theolojia hawa wafuatao. Dr. Kenneth Hovind, Dr. Perry Stone na Dr.Finnis Dake.

Dr. Finnis Dake wanatheolojia wenzake wanamwita a Heretic kwasabababu alifanya utafiti kuhusu uumbaji kwa miaka 30 na akaja na nadharia zake ambapo akadai kwamba kabla ya Uumbaji kulikwa na Pre-Adamites walioishi hapa duniani.
Akatoa na ushahidi wa mistari ya kibiblia ili kuweka uzito.

Akasema dunia iliumbwa mara ya kwanza kabisa lakini kwenye uumbaji anasema hakuna sehemu ambayo maji yaliumbwa hivyo akadai na kusema kwamba kulikuwa na Mafuriko ya kwanza hata kabla ya yale ya Nuhu. Kibaya zaidi ni kwamba Mafuriko ya kwanza yalikuwa yakumtoa Lucifer mbunguni baada ya vita.

Akasema kwamba Lucifer alianguka kabla ya Uumbaji na Mungu akaamua kuumba viumbe wengine (Binadamu) ili kuyhibitisha kwamba yeye huwa hakosei na ndiyo maana Lucifer akawa anawashambulia sana wanadamu. Sasa akauliza swali, kama Lucifer alianguka duniani kabla ya Uumbaji aliangukia dunia ipi hiyo ???

Amezungumzia uwepo wa Pre-Adamites ambao Mungu aliamua kuwagharikisha baada ya kuanguka kwa Lucifer kwasababu walijiunga naye kwenye Uasi dhidi ya Mbingu.

Amezungumzia vitu vingi sana kwa kupitia maandiko mbali mbali. Vitabu vyake na CD vilikuwepo nyumbani kwetu miaka ya nyuma kidogo. Kama bado zipo ntajaribu kuscan baadhi ya kurasa na kurip baadhi ya video halafu ntaviweka hapa.
Mkuu umenifikirisha sana hapo kuhusu uwepo wa pre adamic race...... Dah ntawafuatilia hao manguli na ntafurahi ukitusaidia na hizo tools siku moja tujifunze zaidi. Kwa kweli JF ni home of great thinkers maana kila siku najifunza kitu kipya ubarikiwe sana mkuu
 
Back
Top Bottom