Mfanyabiashara ahukumiwa kunyongwa Dar, alimuua mdai wake aliyempa hela amuagizie Fuso

Mfanyabiashara ahukumiwa kunyongwa Dar, alimuua mdai wake aliyempa hela amuagizie Fuso

Similar scenario imetokea huku kwetu mzee mstaafu aliagiza fuso kwa kumtumia mtoto wa rafiki yake 2018. Mzee kidogo adhulumiwe kabisa fuso imeletwa 2022 mwezi wa 8... Jamaa kamletea mzee baada ya kushinikizwa sana ase. Na fuso lenyewe kamletea namba AZ_.

Cha kusikitisha zaidi ni kwamba nyumba anapoishi mzee kumetokea attempts mbili za kuichoma. Mara ya kwanza walichoma nyumba ya jirani yake ambaye ni mstaafu pia na ana gari ya mizigo pia. Hii iliungua kabisa yani kila kitu, lakini mchomaji alikosea nadhani hakuwa mwenyeji wa haya maeneo yetu.

Baada ya siku moja kupita, Attempt ya pili ilikuwa kwenye target yenyewe lakini nyumba ya mzee ilipona miraculously. Walichoma milango lakini moto haukukolea hadi ndani walijaribu kuchoma mbao za kenchi lakini ilishindikana.

Matukio yote haya yalifanywa wakati wa usiku watu wakiwa wamelala.

Inasemekana huyo jamaa alipewa hela ya kununua fuso yenye ubora lakini ndo hivyo kamletea mzee wa watu garasa na kumpa presha za kuchomewa nyumba.
 
Mimi nakumbuka mke wa Marehemu alienda kuripoti polisi kupotea Kwa Mumewe na kuulizwa NI Nani anaemshuku ndio akamtaja mtuhumiwa Kwa sababu alipoondoka aliaga anaenda Kwa Mtuhumiwa kuchukua gari yake.
Ndipo polisi wakamshika Mtuhumiwa baada msago kidogo akakiri na kuwapeleka polisi alipofanya tukio



Huyo jamaa muuuaji alipewa pesa na marehemu sh 35 millions taslim,
Jamaa amuagizie gari toka nje.

Baada ya kimya kingi, marehemu akaanza kusumbuana Kwa simu kutaka pesa zake..

Siku moja muuaji akampigia simu marehemu aje afate chake pale kwake,

Kumbe muuaji alikuwa ameshaandaa shimo hapo nyumbani alipopanga,

Marehemu bila kujua akajipeleka mwenyewe nyumbani Kwa mdeni wake,
bila kujua kaandaliwa shimo la kuchomwa na kuzikwa humo.

Inasemekana marehemu aliuawa akiwa ndani ya nyumba na baadae akachomwa moto na akazikwa uani humo, huku akiwa amezungushiwa godoro mwili mzima na kuchomwa akiwa shimoni humo, na baadae muuaji alimfukia na kusakafia sakafu na cement Ili asigundulike Kwa urahisi.


Ilipita miezi kadhaa ndiyo muuaji akahama nyumba hiyo bila hata kumaliza Kodi yake,

--Siku moja mpangaji mpya aliyehamia ktk nyumba Ile akawa anapaki gari yake pale pale jamaa alipofukiwa.
Ndy akagunduwa kwamba eneo lile Kuna sehemu panatitia,

Jamaa akapata mashaka maana Ile sehemu ilikuwa imesakafiwa vizuri sana na ni eneo lote la uani,
Iweje pale tu pavunjike? Na kunaonekana Kuna dalili za shimo.

Jamaa akaamua kwenda kutoa riporti kwa Mjumbe na baadae polisi.

Jamaa walipokuja wakavunja lile eneo lililotitia na baadae wakakuta mabaki ya mwili ambao tayari ulikuwa umeshaharibika vibaya sana.

Kilichowashangaza zaidi ni kuona maiti Ile,
Ikiwa imeunguzwa na kuteketea kabisa lakini bado Kuna mabaki ya godoro mwilini mwake huku akiwa ameungua vibaya sana hata kushindwa kutambulika kabisa.

Ndiyo hapo mwenye nyumba akakumbuka kwamba yule mpangaji aliyopita alizungumzia mambo ya kuchimba shimo na kutapisha choo.

Lakini mbona hakuna dalili za kutapisha choo?

Ikabidi jamaa aitwe na mwenye nyumba, jamaa muuaji bila kutambua chochote aliitikia wito na kukamatwa on the scene.

Jamaa muuaji baada ya kutiwa mbaroni akafunguka tukio zima.

Ukweli ni kwamba muuaji ndiye aliyekuwa anadaiwa na marehemu..
 
Tatizo kuna watu wanadaigi kwa jazba kejeli na matusi tena hadharani. Sasa hii inapelekea kumpa nafasi shetani atawale nafsi na akili ya mdaiwa nakusababisha sintomfaham kupelekea kufanya mauaji bila kujijua.

Mnakumbuka kisa cha uriah aluvyokuwa anadai chake mke wake kwa Daudi? Alikomaa hadi akakataa kwenda nyumbani. Daudi alimaindi kichiz akaamua tu kumpoteza.

Dawa ya deni ni kulipa. Tusiwe wachoyo na tamaa zembe. Dhulma ni mbaya inasababisha mdaiwa kuwa na hasira za kijinga akidaiwa nakupelekea kuua nafsi isiyokuwa na hatia.

Saa zingine ukimdai mtu anakukwepa na kukudhulumu muachie Mungu tu. Jamaa angemuachia Mungu asingeuwawa.

Acha anyongwe tu.
Rudi tena ukasome biblia umechanganya habari
 
Kwa hiyo, marehemu aliuawa kwa sababu alidai chake?

Na kwamba hela aliyokuwa anadai marehemu ilinunulia nyumba Magomeni badala ya kununulia Fuso kama marehemu alivyokubaliana na mshtakiwa/muuaji?

Kwa hiyo Marehemu na Muuaji walikuwa wanaaminiana kiasi cha marehemu kumpa hela muuaji akamwagizie Fuso?

Hivyo basi, bwana muuaji aliingia tamaa na kumdhulumu marehemu pesa na roho yake?

Kikulacho ki nguoni mwako!
kesi kama hii iliwatoe kanda ya kati.

Na nyingine kama hii ipo kanda ya kati tenba, tofauti ni kuwa hawa bado hawajauana. Ila tayar washazuruminiana. Ni ndugu na jamaa wa karibu kabisaaaaaaaaaaaaaaaaa.


Dunia hii iman ime kwisha, ................................
 
Tatizo kuna watu wanadaigi kwa jazba kejeli na matusi tena hadharani. Sasa hii inapelekea kumpa nafasi shetani atawale nafsi na akili ya mdaiwa nakusababisha sintomfaham kupelekea kufanya mauaji bila kujijua.

Mnakumbuka kisa cha uriah aluvyokuwa anadai chake mke wake kwa Daudi? Alikomaa hadi akakataa kwenda nyumbani. Daudi alimaindi kichiz akaamua tu kumpoteza.

Dawa ya deni ni kulipa. Tusiwe wachoyo na tamaa zembe. Dhulma ni mbaya inasababisha mdaiwa kuwa na hasira za kijinga akidaiwa nakupelekea kuua nafsi isiyokuwa na hatia.

Saa zingine ukimdai mtu anakukwepa na kukudhulumu muachie Mungu tu. Jamaa angemuachia Mungu asingeuwawa.

Acha anyongwe tu.
Ndg kirahs hivyo unasurrender, hUyo alishakuwa na roho ya kuua na alishajipanga kumpiga. Si rahis kumvungia Mtu unayemdai Chako Hasa pesa nyingi kia's hicho
 
Mara nyingi mauaji yoyote huwa lazima yaache alama ama viashiria vya kuanzia upelelezi!

Ingawa kabla ya kutekeleza mauaji hayo, watu hujidanganya kuficha tukio, lakini hawawezi kuziba mianya yote jambo hilo lisiweze kujulikana milele!
Una elimu ya upelelezi. Nafurahi kule Marekani mafaili hayafungwi.Watu hukamatwa zaidi ya miaka 50 mbele.
 
mbona story yako haijaisha mkuu alikamtwa vipi? maana ni majirani zetu hao ilala

jamaa alihama kabisa ilala na kwenda magomeni,mwenye nyumba akampata mpangaji mwengine ambae ni sharifu aliyekuwa anatibu watu kwa Quran.

sharifu alikuwa kila akilala usiku kuna nafsi inalalamika full maluwe luwe navhasa akienda au kupita hapi alpozikwa marehemu.

Basi ilifanyika dua na kugundua kuwa kuna kitu kibaya kimezikwa sehemu hyo,ndipo alipoitwa mwenye nyumba,baada ya kuja naye akakubali wafukue lakini mjumbe na mwenye kiti awepo na mwenyekiti nae akasema si vibaya wakawepo wale polisi wanaokaaga kata.

kwenye kuchimba ndo wakakutana na mwili wa huyo marehemu mwenye nyumba kubwanwa hana ajuacho mpangaji aliyetoka alipobanwa kidogo tu akafunguka yote.

ni kesi ya muda mrefu nimeshangaa mtu kuhukumiwa leo wakat ushahid ulikuwa waz kabisa
Hasa hivi ndivyo ilivyokuwa maana hata Clouds kipindi cha Gea waliifatilia sana hii habari.
 
Back
Top Bottom