Mfanyabiashara: Kiburi cha TRA kinasababishwa na Bosi wao Mwingulu Nchemba

Mwigulu kama ataendelea kubaki waziri kweli nitathibitisha kuna watu wana roho pea mbili

..anayetoza kodi ni Rais Ssh.

..anayeteua Kamishna Mkuu wa Tra ni Rais Ssh.

..kwanini mnakwepa kuelekeza lawama kunakohusika?
 
Wafanyabiasha Wanasema matatizo yote ni Kwa Sababu viwango vya Kodi vilivyowekwa na serikali hii Chini ya Mwigulu havitekelezeki.
 
We unafikiri hii changamoto haikuwepo kipindi cha Magufuli?

Utofauti unaofanya uone haikuwepo ni kwamba kile kipindi isingewezekana kufanya mgomo kutokana na udikteta wa Magufuli
Inakuaje sasa katika awamu ya kufanya biashara kwa uhuru na uwazi bila bughudha na mama hapendi kodi za dhuruma
Inakuwaje kutokee haya?
 
Usikariri
 
Ni jambo jema sana tena mno!

Nafuatilia mubashara TBC kiukweli angekuwepo Shujaa Magufuli kwa haya maelezo ya Wafanyabiashara Waziri angeliwa kichwa fasta!
Usiwe mwepesi kiasi hicho kichwani.

Lawama hizi siyo za mtu mmoja, Waziri, ingawaje naye ni mchangiaji wa matatizo.

Hao waliosema mambo hapo, wamesema yanayohusu upande wao, hujasikia chochote toka upande wa pili. Ingefaa na wao wakasema kitu tukawasikia.

Wafanya biashara mahali popote duniani hakuna wanaopenda kulipa kodi stahiki. Kukiwa na mwanya, ni lazima watautumia tu kutolipa kodi.

Lawama inaiangukia serikali, inayoshindwa kuweka mfumo unaozuia haya wanayolalamikia wafanya biashara.

Na kwa serikali mbovu kama hii iliyopo sasa, matatizo haya ndiyo yanazidi kuonekana wazi zaidi.
 
Kodi ipi ya hovyo iliyowekwa? Kodi za hovyo alianzisha Magufuli. Kama hujui uliza. Yule Shetani bora alivyokufa maana hata uhuru huo wa wafanyabiashara haukuwepo.
Unapata tabu sana dogo awamu ya mama inapopolewa
 
Ukifanya biashara na ukawa na EFD, tena VAT registered utaelewa
Kwani nchi zingine hakuna mamlaka za mapato? Kwa nini shida ni Tanzania tu?

EFD kila siku unafunga hesabu, na kama una kampuni unalipa return kila mwezi au unajaza nil, tatizo liko wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…