Mfumo wa masaa Afrika Mashariki

Mfumo wa masaa Afrika Mashariki

Chambusiso

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2007
Posts
2,592
Reaction score
4,640
Sijui kama ilishawahi kujadiliwa humu lakini nimekuwa najiuliza sana na kukosa majibu, kwanini mfumo wa masaa wa Afrika Mashariki upo tofauti na sehemu zingine duniani? Sehemu zote siku inaanza saa 6 (0000) usiku lakini kwetu inaanza saa 1 (0700) asubuhi. Kuna sababu ya hii tofauti mahali?

Na tulipatia wapi huu mfumo na kwa nini? Tujiulize wanabodi na tunafaidika nini au tunapata hasara gani kwa hii? Karibuni kwa tafakuri.
 
Hii umeitoa wapi?

Umetumia kigezo gani kufikia hili hitimisho?
-

Sio hitimisho ni swali, toa uelewa wako kiongozi! Dunia ina mambo mengi sana hamna mjuvi wa kila kitu. Asubuhi sisi tunasema ni saa moja wenzetu wanasema ni Seven lakini pia saa zetu zinasoma 7 sio 1
 
Utaratibu wa kujua majira na msimu kwa waafrika ulitegemea mawio na machweo ya jua kwa mchana kwa kuangalia jua lilipo na kivuli, wakati usiku nyota na mkusanyiko wake uliweza kuruhusu ukadiriaji nyakati.

Hiyo ni moja ya urithi wa tamaduni zetu pekee zilizobakia na zimebaki kwa baadhi tu ya makabila kama wamasai au vijijini ndani ndani. Ni mfumo uliokuwepo ambao haukuboreshwa na kukumbatia usasa.
 
Kwakuwa sisi ni special sana?

Mfumo ni ule ule sema tunaandika masaa kwa kuzingatia swahili kama tuavyoyatamka, kwa kuzingatia mawio na machweo ya jua

Saa la kwanza la asubuhi - saa 1 asubuhi

Saa la kwanza la usiku - saa 1 usiku

Tarehe bado inabadilika saa 6 usiku kama mfumo ulivyo
 
Kwakuwa sisi ni special sana?

Mfumo ni ule ule sema tunaandika masaa kwa kuzingatia swahili kama tuavyoyatamka, kwa kuzingatia mawio na machweo ya jua

Saa la kwanza la asubuhi - saa 1 asubuhi

Saa la kwanza la usiku - saa 1 usiku

Tarehe bado inabadilika saa 6 usiku kama mfumo ulivyo

Ndio najiuliza mimi ngumbaru, nikaona nishirikishe na wajuzi wa mambo hapa jamvini! Kwa nini hiyo saa 7 tusingeita saa 1 tu kama ndio siku inaanzia? Bado ingekuwa kiswahili tu pia
 
Ndio najiuliza mimi ngumbaru, nikaona nishirikishe na wajuzi wa mambo hapa jamvini! Kwa nini hiyo saa 7 tusingeita saa 1 tu kama ndio siku inaanzia? Bado ingekuwa kiswahili tu pia
Wao wanatumia am pm
Sisi tunatumia alfajiri/adhuhuri asubuhi mchana jioni/alasiri usiku

Hiyo saa 7 usiku ingekuwa saa 1 which ili ileleweke? Lengo ni kueleweka. Utasema iwe saa 1 nini?
 
Wao wanatumia am pm
Sisi tunatumia alfajiri/adhuhuri asubuhi mchana jioni/alasiri usiku

Hiyo saa 7 usiku ingekuwa saa 1 which ili ileleweke? Lengo ni kueleweka. Utasema iwe saa 1 nini?

Yes ndio kwa nini sisi tuna alfajiri/adhuhuri asubuhi mchana jioni/alasiri usiku wakati dunia ina AM na PM tu? Ndio nachotaka kujifunza au kupata uelewa! Sisi ni special au tuna sababu zingine?
 
Back
Top Bottom