Mgogoro wa KKKT Konde: Tatizo ni hela iliyoliwa na kundi la Askofu

Mgogoro wa KKKT Konde: Tatizo ni hela iliyoliwa na kundi la Askofu

Imebidi niingie chimbo kuchunguza mgogoro huu wa Dayosisi ya Konde.

Wazungu wanasema penye mgogoro usiotaka kuisha- FOLLOW THE MONEY!

Kiti cha Askofu kimeshindwa kurudishwa Tukuyu maana ofisi ya Tukuyu ilimokuwa Dayosisi imeuzwa au kupangishwa kwa milioni 200.

Ofisi wameuziwa au kupangishwa CRDB.

Hela hizo zimeliwa na wajanja ambao wamesepa kuenda Mbeya.

Sasa changamoto kiti kitarudi wapi!

Wanaotetea hadi macho kuwatoka ni wafaidika wa hela hizo, na hii ni fraud case.

Nawasilisha

Chanzo: nzi wa Tukuyu
Takukuru mmelala. Sisi Wangonde tumeibiwa sadaka zetu
 
Ultimately Askifu anabeba lawama zite, kama ilivyo sasa.
Huko Konde wale wachungaji ambao wanaonekana wamefaidika, wanatetea hali ya kuhamia Mbeya hadi mishipa inawatoka kichwani.

Na wanajua fika, uchunguzi ukifanyika watabeba lawama pamija na Askofu.
Kwenye pesa ni Mtunza hazina na Katibu Mkuu.hao wachungaji ni chawa wakumsujudu Mwaikali.
Tukio limekaa kipagani sana.
Kiti cha Uaskofu kinakaa kanisa kuu.
Uaskofu anao yeye,sasa alihama kimwili lakini kimamlaka kaacha Cathedral.
 
Tukuyu upangishe kwa mil 200? Impossible, labda useme imeuzwa.
Hajataja muda mkuu, vipi ikiwa ni kwa miaka 100?? Na je jengo lenyewe unalijua??

Jengo liko mahali pazuri kabisa kibiashara na pia ni kubwa, ulinzi upo kwani limezungukwa na halmashauri kwa nyuma, pembeni kuna benki ya nbc.
Usibishe bila sababu kijana.
 
Hajataja muda mkuu, vipi ikiwa ni kwa miaka 100?? Na je jengo lenyewe unalijua??

Jengo liko mahali pazuri kabisa kibiashara na pia ni kubwa, ulinzi upo kwani limezungukwa na halmashauri kwa nyuma, pembeni kuna benki ya nbc.
Usibishe bila sababu kijana.
Hao wapangaji ni taasisi na mpangishaji ni taasisi hivyo hapo Mwaikali mtamuonea.Malipo hayafanyiki kirafiki
 
Hao wapangaji ni taasisi na mpangishaji ni taasisi hivyo hapo Mwaikali mtamuonea.Malipo hayafanyiki kirafiki
Tatizo hela imeota mabawa.
Na ni ukosefu wa busara kwa zoezi zima lilivyofanyika.

Sasa wanatakiwa warudi Tukuyu, mafsili wataweka chini ya miparachichi?
 
Tatizo hela imeota mabawa.
Na ni ukosefu wa busara kwa zoezi zima lilivyofanyika.

Sasa wanatakiwa warudi Tukuyu, mafsili wataweka chini ya miparachichi?
Uzuri kiti cha Uaskofu hawakukipangisha,muda wowote anaweza kukalia mtu mambo yakithibitika yalikiukwa.
 
Uzuri kiti cha Uaskofu hawakukipangisha,muda wowote anaweza kukalia mtu mambo yakithibitika yalikiukwa.
Urudishwaji wa kiti unabeba tuhuma nzito dhidi ya kundi lake Askofu.
Tumesikia ya CRDB, yapo na mengine.
 
Urudishwaji wa kiti unabeba tuhuma nzito dhidi ya kundi lake Askofu.
Tumesikia ya CRDB, yapo na mengine.
Mkuu wa kanisa anataarifa zote.
Maaskofu waliotumwa kabla yake nakuwahoji wachungaji na wakristo ndio waliomaliza mchezo.
Hapo ni HATUNA IMANI NAYE.
Kaa pembeni achunguzwe huku Dayosisi ikiwa chini ya uangalizi wa mtu mwingine.
Busara tu zimtume Mwaikali ajiuzuru.
Huo mwendo wa Mkuu wa kanisa kumshauri kirudishe kiti ulikosimikwa amemstahi.
Alikaidi kwa wakristo
Je atakaidi mamlaka ya makao makuu kisheria?
 
KKKT ya enzi za Kibira, Kolowa, Sendoro, Uhahula and the like haitakuja kutokea tena, hawa walimwogopa Mungu na kutambua uwepo wake kwa dhati, hakuna wa kuwafananisha nao hivi sasa.
Sidhani kama ni sahihi kusema hivyo Mungu anao watu wengi bado
 
Mkuu wa kanisa anataarifa zote.
Maaskofu waliotumwa kabla yake nakuwahoji wachungaji na wakristo ndio waliomaliza mchezo.
Hapo ni HATUNA IMANI NAYE.
Kaa pembeni achunguzwe huku Dayosisi ikiwa chini ya uangalizi wa mtu mwingine.
Busara tu zimtume Mwaikali ajiuzuru.
Huo mwendo wa Mkuu wa kanisa kumshauri kirudishe kiti ulikosimikwa amemstahi.
Alikaidi kwa wakristo
Je atakaidi mamlaka ya makao makuu kisheria?
Ni kweli Askofu Shoo alimstahi tu, huyu Askofu wetu Mwaikali.
Kimsingi Askofu hatakiwi kuwa mtu anayebebeshwa lawama za kukosa uaminifu, hasa sadaka za waumini.
Zitamdhuru.
 
Sidhani kama ni sahihi kusema hivyo Mungu anao watu wengi bado
Wameshakuwa suppressed hawawezi kiibuka ni kama leo tuongelee Tanzania kumpata Julius K. Nyerere
 
Wa proestanti rudini kanisa katoliki mkapige magoti kwa papa awape mwongozo kwa kuchagua vingozi na kuedesha kanisa. Uongozi wa kanisa ukichaguliwa kwa kampeni na kura kama viongozi wa siasa kamwe migogoro haiwezinkuisha.ROMA LUCUTA CAUSA FINITA
Hata Papa mwenyewe huchaguliwa kwa kura za makadinali. Kura ndio njia rahisi na sahihi zaidi kwenye kuamua jambo ambalo linashindaniwa na pande tofauti tofauti.
 
Huyo askofu mwaikali ndio chanzo kikuu Cha mgogoro huu ingekuwa busara Kama angejiuzuru kuliiko kung'ang'amiahicho cheo
 
O
Huyo askofu mwaikali ndio chanzo kikuu Cha mgogoro huu ingekuwa busara Kama angejiuzuru kuliiko kung'ang'amiahicho cheo
Kuna hotuba Fulani aliitoa Prof Mwandosya mwanzoni kwa mgogolo.Nadhani nimda mwafaka Mwaikali ashauriwe kuachia kiti kulinda heshima.
Sababu ni hizi
1.Akiwa mradi LCCB aliboronga.
2.Akiwa msaidizi aliboronga.Hadi akaishi uhamishoni.
3.Amekuwa Askofu,anatuhumiwa na baadhi ya tuhuma zimethibitika.
4.Amefukuza wachungaji zaidi ya 20
5.Amefukuzwa kanisani na wakristo hadi kuokolewa na Polisi.

Kwa kifupi ni mbabe na anapenda kuabudiwa.
Wazee wa Tukuyu mmshauri apishe kama ambavyo mlimsihi arudi alipokuwa uhamishoni.
Mwaikali,yakumbuke machozi yako siku ya kusimikwa kuwa Askofu.
 
Wa proestanti rudini kanisa katoliki mkapige magoti kwa papa awape mwongozo kwa kuchagua vingozi na kuedesha kanisa. Uongozi wa kanisa ukichaguliwa kwa kampeni na kura kama viongozi wa siasa kamwe migogoro haiwezinkuisha.ROMA LUCUTA CAUSA FINITA
Huwa wanachagua kwa kuinua vidole au kupanga foleni na kampeni huwa zinagubikwa rushwa na wengine kutandikana mikwaju na bakora kama inavyokuwa kwenye kura za maoni za baadhi ya wanasiasa!
 
Hivi Askofu Mwaikali anaweza kuiba hela kweli, nafikiraaaaa, narudia tena nawazaaaaa,
sipati jibu
Anaeweza kuiba kwa sababu na yeye ni binadamu anayependa hela kama binadamu mwingine yeyote! SIYO MALAIKA.
 
Anaeweza kuiba kwa sababu na yeye ni binadamu anayependa hela kama binadamu mwingine yeyote! SIYO MALAIKA.
Mwaikali peke yake hawezi kuiba hata kidogo.
Hata umshitaki humpati kwenye nyaraka.
Yeye hapokei wala kutoa hela.
Hapo wakubanwa ni
Katibu mkuu
Mhasibu
Cashier.
Kamati ya fedha
 
Huwa wanachagua kwa kuinua vidole au kupanga foleni na kampeni huwa zinagubikwa rushwa na wengine kutandikana mikwaju na bakora kama inavyokuwa kwenye kura za maoni za baadhi ya wanasiasa!
Ni hakika huo ni utatatibu mbaya na dini zote sio makanisa tu yenye mfumo huo wa uchaguzi migogoro ya madaraka huwa haiishi. Kwani zinakuwepo kambi za kampeni na wapambe kama kwenye siasa na mtu wao akikosa basi ni hujuma meanzo mwisho hawakubaliani na matokeo maana wanajua tenda na miradi ya kanisa wataikosa
 
Back
Top Bottom