Mgogoro wa KKKT Konde: Tatizo ni hela iliyoliwa na kundi la Askofu

Mgogoro wa KKKT Konde: Tatizo ni hela iliyoliwa na kundi la Askofu

Mwaikali peke yake hawezi kuiba hata kidogo.
Hata umshitaki humpati kwenye nyaraka.
Yeye hapokei wala kutoa hela.
Hapo wakubanwa ni
Katibu mkuu
Mhasibu
Cashier.
Kamati ya fedha

Hata yeye anatakiwa kufurushwa mara moja ndipo mambo yatarudi kuwa dhwari!
 
KKKT ya enzi za Kibira, Kolowa, Sendoro, Uhahula and the like haitakuja kutokea tena, hawa walimwogopa Mungu na kutambua uwepo wake kwa dhati, hakuna wa kuwafananisha nao hivi sasa.
Sure hawa wa sasa hivi ukitokea uchaguzi wa askofu wanavyobagazana utafikiri ndugai
 
Wameshakuwa suppressed hawawezi kiibuka ni kama leo tuongelee Tanzania kumpata Julius K. Nyerere
Kwa Mungu haipo hivyo kamwe haishiwi watu muulize Eliya Mtshibi atakueleza.
 
O

Kuna hotuba Fulani aliitoa Prof Mwandosya mwanzoni kwa mgogolo.Nadhani nimda mwafaka Mwaikali ashauriwe kuachia kiti kulinda heshima.
Sababu ni hizi
1.Akiwa mradi LCCB aliboronga.
2.Akiwa msaidizi aliboronga.Hadi akaishi uhamishoni.
3.Amekuwa Askofu,anatuhumiwa na baadhi ya tuhuma zimethibitika.
4.Amefukuza wachungaji zaidi ya 20
5.Amefukuzwa kanisani na wakristo hadi kuokolewa na Polisi.

Kwa kifupi ni mbabe na anapenda kuabudiwa.
Wazee wa Tukuyu mmshauri apishe kama ambavyo mlimsihi arudi alipokuwa uhamishoni.
Mwaikali,yakumbuke machozi yako siku ya kusimikwa kuwa Askofu.
Kwa kifupi Askofu Mwaikali amelifedhehesha Kanisa.
Busara imjie na ajiuzulu tu.
 
Wanashinda kwa waganga
Kama ni kweli basi wala hawakulijua Neno toka zamani.
Na hakuna adhabu kali kutoka kwa Mungu kwa yule anayeabudu miungu mingine.
Kwa hili, tusubiri tu, muda si mrefu wataanza kuanguka mmoja baada ya mwingine.
 
Moja kati ya Diocese ambazo wana miradi mingi ya kuingiza pesa ni hii ya KONDE
 
Inasikitisha sana...
Tena aibu kubwa Bwana Mungu atuhurumie tuishi katika Neno.

Neno lasema hivi:

1 Tim 3:1-10 SUV

"Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?) Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi. Vivyo hivyo mashemasi8 na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu; wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia"
 
Mch. Mwakihaba ndiye Askofu Mteule wa Dayosisi ya Konde baada ya Uchaguzi uliofanyika Leo 22.03.2022.

Tumombee Hekima ya Ki-Mungu ya kutengeneza pale palipo bomoka.
 
Mch. Mwakihaba ndiye Askofu Mteule wa Dayosisi ya Konde baada ya Uchaguzi uliofanyika Leo 22.03.2022.

Tumombee Hekima ya Ki-Mungu ya kutengeneza pale palipo bomoka.
Aliekuwepo amestqafu?
 
KKKT yote tu inasumbuliwa sana na money related conflicts
 
Siku hizi KKKT imevamiwa na watu wenye tabia za kinabii na mitume.

Muda wote na mahali popote wao wanachungulia jinsi ya kuvuta hela kutoka kwa kondoo.
Hata sauti zao wakati wa kuhubiri wameanza kuiga mitume na manabii..kupayuka na kukoroma.

Hili kanisa linahitaji tena 'reformation', laa sivyo litakufa.
Madhehebu na Makanisa karbia yote tuu upigaji wa Pesa za Bwana imekuwa changamoto kubwa Sana ...!! Watu wapo after money
 
Mch. Mwakihaba ndiye Askofu Mteule wa Dayosisi ya Konde baada ya Uchaguzi uliofanyika Leo 22.03.2022.

Tumombee Hekima ya Ki-Mungu ya kutengeneza pale palipo bomoka.
Mwaikali amepata kura ngapi? Huyu kiti atakirudisha tukuyu?
 
Nani alikuambia Papa huwa anachagua viongozi.Dunia nzima anawajua yeye amekuwa malaika?
Mbona husemi wale walioshitakiwa kwa kulawiti watoto na Papa akakili
We ulishasikia uchaguzi wa askofu rc?Papa ndo huteua askofu kwa Jimbo lolote duniani
 
Tena aibu kubwa Bwana Mungu atuhurumie tuishi katika Neno.

Neno lasema hivi:

1 Tim 3:1-10 SUV

"Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?) Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi. Vivyo hivyo mashemasi8 na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu; wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia"
Umequote biblia gan mkuu...
 
Back
Top Bottom