Uchaguzi 2020 Mgombea kupitia CHADEMA, Tundu Lissu achukua fomu za Kugombea Urais wa Tanzania ofisi za NEC Dodoma

Mkipata mbunge hata mmoja, mutakua mumejitahidi sana. Mhe rais Magufuli ameahidi uchaguzi kua huru na haki ili mkose kichaka cha kufichia aibu itakayowapata.
Kuahidi kwa maneno ndio vitendo? Basi akubali kura zihesabiwe kama za watia nia wa ubunge na udiwan wa ccm. Zihesabiwe kituoni na ziende kata kwa mtazamo huo huo uone
 
Cha ajabu na uchaguzi huu kitapita Kwa kishindo ambacho Hatujawahi kutokea tangu uwepo wa vyama vingi, sijui wanatumia dawa wale, au nadhani washindani Wao huwa hawatahamiki Kwa wananchi, au huwa hawana sifa
Mwaka huu CCM hawashindi. Tutafanya kampeni ya kufa na kupona kuwaelimisha wananchi kuwa CCM haifai na tutawaeleza vizuri wachague Chama sahihi na chenye Sera sahihi na watu sahihi Chadema ili waweze pata maendeleo ya kweli.
 
Kiwanda mpaka kijengwe chumbani mwako ndiyo uamini kwamba kuna viwanda vimejengwa?
 
Huyo ni yule binti aliye mshitaki Lowasa kwa Makonda kuwa alizaliwa nje ya ndoa na lowasa.

Unakumbuka kipindi kile Lowasa bado yupo cdm?
Hii Lowassa ni ukoo, binti wa yule mzee au mchepuko?
Maana sijajua kwa nini nikiona hili jina namkumbuka sana Mwenyekiti wenu wa ccm Geita bwana Msukuma kisha nasikia kichefuchefu napoteza hamu ya kula!
 
Kwa ufupi hakuna chombo chochote cha habari kinachoripoti live!!! kulikoni hata hizo youtube channels zilizojaribu kurusha pia sio nzuri na hazionyeshi inavyotakiwa. zina noise nyingi!
 
Choo tu cha soko hadi Rais atoe tamko la kujengwa kwake,bado unaamini kuwa hawa watu watalikomboa Taifa hili dhidi ya Ujinga,Maradhi na Umaskini wa Watanzania?Ni aibu kuendelea kuongozwa na CCM katika karne ya 21.
Dunia inaenda mbele kwa kasi huku sisi tukirudishwa tulikotoka kwa kasi ile ile ambayo wenzetu wanasongea nayo mbele kimaendeleo kwa sababu ya hawa Migomba.Tubadilike ili tunusurike kwa kuwachagua viongozi wa watu siyo vitu maana vitu vinatengenezwa/kuundwa na watu na hivyo watu kwanza.
CCM haikubaliki.
 
Ni aibu ndugu yangu. Nchi hii chini ya CCM imekuwa aibu. Nasema hili kwa uhakika wa asilimia 100 , hakuna maendeleo thabiti na bora nchi hii na wananchi wake watapata chini ya CCM. Kamwe!!!!
 
Kuahidi kwa maneno ndio vitendo? Basi akubali kura zihesabiwe kama za watia nia wa ubunge na udiwan wa ccm. Zihesabiwe kituoni na ziende kata kwa mtazamo huo huo uone
Kwani kura zinahesabiwa mafichoni?. Huko kwenye vituo vya kupigia kura hamuna mawakala wenu muliowachagua wenyewe?. Nawapenda sana chademai ila tatizo lenu wengi sio wazalendo. Lissu alisema hali ya corona tz ni mbaya sana lakini leo karundikana na kikundi kidogo cha watu bila kuchukua tahadhari yoyote.
 
Hata sisi mnatushangaza sana. Magu alisema anataka kuifanya TZ iwe kama ulaya lkn miaka 5 ameshindwa kuifanya iwe kama Rwanda tuu.

Alisema hatanhuko ulaya kuna sehe ziko TZ tuu hawana kila kitu sasa je ni ulaya gani.iyo anayotufananishia?
 
Kwa ufupi hakuna chombo chochote cha habari kinachoripoti live!!! kulikoni hata hizo youtube channels zilizojaribu kurusha pia sio nzuri na hazionyeshi inavyotakiwa. zina noise nyingi!
Unataka kurushwa bure? Media Sio charity organization!! Watu wanalipia leseni na TRA wewe unataka free ride?
 
Wewe umesomea taaluma gani kwanza? Kwa maelezo yako unazungumza porojo. Wapi duniani ambako serikali ndio inalisha watu? Yaani wewe ukae serikali ikujengee, ikusomeshee watoto, ikutibie. Endelea kujidanganya nyuma ya key board huku wenzio tukihangaika kuniletea maendeleo.
Jukumu la serikali ni kuweka sera, sheria, kusimamia amani , usalama , kukusanya kodi na kutumia kwa huduma zinazochichea ukuaji wa kiuchumi.
Tafuta mtu aliyesomea uchumi akuelezee abc za uchumi ili usikalie ndoto za alinacha. Mwananchi analo jukumu la kufanya ili aweze kuwa na maisha bora na sio kuwa serikali ndio itamletea maisha bora.
Jiulize unatoa mchango gani katika maendeleo ya nchi.
 
Aisee nieamini makamanda wa hapa JF ni bendera fuata upepo, hakuna hata mmoja mwanachama halisi wa Chadema, pereree tu

Mpaka sasa jamaa ameshachukua fomu hakuna hata picha moja

Chadema ni mitandaoni tu, tena kwa watu wachache wenye ID's nyingi
 
Aisee nieamini makamanda wa hapa JF ni bendera fuata upepo, hakuna hata mmoja mwanachama halisi wa Chadema, pereree tu

Mpaka sasa jamaa ameshachukua fomu hakuna hata picha moja

Chadema ni mitandaoni tu, tena kwa watu wachache wenye ID's nyingi
Haya tema mate tumchape[emoji871]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…