Uchaguzi 2020 Mgombea kupitia CHADEMA, Tundu Lissu achukua fomu za Kugombea Urais wa Tanzania ofisi za NEC Dodoma

Uchaguzi 2020 Mgombea kupitia CHADEMA, Tundu Lissu achukua fomu za Kugombea Urais wa Tanzania ofisi za NEC Dodoma

Mkipata mbunge hata mmoja, mutakua mumejitahidi sana. Mhe rais Magufuli ameahidi uchaguzi kua huru na haki ili mkose kichaka cha kufichia aibu itakayowapata.
Kuahidi kwa maneno ndio vitendo? Basi akubali kura zihesabiwe kama za watia nia wa ubunge na udiwan wa ccm. Zihesabiwe kituoni na ziende kata kwa mtazamo huo huo uone
 
Cha ajabu na uchaguzi huu kitapita Kwa kishindo ambacho Hatujawahi kutokea tangu uwepo wa vyama vingi, sijui wanatumia dawa wale, au nadhani washindani Wao huwa hawatahamiki Kwa wananchi, au huwa hawana sifa
Mwaka huu CCM hawashindi. Tutafanya kampeni ya kufa na kupona kuwaelimisha wananchi kuwa CCM haifai na tutawaeleza vizuri wachague Chama sahihi na chenye Sera sahihi na watu sahihi Chadema ili waweze pata maendeleo ya kweli.
 
Watake wasitake ila kwa mujibu wa wananchi wa Tanzania wesha amua kuwa ni... YEYE...
Ni Yeye 2020
photo%20266%2012-18-0.jpeg
 
Hivi kuna mtu mwenye akili timamu atampigia kura mgombea wa CCM?

CCM inawadanganya Watanzania kuwa ndani ya miaka 4-5 wamejenga viwanda 8477 , viwanda vingi kuliko vile vya Japan vilivyojengwa kwa miaka 100. Very stupid.
Ajira za kwenye miradi mikubwa tu ni zaidi ya milioni 6.

Utawapaje kura watu waongo, wanafiki na wazandiki kiasi hiki.

Ajira zingekuwa nyingi hivi nisingeona classmates wangu wengi wakilishwa na mama zao.
Kiwanda mpaka kijengwe chumbani mwako ndiyo uamini kwamba kuna viwanda vimejengwa?
 
Huyo ni yule binti aliye mshitaki Lowasa kwa Makonda kuwa alizaliwa nje ya ndoa na lowasa.

Unakumbuka kipindi kile Lowasa bado yupo cdm?
Hii Lowassa ni ukoo, binti wa yule mzee au mchepuko?
Maana sijajua kwa nini nikiona hili jina namkumbuka sana Mwenyekiti wenu wa ccm Geita bwana Msukuma kisha nasikia kichefuchefu napoteza hamu ya kula!
 
Kutoka maeneo mbalimbali kwenye viunga vya mji wa Dodoma, Tundu Lissu leo anachukua Fomu ya Urais
View attachment 1530697
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA Tundu Lissu akiwa amewasili katika Ofisi za Chadema Kanda ya Kati zilizopo jijini Dodoma na kupokelewa na viongozi mbalinbali wa Chama, wanachama, wapenzi na mashabiki wa Chadema, kabla ya kuelekea Ofisi za Tume ya Uchaguzi kuchukua fomu, leo Jumamosi 08/08/2020
Kwa ufupi hakuna chombo chochote cha habari kinachoripoti live!!! kulikoni hata hizo youtube channels zilizojaribu kurusha pia sio nzuri na hazionyeshi inavyotakiwa. zina noise nyingi!
 
Ni shida ndugu yangu. Chini ya CCM hakuna tuliloweza kuliendesha kwa ufanisi. Kupanga makazi yetu tu na miji yetu imekuwa shida kila sehemu mitaa ya hovyo na uchafu tu. Chama kilichoshindwa hata kusimamia tu watu wajenge kwa ustaarabu na miji yetu na makazi yetu yapendeze leo hii wanasema eti wao tu ndo wanaweza kuongoza hii nchi. Ni aibu sana.

Nimejifunza kitu kuwa nikiona mtu anashabikia CCM basi uwa ninatia mashaka sana uelewa wake wa mambo
Choo tu cha soko hadi Rais atoe tamko la kujengwa kwake,bado unaamini kuwa hawa watu watalikomboa Taifa hili dhidi ya Ujinga,Maradhi na Umaskini wa Watanzania?Ni aibu kuendelea kuongozwa na CCM katika karne ya 21.
Dunia inaenda mbele kwa kasi huku sisi tukirudishwa tulikotoka kwa kasi ile ile ambayo wenzetu wanasongea nayo mbele kimaendeleo kwa sababu ya hawa Migomba.Tubadilike ili tunusurike kwa kuwachagua viongozi wa watu siyo vitu maana vitu vinatengenezwa/kuundwa na watu na hivyo watu kwanza.
CCM haikubaliki.
 
Choo tu cha soko hadi Rais atoe tamko la kujengwa kwake,bado unaamini kuwa hawa watu watalikomboa Taifa hili dhidi ya Ujinga,Maradhi na Umaskini wa Watanzania?Ni aibu kuendelea kuongozwa na CCM katika karne ya 21.
Dunia inaenda mbele kwa kasi huku sisi tukirudishwa tulikotoka kwa kasi ile ile ambayo wenzetu wanasongea nayo mbele kimaendeleo kwa sababu ya hawa Migomba.Tubadilike ili tunusurike kwa kuwachagua viongozi wa watu siyo vitu maana vitu vinatengenezwa/kuundwa na watu na hivyo watu kwanza.
CCM haikubaliki.
Ni aibu ndugu yangu. Nchi hii chini ya CCM imekuwa aibu. Nasema hili kwa uhakika wa asilimia 100 , hakuna maendeleo thabiti na bora nchi hii na wananchi wake watapata chini ya CCM. Kamwe!!!!
 
Kuahidi kwa maneno ndio vitendo? Basi akubali kura zihesabiwe kama za watia nia wa ubunge na udiwan wa ccm. Zihesabiwe kituoni na ziende kata kwa mtazamo huo huo uone
Kwani kura zinahesabiwa mafichoni?. Huko kwenye vituo vya kupigia kura hamuna mawakala wenu muliowachagua wenyewe?. Nawapenda sana chademai ila tatizo lenu wengi sio wazalendo. Lissu alisema hali ya corona tz ni mbaya sana lakini leo karundikana na kikundi kidogo cha watu bila kuchukua tahadhari yoyote.
 
Kwani kura zinahesabiwa mafichoni?. Huko kwenye vituo vya kupigia kura hamuna mawakala wenu muliowachagua wenyewe?. Nawapenda sana chademai ila tatizo lenu wengi sio wazalendo. Lissu alisema hali ya corona tz ni mbaya sana lakini leo karundikana na kikundi kidogo cha watu bila kuchukua tahadhari yoyote.
Hata sisi mnatushangaza sana. Magu alisema anataka kuifanya TZ iwe kama ulaya lkn miaka 5 ameshindwa kuifanya iwe kama Rwanda tuu.

Alisema hatanhuko ulaya kuna sehe ziko TZ tuu hawana kila kitu sasa je ni ulaya gani.iyo anayotufananishia?
 
Kwa ufupi hakuna chombo chochote cha habari kinachoripoti live!!! kulikoni hata hizo youtube channels zilizojaribu kurusha pia sio nzuri na hazionyeshi inavyotakiwa. zina noise nyingi!
Unataka kurushwa bure? Media Sio charity organization!! Watu wanalipia leseni na TRA wewe unataka free ride?
 
Sijaelewa swali lako. Unamaanisha kuvunjiwa nyumba au kukosa makazi ili eneo lipangwe???

Kama ni kuvunjiwa nyumba ndio, Nipo tayari.

Kama kukosa makazi hapo ndo sipo tayari!! Ninamaanisha nini kusema hivi???
Katika kutengeneza mipango miji na makazi bora, hili jambo linaweza kufanywa kwa hatua na likafanikiwa hakika!!! Litafanikiwaje???

Kama nchi tuna maeneo ambayo hayajaendelezwa, tunaweza kusema tunajenga nyumba za wakazi 5000- 10000 kwenye eneo ambalo likizo wazi tuliloamua kuliendeleza na tukishamaliza tunawahamishia Mf. Wakazi wa tandale kwenye eneo hilo. Tukiwahamishia tunachofanya sasa ni kupabomoa pale tandakte tulippwatoa watu na kupajenga kisasa. Tukimaliza kupajenga hapo tunawahamishia wengine ambao tutaenda kupabomoa kwao ili kupajenga na kupapanga vizuri.

Tatizo CCM mmeishiwa watu wenye akili mmeishia kuwa na watu wasio na akili wanaowaza matumbo yao.
Haya mambo ni CHADEMA tu wanaweza kuyafanya kwa ufanisi
Wewe umesomea taaluma gani kwanza? Kwa maelezo yako unazungumza porojo. Wapi duniani ambako serikali ndio inalisha watu? Yaani wewe ukae serikali ikujengee, ikusomeshee watoto, ikutibie. Endelea kujidanganya nyuma ya key board huku wenzio tukihangaika kuniletea maendeleo.
Jukumu la serikali ni kuweka sera, sheria, kusimamia amani , usalama , kukusanya kodi na kutumia kwa huduma zinazochichea ukuaji wa kiuchumi.
Tafuta mtu aliyesomea uchumi akuelezee abc za uchumi ili usikalie ndoto za alinacha. Mwananchi analo jukumu la kufanya ili aweze kuwa na maisha bora na sio kuwa serikali ndio itamletea maisha bora.
Jiulize unatoa mchango gani katika maendeleo ya nchi.
 
Aisee nieamini makamanda wa hapa JF ni bendera fuata upepo, hakuna hata mmoja mwanachama halisi wa Chadema, pereree tu

Mpaka sasa jamaa ameshachukua fomu hakuna hata picha moja

Chadema ni mitandaoni tu, tena kwa watu wachache wenye ID's nyingi
 
Aisee nieamini makamanda wa hapa JF ni bendera fuata upepo, hakuna hata mmoja mwanachama halisi wa Chadema, pereree tu

Mpaka sasa jamaa ameshachukua fomu hakuna hata picha moja

Chadema ni mitandaoni tu, tena kwa watu wachache wenye ID's nyingi
Haya tema mate tumchape[emoji871]
 
Back
Top Bottom