Elections 2015 Mgombea Urais CCM 2015: Ni Bernard Membe au January Makamba

Hivi ni kwanini tunatumia muda mwingi sana kujadili nani atakuwa Rais wakati matatizo yanayokabili maisha ya kila siku tunapishana nayo bila kuyapa nafasi ya kuyajadili?
Swali zuri kaka, na hii ndio jibu la kwanini tumekuwa na wanasiasa wajinga wajinga, siasa imegeuka kuwa mtaji wa kutokea kimaisha. Ndio maana unaona watu wanaagalia tu hizo nafasi za kisiasa na kuzipigania lakini sio kuleta mabadiriko yoyote kimaendeleo kwa watanzania.
 
Mchambuzi,

Well said man, kwangu mimi kiongozi bora ni yule ambaye atakuwa mzalendo wa kweli, yule ambaye atauchukia umaskini wa watanzania kwa dhati, yule ambaye ataweka mbele maslahi ya Tanzania na sio ya chama atakachotoka,....

Sina hakika sana na hawa kwa sababu mfumo tulionao hauruhusu sana kama sio kidogo baadhi ya sifa hapo juu, ndio maana unaweza kukuta mtu anachaguliwa kwa sifa kama
1. mwenzetu
2, hana makuu,
3. mpole, nk.

Pamoja na mapungufu yote ni bora mara January Makamba ukiachilia mbali uwezo wake uliojipambanua katika kuongoza na ukuacha mapungufu ya kimfumo, ukilinganisha na Membe ambaye kwa bahati mbaya sana mimi namwona kama ni mtu mwenye ndimi mbili,siasa za visasi, kulindanda, kulipa fadhila ndio kutashika kasi ukilinganisha maadui aliojijengea kuanzia mchakato wa kumweka jk madarakani.(mtazamo wangu)
 
Last edited by a moderator:
Circumstances zitaamua mgombea wa CCM 2015. Membe na January hasa Membe ana uafadhali compare na wengine lakini wapi Lowasa atacheza kwenye picha hii ina maana nguvu tunazoaminishwa anazo ni maneno tu?
 
Mnataka kuniambia Nchimbi atakubali Membe ashinde kiurahisi rahisi tu!. Please rule January Makamba out!
 
Mie naomba kuuliza:

Wapi na lini Lowassa alisema atagombea urais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania?

Hilo tu
 
Naomba niambiwe Makamba January amefanya nini, record yake ni ipi hadi atajwe kama potential presidential material?

Hizi sifa anazopata zinatoka kwenye nini?
 
Mchambuzi

Siku waTanzania wakimchagua January Makamba kuwa Rais, ndio siku ambayo nchi hii itaanza kupiga hatua za kweli za kuondoa umasikini.

Membe is incompetent.

Tundu Lissu is borderline crazy.

Analysis nzuri mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Mnasuka mpango tutawaliwe na chinga mwingine siyo! To hell with this. Heri kura yangu ya kula niwape CDM.
Na CHADEMA inayosemwa hapa ya Tundu Lissu ambaye ni mropokaji halafu anakimbilia kusema....eti ilikuwa HEARSAY. Hivi mimi si naweza nikasema mkulu ni shoga story ikapewa front page coverage nikiulizwa nitasema hearsay pia

CHADEMA wasipomsimika Dr. Slaa, heri kura yangu nichambie na KUI-FLUSH chooni
 
Mkuu Mchambuzi, I saw this coming! Actually we were thinking pretty much along the same lines. I knew these results would be tempting to January Makamba.

January Makamba can hold his hopes high but not run for president just yet.

If you ask me, those results reflect internal power struggle. Remember Wasira na January were initially not presidential hopefuls.

Sometimes I'm convinced Membe still has an uphill climb because what happened there is that rather than give a vote to Membe because Lowassa, their favorite, was not there they decided to give it to the less prominent contestant who will not think of running for president. They could be right in giving their votes to Wasira as this man will never think of running for president but they were wrong on January. Look now, he is hiring people to campaign for him
 
Hivi umesoma post yangu yote kweli? Swali lako linaashiria umesoma kichwa cha uzi tu; Vinginevyo nimefafanua kwa kirefu sana kwanini nime pick hao wawili;


ninadhani 2015 tutashuhudia mgombea URAIS ANATEULIWA MTU AMBAYE SI MJUMBE WA NEC NA UPEPO UTAVUMISHWA TU KWA HUYO MTU NA ATATEULIWA KWA KURA ZA KISHINDO NA MKUTANO MKUU!!!
 
Mkuu Mchambuzi umejieleza vizuri sana na kwa watu waelewa kama mimi hivi na kwa watu ambao siku zote thinking yao iko possitive tumekuelewa na kwa mara ya kwanza naanza kukubaliana na wewe kwa sababu una hoja nzito sana.

Nimebanwa kwa sasa niko ndani ya machimbo huku Nyarugusu Geita ndio kwanza nimeufikia mwamba wa dhahabu naanza kuupasua ili nipate mawe, nikimaliza nitakuja kukuongezea hoja juu ya hoja zako na kuunga mkono kwa hoja zaidi badala ya haya maneno mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi naona leo umepitiwa tena sana tu, hivi January Makamba ana umri gani na aliwahi lini kupigiwa kura na Wananchi?

Kanda ya kusini haiwezi kutoa Rais tena kwa mara ya pili sawa na Muislamu hawezi kuwa Rais baada ya Kikwete. sorry for my Ignorance lakini huo ndio ukweli, atakayeniona mdini shauri yake lakini sifa ya kwanza ya Rais ajaye ni lazima awe Mkristo.
 
sifa zote njema kwa mazingira ya sasa kwa nafasi ya urais mh.lissu ndo mwenye nazo.lakini bado tuna muda wa kuendelea kuwafuatilia kwa ukaribu wale wote tunaodhani ni presidential materials Mchambuzi umejikita ktk kuonesha watz tuanze kujikita kumwandaa rais,kwamba si muda ufike ndipo tuanze kukurupuka pasi ya kujua nani mwenye kutufaa.hapo kwenye jina la mh.lissu nimeamini jamaa yangu ulizaliwa mchana na kulia faster.good analysis
 
Last edited by a moderator:
Mkuu waswahili wanasema pumu imepata mkoozi! Kwa maoni yangu binafsi(nalindwa na Katiba ya sasa), na bila kuathiri kitu chochote, Membe anaweza kututawala( siyo kuongoza)!
 
Kwa Upande wangu Kuhusu Nani atakuwa Rais 2015 kati ya Lowasa na Asha ROse kwani kwakuwa Philipo Mang'ula yeye hao ndio wanajuana sana sasa hapo kazi
 
What about the Zanzibar factor? - Shein kwa mfano.
 
Nimekusoma vizuri sana Mchambuzi.

Mchango wangu unalenga pande zote mbili, Chama tawala na Upinzani. kwenye swala la urahis sio lele mama, kuna mdau mmoja ametolea mfano kumpa dereva funguo wa gari then akushushe mlima kitonga, dereva kama atakuwa msanii itakuwa ni hatari.

Ninachotaka kukizungumza ni kwamba inatakiwa wagombea wote wabase kwenye hoja na sio rushwa. tuna mifano mingi ya wagombea walitajwa kutumia rushwa hata kupata huo ubunge, sasa watu kama hao ukimpa urahisi itakuaje? Mbali na hoja zao pia uadilifu ni kiti cha msingi, unakuta m2 ananuka kashfa za rushwa kila kona, unamdadi eti agombee urahisi, kitu ambacho ni kichekesho.

So kwa maoni yangu mwadilifu yeyote awe kutoka chama tawala au upinzani anafaa kuwa raisi pia asiwe mtu wa dini fulani basi awe ni mtu wa utaifa. Kwa kumalizia, nafasi nawapa chadema kwan waadilifu wako wengi ukilinganisha na chama tawala, unless otherwise chama tawala kweli kijisafishe kutokana na kashfa mbaya juu yake.
 
Last edited by a moderator:

Nimeupenda sana uchambuzi wako lakin nimepata mush'kira na hitimisho lako la kusema TUNDU LISSU kuwa rais. Hakika huyu ni mtendaji tu lakin hafai kabisa kupata uongozi tena huo wa juu kwa sababu zifuatazo
1. Ni mtu mwenye jazba sana. Na siku zote tunaamini penye Jazba hakuna HIKMA.
2. Ana hasira sana. na siku zote tunaamini penye hasira pana khasara.

Mwangalie akiwa anatoa hoja zake Bungeni au hata hotba zake bungeni utayagundua hayo.

Mimi kama ningekuwa MTz ningeshauri nafasi hiyo ya Juu apewe Dr Hussein Ali Hassan Mwinyi.
 
Mchambuzi, nashindwa kuelewa na nashangaa kwanini una m-exclude kipenzi chetu Dr. W. P. Slaa!

Nani alisema Dr.Slaa siyo kipenzi cha vijana?

I wonder!
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…