Uchaguzi 2020 Mgombea Urais kupitia ACT-Wazalendo, Bernard Membe achukua fomu za Kugombea Urais wa Tanzania ofisi za NEC

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais kupitia ACT-Wazalendo, Bernard Membe achukua fomu za Kugombea Urais wa Tanzania ofisi za NEC

Ni vizuri Membe analeta amshaamsha, lakini kama hajatumwa basi hii kitu inaweza mpotezea umaarufu.
 
Hivi Membe kabisa yupo serious ?Hope mbeleni atamwachia Lissu. To be honest Ukijumlisha kura za zote upinzani mwaka 2015 ,upinzani walimshinda Magufuli tatizo ushindi wao waliugawana.

Wewe utakuwa either ni mchaga wa siasa za Tanzania au hujui mahesabu ... Hata wapinzani wakiungana kamwe hawawezi kuishinda CCM!
 
hili ni pandikizi kuu la ccm, kazi yake kuu ni kuhakikisha anapunguza kura za upinzani.........mtanielewa siku fulani..
 
Ila Membe anahangaika nini?

Washauri wake naoni viazi.
Hisia zangu zinanituma kuwa Membe huenda yupo ACT kimkakati! Atagawa kura za Tundu Lissu na kumpa gap kubwa la kiuongozi Mzee baba.
 
Huyu mtu si alisema bila muungano wa vyama vya upinzani (grand coalition) hatagombea urais??? Akatudanganya kuna "tsunami" ya wanachama wapya toka upande ule wanakuja kumfuata! So far hatujasikia hata mwenyekiti wa kitongoji kamfuata huko aliko.
 
Eti akaleta usanii kule kwao Rondo.
Akajisemea wanaCCM zaidi ya mia tatu wamerudisha kadi zao. Kadi zenyewe zote mpya . CCM ilaaniwe kwa kueneza ujinga na upumbavu Tanzania


Chama cha upinzani Tanzania ni kimoja tu nacho ni CHADEMA na Mgombea wake ni Tundu Lissu. Vyama vingine vyote ni matawi ya CCM.

Kwa maana hiyo CCM ina wagombea wengi ambao watazigawa kura za CCM, na upinzani una mgombea mmoja tu Tundu Lissu ambae atapigiwa kura zote za upinzani. Sijui hofu yako kwa Membe kugawanya kura za upinzani inatoka wapi? Wewe shangilia tu CCM inagawanya kura zake hivyo kumpa uhakika wa ushindi Mgombea wetu wa upinzani Tundu Lissu.
 
Mgombea Urais kupitia chama cha ACT Wazalendo pamoja na mgombea mwenza Profesa Omar Hamad leo Agosti 7, 2020, wamechukua fomu ya kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za NEC Jijini Dodoma.

View attachment 1529783
View attachment 1529827
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mh. Jaji wa Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage akikabidhi fomu za kugombea kiti cha Rais kwa Mgombea wa Chama cha ACT-Wazalendo, Bernard Membe katika Ofisi za NEC Njedengwa Jijini Dodoma leo Agosti 7,2020, kushoto ni Mgombea Mwenza, Prof. Omar Faki Hamad . Chama hicho kinakuwa cha nane kuchukua fomu.

View attachment 1529828

====
TAARIFA KWA UMMA

MEMBE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

Mgombea Urais wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ndugu Bernard Kamilius Membe leo tarehe 7, Agosti 2020 amechukua fomu ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Membe amekabidhiwa fomu hiyo ya uteuzi na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage Jijini Dodoma.

Katika uchukuaji huo wa fomu, Membe aliambatana na Mgombea mwenza wake, Profesa Omary Fakih Hamad.

Aidha msafara huo wa Membe uliongozwa na Mwenyekiti wa Chama, Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu, Ndugu Ado Shaibu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Ndugu Mhonga Said Ruhwanya, Katibu wa Mambo ya Nje Ndugu Bonifasia Mapunda, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma, Ndugu Janeth Rithe, Katibu wa Ngome ya Vijana Ndugu Mwanaisha Mndeme na viongozi wengine waandamizi wa Chama.

Akiongea na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Ndugu Bernard Membe amesema kuwa amejiandaa kufanya kampeni kabambe kila Kona ya nchi ili kuipatia ACT Wazalendo ushindi mnono na kuhakikisha ifikapo tarehe 28 Oktoba 2020, utawala wa Rais Magufuli unafikia tamati.

Imetolewa na:
Janeth Joel Rithe
Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma.

Imetolewa leo tarehe 07 Agosti 2020.
Halafu wanadai eti wataungana na CDM thubutu. Labda kama kuachiana itakuwa ubunge na udiwani lakini urais wa Tanzania Lissu na Membe kila mmoja atashiriki. Ila mmojawapo akienguliwa na Tume hapo ndipo watashirikiana. Kwa Zanzibar no choice CDM hata wakishiriki mgombea wao hana impact kwa Maalim.
 
Back
Top Bottom