Mgonjwa kulipia 'Kumuona Daktari' Hospitali si sahihi

Mgonjwa kulipia 'Kumuona Daktari' Hospitali si sahihi

Waache wafe Wakilalamika.
Watanzania ni watu wajinga sana. Hata hawajui wanataka
nini. MagufuliJP walimtukana
sana ila sasa wanakumbuka, JK
the same.
Kufa kupo tu ndio maana wengi wanakufa kwa maradhi ambayo madaktari hamjui tiba zake au hamkubaliani na tiba zake ambazo ni nje ya mlichofundishwa na matokeo mgonjwa anawafia hospitali bila kujaribu njia nyengine mbadala.
 
Naona kama Serikali imechelewa sana kufuta hii gharama inayozidi kumuongezea machungu mgonjwa pindi anapoamua kwenda kutafuta tiba hospitali.

Ni kijambo kidogo lakini huwezi jua pengine kimewahi hata kusababisha vifo.

Huenda ilishatokea mtu aliumwa sana na akatamani aende hospitali lakini akajikuta hata pesa ya kumuona daktari hana, pengine ikapelekea akasusa hata baadae maradhi yakamzidi na akafariki kwa kuchelewa kupata matibabu!

Nimewaza sana na kujiuliza kuna uhalali gani wa malipo haya? Si hospitali ya serikali si private, yaani hata daktari hajasema chochote anaku chaji pesa ambayo imeshapangwa wewe na yeyote yule atakayeingia chumba hicho atoe kwanza kabla ya gharama zingine za matibabu.

Tuombe serikali iondoe gharama hizi kutupunguzia mzigo wa maisha angalau tuwe tunalipia vipimo na dawa tu.
Ni kweli upo sahihi mwanchi kulipia hiyo ghalama ya kumuona daktali kwa sababu

Huyu mgonjwa tayari analipa makodi kibao
 
Ni kweli upo sahihi mwanchi kulipia hiyo ghalama ya kumuona daktali kwa sababu

Huyu mgonjwa tayari analipa makodi kibao
HELA YA CONSULTATION HACHUKUI DAKTARI ILE NI KWA AJILI YA HOSPITAL KUWEZA KUJIENDESHA NA KUMLIPA MSHAHARA YULE DAKTARI ANAYEKUHUDUMIA .

Sent from my Redmi Note 8 using JamiiForums mobile app
 
Unajua kua kama kuna mashirika ya bima yanafanya biashara?[emoji16][emoji16]
Watu wananunua pombe hadi za milioni usiku mmoja tu,ndio iwe kulipia Bima mwaka mzima milioni,kwa ajili ya kumuona daktari kila anapoumwa?
Hapo utagundua tatizo ni umasikini na si kumuona daktari

Wewe ni daktari sio!! Naona unatumia nguvu kujitetea
 
Na hilo ndio tatizo lenu, hao wanaokufa kwenye uangalizi wenu huko hospitali kutokana na aina za tiba zenu au uzembe wenu hayo hamuyazungumzii ila mkisikia mtu katumia dawa ya kienyeji au kanywa dawa bila ushauri wenu na kafariki au kapata madhara basi hayo ndio mnayaona na kuyaongea.
Suala la afya liko kwenye jukumu lako mwenyewe.....
Ukiona unahisi unatofauti mwilini,au unajisikia ndivyo sivyo muone daktari
Aliyebobea kwenye kazi yake
Ova
 
Labda useme kuwe na kiwango kimoja kwa nchi nzima...

Ukiondoa hiyo fee, mahospitali yatafurika wakati bado uwiano wa daktari mmoja kwa wagonjwa ni mkubwa...
Unaonaje pia kama watakuwa wanawajibishwa severely wakimsababishia mtu/mgonjwa kufanya irrelevant diagnosis au hata kumpa dawa zisizotakiwa?

Maana kama ni usumbufu kumuona, vipi kuhusu kufanyia mafunzo mwili wa mtu?

Wengi wanaotea!
 
Sasa daktari atalipwaje,
Gharama za kumlipa daktari ziwekwe kwenye vipimo au kwenye madawa, au kwenye getini kama get pass ukiingia tu utoe hela?
 
Hujawahi fanya kazi au kupata shida.

Maeneo yote hayo imetaja wanalipa consultancy fee.

Kumuona mwanasheria kukushauri ni 50000 unatoa papo kwa papo. Na sijawahi ona mwananchi analalamika na hizi zinalipwa bila shuruti.

Mwanasheria kucertify cheti kimoja ni 20,000 bila hiyo hupati huduma. Sijawahi ona mwananchi analalamika.

Ukienda kwenye firms za wahasibu unalipa consultant fee, ukienda kwenye firms za Manunuzi unalipa. Sema wewe hujui. Na ni hujui kwasababu hizo huduma so kila mtu atataka. Na anayetaka hizo huduma ni mwenye pesa haoni shida. But huduma za afya ni mtakuja kuanzia masikini hadi tajiri lazima mje tu. Ndo maana vitu vidogo mnaona vikubwa but ukienda kwa mwanasheria kule au consultation kwaajili ya projects unalipa tu.

Na ukiona hivi ujue ndo umuhimu wa hiyo huduma. So chutama na omba iboreshwe

Ila afya mnaona ni kitu cha bure. Duniani kote huduma za afya ni very expensive ukisema uendeshe kwa hivi mnataka. Ipo siku utapakwa Mavi ya mgonjwa badala ya spirit.

If you think health is expensive try ignorance.
Hahahaha

Sio education.

Ila sielewi bado. Hujanishawishi.

Health care ni basic needs.

Inatakiwa itolewe for free au kwa very minimal cost ambayo kila mtu anaweza afford. Over
 
Mfano usmbiwe kafanye full blood picture...
Umefanya,umepewa report sasa ukipewa hiyo report utaisoma mwenyewe kujua na kuielewa
Si itabidi umrudishie daktari akakusome

Ova
Bwana wewe si anapokea mshahara kutokana na kodi za wananchi.

Private its okay hata consultation fee ikiwa milioni.
 
Either hauna akili ama wewe ni mpumbavu.....majibu ni mawili tu.
"Consultation fee" ni huduma sio bidhaa,ni kazi ya daktari kujua upime kipimo kipi na kwa sababu gani?,utumie ama usitumie dawa ipi na kwa nini?,unadhani ni rahisi hio kazi?
Daktari amekaa shule miaka 6 na udaktari ndio degree pekee ambayo mtu analipa ada nyingi kuliko kozi yeyote ile,ada ya MD pale KCMC ya mwaka mmoja unaweza lipia kozi zingine za miaka mitatu na chenji ikabaki.
Ulizia gharama za kusoma MD hata dunia ya kwanza huko,U.S,Canada,Germany etc.
Daktari hana bidhaa,daktari anatoa huduma ya "materials" aliyoyasoma miaka kazaa shule,ile unayolipia ni elimu ya daktari,ni Sheria ya dunia,ukiwa mjinga lazima ulipie elimu ya kitu usichokijua.
Ukienda bar unalipia pombe,ukipanda basi unalipia nauli ufike.
Ukienda kwa daktari unalipia "fee"ya kulipia elimi usiyoijua kuhusu ugonjwa wako,ukienda maabara,unalipia vipimo,ukienda pharmacy unalipia gharama ya dawa.
Kwenye ada umepuyanga. Na wanaosoma Aerospace au aircraft engineering wasemeje.
Mnakurupuka tu.

Fee hio ifutwe.
 
Kupitia uzi huu..
Nmegundua kuwa wabongo wengi hawaelewi vitu vingi kuhusu madaktari na udaktari..

Kubwa kuliko ni kuwa mtoa uzi ulitakiwa ku moderate uzi na kuwarudisha kwenye njia wanao potosha kuhusu mnufaika wa hizo gharama...

Inabidi ieleweke kwamba.

1. CONSULTATION FEE = (gharama ya kumuona daktari) haichukuliwi na Daktari.. Hata madaktari wengi wanaon siyo fair kuwa na amount kubwa hivo. Na mara nyingi utakuta daktari anajitolea hela yake ya mfukoni kumlipia mgonjwa maskini...

2. KUMUONA DAKTARI.. siyo sawa na kumuona mkiwa mna piga gambe, ama kumuona padre ukienda kuungama.. Ile ni sehemu ya Matibabu.. Kama ni kuchangia basi Ni lazima kuchagia sawa na unavyo changia dawa.

3. Kama unaona consultation services siyo muhimu kuchangia.. Basi hata dawa ziwe bure.. Kwa mantiki hiyo hiyo. Kwa maana zote ni aina za Matibabu..

4. Elimu elimu elimu itolewe kwa wagonjwa kuhusu huduma wanazo changia.

Kwa sehemu kubwa mfumo wetu wa afya ni kuchangia na siyo kulipia huduma.


Tujifunze kupitia kisa hiki:

Kuna mgonjwa yeye mwnyewe alijiona kama ana uvimbe usio uma tumboni akijishika.

Aka amua kwenda Hospital ya wilaya. Akalipia gharama za kumuona dokta.. Dokta kambinya binya Ikaonekana ni kweli ana uvimbe tumboni.. Ile hospital haikuwa na ultrasound machine. Ikabidi aandikiwe barua kwenda hospital ya mkoa "for further evaluations and managements"


Kufika hospital ya mkoa, napo akalipia gharama ya kumuona daktari, dokta akamuandikia alipie kipimo cha ultrasound.. Bada ya majibu ya ultrasound akamuandikia barua ya rufaa kwenda hospital ya kanda.


Hospital ya kanda akalipishwa tena gharama ya kumuona daktari.. Na Daktari alipomuona akasema haamini kipimo kutoka hospital ya chini, hata hivyo kuna details hazijatajwa kwenye report hiyo.. Hivyo apime upya kipimo cha ultrasound aongezee na CT - Scan.

Mgonjwa aka hamaki, hela zime isha, uvimbe upo vile vile, na anaona kama hajatibiwa..
Akaanzisha varangati eti arudishiwe hela zake za kumuona daktari.. Kwani daktari haja fanya chochote.

**************
 
Hahahaha

Sio education.

Ila sielewi bado. Hujanishawishi.

Health care ni basic needs.

Inatakiwa itolewe for free au kwa very minimal cost ambayo kila mtu anaweza afford. Over
Kwa sheria ipi Tanzania, unatakiwa kutoa huduma bure. Ukinipa basi naacha ubishi hapa
 
Naona kama Serikali imechelewa sana kufuta hii gharama inayozidi kumuongezea machungu mgonjwa pindi anapoamua kwenda kutafuta tiba hospitali.

Ni kijambo kidogo lakini huwezi jua pengine kimewahi hata kusababisha vifo.

Huenda ilishatokea mtu aliumwa sana na akatamani aende hospitali lakini akajikuta hata pesa ya kumuona daktari hana, pengine ikapelekea akasusa hata baadae maradhi yakamzidi na akafariki kwa kuchelewa kupata matibabu!

Nimewaza sana na kujiuliza kuna uhalali gani wa malipo haya? Si hospitali ya serikali si private, yaani hata daktari hajasema chochote anaku chaji pesa ambayo imeshapangwa wewe na yeyote yule atakayeingia chumba hicho atoe kwanza kabla ya gharama zingine za matibabu.

Tuombe serikali iondoe gharama hizi kutupunguzia mzigo wa maisha angalau tuwe tunalipia vipimo na dawa tu.
Hii ishu Isikusumbue Sana mkuu hakuna mabadiliko yoyote yatakayotokea. Hili ni suala la cost sharing.. Limeanzia miaka y 80s huko. Sio zuri Kwa wenye kipato kidog zaidi kama mm n wew Lakin tayar lishakuwa zuri Kwa sabb ni kesi y kupata mapato Kwa Serikali.
 
Hujawahi fanya kazi au kupata shida.

Maeneo yote hayo imetaja wanalipa consultancy fee.

Kumuona mwanasheria kukushauri ni 50000 unatoa papo kwa papo. Na sijawahi ona mwananchi analalamika na hizi zinalipwa bila shuruti.

Mwanasheria kucertify cheti kimoja ni 20,000 bila hiyo hupati huduma. Sijawahi ona mwananchi analalamika.

Ukienda kwenye firms za wahasibu unalipa consultant fee, ukienda kwenye firms za Manunuzi unalipa. Sema wewe hujui. Na ni hujui kwasababu hizo huduma so kila mtu atataka. Na anayetaka hizo huduma ni mwenye pesa haoni shida. But huduma za afya ni mtakuja kuanzia masikini hadi tajiri lazima mje tu. Ndo maana vitu vidogo mnaona vikubwa but ukienda kwa mwanasheria kule au consultation kwaajili ya projects unalipa tu.

Na ukiona hivi ujue ndo umuhimu wa hiyo huduma. So chutama na omba iboreshwe

Ila afya mnaona ni kitu cha bure. Duniani kote huduma za afya ni very expensive ukisema uendeshe kwa hivi mnataka. Ipo siku utapakwa Mavi ya mgonjwa badala ya spirit.

If you think health is expensive try ignorance.
Mkuu, daktari anapokuwa ofisini (wodini) pale ile ndio ofisi yake, kama ilivyo kwa accountant na kada nyingine! ambao wanalipwa mashahara kupitia kodi,
Je, nao wawe wanalipisha wananchi wanao enda kupata huduma za kiuhasibu?
 
Mtu aliyetakiwa apate hela nyingi katika hii dunia, ni daktari;kwa sababu anaokoa maisha yako
 
Back
Top Bottom