Mgonjwa kulipia 'Kumuona Daktari' Hospitali si sahihi

Mgonjwa kulipia 'Kumuona Daktari' Hospitali si sahihi

nani sasa wa kuachana na mwenzake,
ww ndio uachane na kwenda kumuona kama hautaki kulipa.. uumwe hadi ufe
Kufa utakufa tu hata usipoumwa hata ufanyeje, zikifika zimefika tu na haina namna maana ni sheria ya aliyekuumba.

Usirudie tena kula kiporo cha makande na wanzuki asubuhi sana.
 
Tafsiri yake kila mtu anapaswa achunge Afya yake Kwa umakini ili Kupunguza gharama Kama hizo.

Pili, Gharama ya kumuona Daktari haipaswi kuondolewa Ila inatakiwa kuwa Affordable kulingana na Hali za Watu husika.
Hospital ziwekwe kulingana na hadhi za watu.

Kumuona Daktari lazima ulipie ili ujue umuhimu wa kutunza Afya yako mwenyewe.

Kama unaona gharama kumuona Daktari basi yakupasa uzingatie sana mambo ya Afya ili kuepuka Gharama.

Magonjwa mengi yanatokana na uzembe, na siku zote uzembe ni gharama.
Lengo hasa la consultation fee ni nini? na je what if kila Fani wakijiwekea utaratibu huo wa consultation fees? maana wote wameingia darasani na wamesota.

1. Mfano, wahasibu- Degree ya kwanza + miaka ya CPA.
2. Wanasheria wasomi - Degree ya kwanza + miaka ya Law School.
3. Maafisa manunuzi - Degree ya kwanza + miaka ya kupata CPSP
4. Maafisa Utumishi- Degree ya kwanza + Mitihani yao ya utumishi.

Utakuta hata hao walio kwenye kada nyingine wamesoma miaka almost the same kama hao madaktari.

Nikweli naunga mkono, consultation fee ifutwe.
 
Labda useme kuwe na kiwango kimoja kwa nchi nzima...

Ukiondoa hiyo fee, mahospitali yatafurika wakati bado uwiano wa daktari mmoja kwa wagonjwa ni mkubwa...
Kwahiyo hiyo fee imewekwa kupunguza magonjwa/wagonjwa?
 
Kitu usichokijua ni kwamba kuonana na Dr ni muhimu Zaid maaana ni yeye atakayekuandikia vipimo kama inabidi, ni yeye utamrudishia vipimo akusomee majibu, ni yeye atakuandikia dawa kulingana na majibu ya vipimo vyako pia hata kama hatokuandikia vipimo Wala dawa atakushauri vizur tu nayo ni matibabu, Sasa kwann umuone bure?

Lakini ukitaka kujiepusha na hiyo consultation fee ya Dr unaruhusiwa pia kwenda hospitali yeyote ( za serikali excluded) na vipimo vyako ukalipia ukapima na majibu ukapewa ukaondoka nayo ukijua utampelekea nani.
Ni kazi yake.. na analipwa kwenye mshahara
 
Hapo issue siyo kumuona Daktari.

Unacholipia Ni consultation fee.

Yaani kupima vital signs ( pressure, air tract, Breathing rate na kumwelezea Daktari unavyojisikia, halafu akakupa USHAURI na matibabu yake kwa kukuandikia.

Akishakuandikia hiyo 'Kumuona Daktari inaishia hapo"
Kumuona mwanasheria ni 50000/= kabla ya chochote. Hiyo ni consultation fee.
 
Mleta mada una tafsiri potofu kuhusu gharama ya kumuona Daktari. Kiuhalisia ile sio gharama ya kumuona Daktari bali ni gharama ya kutibiwa na Daktari. Kuonana na Daktari kwa lengo la kutibiwa ndio msingi wa huduma zote za matibabu kwa mgonjwa, na pesa unayolipa ndio inalipia muda wake, juhudi zake na akili yake itakayo tumika kutambua ugonjwa wako na kupangilia matibabu ya ugonjwa wako na wagonjwa wengine. Gharama hizo hutofautiana baina ya hospitali na hospitali au Daktari na Daktari. Kwa hospitali za umma (serikali) ile pesa inaingia kwenye mapato ya serikali na kwa hospitali za binafsi ile pesa inaingia kwenye hospitali husika, Daktari yeye hulipwa na taasisi husika kwa mapatano binafsi.
 
Sijasema madktari sio muhimu bali madktari hujiona wao ndio special kuliko wengine na watu kudhani madaktari wanajua kila kitu kuhusu tiba, mnapenda mtukuzwe muonekane ni watu muhimu kuliko wengine kisa tu
nyie madktari mnajua kila kitu.
Kuna siku nusu tupoteze maisha ya bi mkubwa wangu kama nisingejiongeza na kubaki kutegemea mawazo ya daktari ambaye nilishaona kabisa alikuwa anacheza na uhai wa mtu.
Na ni special kuliko taaluma yeyote. Kama unaona siyo special njoo usome.

Daktari katika maisha yake yote mitano anasoma yafuatayo pamoja vingine ni partial but muhimu asome

1. Anasoma udaktari
2. Anasoma maabara
3. Anasoma famasia
4. Anasoma mazingira
5. Anasoma uongozi
6. Anasoma sheria
7. Na vitu vingine vingi


So udaktari ni noble professional ambayo duniani kote inaheshimiwa. Nashangaa Tanzania tu tunaona kila mtu anaweza kuwa daktari.

Hiyo hela ya consultation siyo hela ya kumuona daktari na wala daktari hapati hiyo hela. Hela hiyo ni kwaajili ya

1. File, mifumo
2. Uendeshaji wa mifumo
3. Viandikwa
4. Vifaa tiba vinavyotumika kumuona mgonjwa hivi vyote vinanunuliwa kwa hela ya consultation.


Bahati mbaya sana watanzania wanapenda vya bure. Wanapenda kila anachotoa ajue matumizi yake utafikiri hicho kituo kaweka yeye. Ndo maana tutaendelea kuwa masikini tu.
 
Mleta mada una tafsiri potofu kuhusu gharama ya kumuona Daktari. Kiuhalisia ile sio gharama ya kumuona Daktari bali ni gharama ya kutibiwa na Daktari. Kuonana na Daktari kwa lengo la kutibiwa ndio msingi wa huduma zote za matibabu kwa mgonjwa, na pesa unayolipa ndio inalipia muda wake, juhudi zake na akili yake itakayo tumika kutambua ugonjwa wako na kupangilia matibabu ya ugonjwa wako na wagonjwa wengine. Gharama hizo hutofautiana baina ya hospitali na hospitali au Daktari na Daktari. Kwa hospitali za umma (serikali) ile pesa inaingia kwenye mapato ya serikali na kwa hospitali za binafsi ile pesa inaingia kwenye hospitali husika, Daktari yeye hulipwa na taasisi husika kwa mapatano binafsi.
Acha uongo. Madaktari hawapati hiyo hela na wala siyo kwaajili ya kumuona daktari. Madaktari tunafeli sana kujieleza.

Hiyo consultation ni kwaajili ya taasisi husika. Matumizi yake ni mifumo, , viandikwa, nursing care, na kwa private kidogo inamlipa daktari kuja kufanya kazi pale kama mshahara wake nk.

Madaktari tujue kujieleza tunabaki kusemewa mno. Tunapata tuhuma zote za Hospitali. Dawa zikiibwa na Mfamasia kaiba daktari, muuguzi akila rushwa kala daktari, mtu wa mapokezi akiljibu vibaya mgonjwa daktari kafanya. Hivi huyu daktari ataendelea kubeba matatizo ya hawa watu hadi lini.


Madaktari tunatakiwa kuwa na umoja, tupendane.
 
Naona wangepunguza au iwe sawa hospital zote ukitoa kabisa kutatokea usumbufu kila mmoja atataka kumuona daktar mwingine Hana ugonjwa ambao n serious lakin atataka kumuona Dr
Consultation fee ni sawa nchi nzima.

Kwa bima ya afya
1. Hospital za rufaa 25000 hadi 35,000
2. Wilaya 15,000 hadi 3000
3. Vituo vya afya ni 2000
4. Zahanati ni 1000

But inalipwa kulingana na elimu ya daktari

Specialist 15,000
MD 7000
AMO 5000
Co 3000

Hizi ni kwa ngazi za Clinics na hospitali za wilaya na mikoa zenye hadhi hiyo.
 
Lengo hasa la consultation fee ni nini? na je what if kila Fani wakijiwekea utaratibu huo wa consultation fees? maana wote wameingia darasani na wamesota.

1. Mfano, wahasibu- Degree ya kwanza + miaka ya CPA.
2. Wanasheria wasomi - Degree ya kwanza + miaka ya Law School.
3. Maafisa manunuzi - Degree ya kwanza + miaka ya kupata CPSP
4. Maafisa Utumishi- Degree ya kwanza + Mitihani yao ya utumishi.

Utakuta hata hao walio kwenye kada nyingine wamesoma miaka almost the same kama hao madaktari.

Nikweli naunga mkono, consultation fee ifutwe.
Hujawahi fanya kazi au kupata shida.

Maeneo yote hayo imetaja wanalipa consultancy fee.

Kumuona mwanasheria kukushauri ni 50000 unatoa papo kwa papo. Na sijawahi ona mwananchi analalamika na hizi zinalipwa bila shuruti.

Mwanasheria kucertify cheti kimoja ni 20,000 bila hiyo hupati huduma. Sijawahi ona mwananchi analalamika.

Ukienda kwenye firms za wahasibu unalipa consultant fee, ukienda kwenye firms za Manunuzi unalipa. Sema wewe hujui. Na ni hujui kwasababu hizo huduma so kila mtu atataka. Na anayetaka hizo huduma ni mwenye pesa haoni shida. But huduma za afya ni mtakuja kuanzia masikini hadi tajiri lazima mje tu. Ndo maana vitu vidogo mnaona vikubwa but ukienda kwa mwanasheria kule au consultation kwaajili ya projects unalipa tu.

Na ukiona hivi ujue ndo umuhimu wa hiyo huduma. So chutama na omba iboreshwe

Ila afya mnaona ni kitu cha bure. Duniani kote huduma za afya ni very expensive ukisema uendeshe kwa hivi mnataka. Ipo siku utapakwa Mavi ya mgonjwa badala ya spirit.

If you think health is expensive try ignorance.
 
Nenda JKCI Muhimbili
Kumuona daktari ni 35000. kwa consultansion isiyo zidi dk 10
Dawa ni balaa
Dawa ya gout 45000 mtaani 22000
Elenopril ya BP 15000 mtaani 7500
Huo ni mfano mdogo tuu na hospital inapewa ruzuku na mishahara inalipwa na serikali
Ukienda kwenye vipimo Kama huna bima katafute dawa mbadala ni balaa tupu
Mkuu naomba nikuone pm
 
Mkuu kumuona mganga wa kienyeji tu unalipia sembuse mtu alie ingia na kusota darasani miaka 6 au zaidi? Itabidi hata tukiwapigia simu tulipie maana tunawasumbua mno.
Mganga wa kienyeji analipwa mshahara toka kwenye kodi ya nani! Tuanzie hapo.
Kada ya afya haina tofaut na kada nyingine za huduma chini ya serkali. Bas na kila dr akienda polis kupewa huduma alipie kwanza cro?
Na mahakaman bas hakimu alipwe kumwambia kesi yako ya jinai?
Au bas ma dr wawe wanaishi kwa hizo posho za kuwaona sio kutupiga kodi yetu na charge za kuwaona.
Kila huduma ya kitaaluma ina thaman sawa ikishakuwa chini ya serkali.
 
Hujawahi fanya kazi au kupata shida.

Maeneo yote hayo imetaja wanalipa consultancy fee.

Kumuona mwanasheria kukushauri ni 50000 unatoa papo kwa papo. Na sijawahi ona mwananchi analalamika na hizi zinalipwa bila shuruti.

Mwanasheria kucertify cheti kimoja ni 20,000 bila hiyo hupati huduma. Sijawahi ona mwananchi analalamika.

Ukienda kwenye firms za wahasibu unalipa consultant fee, ukienda kwenye firms za Manunuzi unalipa. Sema wewe hujui. Na ni hujui kwasababu hizo huduma so kila mtu atataka. Na anayetaka hizo huduma ni mwenye pesa haoni shida. But huduma za afya ni mtakuja kuanzia masikini hadi tajiri lazima mje tu. Ndo maana vitu vidogo mnaona vikubwa but ukienda kwa mwanasheria kule au consultation kwaajili ya projects unalipa tu.

Na ukiona hivi ujue ndo umuhimu wa hiyo huduma. So chutama na omba iboreshwe

Ila afya mnaona ni kitu cha bure. Duniani kote huduma za afya ni very expensive ukisema uendeshe kwa hivi mnataka. Ipo siku utapakwa Mavi ya mgonjwa badala ya spirit.

If you think health is expensive try ignorance.
Mifano uliyotoa ni endapo umepata huduma hizo katika mfumo wa private.
Niambie sasa dr aliyeko payroll ya kodi yetu hiyo fee ya nini? Si kama pesa haitosh serkali iongeze kwenye mshahara yeye afanye kuhudumia kama mtumishi? Kama ilivyofanyika malipo ya gari kuingizwa kwenye mafuta.
 
Mifano uliyotoa ni endapo umepata huduma hizo katika mfumo wa private.
Niambie sasa dr aliyeko payroll ya kodi yetu hiyo fee ya nini? Si kama pesa haitosh serkali iongeze kwenye mshahara yeye afanye kuhudumia kama mtumishi? Kama ilivyofanyika malipo ya gari kuingizwa kwenye mafuta.
Sijatoa mfano huo ndo ukweli wa matumizi yake. Tena kwa serikali ndi6kabisa hiyo hela daktari hapati hata sent 1. Hiyo yote ni mapato ya serikali pure. Na matumizi yake ni kama nimetaja hapo ukiondoa mshahara kwa private.


Kama tu sasa wameongeza tozo hii kuitoa sahau. Wakiondoa lazima wataweka mahali.


Hata private watu hawajui anakuja anataka kipimo tu. Mwisho wa siku consultation mazuma ulipe utalipa kwa njia gani siwez sema hapa. But utalipa tu.
 
Back
Top Bottom