Mhasibu, Afisa TEHAMA wa Kanisa la SDA wapandishwa kizimbani kwa Wizi wa Tsh. Milioni 717

Mhasibu, Afisa TEHAMA wa Kanisa la SDA wapandishwa kizimbani kwa Wizi wa Tsh. Milioni 717

Watu watatu wakiwemo Mhasibu na Ofisa Tehama wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania (SDA), wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka manane, likiwamo la kutakatisha fedha na wizi wa Sh717 milioni mali ya kanisa hilo.

Washitakiwa hao ni ofisa Tehema, Wilson Mapande (35) mhasibu, Winnie Owino (33) na mfanyabiashara, Nicolaus Owino (29).

Watatu hao wamefikishwa mahakamani hapo jana Septemba 25, 2024 na kusomewa mashitaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga akishirikiana na Wakili wa Serikali, Aaron Titus.

Kabla ya kuwasomea mashitaka, hakimu Malewo alisema washitakiwa hawatakiwi kujibu chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi.

Amesema mashitaka ya kutakatisha fedha yanayowakabili washitakiwa hayana dhamana kwa mujibu wa sheria, hivyo wanatakiwa kusikiliza mashitaka na hawatatakiwa kujibu chochote.

Akiwasomea mashitaka, wakili Katuga amedai wanakabiliwa na mashitaka manane, la kwanza likiwa ni kuongoza genge la uhalifu, la pili wizi na la tatu hadi la nane ni utakatishaji fedha.

Katika shitaka la kwanza linalowakabili washitakiwa wote, amedai kati ya Mei 2021 na Januari 2023, waliongoza genge la uhalifu kisha kujipatia Sh717.126 milioni kutoka kwenye akaunti ya benki ya CRDB mali ya kanisa hilo.

Shitaka la pili la wizi linamkabili Mapande pekee, anayedaiwa kati ya Mei 2021 na Januari 2023 akiwa mtumishi wa kanisa hilo aliiba Sh717 milioni.

Katika shitaka la tatu la utakatishaji fedha, inadaiwa kwa kipindi hicho Mapande alifungua akaunti benki ya CRDB yenye jina lake akaingiza Sh396.629 milioni.

Shitaka la nne linawakabili Mapande na Winnie wanaodaiwa katika kipindi hicho walifungua akaunti benki ya CRDB yenye jina la Winnie wakaingiza Sh208.468 milioni.

Mbali na hilo, Mapande na Owino wanadaiwa katika shitaka la tano walifungua akaunti benki hiyo na kuingiza Sh112.029 milioni kwa jina la Owino.

Shitaka la sita hadi la nane, linamkabili Mapande na Winnie wanaodaiwa katika kipindi hicho walitumia fedha hizo kununua magari mawili aina ya Toyota Harrier na Toyota Crown. Pia wanadaiwa kununua nyumba eneo ambalo halijapimwa katika Mtaa wa Mtambani, Mapinga, Bagamoyo.

Upande wa mashitaka umedai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika, hivyo umeiomba Mahakama kuipangia kesi hiyo tarehe kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Malewo ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 9, 2024 kwa ajili ya kutajwa. Washitakiwa wote wamepelekwa rumande.

MWANANCHI

Ukiwaona wanavyosimuliana jinsi wakatoliki wanavyoabudu sanamu unaweza kufikiria kila mtu yuko serious. Kumbe binadamu ni wale wale. Na mambo yetu yale yale. Na kibaya, tuna share hata namna yadhambi zinazoendelea.
Tuache kujihesabia haki tukiwa tunaishi duniani
 
Wakati waumini wanajikamua pesa za sadaka kwa ajili ya maendeleo ya kanisa, kuna wajanja wachache wanazivizia na kuzitafuna kisawasawa. Kuna mhasibu mmoja wa SDA ambaye ni jamaa yangu yaani anazikula sana hizo hela za sasaka, hadi raha!


MKUU Sadaka humpi mtu au kanisa, unaitoa kwa MUNGU wako kwa Njia ya IMANI

We Kama unajua NDANI yako huwa unaoelekea MTU au kanisa sadaka na Sio MUNGU wako bora uache kutoa izo sadaka b'se hakuna mavuno B'se tunamuendea MUNGU kwa IMANI tu pekee yake

Hao watu waibe, wasiibe ni wao wenyewe na nafsi zao ila Kama umetoa sadaka yako kwa IMANI hiyo ni hadhina kubwa Sana mbele za MUNGU wako

Note: Kuna tofauti kubwa kati ya MUNGU na dini

Dini ilimkataa na kumpinga hata kumsulubisha YESU Kwaiyo chunguza NDANI yako wewe ni muumini wa dini au muumini wa MUNGU?🤔
 
Sitoi
Watu watatu wakiwemo Mhasibu na Ofisa Tehama wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania (SDA), wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka manane, likiwamo la kutakatisha fedha na wizi wa Sh717 milioni mali ya kanisa hilo.

Washitakiwa hao ni ofisa Tehema, Wilson Mapande (35) mhasibu, Winnie Owino (33) na mfanyabiashara, Nicolaus Owino (29).

Watatu hao wamefikishwa mahakamani hapo jana Septemba 25, 2024 na kusomewa mashitaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga akishirikiana na Wakili wa Serikali, Aaron Titus.

Kabla ya kuwasomea mashitaka, hakimu Malewo alisema washitakiwa hawatakiwi kujibu chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi.

Amesema mashitaka ya kutakatisha fedha yanayowakabili washitakiwa hayana dhamana kwa mujibu wa sheria, hivyo wanatakiwa kusikiliza mashitaka na hawatatakiwa kujibu chochote.

Akiwasomea mashitaka, wakili Katuga amedai wanakabiliwa na mashitaka manane, la kwanza likiwa ni kuongoza genge la uhalifu, la pili wizi na la tatu hadi la nane ni utakatishaji fedha.

Katika shitaka la kwanza linalowakabili washitakiwa wote, amedai kati ya Mei 2021 na Januari 2023, waliongoza genge la uhalifu kisha kujipatia Sh717.126 milioni kutoka kwenye akaunti ya benki ya CRDB mali ya kanisa hilo.

Shitaka la pili la wizi linamkabili Mapande pekee, anayedaiwa kati ya Mei 2021 na Januari 2023 akiwa mtumishi wa kanisa hilo aliiba Sh717 milioni.

Katika shitaka la tatu la utakatishaji fedha, inadaiwa kwa kipindi hicho Mapande alifungua akaunti benki ya CRDB yenye jina lake akaingiza Sh396.629 milioni.

Shitaka la nne linawakabili Mapande na Winnie wanaodaiwa katika kipindi hicho walifungua akaunti benki ya CRDB yenye jina la Winnie wakaingiza Sh208.468 milioni.

Mbali na hilo, Mapande na Owino wanadaiwa katika shitaka la tano walifungua akaunti benki hiyo na kuingiza Sh112.029 milioni kwa jina la Owino.

Shitaka la sita hadi la nane, linamkabili Mapande na Winnie wanaodaiwa katika kipindi hicho walitumia fedha hizo kununua magari mawili aina ya Toyota Harrier na Toyota Crown. Pia wanadaiwa kununua nyumba eneo ambalo halijapimwa katika Mtaa wa Mtambani, Mapinga, Bagamoyo.

Upande wa mashitaka umedai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika, hivyo umeiomba Mahakama kuipangia kesi hiyo tarehe kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Malewo ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 9, 2024 kwa ajili ya kutajwa. Washitakiwa wote wamepelekwa rumande.

MWANANCHI
Sitoi sadaka kanisani tena,wataomba na kaomba lkn nitakuwa mpenzi msikilizaji na mtazamaji.
 
Dini ilimkataa na kumpinga hata kumsulubisha YESU Kwaiyo chunguza NDANI yako wewe ni muumini wa dini au muumini wa MUNGU?🤔
Mkuu kama ni hivyo basi hakuna haja ya kwenda kanisani bali unaweza ukamuabudu Mungu yako ukiwa nyumbani na kumtolea dhabihu badala ya kwenda kanisani kukamuliwa sadaka na wafuata dini.
 
Hapo kesi ni moja tu kutakatisha pesa japo sidhani kama ni kweli hii wamepewa kama kifungashio tu wasichomoe (Kanisa limewasingizia kupitia Wakili wao)

Swala la wizi wa Pesa za Kanisa kama kweli Sadaka huwa ni ya Mungu basi aachiwe mwenyewe sidhani kama Mungu anahitaji mtetez binadamu na kila Sabatho wanafundisha Mungu haibiwi twajiibia wenyewe. Shida iko wapi sasa?

Kimsing wameupiga mwingi waendelee kusafisha Mitaa, Conference na Union zote mpaka GC.

#Biashara ya dini inaimaliza Afrika yetu.
 
Watu watatu wakiwemo Mhasibu na Ofisa Tehama wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania (SDA), wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka manane, likiwamo la kutakatisha fedha na wizi wa Sh717 milioni mali ya kanisa hilo.

Washitakiwa hao ni ofisa Tehema, Wilson Mapande (35) mhasibu, Winnie Owino (33) na mfanyabiashara, Nicolaus Owino (29).

Watatu hao wamefikishwa mahakamani hapo jana Septemba 25, 2024 na kusomewa mashitaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga akishirikiana na Wakili wa Serikali, Aaron Titus.

Kabla ya kuwasomea mashitaka, hakimu Malewo alisema washitakiwa hawatakiwi kujibu chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi.

Amesema mashitaka ya kutakatisha fedha yanayowakabili washitakiwa hayana dhamana kwa mujibu wa sheria, hivyo wanatakiwa kusikiliza mashitaka na hawatatakiwa kujibu chochote.

Akiwasomea mashitaka, wakili Katuga amedai wanakabiliwa na mashitaka manane, la kwanza likiwa ni kuongoza genge la uhalifu, la pili wizi na la tatu hadi la nane ni utakatishaji fedha.

Katika shitaka la kwanza linalowakabili washitakiwa wote, amedai kati ya Mei 2021 na Januari 2023, waliongoza genge la uhalifu kisha kujipatia Sh717.126 milioni kutoka kwenye akaunti ya benki ya CRDB mali ya kanisa hilo.

Shitaka la pili la wizi linamkabili Mapande pekee, anayedaiwa kati ya Mei 2021 na Januari 2023 akiwa mtumishi wa kanisa hilo aliiba Sh717 milioni.

Katika shitaka la tatu la utakatishaji fedha, inadaiwa kwa kipindi hicho Mapande alifungua akaunti benki ya CRDB yenye jina lake akaingiza Sh396.629 milioni.

Shitaka la nne linawakabili Mapande na Winnie wanaodaiwa katika kipindi hicho walifungua akaunti benki ya CRDB yenye jina la Winnie wakaingiza Sh208.468 milioni.

Mbali na hilo, Mapande na Owino wanadaiwa katika shitaka la tano walifungua akaunti benki hiyo na kuingiza Sh112.029 milioni kwa jina la Owino.

Shitaka la sita hadi la nane, linamkabili Mapande na Winnie wanaodaiwa katika kipindi hicho walitumia fedha hizo kununua magari mawili aina ya Toyota Harrier na Toyota Crown. Pia wanadaiwa kununua nyumba eneo ambalo halijapimwa katika Mtaa wa Mtambani, Mapinga, Bagamoyo.

Upande wa mashitaka umedai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika, hivyo umeiomba Mahakama kuipangia kesi hiyo tarehe kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Malewo ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 9, 2024 kwa ajili ya kutajwa. Washitakiwa wote wamepelekwa rumande.

MWANANCHI

Hata kama umeamua kuwa mwizi, huu ni wizi wa kipumbavu.

Auditor wa kawaida hata wa for four angeweza gundua huo wizi ndani ya mwezi.
 
Mkuu kama ni hivyo basi hakuna haja ya kwenda kanisani bali unaweza ukamuabudu Mungu yako ukiwa nyumbani na kumtolea dhabihu badala ya kwenda kanisani kukamuliwa sadaka na wafuata dini.


MUNGU haabudiwi kanisani mkuu, MUNGU anaabudiwa katika Roho na katika kweli


Yohana


4.20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.
4.21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.


MWANAMKE msamaria alimwambia YESU 👉 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

Hapa alikuwa akimaanisha kumuabudu MUNGU ni Mahali/SEHEMU fulani


katika mlima huu 👉 sehemu


huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia 👉 sehemu


Tazama jibu la YESU kwa mwanamke Msamaria👇
 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.


Yohana 4.24


"Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli"


Kumuabudu MUNGU ni katika Roho na katika Kweli na Sio kama dini inavyosema Kwamba kumuabudu MUNGU ni mahali au sehemu fulani hiyo hali ilikuwa katika Agano la kale kabda ya MUNGU kutupatanisha na yeye kwa njia ya YESU KRISTO, Ndio maana YESU alimjibu MWANAMKE kwamba ninyi mnaabudu msichokijua 😁
 
Back
Top Bottom