Job K
JF-Expert Member
- Oct 4, 2010
- 9,314
- 7,149
Pasco tafadhali Mkuu!
Hapo hakuna cha Uke wala nini? Acha wamtandike mpaka atie akili mu-kichwa! Kwani alilazimishwa na nani kuwa Supika? Kila siku akinamama wanaimba wanawake tunaweza, sasa atudhihirishie hilo kwa vitendo (ingawa ameshashindwa tayari), si ameshawezeshwa kuwa Spika kazi ni kwake!!
Hakuna kitu kibaya kama kuvaa kiatu cha mtangulizi wako halafu kikakupwaya kiasi kile yaani ni aibu! Nilimwona mzee wa standards and speed akicheki kwa pembeni mama anavyosulubiwa!! Yaani kama kuna kuombwa apewe tena awamu ijayo naamini ataitema hiyo nafasi. Wote wamepwaya vibaya.
Hapo hakuna cha Uke wala nini? Acha wamtandike mpaka atie akili mu-kichwa! Kwani alilazimishwa na nani kuwa Supika? Kila siku akinamama wanaimba wanawake tunaweza, sasa atudhihirishie hilo kwa vitendo (ingawa ameshashindwa tayari), si ameshawezeshwa kuwa Spika kazi ni kwake!!
Hakuna kitu kibaya kama kuvaa kiatu cha mtangulizi wako halafu kikakupwaya kiasi kile yaani ni aibu! Nilimwona mzee wa standards and speed akicheki kwa pembeni mama anavyosulubiwa!! Yaani kama kuna kuombwa apewe tena awamu ijayo naamini ataitema hiyo nafasi. Wote wamepwaya vibaya.
Wanabodi,
Leo nimepata fursa ya kuliangalia bunge live asubuhi hii kupitia TBC-1,
Spika wa Bunge, Mhe. Anne Makinda ameshindwa kabisa kuliendesha bunge!, amepwaya sana na ameendesha kika bila confidence kabisa na mwisho wa maelezo yake, akamtaja Mhe. Tundu Lissu kama ndiye mbunge anayeongoza kwa kuleta vurugu bungeni, na Lissu aliponyanyuka kuomba muongozo wa Spika, akamvurumishia tena Spika Makombora mazito, na kama angeendela kidogo tuu!, Spika Makinda ange break down kwa machozi!. (Naamini akifika ofisini kwake, atajifungia kidogo na kuimalizia hasira yake the same way wanawake wote wanamalizaga hasira zao!.
Kwa kuzingatia sifa kuu iliyomfanya Mhe. Mama Makinda kuchaguliwa kuwa spika, huku Mhe. Tundu Lissu akiujua fika uwezo wa Madam Spika, kwanini anaendelea kumsulubisha kila apatapo fursa?!. This is not fair!.
Kwa vile Mama Makinda amepewa uspika because she is a lady, kwa uzi huu, namuomba Mhe. Tundu Lissu na wabunge wengine wa Kambi ya Upinzani, wanapokuwa na hoja za msingi, wamuaddress Madam Spika with courtesy of addressing a lady, ili ku restore confidence yake kuliendesha bunge ambapo kwa sasa, ameshindwa kabisa, amezuia hoja zote binafsi, hivyo leo bunge limekutana asubuhi tuu kwa kipindi cha maswali na majibu na kuahirishwa, natumaini kesho na keshokutwa itakuwa vivyo hivyo!, huu ni ufujaji bure wa rasilimali za Taifa!.
Nawauliza wajameni, hivi hiki anachofanya Mhe. Lissu na wabunge wengine wa upinzani, kumsubulu Madam Spika ambaye ni mwanamke bila huruma, ni sawa kweli?!.
Kiafrika, wanawanake ni ni watu wa kubembelezwa na kuonewa huruma!, hivi hawa wabunge wa upinzani ni watu wa aina gani wasio hata na huruma kwa wanawake?!, leo ilibakia kidogo tuu madam spika angelia!, jee hiki wanachofanya ni sawa kweli?!. Ni haki?!.
Nawaombeni tumtendee haki Spika wetu aendesha bunge kwa haki na kujiamini!.
Pasco.