Mi natoa ONYO: Kuna Member wa Humu JF ana mahusiano na mchumba wangu. Tusije Kulaumiana Bure

Mi natoa ONYO: Kuna Member wa Humu JF ana mahusiano na mchumba wangu. Tusije Kulaumiana Bure

Wewe umesema upo na huyo mchumba wako huu ni mwezi wa tano sasa inakuwaje unasema ulimsomesha chuo akamaliza???? Muongo wewe sema ushampenda mschana wa humu JF ila unasikia wivu alivyo karibu na member mwingine
 
nashukuru ndugu yangu wewe mwenzangu kitandani upo vizuri. sisi ambao hatupo vizuri huwa hatuna maneno mengi na ndo maana nasema kwa mhusika mimi simkatazi.ila natoa hili kwake kama onyo.... ili siku akija kupatwa na lolote asije sema hakuambiwa. mwaka jana kuna threads ilianzishwa humu kuzungumzia tukio ambalo nililifanya kwa mtu mwaka 2015. sisi wanaume wapole mara nyingi wanawake hutuona kama mazoba . mimi sina nguvu za kupigana. lakini najua tu kuwa siwezi shindwa kabisa kumpa adhabu mtu ambaye amenitesa moyo wangu. inawezekana nikawa napiga biti na hamna madhara ila mhusika nadhan atakuwa amesoma huu ujumbe. anaweza kuendelea au kuacha.
Ina maana 2015 ulikuwa na demu mwingine???? Maana huyu umesema mwenyewe uko nae sasa mwezi wa tano!!!!!! Hata wewe ni muhuni tu kubali hivyo!!!
 
Hii story ya kutunga au jamaa alivyo kuwa anaandika alikuwa kajawa na hasira.....

Kwanza amesema yupo na Mchumba wake huyo sasa ni miezi 5 ..........
Sehem nyingine anasema Mchumba wake huyo muda mwingi yupo nyumbani kwani alisha maliza chuo miaka 2 iliyo pita.............
Sehem nyingine anasema ametumia gharama nyingi kumsaidia kwenye Elimu yake.

Kwahiyo kuwa na Mchumba kwa Miezi 5 unaweza fanya yote hayo.
 
mi nipo tayari kuachana naye ... na gharama zangu ningependa zirudishwe...najua hazitarudishwa direct ila zitarudishwa kwa njia nyingine....kabisa hata kama si mimi nitakayepokea hizo pesa....ila zitarudishwa tu. wanawake nao sometime wengine wana udhaifu wao ambao wanaume kadhaa huutumia kwa faida yao. mi nasikitikia tu gharama zangu sababu kabis anlimwambia huyo dada kama hana nia ya kuwa nami aseme ili nisipoteze muda ...akanambia ananipenda na yupo tayari kuishi nami.kazi zangu ni za kusafiri safiri sana sometime nakuwa mbali hata kwa miezi miwili au zaidi lakini ni katika kutafuta pesa. so nitamwacha ila nitakayemwachia atalipa muda na pesa zangu.... sitomwacha salama.
Usijidanganye!!!! Gharama haziwezi kulipwa hata mahakamani utaulizwa UNADAI GHARAMA JE ULIOA, ONYESHA CHETI CHA NDOA" Kama huna wewe ni sawa na watu wanaohonga pesa michepuko huko nje ambapo ukitoa sahau kurudishiwa.
 
nashukuru ndugu yangu wewe mwenzangu kitandani upo vizuri. sisi ambao hatupo vizuri huwa hatuna maneno mengi na ndo maana nasema kwa mhusika mimi simkatazi.ila natoa hili kwake kama onyo.... ili siku akija kupatwa na lolote asije sema hakuambiwa. mwaka jana kuna threads ilianzishwa humu kuzungumzia tukio ambalo nililifanya kwa mtu mwaka 2015. sisi wanaume wapole mara nyingi wanawake hutuona kama mazoba . mimi sina nguvu za kupigana. lakini najua tu kuwa siwezi shindwa kabisa kumpa adhabu mtu ambaye amenitesa moyo wangu. inawezekana nikawa napiga biti na hamna madhara ila mhusika nadhan atakuwa amesoma huu ujumbe. anaweza kuendelea au kuacha.
acha kulialia sasa unaishi na malaya hapo unapaswa ujue
 
nmegundua nyie watu mnaniombea mabaya sana..hamwoni kwua sasa ndo mnampa uthibitisho kabisa????????????????????????? nmewakosea nini mimi jamani mpaka mnaniombea mabaya hivi.......................
Anayeshikwa na ngozi ndio mla nyama sikuzote. Wanakuhisi wewe maana ndio bingwa wa kuleta story za kipuuzi na matusi. Lazima utakuwa wewe na utakoma ubishi ngoja akutie mikononi mwake.
 
Mkuu hapo huna mchumba. Piga chini tafuta mwingine coz mchumba anayecheka cheka kwenye social media sio mchumba huyo ni kahaba tu.Miez 5 imetosha kabisa kujua huyo sio mwanamke hafai. Piga Windows chini
Hawezi kukuelewa kushtaki tu anaashiria kafa kaoza sioni sababu ya kumlaumu mshikaji na dem wako unae
 
Ninavoina mimi mtoa mada wa uzi huu alikuwa anataka kupiga soga tu maana sijaona hoja zenye mashiko kwa kumtishia huyu anaemsumbua mwenza wako.
Watoto wa mtaani wanasema demu kama bahari we ukilinda KIGAMBONI wenzio BEACH KOKO wanogelea.


viWaNdA
 
Pole sana mkuu,haya mambo ya mahusiano ukikosea kuchagua utaumia sana,Anyway naamini huyo mchumba wako ndio anamakosa kama anajua ana mtu wake kwa nini ajilegeze na kujilengesha kwa mwanaume mwingine? Kama kweli unaushahidi wa kutosha nakushauri mpige chini huyo uendelee na maisha yako.
 
Unazunguka mbuyu wakati njia iko wazi!
Mwaga mchele kuku wapate chakula chao.
Na inaonesha hujiamini
Umesema umemsomesha chuo kwa kumlipia mpaka tuition fee wakati uchumba wenu una miezi 5 how comes??
Au kipindi unamsomesha chuo alikua Dada yako baada ya kumaliza chuo ndio amekua mchumba?
Since amemaliza chuo huu ni mwaka wa pili na nyinyi uchumba wenu una miezi mi5 huoni kama kuwa na jamaa mwingine ni very possible?
Bed performance is very important for strong relationship!
 
Mkuu, kama ni kweli uyasemayo naomba nikushauri jambo kitaalamu, huyu mwanamke sio mke na nikwambie tu mshukuru Mungu wako, ujue watu wengi huumia kwa kutokukubaliana na hali, hii imegawanyika sehemu nyingi, kuna watu the way walivyo ni kutokana na ubishi wa kutokukubali hata kama akiambiwa ukweli, kwa jumla huyo unaedai mchumba wako ni malaya wa kutupwa, tena muogope kama ukoma. Maana ikiwa hutakubali kuwa umeshapoteza mapema basi jiandae kujinyonga kama sio kufa kwa pressure, pesa inatafutwa, ila furaha ya moyo haiuzwi popote, ni kweli ulimhudumia lkn waweza pia kumlisha mbwa wako mwenyewe na siku akakudhuru pia, haya yapo, mapenzi ndivyo yalivyo wala usione kama ni jipya kwako. Ikiwa mwanamke wako ana udhubutu wa kumwambia mtu eti nimeloa, dah. Halafu wanawake kuweni makini, huu mtindo wa watu kujifanya wanajua mapenzi ni storry tu kama za kina shigongo, wengi mnapotea na kuvunja ndoa zenu pasipo kujielewa, iweni na maarifa ili msiangamie.
Jamaa kashindwa kabisa kuelewa kama kapata bahati mbaya

Yani agungwe kwa kuchekeshwa tu bado unamganda???
 
Back
Top Bottom