Miaka 63 baba mdogo hajawahi kurudi nyumbani

Miaka 63 baba mdogo hajawahi kurudi nyumbani

Siwajui ndugu wa upande wa mama,sujawahi hata kuona

mama ni mzaliwa Wa shinyanga,aliolewa na baba miaka ya 1986. Walitengena na family baada ya kuolewa wakahama na mkoa

Tangu 1986 hadi Leo 2020 mama hakuwahi kurudi nyumbani kwao

Natamani sana siku moja niwaone ndugu zangu upande Wa mama angalau hata mmoja tu lakini ilishashindika kabisa

Tafadhali kama kuna msaada mnaweza nisaidia niwapate hata mmoja

Muda mwingine nikikutana na mtu alitokea shinyanya huwa namchulia kama ndugu yangu.
Mama jina lake anaitwa Modesta misalaba, aliolewa kwenye ukoo Wa maganiko
 
Ndugu zako ni ndugu zako tu.
Ni kweli ila kuna ndugu wanapotea kutafuta maisha wakienda sehemu kama alikuwa na jina la asili linabadilishwa anaanza maisha upya...kama alikuwa mhaya akaenda Unyirambani ataitwa jina la utani la kinyiramba (kama vile mvamizi,mkosa makazi,mkosa kwao,mzururaji ila wanamuita kwa kilugha) anazaa huko watoto atawaita majina ambay sio relatives(kinship) yaani ya ukoo...hapo tena inakuwa ngumu kumpata.
 
Katika familia kuna siri nyingi sana ambazo unaweza usizijue na ukadhani aliyeondoka ni mjinga na hajielewi. Familia nyingi duniani ni za kijinga na kipuuzi sana, zimejaa chuki, khusda, mauaji ya kichawi, kuharibiana nyota n.k. wengi huondoka na wasirudi tena na haijaanzia leo ni tangu kuja kwa mwanadamu.....jambo pekee ni kumuamini Mungu pekee na sio hao wazazi, ndugu au rafiki kwani nao hao ni binadamu na wanayo mapungufu yao kibao.
Binafsi naishi Mkoa tofauti na sifikirii si tu kurudi bali hata kupata Mke kutoka eneo hilo maana hilo eneo kwangu ni hatari, kwasasa narudi kwakuwa mmoja wa walionizaa yupo hai na si vinginevyo.
Binadamu ukiwaweka sana kichwani mambo yako hayaendi, utalost, na mbaya zaidi ukisimamia future yao na yako mtalost nyote maana kuna wengine ni masikio ya kufa na umasikini.
Kijana amka na upambane na uache imani kuwa zipo dawa utafanya kumrudisha ndugu aliyepotea home muwe nae, zaidi mutamsema kuwa kala maisha na hakuwajali.... jitahidini mfanye yenu na yake muachieni Mungu kwani uliyeandika huu uzi hauwezi kujua hao unaoita nduguzo ulionao hapo home walimfanyia jambo gani huyo Mzee.. maybe walitaka kumuua, kumuweka msukule, kumharibia kwa namna yoyote ile, jitahidi uwafahamu binadamu.....itakusaidia sana pale watakapokufanyia mambo ya hovyo.
USIMWAMINI HUYO ULIYEKAA NAYE KARIBU YAWEZEKANA ANAKUFICHA UKWELI WA HILI ULILOLIANDIKA HAPA, SIKU UKIJUA UKWELI UTAMCHUKIA NA KUMSIFU SHUJAA ALIEKIMBIA TANGU 1957
Ndo maaan nimesema maisha ya utafutaji yana maana pana...n kweli kuna watu wanaenda kutafuta maisha sehemu tofauti kwa sababu tofauti ...na ukuchulia huyo ba mkubwa aliondoka 1957 enzi hata hatupata uhuru...uchawi...ushirikina dhuruma na chuki nje nje .hatuwez jua labda utafutaji tu wa kawaida na maisha kumpiga asiwez rudi ...sisi jirani yetu pia aliondoka kwenda mbeya alimaliza miaka 30 anadai alikuwa mgodini lakn hapati akaanza kulima mahindi anapata ila kipindi hicho akiuza anajikuta nauli haifiki kutoka na bei kuwa chee..alikuja mwishoni mwa miaka ya 2000 hivi na tyr alishapata HIV plus TB.
 
Kuna jamaa alizamia ( wale wa kitambo mnajua hii mambo) tukajua yupo mtoni (Ulaya)..akarudi baada ya miaka 20...kumbe miaka yote hiyo yupo Pwani ya Mombasa....akarudi age imesonga,na maisha yamempiga...
Yani huwa wanapikiga hadi mnasema jamaa walimgeuza ndondocha nini ?
 
Watu wanapigwa tunguli hadi wanasahau kwao.
Wanawake ni shiiida!
Hahahaaa...ila ukienda ugenini kuna akili fulani unasahau nyumban unakuwa kama fala fala flani ...usipoangalia dishi linayumba....na network ikate...manake ukienda ugenini bila hesabu unaweza kujikuta wewe ndo uwe houseboy ..utatumwa hadi condom na wenyeji hata kama ni wadogo
 
Kuna mama family friend wetu alimtumaga mwanae wa kwanza wa kiume dukani late 1970s mpaka leo hajarudi, huyo mtoto alikua hajafika miaka 10, walimtafutaga kila mahali hawakumwona, mpaka miaka ya mwanzoni mwa 2000s walikua Bado wanamuulizia na walikua wanaamini ipo siku watamwona
IPO siku atarudi sema watafutaji napo wakienda ugenini dish linakata network....Tz hii ni ndogo lakni kutokana na miundombinu ya mawasiliano ndugu yako akipotea kumpata ni shida..Nimesema Tz n ndogo kwa minajili kwamba kuna nchi zinaizid Tz mara 6 lkn kumpata mtu ni rahis...
 
Kaka yangu ambaye ni mzaliwa wa kwanza aliondoka nyumbani tarehe 22/9/1970 akiwa na umri wa miaka 20 akakaa Mwanza mjini kwa muda wa miaka 18 mfululizo bila kurudi nyumbani Geita vijijini. Hata baba alipofariki mwaka 1979 hakuhudhuria mazishi. Tarehe 1/9/1988 ndipo akaja nyumbani kwangu na kuniomba nimpeleke nyumbani. Nikampeleka tarehe 3/9/1988 akuwa na umri wa miaka 38. Hadi leo hajaondoka nyumbani.
 
Kaka yangu ambaye ni mzaliwa wa kwanza aliondoka nyumbani tarehe 22/9/1970 akiwa na umri wa miaka 20 akakaa Mwanza mjini kwa muda wa miaka 18 mfululizo bila kurudi nyumbani Geita vijijini. Hata baba alipofariki mwaka 1979 hakuhudhuria mazishi. Tarehe 1/9/1988 ndipo akaja nyumbani kwangu na kuniomba nimpeleke nyumbani. Nikampeleka tarehe 3/9/1988 akuwa na umri wa miaka 38. Hadi leo hajaondoka nyumbani.
Hongereni sana
 
Unajua huwa najiulizaga sana wewe ni mtu wa namna gani..Yaani kila tukio lazma liwe lishawahi kukupata, kila Aina ya biashara umefanya, majanga yote yamekugusa na ushuhuda unatoa, kila ishu ikizungumzia unaijua kasoro siasa tu ndio sikuoni.

Aisee wengine mmebarikiwa sana
Siasa nimeacha rasmi mwaka huu huu!
Jingine?
 
Kaka yangu ambaye ni mzaliwa wa kwanza aliondoka nyumbani tarehe 22/9/1970 akiwa na umri wa miaka 20 akakaa Mwanza mjini kwa muda wa miaka 18 mfululizo bila kurudi nyumbani Geita vijijini. Hata baba alipofariki mwaka 1979 hakuhudhuria mazishi. Tarehe 1/9/1988 ndipo akaja nyumbani kwangu na kuniomba nimpeleke nyumbani. Nikampeleka tarehe 3/9/1988 akuwa na umri wa miaka 38. Hadi leo hajaondoka nyumbani.
Kama kawaida yenu wasukuma kutotoka hom🤭
 
Siwajui ndugu wa upande wa mama,sujawahi hata kuona

mama ni mzaliwa Wa shinyanga,aliolewa na baba miaka ya 1986. Walitengena na family baada ya kuolewa wakahama na mkoa

Tangu 1986 hadi Leo 2020 mama hakuwahi kurudi nyumbani kwao

Natamani sana siku moja niwaone ndugu zangu upande Wa mama angalau hata mmoja tu lakini ilishashindika kabisa

Tafadhali kama kuna msaada mnaweza nisaidia niwapate hata mmoja

Muda mwingine nikikutana na mtu alitokea shinyanya huwa namchulia kama ndugu yangu.
Mama jina lake anaitwa Modesta misalaba, aliolewa kwenye ukoo Wa maganiko
Ukimwambia aende kwao kusalimu anasemaje sasa? Kwa hiyo Hana hata mawasiliano na nyumbani?
 
Siwajui ndugu wa upande wa mama,sujawahi hata kuona

mama ni mzaliwa Wa shinyanga,aliolewa na baba miaka ya 1986. Walitengena na family baada ya kuolewa wakahama na mkoa

Tangu 1986 hadi Leo 2020 mama hakuwahi kurudi nyumbani kwao

Natamani sana siku moja niwaone ndugu zangu upande Wa mama angalau hata mmoja tu lakini ilishashindika kabisa

Tafadhali kama kuna msaada mnaweza nisaidia niwapate hata mmoja

Muda mwingine nikikutana na mtu alitokea shinyanya huwa namchulia kama ndugu yangu.
Mama jina lake anaitwa Modesta misalaba, aliolewa kwenye ukoo Wa maganiko

Samahani akili za usingiz hizi bado...wewe alikuacha kwa Bibi au?
 
Nna bamdogo wangu tangu miaka ya 1990 hadi leo hajawai kurudi, baba yake kafariki hakuonekana na inasemekana yupo ndani ya jiji la makonda anakula maisha.
Kilichomkimbiza nyumbani miaka hiyo ni kesi ya wizi baada ya vijana mtaani kukamatwa na kuwekwa lock up. Alipowekewa dhamana akatoka ndio akatoroka jumla hadi leo hatujawai muona na kesi ilishaisha lakini bado hataki kujitokeza.
 
Nna bamdogo wangu tangu miaka ya 1990 hadi leo hajawai kurudi, baba yake kafariki hakuonekana na inasemekana yupo ndani ya jiji la makonda anakula maisha.
Kilichomkimbiza nyumbani miaka hiyo ni kesi ya wizi baada ya vijana mtaani kukamatwa na kuwekwa lock up. Alipowekewa dhamana akatoka ndio akatoroka jumla hadi leo hatujawai muona na kesi ilishaisha lakini bado hataki kujitokeza.
Kesi huwa haishi sema maafande ndo walishahama....ila kama ni wizi tu automatic ilishaisha...mtafuteni asije akawa teja huko Dar.
 
Back
Top Bottom