Midahalo hata irudiwe mara kumi, kiufundi Trump hataweza kumshinda Harris katika mdahalo!

Midahalo hata irudiwe mara kumi, kiufundi Trump hataweza kumshinda Harris katika mdahalo!

Kwa ulichokiandika, nadhani hii mada ni nzito sana kwako. Kwa nia njema sana nakushauru, jaribu kwanza kuufuatilia uchaguzi wa USA, ukiweza kapitie Youtube hii Debate ya kuamkia leo, kisha utakuja kuandika kitu kikubwa sana hapa JF na sote tutakuelewa vizuri sana.

Kwa kukusaidia tu, Trump amepanga kuinyoosha vizuri Africa na kuibeba USA tu. Hivyo ushindi wowote wa Trump unaweza kuja kuwa ni kilio kikubwa sana kwa Afrika.
Wewe ndio unaijua siasa kuliko wengine.
Ukweli mchungu hah! He is right, America First.
Akitaka kudeal na Africa iwe Asia so be it! Acha atunyooshe tu.
 
  • Thanks
Reactions: I M
Haina shida! Kika mmoja ameshinda kwenye eneo alilo na uwezo nalo:
1. Mdahalo - Harris
2. Urais - Trump
Ngumu sana mzee wa miaka 70+ kumshinda mwanasheria wa calibre ya kamala,hakupewa ile ofisi ya umma kwa upendeleo bali merit,sikuangalia mdahalo lakini kama takwimu za uchumi wa biden ni bora kuliko trump basi sidhani kama trump alikua na hoja,by the way taarifa zinadai wamarekani wengi wameona kamala kashinda mdahalo
 
Mdahalo wa kwanza baina ya Donald Trump na Kamala Harris katika kinyang'anyiro cha urais wa USA umefanyika usiku wa kuamkia leo huko marekani, baadhi yetu tulifanikiwa kuufatilia kwa kina katika kujifunza nk.

Mbali na sera za wagombea kuna vitu vingi mnoo huangaliwa katika midahalo hiyo ili kuwavutia wamerekani wengi ili kuja kuwapigia kura hao wagombea.

Haya machache nitaweka hapa kuhusu mambo ya kiufundi katika mdahalo. Tukianza na upande wa Trump, mtindo wake wa kulumbana katika midahalo ni ule ule, ni mwendo wa kuporomosha mashambulizi mazito dhidi ya mpinzani wake na kusema lolote lile ilimradi litambeba katika mbio zake za urais. Na ndicho hicho hicho alikifanya tena katika mdahalo huo. Ni mtindo wa wanasiasa katika kusaka kura kishabiki. Bahati mbaya sana waendesha mdahalo walikuwa makini na wakali kwake, mara kadhaa walimuonya au kumrekebisha.

Upande wa Kamala Harris alikuja na mtindo wa kujibu mashambulizi papo hapo, kupeleka mashambulizi ya kimkakati kwa ujanja na kusukuma sera zake mbele kwa haraka. Huu ni mtindo wa wanasheria mahiri hupenda kuutumia wakiwa mahakamani.

Kwa kifupi sana mdahalo ule umefanikiwa zaidi kumtambulisha zaidi Kamala Harris kama mgombea urais wa namna gani mbele ya wamerekani. Kwa haraka haraka unaweza ukahisi mdahalo ule uliandaliwa na Democrat ili kumpa jukwaa Kamala Harris.

Kwa style hii ya leo, hata midahalo ikarudiwa mara kumi tena huenda Kamala Harris akaonekana anabebwa au midahalo inambeba.
Duh!!
Kwa hiyo kwako Kamala ndiye mshindi? Mtu aliyekuwa akiulizwa swali analikwepa swali na kuanza kuingelea ambayo hakuulizwa?
Au unafikiri Kamala na timu yake ni wajinga kwa kuimba mdaharo mwingine ?
 
Hisia zako kuhusu upendeleo kwa uhakika zimetokana na namna Kamala Harris alivyomudu mjadala mzima na kwa jinsi Trump alivyohenyeshwa pasipo kutegemea. Na hii ni kwa sababu moja kuu, mwanamama ni mahiri mnoo kwenye hiyo mijadala ya one to one, fuatilia hayo hata uchaguzi uliopita alivyoweza kumbeba Biden kupitia hizo Debate.

Ndio maana nakwambia, hiyo mijadala ikirudiwa hata mara kumi,n huenda Trump hataweza kutoboa mbele
 
CCM wakisikia midahako ya wagombea Urais inavyofanyika Duniani - wanakwazika mno.
Wao ni mambo ya giza kwa giza - funika kombe.
 
Ngumu sana mzee wa miaka 70+ kumshinda mwanasheria wa calibre ya kamala,hakupewa ile ofisi ya umma kwa upendeleo bali merit,sikuangalia mdahalo lakini kama takwimu za uchumi wa biden ni bora kuliko trump basi sidhani kama trump alikua na hoja,by the way taarifa zinadai wamarekani wengi wameona kamala kashinda mdahalo
Mbina kamshinda? Hao wamatekani wengi ni wakina nani? Unajua hata maistream medias zote pamija na kumbbackup Kamala na Democrat lakini wana report kiuiaiasi na kinazi sana.
Hata ule Mdaharo wa Trump na Biden those maistream zili report pia kwamba Biden amemshinda Trump
 
Duh!!
Kwa hiyo kwako Kamala ndiye mshindi? Mtu aliyekuwa akiulizwa swali analikwepa swali na kuanza kuingelea ambayo hakuulizwa?
Au unafikiri Kamala na timu yake ni wajinga kwa kuimba mdaharo mwingine ?
Kamala anajaribu kujipambanua kupitia midaharo na hiyo hiyo midaharo ndo itamuangusha
 
Kumbe na humu Kuna wamarekani wa Bunju na pugu kajiungeni na hamsemi?

Haya wamarekani sifa mnazo za kuchagua Kamala wenu ama trump?
 
Hata kama Trump ana attack kwenye midahalo lakini anazungumza ukweli kuhusiana na Marekani kiuchumi,kisiasa,kijeshi!
 
Wamarekani weusi wa Buguruni tujuane hapa jukwaani.
 
Clinton alimshinda Trump kwa kura za wananchi. Ila kundi la watu wasiozidi 300 wakampitisha Trump.

Rais wa Marekani eshajulikna hata kabla ya kura kupigwa
Hapana. Hauko sahihi.

Watu wengi sana hamuelewi jinsi ambavyo Rais wa Marekani anavyochaguliwa.

Hao “watu wasiozidi 300” [btw, Trump alipata electoral votes 306] hawakujiamulia tu ‘wampe’ Trump urais.

Mgombea ni lazima ashinde statewide popular vote ili aweze kuzipata electoral college votes za jimbo.

Wingi wa kura za Clinton zilitokana na yeye kushinda kwa asilimia kubwa kwenye majimbo yenye watu wengi, mfano California na New York, lakini ikija kwenye idadi ya majimbo na electoral votes, hakushinda vya kutosha.

Kusema ukweli, ni mfumo rahisi sana kuuelewa. Siyo rocket science kabisa.

Ila pengine labda Watanzania wengi wana vichwa vigumu tu vya kuelewa hata mambo yaliyo marahisi.

Halafu Trump wala hakuwa wa kwanza kushindwa national popular vote lakini akashinda electoral college votes.

Hiyo ilishatokea kuanzia miaka ya 1800 huko. Ni kiasi cha kujifunza tu.

Halafu kuna scenario ingine ambayo wengi hamuijui.

Jumla ya electoral college votes ni 538.

538 ukiigawanya kwa mbili unapata 269.

Ili mgombea ashinde, anahitaji kupata 270.

Sasa ikitokea wagombea wote wawili wanapata 269, hapo inakuwaje?

Jibu nalijua. Ila naamini wabongo wengi hawajui hata kuwa scenario kama hiyo inaweza kutokea.
 
Mbina kamshinda? Hao wamatekani wengi ni wakina nani? Unajua hata maistream medias zote pamija na kumbbackup Kamala na Democrat lakini wana report kiuiaiasi na kinazi sana.
Hata ule Mdaharo wa Trump na Biden those maistream zili report pia kwamba Biden amemshinda Trump
Nimesikia dw,kura za maoni baada ya mdahalo,hata trump ana main stream media zake
 
Babu tr

Babu trump leo amepuyanga...kama umeangalia mdahalo Live unaweza kuona kabisa pumzi Hana ila anachojua yy ni kushambulia personality na uongozi wa Biden badqlq ya kuelezeq kwa kina sera zake...nn atakifanya kwa America hii anayosema Kila kitu kimevurugika...Kamala ni smart alikuwa mjanja kujibu mapigo, kumpondq Babu na kuelezq nn atqfanya iwapo atqchaguliwa...trump asikubali midahalo tena...asuburi uchaguzi maybe atqchaguliwa maana bdo kaupepo kqnavumq kwake....ila akizidi kukubali midahalo atqzidi kugaragazwa Kila siku
Ule mdahalo ulikuwa 3 v/s 1 na kiuhalisia Trump kashinda. Hata watangazaji walikuwa wakimuita "Mr. President" hoja za Kamala ni za kitoto sana. Angalia closing speech tu. Sentesi chache za Trump zitakuonyesha kila unalotaka kujua.
 
Nasikia Harris alivaa hereni zinafanana na speaker ndogo za wireless kumsaidia kwenye kujibu maswali.
 
Nimesikia dw,kura za maoni baada ya mdahalo,hata trump ana main stream media zake
Mainstream media za west, including Ulaya hakuna zinazom support Trump.
Trump alipopigwa risasi, CNN waliirusha ile habari na kusema "Trump aanguka Jukwaani"
Hapo unaweza ukapima kiwango cha chuki.

Medias zinazom support Trump wala siyo mainstream, wakina "Daily wire" siyo mainstream.
Maistream inayooneksna kum support Trump ni ile ya Australia iitwayo ABC News, sasa hivi inafuatiliwa sana na Wamerekani sababu ndiyo pekee ambao wana report habari za Trump kama zilivyokusudiwa ja kuacha audience ndiyo iamue. Hata hiyo aaabC News siyo kwamba inam support bali ina report ukweli bila kuupotosha au kupendelea popote. Hata Trump alivyopigwa risasi, ABC ndiyo ili report tukio lile kwa usahihi huku wakihoji watu waliokuwa eneo la tukio wakati wakina CNN, Fox News Bloomberg, na wengineo wao waki report mitazamo yao na hisia zao kujaribu kuonyesha Trump ndiye wa kulaumiwa kwa tukio kama lile kutokea US.
 
Mainstream media za west, including Ulaya hakuna zinazom support Trump.
Trump alipopigwa risasi, CNN waliirusha ile habari na kusema "Trump aanguka Jukwaani"
Hapo unaweza ukapima kiwango cha chuki.

Medias zinazom support Trump wala siyo mainstream, wakina "Daily wire" siyo mainstream.
Maistream inayooneksna kum support Trump ni ile ya Australia iitwayo ABC News, sasa hivi inafuatiliwa sana na Wamerekani sababu ndiyo pekee ambao wana report habari za Trump kama zilivyokusudiwa ja kuacha audience ndiyo iamue. Hata hiyo aaabC News siyo kwamba inam support bali ina report ukweli bila kuupotosha au kupendelea popote. Hata Trump alivyopigwa risasi, ABC ndiyo ili report tukio lile kwa usahihi huku wakihoji watu waliokuwa eneo la tukio wakati wakina CNN, Fox News Bloomberg, na wengineo wao waki report mitazamo yao na hisia zao kujaribu kuonyesha Trump ndiye wa kulaumiwa kwa tukio kama lile kutokea US.
Nyt,wsj, bloomberg nk ni pro trump,acha ngendembwe
 
Back
Top Bottom