Miili 6 ya familia moja iliyouawa Kigoma inaweza kufukuliwa, mtoto aliyefariki maziko yake yasitishwa

Miili 6 ya familia moja iliyouawa Kigoma inaweza kufukuliwa, mtoto aliyefariki maziko yake yasitishwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma limezuia maziko ya James Januari (4) aliyejeruhiwa usiku wa kuamkia Jumapili na kufariki dunia Julai 5, 2022 katika Hospitali ya Rufaa Morogoro.

Aidha, kuna uwezekano wa kufukua miili sita iliyozikwa Jumapili Julai 3, 2022 baada ya tukio la mauaji ya watu sita wa familia moja kwenye Kijiji cha Kiganza Mkoani Kigoma.

Akizungumza katika shughuli ambayo ilitakiwa kuwa ya maziko yam toto huyo, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ester Alexander Mahawe alitoa kauli ya kuahirisha maziko hayo na kusema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi.

“Mkemia Mkuu wa Serikali yupo Kigoma, wanahitaji kukamilisha ushahidi wa damu ya mtoto James na wale sita waliozikwa pia miili yao inaweza kufukuliwa kwa ajili ya kuchukua sample ya damu ili ushahidi usije ukapelea. Baada yah apo kama hakutakuwa na mabadiliko miili yote saba inaweza kuhifadhiwa.”

Tayari Jeshi la Polisi limeshatangaza kumkamata Peter Moris (33), Mkazi wa Mlole Manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye ni fundi ujenzi akituhumiwa kwa mauaji hayo yaliyotokea usiku wa kuamkia Julai 3, 2022

Mkuu wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Tanzania, Kamishna Liberatus Sabas alinukuliwa akisema: “Tumemkamata akiwa Kigoma, tumejiridhisha mtuhumiwa ametekeleza mauaji hayo peke yake kwa kutumia panga na kwamba baada ya kumhoji amedai sababu ni marehemu January Mussa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mke wake (mtuhumiwa).”


Chanzo: Azam TV
 
Itoshe kusema bara wanaume wengi ni malimbukeni wa mapenzi.
Unaua watu saba wasiohusika kwa sababu mke wako ameliwa??!
Wakati mwingine ni ushahidi unatengenezwa ili kuridhisha mamlaka na wananchi. Ingawa yote pia yanawezekana.
 
Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma limezuia maziko ya James Januari (4) aliyejeruhiwa usiku wa kuamkia Jumapili na kufariki dunia Julai 5, 2022 katika Hospitali ya Rufaa Morogoro.

Aidha, kuna uwezekano wa kufukua miili sita iliyozikwa Jumapili Julai 3, 2022 baada ya tukio la mauaji ya watu sita wa familia moja kwenye Kijiji cha Kiganza Mkoani Kigoma.

Akizungumza katika shughuli ambayo ilitakiwa kuwa ya maziko yam toto huyo, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ester Alexander Mahawe alitoa kauli ya kuahirisha maziko hayo na kusema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi.

“Mkemia Mkuu wa Serikali yupo Kigoma, wanahitaji kukamilisha ushahidi wa damu ya mtoto James na wale sita waliozikwa pia miili yao inaweza kufukuliwa kwa ajili ya kuchukua sample ya damu ili ushahidi usije ukapelea. Baada yah apo kama hakutakuwa na mabadiliko miili yote saba inaweza kuhifadhiwa.”

Tayari Jeshi la Polisi limeshatangaza kumkamata Peter Moris (33), Mkazi wa Mlole Manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye ni fundi ujenzi akituhumiwa kwa mauaji hayo yaliyotokea usiku wa kuamkia Julai 3, 2022

Mkuu wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Tanzania, Kamishna Liberatus Sabas alinukuliwa akisema: “Tumemkamata akiwa Kigoma, tumejiridhisha mtuhumiwa ametekeleza mauaji hayo peke yake kwa kutumia panga na kwamba baada ya kumhoji amedai sababu ni marehemu January Mussa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mke wake (mtuhumiwa).”


Chanzo: Azam TV
Sijapata maelezo kamili kuhusu hii issue zaidi ya kusoma headlines, lakini how comes mtu mmoja anaweza kuua watu 6 peke yake? Au wengi walikuwa ni watoto? How comes uue family nzima iwapo mbaya wako ni mmoja tu? Why unaenda mpaka kujeruhi mtoto wa 4 years? Anajua nini kuhusu huo ugomvi wenu?

Kama amekiri huyo ni wa kula kitanzi tu
 
yani unless aliwapulizia dawa za usingizi ilaa hawezi kutekeleza huu unyama mwenyewe kamwe..
 
Itoshe kusema bara wanaume wengi ni malimbukeni wa mapenzi.
Unaua watu saba wasiohusika kwa sababu mke wako ameliwa??!
Wa Pwani si mnapandana hovyo kama mbwa? Biashara ya mafiga 3 sio?
Bara ujiandae kuliwa mkei kabla hujakatwa shingo.
 
Inasikitisha sana... Kisa Nyuchi uende kuua familia nzima...
 
Sijapata maelezo kamili kuhusu hii issue zaidi ya kusoma headlines, lakini how comes mtu mmoja anaweza kuua watu 6 peke yake? Au wengi walikuwa ni watoto? How comes uue family nzima iwapo mbaya wako ni mmoja tu? Why unaenda mpaka kujeruhi mtoto wa 4 years? Anajua nini kuhusu huo ugomvi wenu?

Kama amekiri huyo ni wa kula kitanzi tu
Ni rahisi sana ukiwa nje ya box kuuliza haya maswali. Umjui shetani wewe kikubwa ni kimkaribia Mungu tu na kumpinga shetani naye atakimbia ila vinginevyo waweza kuuwa kwa deni la tsh 100 tu
 
Ni rahisi sana ukiwa nje ya box kuuliza haya maswali. Umjui shetani wewe kikubwa ni kimkaribia Mungu tu na kumpinga shetani naye atakimbia ila vinginevyo waweza kuuwa kwa deni la tsh 100 tu
Namuamini Mungu na kila siku ninamuomba.
Ni rahisi sana ukiwa nje ya box kuuliza haya maswali. Umjui shetani wewe kikubwa ni kimkaribia Mungu tu na kumpinga shetani naye atakimbia ila vinginevyo waweza kuuwa kwa deni la tsh 100 tu
Huko ni kujiendekeza. Kila mtu ambaye amekosewa angekuwa anafanya hayo sijui kama kungekuwa na watu tunaandika himu JF. Hutakiwi kuua family eti kwa sababu kuna mtu katafuna mke wako. Kwanza jiulize kwa nini mke wako kakubali kugawa huko alikogawa.
 
Hii nchii aisee!! What's wrong!!!!??
 
Hii nchi always miracle,
Walipozika waliwaza nini?

Au huyo muuaji kasema jamaa alizaa na mkewe ndo wanajihakikishia.

Mtu mmoja anaua watu saba, yaani hata mmoja hakuweza kupiga kelele au na majirani walimpingia ?
Kabisa...inashangaza sana sasa hata specimen hawakuchukua?....
Mtu mmoja kauwa familia yote na hakuna kelele?..Aisee
Nchi ngumu sana hii....
 
Back
Top Bottom