Miji midogo midogo Tanzania ambayo ina vibe na fursa za kibiashara lakini haivumi

Miji midogo midogo Tanzania ambayo ina vibe na fursa za kibiashara lakini haivumi

Mwisho wa siku hii nchi sehemu zote zinafanana, ujinga ni ule ule kila mahali!
Labda kwenu ila Tanzania hii kuna sehemu ukipita unaona utofauti sana nilipita kule ubaruku Kwa zile mashine nilizoziona kweli kuna watu wako advanced na wanaelewa nini wanafanya
 
Mimi kwa experience yangu nliushobokea mji wa Katoro kwa story kama hizi za mji wenye fursa nikahama zangu dar, lengo lilikuwa ni kufanya biashara ya nafaka ila muda nilipofika ilikuwa nimepishana na msimu Yani alifika July na mavuno ni April sasa nikapata wazo la kufungua grocery maana huko kuna walevi dar ikasome.. nikachukua eneo pale stendi kuu ya Katoro maboresho kidogo nikatia mzigo.. kilichonikuta ni hatari japo nlifata ethics za biashara niliweka mademu weupe wenye msambwanda, mziki na chakula quality kabisa ila nilikutana na vimbweka sitasahau huo mji watu wanaroga saa moja jioni live bila chenga, mademu weupe wasukuma wanawaoa kwa gharama yoyote Yani bado wanakopesha plus wateja wakawa kama umeme wa TANESCO nikaona nirudi mjini huko wanaoweza kutusua ni wasukuma au wafanyabishara wa madini na wenye mitaji mikubwa ila milioni 5 kushuka chini unachoma pesa yako
 
Mimi kwa experience yangu nliushobokea mji wa Katoro kwa story kama hizi za mji wenye fursa nikahama zangu dar, lengo lilikuwa ni kufanya biashara ya nafaka ila muda nilipofika ilikuwa nimepishana na msimu Yani alifika July na mavuno ni April sasa nikapata wazo la kufungua grocery maana huko kuna walevi dar ikasome.. nikachukua eneo pale stendi kuu ya Katoro maboresho kidogo nikatia mzigo.. kilichonikuta ni hatari japo nlifata ethics za biashara niliweka mademu weupe wenye msambwanda, mziki na chakula quality kabisa ila nilikutana na vimbweka sitasahau huo mji watu wanaroga saa moja jioni live bila chenga, mademu weupe wasukuma wanawaoa kwa gharama yoyote Yani bado wanakopesha plus wateja wakawa kama umeme wa TANESCO nikaona nirudi mjini huko wanaoweza kutusua ni wasukuma au wafanyabishara wa madini na wenye mitaji mikubwa ila milioni 5 kushuka chini unachoma pesa yako
kwa nini ulienda bila kufanya na wewe utafiti wako kidogo
 
Wakuu,

Uzi huu ni kwa ajili ya kutaja miji midogomidogo ndani ya nchi yetu ambayo ina vibe kubwa kama miji mikubwa na ina fursa za kibiashara lakini haivumi wala kujulikana sana na watu.

Mimi naanza kama ifuatavyo:

1. MLOWO
Huu ni miongoni mwa miji midogomidogo inayokuwa kwa Kasi, ni Mji Mdogo unaopatikana Mkoa mpya wa Songwe, Wilaya ya Mbozi. Mji huu upo barabara kuu ya kutoka Mbeya Jiji kuelekea Tunduma. Ni Mji unaokua kwa kasi na unafursa ya kibiashara hasa mazao. Mji huu unazungukwa na vijiji vingii ambavyo wakazi wake wanajishughulisha na kilimo cha Mahindi, karanga, Maharagwe Alizeti, parachichi, kahawa n.k

Mji huu wa Mlowo una pacha/njia ya kuelekea miji mingine kama Kamsamba, Momba na Chunya. Pacha hii ndio pacha inayofika hadi kwenye Shamba kubwa la serikali la mahindi ambalo kwa sasa liko chini ya Wakala wa Mbegu wa Taifa(ASA).

2. MPEMBA
Huu pia ni Mji unaokua kwa kasi, upo mkoani Songwe Wilaya ya Tunduma, kilometers 10 kutoka Tunduma mji. Mji huu una fursa za kibiashara na Kilimo.

3. VWAWA
Hapa ndipo Makao makuu ya Mkoa wa Songwe ambapo kwa sasa Mkuu wa Mkoa huu ni Daniel Chongolo. Ni Mji unaokua kwa kasi kutokana na kusimikwa kwa huduma nyingi za kijamii zenye hadhi ya mkoa. Miaka michache Mji huu utaungana na Mji wa Mlowo kutokana na ukaribu bila kusahau mijengo mikali inayoendelea kuporomoshwa ndani ya Mji huu.
Karibu Vwawa.

4. NYANGAO
Ni Mji unaopatikana Kusini Mashariki mwa Tanzania ndani ya Mkoa wa Lindi, Wilaya ya Lindi DC. Mji huu mkongwe ambao wajerumani waliweka ngome yao hapa na kufanikiwa kujenga kanisa kubwa na Mission yao. Mbali na hilo wajerumani walijenga hospital kubwa sana ndani ya Mji huu(St Walburgus referral Hospital Nyangao).

Wakazi wengi wa Mji huu ni wakulima wa mazao kama Mahindi, mpunga, Alizeti, karanga na mazao ya biashara Kam Ufuta na Korosho, bila kusahau biashara za samaki/dagaa.. ambapo Mji huu umekuwa kama center ya biashara hii ambapo samaki/dagaa wengi wanaotoka bahari ya Kilwa na kuja Nyangao. Watu mbalimbali kutoka katika vijiji vilivyo karibu na Mji wa Nyangao wanakuja kujumua samaki/dagaa hapa.

Kitu lingine Cha kufahamu ni kuwa Mji huu upo mpakani kati ya Mkoa wa Lindi na Mtwara kutokea Masasi Town, Pia ni sehemu ambapo Mbunge wa Mtama na Waziri mwenye dhamana ya habari, masiliano na Teknolojia(Nape Nnaye) huwa anapategemea sana kuchukuwa/kupigiwa kura za kutosha katika chaguzi zinazofanyika, hii ni kutokana na idadi ya watu waliopo Mji huu ambao ni wanachama wa Chama Mapinduzi.

Nyangao kuna shule za level ya juu (High) kama MAHIWA HIGH SCHOOL na NYANGAO HIGH SCHOOL ambayo inasemekana inamilikiwa na Waziri mkuu(Mh : Kassim M Kassim). Ukitaka kufahamu shule hii kwa undani basi fuatilia Zamaradi TV. Pia kuna chuo cha kati cha Afya kilichopo karibu na Hospital ya Nyangao na vyuo vingine vya ufundi.

KIDATU/RUAHA
Mji huu upo ndani Wilaya ya Kilosa japo watu wengi wanachanganya kwa kufahamu kuwa upo wilayani kilombero. Mji huu unakuwa kwa Kasi sana, hii inachagizwa na uwepo wa kiwanda kikubwa Cha sukari almaarufu kama Kilombero Sugar Company. Wakazi wengi wa mji huu ni wakulima hasa Kilimo cha miwa ambapo soko lake kuu la miwa linapatikana katika kiwanda hicho cha sukari. Mji huu una fursa za kibiashara hasa kutokana na wageni wanaokuja kununua sukari kiwandani hapo bila kusahau Crew kubwa ya wataalam kutoka kiwandani hapo.

Kuna chuo kimoja kikongwe sana kinachofahamika kama NATIONAL SUGAR INSTITUTE. Chuo hiki kinatoa kozi mbalimbali za Stashahada ya uhandizi Umeme, Kilimo na Sukari n.k

Pia Mji unahuduma za kibenki na sehemu nyingi za starehe bila kusahau Mji huu umepitiwa na barabara kuu ya kuelekea Mji wa Ifakara.

Karibu Kidatu/Ruaha.

ITAENDELEA...
Unapajua vinzuri kidatu kile kiwanda kinaitwa illovo nimeishi kwa baba yangu mdogo anafahamika kwa jina la matungira,miaka ile ya 2012 nikasoma udereva kwenye chuo hicho kipindi hicho nilikuwa nalima mboga na kufunga nguruwe daah umenikumbusha mbali sana,baba mdogo anapakana na mzee mmoja maarafu sana alikuwa mbunge pia ana mtoto wake anaimba singeli anaitwa dragon
 
Mkwajuni unaweza paelezea kidogo, kuhusu fursq zake na jamii husika kiujumla, vipi mzunguko unategeme nn zaid?
Uvuvi kutoka ziwa Rukwa, kilimo ktk bonde la Ziwa Rukwa, biashara, uchimbaji madini (dhahabu-japo si sana).
 
Napajua vizuri mkuu, Illovo moja hiyo.. kule K1 kuna Hospital ya kiwanda kabisa,, ni nzuri sana
Unapajua vinzuri kidatu kile kiwanda kinaitwa illovo nimeishi kwa baba yangu mdogo anafahamika kwa jina la matungira,miaka ile ya 2012 nikasoma udereva kwenye chuo hicho kipindi hicho nilikuwa nalima mboga na kufunga nguruwe daah umenikumbusha mbali sana,baba mdogo anapakana na mzee mmoja maarafu sana alikuwa mbunge pia ana mtoto wake anaimba singeli anaitwa dragon
 
Mimi kwa experience yangu nliushobokea mji wa Katoro kwa story kama hizi za mji wenye fursa nikahama zangu dar, lengo lilikuwa ni kufanya biashara ya nafaka ila muda nilipofika ilikuwa nimepishana na msimu Yani alifika July na mavuno ni April sasa nikapata wazo la kufungua grocery maana huko kuna walevi dar ikasome.. nikachukua eneo pale stendi kuu ya Katoro maboresho kidogo nikatia mzigo.. kilichonikuta ni hatari japo nlifata ethics za biashara niliweka mademu weupe wenye msambwanda, mziki na chakula quality kabisa ila nilikutana na vimbweka sitasahau huo mji watu wanaroga saa moja jioni live bila chenga, mademu weupe wasukuma wanawaoa kwa gharama yoyote Yani bado wanakopesha plus wateja wakawa kama umeme wa TANESCO nikaona nirudi mjini huko wanaoweza kutusua ni wasukuma au wafanyabishara wa madini na wenye mitaji mikubwa ila milioni 5 kushuka chini unachoma pesa yako
Kweli... katoro inapewa sana promo ila kiukweli kibiashara bado sana, huwezi amini serengeti walifungua depot yao katoro mwisho wa siku waliifunga kutokana na wana katoro sio wanywaji wa bia kiviiile wenyewe wamezoea pombe za bei rahisi
 
Bila kuisahau katoro-Geita! Alaf mleta uzi umesema kidatu/ruaha ipo kilosa lakini sio kweli hyo ipo wilay ya kilombero hat ukiangalia google map, alfu tunduma sio wilaya hyo ni wilaya ya Momba.
 
Chalinze ilishakuwa na sasa inazidi kujitanua, ni Mji uliobeba mamlaka ya Wilaya kwa sasa,, fursa za biashara zipo kama biashara za mananasi, machungwa n.k😃
Chalinze ndio lango la kuingilia Mikoa ya Kaskazini yaan Tanga, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na kwingineko.
Naona toka Mhe: RizOne kapewa hili Jimbo basi Chalinze inazidi kuneemeka, Sasa wamepata hadi kituo cha mabusi kizuri kabisa sio kama kile cha Wilaya ya Gairo kinachotia aibu😃

Ridhiwan Kikwete Hoyeeee
Aiseeee
 
Back
Top Bottom