Evelyn Salt
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 70,916
- 141,437
Uko wapi.....
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Niko DaslamUko wapi.....
Eti ee? Nimehisi piaChai
🤣Dah! We acha tu mkuu, dashboard lao linavutia kweli, kile kindege kwa jinsi kinavyoend unaeza ishia kusema Mambo Bado ngoja kisogee sogee, kumbe ndo kinapeperuka hivyo
Kuna manzi nimemuahidi 30,000 ya kusuka. Nimeshamlima bloku, tukutane mwisho wa mwezi
Afu nne ama afu sabuni? Kumbuka kuna kupoteza muda mkuu. Duh! Halafu huwezi amini muda huu naelekea kwa wakala kutia mzigo tenaHizi kelele zote umeliwa afu nne tu!! Umasikini ni kipaji
Pokea simu basi.....Niko Daslam
Kuna kibunda huko Nina mentorship program kwa ajili ya mabingwa wa aviator natoza kiasi kidogo tu Cha pesaDuh! Jana usiku jirani yangu alikuwa busy sana na simu kiasi kwamba kila ninapomtupia salamu anajibu majibu ambayo hayaeleweki eleweki. Kufuatilia vizuri nakuta kuna kitu wanaita aviator ambacho nimekifahamu jana hiyo hiyo. Ndipo kunipatia dar'sa la namna ya kucheza. Kwenye dashboard yake akikuwa na 40,000 huku akinitambia kuwa kesho haingii kazini, anasema mtaji wa Tsh.2000 umemtengenezea kiasi hicho
Basi bhana, usiku huo mida ya saa nne nikaweka 4,000 aviator na vouda walivyo ndezi wananitumia na ka-sms ka pesa yako imehamishiwa kunako majariwa😋. Tumpafu sana! Basi bhana nikaweka na kavocha ka Tsh.1000 kwa ajili ya mb. Nikadownload Operamini, nikaingia mzigoni
Nilianza na dau la 200 200, nika advance 1000 1000 ukawa ni mwendo wa nipe nikupe, kula na kuliwa! Mwisho wa siku nikaibuka na 50,080 kwa mkupuo mmoja wa dau la 1000 na muda huo nilikuwa nasinzia sinzia, nilishtuka ghafla nikajikuta nawatumia ndugu, jamaa na marafiki sms iliyoandikwa Kheri ya sikukuu ya Pasaka. Mola awe nanyi nyote. Basi bhana nikapitiwa na usingizi
Asubuhi na mapema nikampigia simu boss kumueleza kuwa tumbo linaniuma sana, siwezi kuja kazini. Lakini wakati natoka nje, nalimuona jirani yangu akiwa amenywea sana, mi nikajua ni uchovu wa kutolala usiku wote ule. Nikaingia zangu mgahawani nikapata supu la kongoro kwa pesa yangu ya mfukoni
Mawazo yakaanza kuja mengi mengi. Hivi ni kwanini nisiende kupangisha fremu karibu na barabara ya lami. Niwekee ka PC uchwara na kiyoyozi, kazi yangu kubwa iwe ni ku-aviator? Nikaona ni sawa. Nikiweka dau la 100k ninaweza kula mpaka 10m nikafanyia either kujenga shule ya bweni ya watoto wa kike wa sekondari, halafu mimi nikawa mwalimu wa nidhamu or nijenge jumba kubwa niajiri vijana wawe wana-aviator tu, jioni nakuja kuchukua hesabu
Basi bhana, nikakamatilia simu yangu, nikaanza ku-aviator, ile kuhamaki, pesa imepungua mpaka 12,000. Nikaona wacha niongeze bidii, hakuna kitu kinauma kama pesa ihesabu ifike mpaka 48,000 halafu ujisemee ngoja nisubiri ako ka 2,000 kajijazie ili nipate hela Shufwa inayoeleweka, kama ni 50k, iwe 50k sio pesa mbudule zenye desimali. Ile imefika 49,120 unajiandaa kubofya Toa pesa unasikia Nyweeeeeeeeeeeee. Huo mshtuko wake unaweza kujinyea kama sio kukitupa
Basi bhana, mpaka saa 9 kasoro nikawa nimefikisha 70,000. Nikaona sasa wacha nianze kuweka teni teni. Mi hata sielewi ni nani kanishauri. Ila muda huu nimejikuta nshalifuta file lenyewe la Opera mini, yaani nimebaki na uzuni tu kama kuku mbudule
Aviator Aviator Aviator, haya yote kasabisha yule shabiki wangu Manywele wa Mkuranga kutoka Mweupe Family akishirikiana na huyu rafiki yangu. Msichokijua, hata rafiki yangu aliliwa alfajiri
nashukuru sana nimefurahi kuona nyota ipo kiaina😅😅😅😅7YGKJ7C
SGR betpawa, najifurahisha tu na Shilingi moja
We jamaa story zako sometimes ni chai, na nilijua tuu ukiwa kimya muda mrefu ukija lazima utatugea chai ya motooooDah! Ndo hivyo mkuu, yaani kule wanakushawishi kivyovyote vile ili wakupige na vitu vizito. Nimepoteza muda. Yaani mpaka tumbo linaanza kuuma
😂😂Mkuu, nilichogundua hawa watu wanasoma algorithms za mtu, kuna ka ai kanatumika. Wakiona huyu jamaa anavizia ndege ikiwa inachochea mafuta ndo abofye toa pesa, wanaamua kukuwahi vile ndege inatokeza tu hivi, utaskia Mweeeeeeeeee! Yaani hata kama odds zinasoma 1.00 ili tu wakule wafurahiHako kandege kakitoka tu bonyeza,usisubiri eti kafike sijui wapi kule souz sudani no, we ukicheza na ukaona kameruka fasta bofya batani 😂, utanishukuru.