Mikeka: Wazee wenzangu wa kuweka mzigo, karibuni tubashiri mechi za leo

Mikeka: Wazee wenzangu wa kuweka mzigo, karibuni tubashiri mechi za leo

Nimeshutuka sana mbaka nikalibie kuunguza chips
 

Attachments

  • FB_IMG_1721234660089_1.jpg
    FB_IMG_1721234660089_1.jpg
    168.4 KB · Views: 9
Dah! We acha tu mkuu, dashboard lao linavutia kweli, kile kindege kwa jinsi kinavyoend unaeza ishia kusema Mambo Bado ngoja kisogee sogee, kumbe ndo kinapeperuka hivyo

Kuna manzi nimemuahidi 30,000 ya kusuka. Nimeshamlima bloku, tukutane mwisho wa mwezi
🤣
 
Duh! Jana usiku jirani yangu alikuwa busy sana na simu kiasi kwamba kila ninapomtupia salamu anajibu majibu ambayo hayaeleweki eleweki. Kufuatilia vizuri nakuta kuna kitu wanaita aviator ambacho nimekifahamu jana hiyo hiyo. Ndipo kunipatia dar'sa la namna ya kucheza. Kwenye dashboard yake akikuwa na 40,000 huku akinitambia kuwa kesho haingii kazini, anasema mtaji wa Tsh.2000 umemtengenezea kiasi hicho

Basi bhana, usiku huo mida ya saa nne nikaweka 4,000 aviator na vouda walivyo ndezi wananitumia na ka-sms ka pesa yako imehamishiwa kunako majariwa😋. Tumpafu sana! Basi bhana nikaweka na kavocha ka Tsh.1000 kwa ajili ya mb. Nikadownload Operamini, nikaingia mzigoni

Nilianza na dau la 200 200, nika advance 1000 1000 ukawa ni mwendo wa nipe nikupe, kula na kuliwa! Mwisho wa siku nikaibuka na 50,080 kwa mkupuo mmoja wa dau la 1000 na muda huo nilikuwa nasinzia sinzia, nilishtuka ghafla nikajikuta nawatumia ndugu, jamaa na marafiki sms iliyoandikwa Kheri ya sikukuu ya Pasaka. Mola awe nanyi nyote. Basi bhana nikapitiwa na usingizi

Asubuhi na mapema nikampigia simu boss kumueleza kuwa tumbo linaniuma sana, siwezi kuja kazini. Lakini wakati natoka nje, nalimuona jirani yangu akiwa amenywea sana, mi nikajua ni uchovu wa kutolala usiku wote ule. Nikaingia zangu mgahawani nikapata supu la kongoro kwa pesa yangu ya mfukoni

Mawazo yakaanza kuja mengi mengi. Hivi ni kwanini nisiende kupangisha fremu karibu na barabara ya lami. Niwekee ka PC uchwara na kiyoyozi, kazi yangu kubwa iwe ni ku-aviator? Nikaona ni sawa. Nikiweka dau la 100k ninaweza kula mpaka 10m nikafanyia either kujenga shule ya bweni ya watoto wa kike wa sekondari, halafu mimi nikawa mwalimu wa nidhamu or nijenge jumba kubwa niajiri vijana wawe wana-aviator tu, jioni nakuja kuchukua hesabu

Basi bhana, nikakamatilia simu yangu, nikaanza ku-aviator, ile kuhamaki, pesa imepungua mpaka 12,000. Nikaona wacha niongeze bidii, hakuna kitu kinauma kama pesa ihesabu ifike mpaka 48,000 halafu ujisemee ngoja nisubiri ako ka 2,000 kajijazie ili nipate hela Shufwa inayoeleweka, kama ni 50k, iwe 50k sio pesa mbudule zenye desimali. Ile imefika 49,120 unajiandaa kubofya Toa pesa unasikia Nyweeeeeeeeeeeee. Huo mshtuko wake unaweza kujinyea kama sio kukitupa

Basi bhana, mpaka saa 9 kasoro nikawa nimefikisha 70,000. Nikaona sasa wacha nianze kuweka teni teni. Mi hata sielewi ni nani kanishauri. Ila muda huu nimejikuta nshalifuta file lenyewe la Opera mini, yaani nimebaki na uzuni tu kama kuku mbudule

Aviator Aviator Aviator, haya yote kasabisha yule shabiki wangu Manywele wa Mkuranga kutoka Mweupe Family akishirikiana na huyu rafiki yangu. Msichokijua, hata rafiki yangu aliliwa alfajiri
Kuna kibunda huko Nina mentorship program kwa ajili ya mabingwa wa aviator natoza kiasi kidogo tu Cha pesa

Remember aviator is not for everybody but for the champions
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 Uliwaza hadi kufungua na shule
 
Dah! Ndo hivyo mkuu, yaani kule wanakushawishi kivyovyote vile ili wakupige na vitu vizito. Nimepoteza muda. Yaani mpaka tumbo linaanza kuuma
We jamaa story zako sometimes ni chai, na nilijua tuu ukiwa kimya muda mrefu ukija lazima utatugea chai ya motoooo
 
Unakataza serikali isinunue LC unaenda kutupa pesa. Jamaa wakiangalia fedha zinazopotezwa kwenye betting lazima waongeze tozo.
 
Hako kandege kakitoka tu bonyeza,usisubiri eti kafike sijui wapi kule souz sudani no, we ukicheza na ukaona kameruka fasta bofya batani 😂, utanishukuru.
 
Hako kandege kakitoka tu bonyeza,usisubiri eti kafike sijui wapi kule souz sudani no, we ukicheza na ukaona kameruka fasta bofya batani 😂, utanishukuru.
😂😂Mkuu, nilichogundua hawa watu wanasoma algorithms za mtu, kuna ka ai kanatumika. Wakiona huyu jamaa anavizia ndege ikiwa inachochea mafuta ndo abofye toa pesa, wanaamua kukuwahi vile ndege inatokeza tu hivi, utaskia Mweeeeeeeeee! Yaani hata kama odds zinasoma 1.00 ili tu wakule wafurahi

Ukimuuliza vizuri Chat GPT 3.5 anakupa maelezo ya kutosha
 
Back
Top Bottom