Mikopo ya bank za kibiashara aliyokuwa anakopa Magufuli machungu yake ndio yanaonekana sasa

Ila hii nchi kuna watu wanapaswa wakatwe vichwa ndo tusonge mbele kama huyu mleta uzi

Kwa hiyomatatizo ta sukari kupanda ni Magufuli? Umeme ni magufuli? Shida ya kupanda gharama za maisha ni magufuli
Zitto aliwahi kuyaongea haya kitambo, "we shall pay the price later" ndiyo yanayotokea sasa, tumshukuru sana mama Samia kwa upeo wake wa ajabu na kipekee kwa" quickly economy recovery "uchumi ulikuwa unakwenda kuanguka kifo cha mende!,.....
 
Tatizo kajifia katuachia msala.Ilitakiwa awe hai Ili Wanyonge waisome namba vizuri.

Zile tozo mlizolalamikia Samia ni kwamba zilianzishwa na Mwendazake maana Bajeti ya Nchi Huwa inaandaliwa mwezi Desemba Hadi February.

So Samia anachukua Kijiti Kila kitu Kiko tayari,zinapitishwa msala unakuja kumuangukia.

Na Jiwe ambavyo alikuwa hajui kutafuta pesa Bali anatumia Nguvu saizi watu wangenyooka na hakuna wa kukenua.

Mitikisiko ya Dunia ambayo Tzn imeoigia Jiwe angekuwepo aisee saizi Nchi sijui ingekuaje.

Mwisho alichukua mikopo mikubwa ya kibiashara kujengea reli na bwawa ambayo Ina mature ndani ya miaka 3 -5 matokeo yake Sasa hivi pesa zinaishia kulipa Madeni.

Samia amekopa sana tuu lakini mikopo yake Mingi ni ya masharti nafuu itakuja kuiva miaka 15 plus huko wakati Nchi imeshajipanga vyema.

Mwisho mamiraei yenyewe hakuna Cha maana yatasaidia Kwa maskini sana sana itazidi kuleta hasara tuu.
 
Moja ya mambo ambayo nashukuru ni Magufuli kutokaa miaka kumi kama angekaa miaka 10 damage kwenye uchumi ingekua kubwa sana
 
Mikopo mingi ni miaka 10 kuendelea, kuanzia mwaka 2030 huko lazima watu walimie meno, jamaa alikopa sana, akawa anaongopea fedha zetu.

Mwigulu naye anakopa kwa spidi ya Boeing 787 .
Bora ingekuwa hata miaka 10,mikopo ya kibiashara kwenye Mabenki ni miaka 3 -5,ukipata wa miaka 10 ni nafuu.

Bora Mwigulu anakopa mikopo ya mda mrefu wa miaka 15 Hadi 30
 
Na mvua ikinyesha wanasema maji hayatiririki kuelekea yalipo mabwawa
 
Dadavua vizuri hiyo mikopo ni kiasi Gani kutoka benki zipi ili uthibitishe kauli yako
 
Mmeanza uongo mwacheni Magufuri apumzike kazi alishafanya ila ninyi nchi imewashinda.
 
Watu wenye akili ndogo hawawezi elewa Magufuli alizingua sana
Kama mtu mwenye akili nyingi anashuhudia umeme kuktwa hovyo bila mpango, watu kufisadi fedha za umma bila uoga na rushwa kukithiri, miradi haina mwelekeo, sukari kupandishwa bei bila utaratibu inshort hamna muongozo wowote zaidi ya kumtesa mwananchi wa hali ya chini. Kama mtu mwenye akili ataona haya yote ni sawa basi atakuwa mbumbumbu wa mwisho na lofa kabisa kumponda Magufuli.
 
Ila uzi hauhusu hayo uliyoyasemea kwanini usijikite kwenye mada ya uzi
Hakuna sehemu nimeongelea umeme au changamoto nyingine
 
Wewe unahisi ungewai kuwa na akili kuliko Magufuli?
Yakwenu yamewashinda; kazi kupambana na Hayati.Fanyeni kazi nanyie mtasifiwa na kupendwa dunia nzima.

Kwanza siyo visibility study.
 
Ila uzi hauhusu hayo uliyoyasemea kwanini usijikite kwenye mada ya uzi
Hakuna sehemu nimeongelea umeme au changamoto nyingine
Mada gani wewe,unataka watu wakupongeze wakati unachapia?Wewe yanayofanyika leo unaona sawa??
 

Katika andiko lako, unetumia hisia na mihemko bila kutumia akili.
Tulitegemea tuone
1. Benki gani binafsi alikopa.
2. Riba ilikuwa kiasi gani.
3. Muda wa kurejesha mkopo una urefu gani.
4. Kiasi alichokopa ni shs ngapi.
5. Concessional loans wanakopesha kwa riba kiasi gani.
6. Nk.
Bila kuainisha mambo kama haya utakuwa unafukuza upepo tu na kupiga ngumi hewani.

Pia faida kwa mabenki haiathiri mzunguko wa fedha kama ulivyokuwa unasema. Kwa taarifa yako, sasa kuna mzunguko wa fedha mkubwa sana hivi kwamba BoT imetoa sera ya udhibiti.
 
Wameshindwa kazi; wanakuwa ni visingizio kila siku.
 
Zitto aliwahi kuyaongea haya kitambo, "we shall pay the price later" ndiyo yanayotokea sasa, tumshukuru sana mama Samia kwa upeo wake wa ajabu na kipekee kwa" quickly economy recovery "uchumi ulikuwa unakwenda kuanguka kifo cha mende!,.....
Chawa kwenye ubora wenu, hata hivyo mna hali mbaya kiasi kwamba mnashindwa kumtetea boss wenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…