ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 21,643
- 51,642
Mimi nikitoboa masaa 12 huwa sihisi njaa kabisaaaaaaWatu wengi hawajawahi ku experience njaa, Njaa wanazosisema ni hizi ambazo imetokea kuvurugika tu kwa ratiba ya Milo yao mfano mtu mwenye ratiba ya kula Milo mitatu ndani ya mda Fulani ikitokea amechelewa kula ndani ya mda huo atakwambia anahisi njaa ila njaa, njaa kweli ni Ile ambayo mtu anatoboa kuanzia masaa 12 na kuendelea bila kula chochote
Ndiyo inavyo takiwa tule kwa kusikia njaa na tule pale tunapo sikia hamu ya kula hata kama njaa hakuna tembea na hamu ...kula kwa ratiba ni ngumu sana pia hupati rahaBinafsi huwa nakula pale ninaposikia njaa hata kama ni mlo mmoja au mitano inategemea na njaa yangu.
Katika hiyo list yako mm nisivovipenda ni nyanyachungu,hoho na biringanyamimi binafsi
Nataka kula chochote ila kichanganywe na
Nyanya
Kitunguu
Karoti
Nyanya chungu
Hoho
Birimganya
Embe bichi
N.k
Iwe nyama au utumbo au samaki au yai..ila liwe na mchemsho huo na kwenye fry pain kikaangiwe pale
Na ndivyo inavyo takiwa mkuu ,njaa ikiuma hata sa nane ya usiku naamka nasonga ugali😁Kuna jamaa yangu siku nimemtembelea nashangaa saa 6 usiku eti anaenda kutafuta msosi kitaa hajala tangu asubuhi..
Nae alikua na hizo pigo, anakula akihisi njaa tu
Msoto wa njaa sio mchezo tumbo lenyewe unalisikia likikupa taarifa Kwa mitetemo na miungurumo mixture kawenge flani hivi kama cha mleviAcha kabisa, msosi ni muhimu jombaa.
Kuna kipindi nikipitia msoto mpaka kwenda toi ukibanwa na gogo unaogopa, maana unaenda kutoa nini huku na hujala chochote cha maana, nikitoa hiki si ndo tumbo litabaki tupu kabisa.
Hapo umechapa uji tu maana unga hata ugali hautoshi.
Basi utakuwa una kaunene flani hiviMimi nikitoboa masaa 12 huwa sihisi njaa kabisaaaaaa
Toa njaa zako. Nenda Chato. asubuhi supu la sato na Ugali, mchana ugali na nchima +Usiku ugali kamongo.Kwanza tufahamu utaratibu wa milo mitatu ni utamaduni wa magharibi ulioibuka karne ya 17 kutokana na mambo mengi mojawapo ikiwa ni mapinduzi ya viwanda yaliyowafanya wafanyakazi wanaofanya kazi ngumu wahitaji kula mara nyingi kuhimili kazi ngumu. Kabla ya hapo binadamu wengi walikuwa wanakula mlo mmoja au miwili kwa siku.
Kwa upande wa daraja tawala na mabepari huko magharibi wao baada ya mafanikio ya kiuchumi walianza kula milo mitatu kama anasa na kufanya networking, baadaye karne ya 19 huko Marekani suala la breakfast(kifungua kinywa) liligeuzwa biashara zaidi baada ya jamaa mmoja kusahau kubeba mahindi yake aliyochemsha kula kazini na yakaharibika ndipo likamjia wazo la kutengeneza cornflakes kwa kuyakandamiza kama chapati na kuyaanika kuyafanya yadumu zaidi, ndipo wazungu wakaibuka na bidhaa chungunzima za breakfast.
Leo hii mtu anakula asubuhi na mchana anashinda dukani, saloon au ofisini anabonyeza keyboard tu ndio mwanzo wa janga la kiribatumbo na vitambi kwa wanawake na wanaume.
Mimi mwembamba mkuu kiliko hata wembamba wenyeweBasi utakuwa una kaunene flani hivi
Kwanza tufahamu utaratibu wa milo mitatu ni utamaduni wa magharibi ulioibuka karne ya 17 kutokana na mambo mengi mojawapo ikiwa ni mapinduzi ya viwanda yaliyowafanya wafanyakazi wanaofanya kazi ngumu wahitaji kula mara nyingi kuhimili kazi ngumu. Kabla ya hapo binadamu wengi walikuwa wanakula mlo mmoja au miwili kwa siku.
Kwa upande wa daraja tawala na mabepari huko magharibi wao baada ya mafanikio ya kiuchumi walianza kula milo mitatu kama anasa na kufanya networking, baadaye karne ya 19 huko Marekani suala la breakfast(kifungua kinywa) liligeuzwa biashara zaidi baada ya jamaa mmoja kusahau kubeba mahindi yake aliyochemsha kula kazini na yakaharibika ndipo likamjia wazo la kutengeneza cornflakes kwa kuyakandamiza kama chapati na kuyaanika kuyafanya yadumu zaidi, ndipo wazungu wakaibuka na bidhaa chungunzima za breakfast.
Leo hii mtu anakula asubuhi na mchana anashinda dukani, saloon au ofisini anabonyeza keyboard tu ndio mwanzo wa janga la kiribatumbo na vitambi kwa wanawake na wanaume.
Wewe ni:Leo hii mtu anakula asubuhi na mchana
Hapo Sasa porti utegemee ratiba ukiufuma msosi,twanda mpaka ucheue!Sitasahau Mwaka 2017-2018 nilipatwa na majanga maisha yangu yaliyumba sana, Kuna siku nilikaa siku tatu bila kula..... Namwelewa sana mtoa mada
Yule sio timamu ukimfuata atakuponza. Kasema sana Hadi akanganyikiwa na kusahau alikuwa ana somea Nini.Janabi alishasema unatakiwa ule pale unapohisi njaa tu siyo unakunywa chai kwasababu ni Asubuhi kama hauhisi njaa skip breakfast kula hata saa 6 mchana ikifika muda wa lunch huskii njaa skip had saa 11 jion ndo ule, usiku siyo muhimu sana kula kama unataka kula usiku basi kula masaa matatu kabla ya kulala
Mkuu kwa muktadha wako huu basi kila kitu tumerithi kwa wakoloniMilo mitatu tumerithi kwa wakoloni
Janabi amesema anakula ugali??Yule sio timamu ukimfuata atakuponza. Kasema sana Hadi akanganyikiwa na kusahau alikuwa ana somea Nini.
Niliacha kumsikiliza pale aliposema yeye anashindia maji ya vuguvugu mara ana kula ugali na tomato sauce tu