Mimi ndoa ilinipotezea muda wangu, iliniacha na Maumivu na kilema cha Maisha yangu

Mimi ndoa ilinipotezea muda wangu, iliniacha na Maumivu na kilema cha Maisha yangu

Ilipoishia “Wala hakuongea chochote akaanza kuniandalia chakula nile, nilikua nahema kwa shida sana.

“Kunywa Maji” alisema, alikua haniangalii usoni, nilikua na kiu ya maji lakini kiu kubwa ilikua ni kumuuliza Nauawa lini, nilimuuliza

“Mnanimalizia lini nikapumzike?” Kiukweli sikuwa na afya nzuri, ndani ya siku chache nilikonda. Yule Bodaboda akanitazama kisha akaniambia

“Kifo ni siri ya Mungu, hakuna anayeijuwa kesho itakuwaje” alisema kisha akanipa maji, sikuwa na nguvu ya kushika kikombe akaninywesha. Jinsi alivyonihudumia alionesha anahitaji niwe hai. Endelea

SEHEMU YA NANE

Niliyafakamia yale maji kwanza hadi yalinipalia, halafu nikahema. Akanitolea vidonge vya kunituliza maumivu. Sikusita kumeza kiukweli maana nilikua na maumivu makali sana kisha nilimshika mkono nikamuuliza

“Ningekuwa mdogo wako ungenifanyia hivi, unajua najisikiaje Kaka?’’ Chozi lilikua linanibubujika bila kuacha, akaniondoa mkono wangu kwa kutumia mkono wake mwingine kisha akasimama, akaniambia

“Kula upate nguvu” hakuzungumza tena, alisimama kisha alipiga hatua lakini alipofika mlangoni alisimama. Kama kuna kitu alitaka kuniambia lakini alighaili, hakujibu swali langu aliondoka na kuufunga mlango kwa funguo, unajua hata kama angeuacha wazi sikuwa na nguvu ya kukimbia kwa namna nilivyokua sina nguvu.

Nilisikia akiondoka, nililia sana Mimi. Hakuna siku inapita bila kudondosha chozi langu, nilimpoteza Kaka Hamidu na nilijiona ni mkosaji, nilijilaumu sababu bila kuolewa na Salehe basi Kaka Hamidu angekuwa hai hadi sasa. Kidogo zile dawa zilipunguza maumivu ya mwili lakini siyo maumivu ya Moyo wangu

Haikuchukua hata dakika nyingi nilisikia yowe la Mwanaume mmoja, yowe lile lilisikika moja kwa moja kutoka kwenye ile nyumba niliyohifadhiwa Mimi. Moyo ulinilipuka, niliamini ilikua ni nyumba ya Mateso makali zaidi hata nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Nilisimama hata nguvu sikujuwa ilitokea wapi

Nilisogea mlangoni ili kuisikia zaidi ile sauti, ndiyo! Ilitoka ndani ya moja ya vyumba vya ile nyumba, nilitamani kupaza sauti ila sikujua alikua akifanywa nini. Nilijiuliza

“Nani yupo ndani ya hii nyumba, anamfanya nini huyu anayepiga yowe” Ilikua ni sawa na kujitekenya kisha kucheka mwenyewe, jibu lingetokea wapi ikiwa hata mimi mwenyewe sijui nipo wapi

Yule Mwanaume baada ya kupiga yowe alianza kusema

“Msaada,Nani yupo ananisikia?” aliendelea kusema hivi, nikapata picha huwenda hata yeye mwenyewe hajui amefikaje na Nani amemleta ndani ya hii nyumba. Kupitia dirishani nilianza kuona jua namna lilivyokuwa likifanya safari ya kwenda kupumzika baada ya kuipiga ardhi kwa siku nzima.

Namna nyumba hii ilivyo ilionekana kujengwa kwa ajili ya kazi ya kuhifadhi Binadamu, hata dirisha lake lilikua kama la Mahabusu, lilikua dogo lanye nondo,hapakuwa na taa ndani ya chumba kiasi kwamba giza litakapoingia basi patakuwa giza tupu. Nilijikuta nikikaa mwenyewe bila hata kuambiwa, kwa namna ilivyo hata ukipiga kelele vipi huwezi kupata Msaada wowote.

Kwanza sikujuwa Mtu yule alikua ni Nani, sauti yake haikufanana na ya Kaka Hamidu. Wala si ya Mtu niliyehisi kuwa niliwahi zungumza naye.

**

Usiku ulipoingia ndiyo nililiona joto la jiwe, niliandamwa na ndoto za ajabu hadi niliamka, siyo Mimi tu hata yule Mwanaume alikua akigugumia nahisi naye alikua kwenye hali kama yangu. Niliamka na kukaa kitako nikaegemea ukuta

Nikiwa hapo nilianza kuona nuru ya mwanga, ikianza taratibu hadi ikaenea chumba chote, hapa nilikua na uhakika kuwa haikuwa ndoto tena bali ni tukio halisi. Nilimuona tena yule Mtoto mdogo anayetisha, safari hii alinionesha sura yake, nilikua kwenye Mshangao wa hali ya juu sana

“Umeshindwa kutoka hapa, umeshindwa kujaribu kufanya chochote. Wewe ni Mtu wa aina gani, unataka kila Mtu afe kama Kaka yako Hamidu” Ooh! Jamani nilishtuka, kama ningekua nina presha kwa haya yote ningekuwa tayari nimepotea kwenye uso wa Dunia, namna alivyokua anaongea alionesha alikua na tumaini na Mimi kwenye jambo fulani hasa la kuokoa uhai wa wengine lakini Mimi mwenyewe nilikua nimeshajikatia tamaa. Japo nilijawa na woga lakini nilimuuliza

“Wewe ni Nani, umetokea wapi?” nilipomuuliza alidondosha chozi la damu, alikua Mtoto wa ajabu sana

“Mimi ni Ashura Mtoto wa Mama Muuza chapati. Nenda kamwambie Mama yangu kuwa bado naishi kwenye nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, Mimi sijafa” alisema kwa kupaza sauti kali ambayo ilinifanya nishindwe kuhimili zile kelele, pale pale nilijikuta nikiishiwa nguvu na kupoteza fahamu. Kitu pekee kilichobakia kwenye akili yangu ni ,kumbukumbu juu ya yule Mama anayeishi nyumba jirani na Mzee Mwinyimkuu, Mama aliyekuwa akiniuzia Chapati

Ndiyo‼ yeye ni Mama Ashura, nakumbuka alinitajia jina hili lakini sikuwahi kumuuliza huyo Ashura yupo wapi, huyu Mtoto wa ajabu alijitambulisha kwangu kama Ashura na alinitaka nimwambie Mama yake kuwa anaishi ndani ya nyumba ya Mzee Mwinyimkuu.

***

Baba yangu aliendelea kuumwa, Mama alikua anamuuguza huku akinitafuta Mimi kwa simu lakini aliendelea kutonipata, zilipita wiki mbili bila kupata mawasiliano yoyote yale. Salehe hakupatikana, hata Mzee Mwinyimkuu hakupatikana, Kaka Hamidu naye ilikua kama ndiyo

kichocheo kipya cha hofu kwa Familia yangu. Mara ya mwisho aliwaeleza anakuja kuonana na Mimi lakini baada ya hapo hawakujua kilichomfika na kupelekea kutopatikana kwenye simu kwa wiki mbili.

Vikafanyika vikao vya kututafuta Mimi na Kaka Hamidu maana hawakujua naishi Rukwa sehemu gani na pia Kaka Hamidu alikutwa na nini. Ni Mimi pekee ndiye niliyekuwa najua Kua Kaka Hamidu alikua ameuawa.

Familia ikamtuma Mjomba wetu aliyeitwa Kambona, alikua Mtu mzima na mwenye busara zake.

Akasafiri kutoka Dar-es-salaam hadi Rukwa akiwa na picha yangu, akaanza kunitafuta bila mafanikio kwa zaidi ya siku kumi. Mwishowe akaenda kituo cha Polisi maana sasa hakuna aliyekua na amani bila kujua tupo wapi, wote waliamini wakinipata Mimi watajua mahali alipo Kaka Hamidu maana mara ya mwisho aliwaambia anakuja kwangu. Polisi wakaanza kunitafuta kila kona ya Rukwa lakini hakuna aliyeweza kujua niko wapi, lakini kupitia jina la Mwinyimkuu Ambalo Salehe alilitaja alipokua ananichumbia, ikawawezesha kufika hadi nyumbani kwa huyu Mzee.

Hapa ndipo mahali ambapo nilikuwepo kabla ya kuhamishwa, nyumba hii ndimo alimouawa Kaka Hamidu tena kikatili sana na Mzee Mwinyimkuu. Walipofika walimkuta tena wala hakuwa na wasiwasi kabisa, najua alitumia akili sana kunihamisha vinginevyo polisi wangenikuta mle

“Wewe ndiye Mwinyimkuu?” aliuliza polisi baada ya salamu fupi

“Mnasemaje?” aliwauliza, alikua haogopi chochote wala Mtu yeyote yule, jeuri na katili mno “Saida anaishi hapa?” akauliza Polisi mmoja.

“Yeye ni Nani?” akawauliza

“Unajibu kwa dharau kiasi hicho Mzee, Saida ni Mpwa wangu Mimi. Ameolewa na Kijana anaitwa Salehe, upelelezi umeonesha kuwa ni Kijana wako huyo Salehe halafu unauliza ni Nani?” akaingilia kati mjomba Kambona na kumshika shati Mzee Mwinyimkuu, Polisi wakaokoa

“Unanivunjia heshiam si ndiyo?” akauliza Mzee Mwinyimkuu kwa hasira

“Siyo heshima tu, ntaivunja hata hii nyumba kama hutonipatia Saida wangu” Mjomba Kambona hakupoa kabisa, alijawa na hasira sana.

“Huyo Salehe unamfahamu?” Polisi wakamuuliza Mjomba Kambona

“Ndiyo, nimeozesha mwenyewe. Picha si hii hapa ya ndoa” akatoa picha, ile picha akapewa Mzee Mwinyimkuu.

“Umemtambua mtajwa pichani?” akauliza Polisi mmoja, Mzee Mwinyimkuu akaangua kicheko kisha akaita kwa sauti

“Salehe, hebu njoo uone maajabu ya Dunia” akaitikia Mtu kutokea ndani na kuwafanya Polisi na Mjomba Kambona wakae mkao wa kula kumuona Salehe. Ikachukua kama sekunde kadhaa tu Kijana mmoja akatoka ndani, Kijana aliyekuja hakufanana na Salehe wa kwenye picha.

“Unamfahamu Saida?” akauliza Mzee Mwinyimkuu akimuuliza huyo Kijana aliyemtambulisha kama Salehe, kiukweli hakuwa yule Salehe aliyeniowa kabisa yaani sura tofauti.

“Hapana, kuna nini?” akauliza huyo Salehe, kiukweli Mjomba Kambona alinywea. Lakini Polisi mmoja akasema

“Ongozana na Mimi Kijana” akamshika mkono Salehe na kwenda naye nje. Lengo la Polisi ni kutaka utambuzi kwa Majirani maana Upelelezi wao uliwaambia Salehe wa kwemye picha anapatikana kwa Mzee Mwinyimkuu. Wakafika hadi nyumbani kwa Mama Ashura maana ndipo palikua na Watu nje

Walipomuona Yule Kijana akiwa na Polisi vijana walikimbia hadi yule Polisi akashangaa, hata Mama Ashura naye alikua anataka kukimbia ila Polisi akamzuia Mama Ashura na Kumwambia asikimbie ana maswali kadhaa anataka kumuuliza, ndipo Mama Ashura akabakia lakini kwa hofu sana

“Unamtambua nani pichani?” Yule Polisi akampa picha yule Mama, Mama Ashura akaipokea picha japo kwa wasiwasi lakini alipoiangalia ile picha alishtuka sana, akameza funda la mate.

“Hapana’’akajibu lakini kwa hofu sana kiasi kwamba yule polisi akahisi pengine kuna jambo analificha. Kilichomshtua Mama Ashura ni kuniona Mimi kwenye ile picha ya ndoa ambayo Mjomba Kambona aliwapatia polisi

“Na huyu Kijana hapa?” akauliza Polisi, Mama Ashura akamtazama yule Kijana. Akaachia tabasamu la hofu kisha akajibu

“Ni Salehe, anaishi pale” akaonesha na kidole kabisa. Majibu haya yakamuacha yule polisi kinywa wazi, basi akarudi hadi nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Hakuna ushahidi wa anachosema Mjomba Kambona. Lakini Mjomba akawaaambia

“Nina namba ya huyu Mzee alikua anawasiliana na Mama yake Saida, hii namba nimepewa na Mama Saida. Jina ni hilo la Mwinyimkuu” akasema Mjomba japo kwa sauti ya kupoa, ikabidi Polisi waipige ile namba.

Ikapokelewa na Mtu mwingine kabisa tena Mwanamke akimuuliza yule Polisi Nani wewe? Yalikua kama maigizo ya Filamu lakini lilikua tukio la kweli, nyakati zote hizo Mzee Mwinyimkuu alikua akitabasamu akiwa anamtazama Mjomba Kambona.

“Mnaona anavyo nitazama, huyu anajua kila kitu” akasema Mjomba lakini hakuwa na ushahidi, maneno yake yalikua ni sawa na kuupaka upepo rangi. Muda wote Mzee katili alikua akitabasamu kwa mpango fulani ulio kichwani pake

Polisi walikosa ushahidi, ikaonekana kuwa Mjomba Kambona aliyakosea maelezo yake. Kibaya zaidi hata picha aliyowaonesha Polisi kuwa ndiye aliyeniowa ilikanwa kwa kuoneshwa Salehe mwingine na kilichotia nguvu kukosekana ushahidi ni maneno ya Mama Ashura. Angefanyaje Mjomba wangu zaidi ya kutoa kitambaa na kujifuta jasho ila moyoni aliamini Mzee Mwinyimkuu alikua anajua wapi nilipo, pia hapakua na ushahidi mwingine sababu Mzee Mwinyimkuu hakuhudhuria ndoa yangu

Polisi wakamwambia Mjomba Kambona

“Tutaendelea na Uchunguzi, kwasasa wewe liachie jeshi la Polisi. Tutakupa taarifa ya Uchunguzi juu ya Saida pia huyo Kaka yake” haikua kauli yenye matumaini, ilimvunja moyo sana Mjomba Kambona. Akamwambia Mzee Mwinyimkuu

“Saida hawezi kutoweka kirahisi, lipo unalolijua. Siondoki Rukwa hadi nihakikishe nampata Mpwa wangu” alisema hivyo kisha aliongozana na Polisi kuondoka, Salehe feki na Mzee Mwinyimkuu wakatazamana kisha wakawa wanawatazama namna Polisi na Mjomba Kambona walivyokuwa wanaondoka.

Wala hawakufika mbali, kabla hata hawajapanda kwenye gari ya Polisi. Mjomba Kambona alianguka na kufariki papo hapo akitokwa na Mapovu mdomoni. Licha ya jitihada za jeshi la polisi kumkimbiza Hospitali lakini alikua tayari amefariki

Taarifa ikarudi Dar-es-salaam kuwa Mtu waliyemtuma kuja kututafuta Mimi na Kaka Hamidu alikua tayari ameshafariki. Yalikua ni majonzi juu ya Majonzi, taarifa hii ilipomfikia Baba yangu alifariki pia kwa presha. Bundi aliizingira familia yangu, misiba miwili ndani ya siku moja, Mzee Mwinyimkuu akashinda tena kwa kishindo kikubwa sana.

**

Nilihesabu siku ambazo nilikua ndani ya ile nyumba ya mateso, zilitimia siku saba ngumu. Nilikonda nikawa kama Mtoto mdogo, niliishiwa nguvu. Kilichokuwa kimebakia kwangu ilikua ni kufa tu. Kila nilipoamka nilijikuta nimeshaondolewa kidole kimoja, pumua yangu ikawa ya

shida sana. Nikakosa uwezo wa kuwatambua Watu kirahisi, yule Bodaboda aliendelea kuniletea chakula kila siku lakini pia sauti ya Mwanaume mmoja kugumia ilikua ni sauti ya Kila siku

Lilikua ni jambo la kawaida sana yeye kupaza sauti, sikuwahi kufahamu alikua akipitia mateso gani, ila dakika za mwisho niligundua kuwa naye alikua akipelekewa chakula na huyu huyu Bodaboda anayeniletea Mimi chakula.

Sikuweza kusimama tena, vidonda vilianza kutoa funza sababu sikuwa na dawa yoyote isitoshe joto la mle ndani liliniathiri kwa kiasi kikubwa, Mwenzenu niliwahi kufika Jehannam nikiwa Hai.

Basi siku moja yule Bodaboda alikuja, siku yenyewe palikua na mvua kubwa. Aliingia akiwa ameloa sana anatetemeka kwa Baridi, japo nilikua katika nyakati za mwisho kabisa za uhai wangu lakini niliweza kugundua kuwa Baridi lilikua tatizo kubwa kwake. Alikua akiniandalia chakula huku akitetemeka nikagundua anasumbuliwa na tatizo linalo sababishwa na Baridi.

Akajikaza, akaniwekea chakula. Alipaswa kunilisha sababu Mimi nilikua siwezi tena hata kushika kijiko, nilikonda mno hadi mishipa ya Damu ilikua ikionekana. Akajitahidi kuniinua ili kunikalisha kitako niweze kuegemea ukuta anilishe vizuri, siku hii nilipanga kuacha kula ili nife mapema maana mateso yalinizidi kabisa, Jamani naposema nilikonda basi ujue nilikonda nikawa na kilo chache sana halafu kichwa kikawa kikubwa.

Nilitamani kumuuliza ana shida gani, huyu Mtu hakuwahi kunitesa wala hakuwahi kunisemea jambo baya isipokua alikua hajibu maswali yangu yote niliyokuwa namuuliza.

Hali yake ilianza kuwa mbaya, akashindwa hata kunishikilia akaanguka chini na kuanza kugala gala kwa maumivu Makali sana, mlango ulikuwa wazi hakuufunga sababu alipoingia alikua tayari ana hiyo hali ya Maumivu, niliona ni nafasi ya kutoroka lakini sikuwa na akiba yoyote ya nguvu iliyobakia

Nikatamani kuendelea kuishi ghafla tu, namna pekee ya kuendelea kuwa hai ni kutoroka. Huko nje mvua ilikua ikinyesha na kusababisha kelele kubwa sana kwenye Bati. Sikuwa na nguvu ya kusimama, nikaona ni bora nijiburuze nione kama naweza kufika nje

Yule Bodaboda alipoona naanza kujiburuza akajua nataka kumtoroka, akili yake ikatamani anizuie lakini mwili ulimsaliti, nguvu zilimwisha akiwa sakafuni anapumua kwa shida sana. Nikaendelea kujivuta taratibu huku nikiwa ninasali Mungu niliyemkatia tamaa azidi kunipa nguvu, unajua kwanini niliamini naweza kuondoka pale?

Kwasababu hapakua na mtu mwingine aliyekuwa anakuja isipokua yeye, hivyo hakuna tena wa kunizuia, halafu niliwaza kufika chumba ambacho yule Mwanaume anagumia ili kama yeye ana nguvu tusaidiane kutoroka.

Nilijiburuza kama nyoka hadi nilipotoka nje ya chumba kile, palikua na funguo kwenye kitasa. Nikapata akili ya dharura kuwa huwenda funguo ile inaweza nisaidia kufungua milango mingine

maana ilikua na funguo tatu zilizowekwa sehemu moja, naipataje Funguo ni lazima nisimame niichomoe

Kivumbi kilianzia hapo, nilikonda Mimi kiasi kwamba upepo unaweza nipeperusha, Malaika Mtoa roho alikua amenisimamia akiniuliza nasimama au achukue roho yangu, sijui nguvu zilitoka wapi nikasimama kwa kuyumba huku nikitetemeka. Nikachomoa funguo, ile nataka kupiga hatua nikaanguka

Basi nikagugumia kwa maumivu, nilihitaji kufanya haraka maana kama yule Bodaboda atapata nguvu basi sitaweza tena kuondoka, nikamkumbuka Mama na Baba yangu, nikamkumbuka Kaka Hamidu. Ghafla nguvu zikaamka

Nikajikaza na kuanza kujiburuza sakafuni kama nyoka vile, kwa mwendo huo huo nilijikuta nikikiacha chumba kwa mbali kidogo, sikuufunga ule mlango wa chumba nilichomuacha Bodaboda.

Basi nilipofika kama chumba cha tano hivi nikasikia Mtu akiugonga mlango kwa nguvu huku akisema

“Njoo unitoe humu Mshenzi wewe, mtauwa wangapi. Siku ikifika mtakufa kama Kuku” alisema kwa hisia sana lakini hakujuwa kuwa Mimi nilikua tayari nipo mlangoni. Mlango ulikua umefungwa, korido lilikuwa refu halafu vyumba vilikua mbali mbali. Nilijitahidi sana kusimama nifungue mlango lakini nilikua nakosa nguvu, nilijaribu kama mara tatu lakini niliishia kuanguka

Wakati nikiwa nimeanguka nikageuka nyuma, ndipo nilipomuona yule Bodaboda akijikongoja kwa maumivu kuja nilipo, alikua amelishikilia tumbo lake. Hapo sasa yule Malaika mtoa roho nikamuona kama anachukua koleo kwa ajili ya kuichukua roho yangu.

Sauti ya yule Mwanaume ilizidi kusema, kibaya zaidi Mimi ndiye mwenye funguo halafu sauti yangu ilikua haitoki. Nikasema kama sisimami basi siondoki. Yule Bodaboda akawa anazidi kuja upande wangu kwa kasi akionekana kuanza kupiga hatua za nguvu. Nikamtaja Mungu nikasema

“Mungu nipe nguvu niishinde hii vita” nikajivuta haraka nikasimama nikiwa ninayumba, nikaanza kusaka tundu la kuweka funguo maana nguvu yenye ilikua sifuri, nikawa najitahidi huku nikiwa natetemeka. Mara naingiza mara nakosea, huku yule Bodaboda akizidi kunisogelea, hata nilipopaatia nilikua nimeingiza funguo isiyo yake.

Akawa karibu zaidi kiasi kwamba akipiga hatua tatu anakuwa amenifikia na kunizuia kuufungua mlango, nikapapasia kwa bahati nzuri nikapatia funguo nikavuta nguvu za mwisho nikatekenya kitasa lakini tayari Bodaboda alikua ameshanivaa na kuniangusha chini, Bahati nzuri ule mlango ulikua tayari umeshafunguka

Akatoka mwanaume mmoja na kuanza kumkita mateke yule Bodaboda hadi akamtupilia mbali huko akiwa hoi sana anatokwa na damu mdomoni, eneo la Korido lilikua linawaka taa isipokua

vyumbani tu. Sikuamini macho yangu Mtu ambaye nilikuja kumuona na kumtambua japo nilimuona mara moja tu

Alikua ni yule Mwanaume niliyemuazimaga simu kule Buchani, Ndio! Ni Abuu, masikini naye alikua mateka wa Mzee Mwinyimkuu baada ya kujulikana ananifuatilia Mimi, kwa muda mfupi naye alikua amepungua sana japo alikua na nguvu.

Hakuniuliza chochote zaidi ya kuninyanyua na kuweka mkono wangu kwapani kwake tukawa tunaelekea nje, mvua bado ilikua inanyesha. Tulipokua tunakaribia kutoka kabisa tukamuona Mtu anakuja Mbio, tena akikimbia kwenye mvua, ikatubidi tujifiche nyuma ya Mlango wa kutokea

Yule Mtu alipofika, breki ya kwanza ilikua vyumbani kisha akamrudia yule Bodaboda aliyekuwa anagala gala. Akamuuliza kwa hasira

“Umefanya nini Mpuuzi wewe?” aliuliza kwa sauti ambayo niliitambua, ilikua ni sauti ya Mzee Mwinyimkuu. Nilishtuka na kupata nguvu, nilipokumbuka kuwa yeye ndiye mtesi wangu basi mkojo ulinibana. Ghafla tu nikajiona ni Binadamu ninayehitaji kujitetea

“Nenda, hatuwezi kuondoka wote. Kaiambie Dunia kuhusu huyu Mzee, kama nitarudi tutakutana na kama nitafia hapa basi Roho yangu itakua salama” alisema Abuu, roho iliniuma. Sikua na uwezo wa kuzungumza. Mdomo wangu wa juu na chini nilihisi kama vimeungana sababu nilikua na vidonda mdomoni hivyo kukaa kimya ndiyo yalikua maisha yangu.

Nikaitikia kwa kutumia kichwa kisha nikasimama kama Mzimu, Mungu akaamua kunikumbuka. Akanipa nguvu na ujasiri, alichotaka Abuu ni kumzuia Mzee Mwinyimkuu. Wakati naanza safari Mzee Mwinyimkuu akaja mbio nahisi alikua anaanza kutusaka, sijui alijuaje kuwa tunatoroka. Huyu Mzee alikua Mchawi haswa, aliponikaribia tayari Abuu alimdaka Mzee Mwinyimkuu wakaanza kupalangana, muda huo nami nikaanza kujivuta kuondoka pale taratibu hadi nikaingia kwenye mvua.

Ulikua mchana lakini anga lilikua na wingu la kutosha kiasi kwamba palikua na giza fulani isitoshe palikua Porini. Nilipopigwa na mvua nikapata nguvu ya kuanza kuchanganya Miguu yangu vizuri. Nikaanza kukimbia huku nikiyumba kama mlevi

Sijui nilikimbia umbali gani lakini nilikimbia bila kuangalia nyuma, nilikimbia sana hadi nilichoka kabisa nikaanguka na kupoteza fahamu zangu.

Nilirudisha fahamu na kuanza kujitambua nikiwa naburuzwa kwa kasi sana, watu walikua kama vile wamenizunguka. Walikua na mavazi ya kufanana, nilikua kwenye kitanda kiendacho kwa kasi mno, nikawasikia wakisema

“Apelekwe ICU Haraka sana, kazi ianze mara moja” niligundua nilikua Hospitalini, wale wauguzi walionekana kunikatia tamaa sababu nilikua na hali mbaya sana. Lakini mimi

mwenyewe nilijiona ni mzima wa Afya zote, mahali nilipokuwepo palikua ni hatari zaidi ya Kuzimu.

Chozi lilinibubujika nikafumba macho yangu huku nikimshukuru Mungu. Madaktari walifanya kazi yao kwa wiki tatu kuhakikisha najitambua zaidi, wakaniweka kwenye uangalizi maalum kwa kipindi chote hicho hadi nilipokumbuka yaliyonisibu.

Nikawaandikia jina Langu, mahali nilipotoka maana nilikua siwezi kuzungumza tena, Hospitali ikasambaza jina na taarifa zangu ndipo Mama yangu alipokuja Mbeya akiongozana na Ndugu wengine kunitambua. Mama alilia sana, sikuwahi kumuona Mama yangu akilia namna ile, yale Maisha yaliniathiri sana kisaikolojia. Nikapoteza uwezo wa kuzungumza kabisa. Taarifa ya Kifo cha Baba ilinihuzunisha mno, ikanitoa chozi.

Polisi walipokuja niliandika maelezo yangu, ilikua baada ya wiki sita. Mwezi mmoja na siku kadhaa, afya yangu ilianza kukaa sawa lakini sikuwa na Uwezo wa kuzungumza chochote isipokua kuandika. Polisi walinichukua ili nikawapeleke mahali nilipoteswa yaani nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu

Mimi na Mama tulienda, palikua ni pale pale kwa Mzee Mwinyimkuu. Namba ya nyumba ilikua ni ile ile, mazingira yale yale, chozi lilinibubujika sana hadi Mama akashindwa kujizuia.

Nilikua natembezwa kwenye kiti cha Walemavu maana bado miguu ilikua haipo sawa pia sikua na vidole nilikua najiuguza. Nikampa ishara Mama yangu kuwa anipeleke kwanza nyumba jirani, pale kwa muuza chapati, nilimkuta Mwanamke mwingine kabisa akitengeneza chapati, nikaandika kwenye karatasi

“Mama Ashura yupo wapi?” nilikua na ujumbe wa Mtoto wake Ashura nilitaka kwanza nimpe ujumbe, wakati huo polisi walikua wameizingira nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. Mama akamsomea yule Mwanamke, lakini cha ajabu eti akadai yeye ndiye Mama Ashura, nilishtuka alafu kingine kilichonipa mshituko ni kumuona Ashura mwenyewe, alikua ni Ashura yule yule niliyemuona Nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu

Haya mambo yalinifanya nianze kuonekana akili yangu bado haiko sawa, nikajitahidi kuwaambia kwa maandishi lakini niliishia kupewa pole tu, kisha nikapelekwa kwa Mzee Mwinyimkuu. Nako nikakutana na stori mpya kabisa

Kwanza ile nyumba si ya Mzee Mwinyimkuu, hawamfahamu. Wao wanaishi hapo Kwa Miaka mingi, nilitokwa na Mchozi, nyumba ile ile mazingira yale yale lakini stori tofauti. Nikaomba niingizwe ndani, nikapelekwa kwenye chumba nilichokuwa nalala

Nikakuta magunia ya vyakula, tena kilikua chumba chenye makorokoro mengi sana na hakikuonekana kua chumba cha kulala Mtu. Mama akaniambia

“Saida, najua umeteseka sana huku lakini hukumbuki chochote tena. Siku ukikumbuka nakuahidi tutarudi, yule Kijana na Baba yake watalipa” Kauli ya Mama yangu ilinimaliza akili yangu,

nilifikia hatua nikakubali kuwa akili yangu haipo sawa, inawezekanaje kila kitu kibadilike kwa haraka vile. Hakuna aliyeniamini

Lakini sasa wakati natoka nikajikuta nikipeleka macho yangu jikoni, nikaiona ile sufuria kubwa ambayo kwa mara ya kwanza nilipika mchicha mwingi, nikashtuka alafu nikauona Mchicha mwingi ukiwa kwenye Beseni. Kilichonishtua ni kwamba nilimuona Msichana wa umri wangu akiutengeneza.

Nilijikuta nikipiga yowe kali sana. Hali ya afya yangu ikawa sio nzuri nikarudishwa tena Hospitali. Tokea siku ile nilikua Msichana ninayekaa kimya hadi leo hii nawasimulia hiki kisa, sikumpata Mzee MwinyiMkuu wala Salehe, lakini sitakubali. Siku moja nitarudi Rukwa ili walipe kwa maumivu na mateso makali ninayoyapitia hadi sasa.

Kwasasa nimerudishwa kwetu Dar-es-salaam, niko Magomeni. Maisha yangu yamekuwa ya Ukimya sana, Sijazungumza tena tokea siku ile nilipozungumza kwa mara ya mwisho Rukwa, sijaandika chochote na wala sitaki kusema chochote kile ila kupitia mkasa huu nataka ujifunze.

Kamwe kwenye Maisha yako usiolewe au kuowa Mtu usiye mfahamu, Dunia ni Kichaka cha Mateso. Wasichana wengi wanayapitia mateso niliyoyapitia, wengi wanauawa, wengi wanapata ugonjwa wa akili. Hata wanaume wapo waliopoteza kila kitu, Siku nikifungua kinywa changu nitawasimulia mengi, kwasasa naishia hapa, naweka kalamu yangu chini.

AHSANTE……….MWISHO
Duuh hakika watu wanapitia mapito pole sana na pia Hongera..
Pia shukran kwa kutupatia kisa chako hakik kuna mamb mengi hatuyajui kuhusu watu.
 
Ilipoishia “Wala hakuongea chochote akaanza kuniandalia chakula nile, nilikua nahema kwa shida sana.

“Kunywa Maji” alisema, alikua haniangalii usoni, nilikua na kiu ya maji lakini kiu kubwa ilikua ni kumuuliza Nauawa lini, nilimuuliza

“Mnanimalizia lini nikapumzike?” Kiukweli sikuwa na afya nzuri, ndani ya siku chache nilikonda. Yule Bodaboda akanitazama kisha akaniambia

“Kifo ni siri ya Mungu, hakuna anayeijuwa kesho itakuwaje” alisema kisha akanipa maji, sikuwa na nguvu ya kushika kikombe akaninywesha. Jinsi alivyonihudumia alionesha anahitaji niwe hai. Endelea

SEHEMU YA NANE

Niliyafakamia yale maji kwanza hadi yalinipalia, halafu nikahema. Akanitolea vidonge vya kunituliza maumivu. Sikusita kumeza kiukweli maana nilikua na maumivu makali sana kisha nilimshika mkono nikamuuliza

“Ningekuwa mdogo wako ungenifanyia hivi, unajua najisikiaje Kaka?’’ Chozi lilikua linanibubujika bila kuacha, akaniondoa mkono wangu kwa kutumia mkono wake mwingine kisha akasimama, akaniambia

“Kula upate nguvu” hakuzungumza tena, alisimama kisha alipiga hatua lakini alipofika mlangoni alisimama. Kama kuna kitu alitaka kuniambia lakini alighaili, hakujibu swali langu aliondoka na kuufunga mlango kwa funguo, unajua hata kama angeuacha wazi sikuwa na nguvu ya kukimbia kwa namna nilivyokua sina nguvu.

Nilisikia akiondoka, nililia sana Mimi. Hakuna siku inapita bila kudondosha chozi langu, nilimpoteza Kaka Hamidu na nilijiona ni mkosaji, nilijilaumu sababu bila kuolewa na Salehe basi Kaka Hamidu angekuwa hai hadi sasa. Kidogo zile dawa zilipunguza maumivu ya mwili lakini siyo maumivu ya Moyo wangu

Haikuchukua hata dakika nyingi nilisikia yowe la Mwanaume mmoja, yowe lile lilisikika moja kwa moja kutoka kwenye ile nyumba niliyohifadhiwa Mimi. Moyo ulinilipuka, niliamini ilikua ni nyumba ya Mateso makali zaidi hata nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Nilisimama hata nguvu sikujuwa ilitokea wapi

Nilisogea mlangoni ili kuisikia zaidi ile sauti, ndiyo! Ilitoka ndani ya moja ya vyumba vya ile nyumba, nilitamani kupaza sauti ila sikujua alikua akifanywa nini. Nilijiuliza

“Nani yupo ndani ya hii nyumba, anamfanya nini huyu anayepiga yowe” Ilikua ni sawa na kujitekenya kisha kucheka mwenyewe, jibu lingetokea wapi ikiwa hata mimi mwenyewe sijui nipo wapi

Yule Mwanaume baada ya kupiga yowe alianza kusema

“Msaada,Nani yupo ananisikia?” aliendelea kusema hivi, nikapata picha huwenda hata yeye mwenyewe hajui amefikaje na Nani amemleta ndani ya hii nyumba. Kupitia dirishani nilianza kuona jua namna lilivyokuwa likifanya safari ya kwenda kupumzika baada ya kuipiga ardhi kwa siku nzima.

Namna nyumba hii ilivyo ilionekana kujengwa kwa ajili ya kazi ya kuhifadhi Binadamu, hata dirisha lake lilikua kama la Mahabusu, lilikua dogo lanye nondo,hapakuwa na taa ndani ya chumba kiasi kwamba giza litakapoingia basi patakuwa giza tupu. Nilijikuta nikikaa mwenyewe bila hata kuambiwa, kwa namna ilivyo hata ukipiga kelele vipi huwezi kupata Msaada wowote.

Kwanza sikujuwa Mtu yule alikua ni Nani, sauti yake haikufanana na ya Kaka Hamidu. Wala si ya Mtu niliyehisi kuwa niliwahi zungumza naye.

**

Usiku ulipoingia ndiyo nililiona joto la jiwe, niliandamwa na ndoto za ajabu hadi niliamka, siyo Mimi tu hata yule Mwanaume alikua akigugumia nahisi naye alikua kwenye hali kama yangu. Niliamka na kukaa kitako nikaegemea ukuta

Nikiwa hapo nilianza kuona nuru ya mwanga, ikianza taratibu hadi ikaenea chumba chote, hapa nilikua na uhakika kuwa haikuwa ndoto tena bali ni tukio halisi. Nilimuona tena yule Mtoto mdogo anayetisha, safari hii alinionesha sura yake, nilikua kwenye Mshangao wa hali ya juu sana

“Umeshindwa kutoka hapa, umeshindwa kujaribu kufanya chochote. Wewe ni Mtu wa aina gani, unataka kila Mtu afe kama Kaka yako Hamidu” Ooh! Jamani nilishtuka, kama ningekua nina presha kwa haya yote ningekuwa tayari nimepotea kwenye uso wa Dunia, namna alivyokua anaongea alionesha alikua na tumaini na Mimi kwenye jambo fulani hasa la kuokoa uhai wa wengine lakini Mimi mwenyewe nilikua nimeshajikatia tamaa. Japo nilijawa na woga lakini nilimuuliza

“Wewe ni Nani, umetokea wapi?” nilipomuuliza alidondosha chozi la damu, alikua Mtoto wa ajabu sana

“Mimi ni Ashura Mtoto wa Mama Muuza chapati. Nenda kamwambie Mama yangu kuwa bado naishi kwenye nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, Mimi sijafa” alisema kwa kupaza sauti kali ambayo ilinifanya nishindwe kuhimili zile kelele, pale pale nilijikuta nikiishiwa nguvu na kupoteza fahamu. Kitu pekee kilichobakia kwenye akili yangu ni ,kumbukumbu juu ya yule Mama anayeishi nyumba jirani na Mzee Mwinyimkuu, Mama aliyekuwa akiniuzia Chapati

Ndiyo‼ yeye ni Mama Ashura, nakumbuka alinitajia jina hili lakini sikuwahi kumuuliza huyo Ashura yupo wapi, huyu Mtoto wa ajabu alijitambulisha kwangu kama Ashura na alinitaka nimwambie Mama yake kuwa anaishi ndani ya nyumba ya Mzee Mwinyimkuu.

***

Baba yangu aliendelea kuumwa, Mama alikua anamuuguza huku akinitafuta Mimi kwa simu lakini aliendelea kutonipata, zilipita wiki mbili bila kupata mawasiliano yoyote yale. Salehe hakupatikana, hata Mzee Mwinyimkuu hakupatikana, Kaka Hamidu naye ilikua kama ndiyo

kichocheo kipya cha hofu kwa Familia yangu. Mara ya mwisho aliwaeleza anakuja kuonana na Mimi lakini baada ya hapo hawakujua kilichomfika na kupelekea kutopatikana kwenye simu kwa wiki mbili.

Vikafanyika vikao vya kututafuta Mimi na Kaka Hamidu maana hawakujua naishi Rukwa sehemu gani na pia Kaka Hamidu alikutwa na nini. Ni Mimi pekee ndiye niliyekuwa najua Kua Kaka Hamidu alikua ameuawa.

Familia ikamtuma Mjomba wetu aliyeitwa Kambona, alikua Mtu mzima na mwenye busara zake.

Akasafiri kutoka Dar-es-salaam hadi Rukwa akiwa na picha yangu, akaanza kunitafuta bila mafanikio kwa zaidi ya siku kumi. Mwishowe akaenda kituo cha Polisi maana sasa hakuna aliyekua na amani bila kujua tupo wapi, wote waliamini wakinipata Mimi watajua mahali alipo Kaka Hamidu maana mara ya mwisho aliwaambia anakuja kwangu. Polisi wakaanza kunitafuta kila kona ya Rukwa lakini hakuna aliyeweza kujua niko wapi, lakini kupitia jina la Mwinyimkuu Ambalo Salehe alilitaja alipokua ananichumbia, ikawawezesha kufika hadi nyumbani kwa huyu Mzee.

Hapa ndipo mahali ambapo nilikuwepo kabla ya kuhamishwa, nyumba hii ndimo alimouawa Kaka Hamidu tena kikatili sana na Mzee Mwinyimkuu. Walipofika walimkuta tena wala hakuwa na wasiwasi kabisa, najua alitumia akili sana kunihamisha vinginevyo polisi wangenikuta mle

“Wewe ndiye Mwinyimkuu?” aliuliza polisi baada ya salamu fupi

“Mnasemaje?” aliwauliza, alikua haogopi chochote wala Mtu yeyote yule, jeuri na katili mno “Saida anaishi hapa?” akauliza Polisi mmoja.

“Yeye ni Nani?” akawauliza

“Unajibu kwa dharau kiasi hicho Mzee, Saida ni Mpwa wangu Mimi. Ameolewa na Kijana anaitwa Salehe, upelelezi umeonesha kuwa ni Kijana wako huyo Salehe halafu unauliza ni Nani?” akaingilia kati mjomba Kambona na kumshika shati Mzee Mwinyimkuu, Polisi wakaokoa

“Unanivunjia heshiam si ndiyo?” akauliza Mzee Mwinyimkuu kwa hasira

“Siyo heshima tu, ntaivunja hata hii nyumba kama hutonipatia Saida wangu” Mjomba Kambona hakupoa kabisa, alijawa na hasira sana.

“Huyo Salehe unamfahamu?” Polisi wakamuuliza Mjomba Kambona

“Ndiyo, nimeozesha mwenyewe. Picha si hii hapa ya ndoa” akatoa picha, ile picha akapewa Mzee Mwinyimkuu.

“Umemtambua mtajwa pichani?” akauliza Polisi mmoja, Mzee Mwinyimkuu akaangua kicheko kisha akaita kwa sauti

“Salehe, hebu njoo uone maajabu ya Dunia” akaitikia Mtu kutokea ndani na kuwafanya Polisi na Mjomba Kambona wakae mkao wa kula kumuona Salehe. Ikachukua kama sekunde kadhaa tu Kijana mmoja akatoka ndani, Kijana aliyekuja hakufanana na Salehe wa kwenye picha.

“Unamfahamu Saida?” akauliza Mzee Mwinyimkuu akimuuliza huyo Kijana aliyemtambulisha kama Salehe, kiukweli hakuwa yule Salehe aliyeniowa kabisa yaani sura tofauti.

“Hapana, kuna nini?” akauliza huyo Salehe, kiukweli Mjomba Kambona alinywea. Lakini Polisi mmoja akasema

“Ongozana na Mimi Kijana” akamshika mkono Salehe na kwenda naye nje. Lengo la Polisi ni kutaka utambuzi kwa Majirani maana Upelelezi wao uliwaambia Salehe wa kwemye picha anapatikana kwa Mzee Mwinyimkuu. Wakafika hadi nyumbani kwa Mama Ashura maana ndipo palikua na Watu nje

Walipomuona Yule Kijana akiwa na Polisi vijana walikimbia hadi yule Polisi akashangaa, hata Mama Ashura naye alikua anataka kukimbia ila Polisi akamzuia Mama Ashura na Kumwambia asikimbie ana maswali kadhaa anataka kumuuliza, ndipo Mama Ashura akabakia lakini kwa hofu sana

“Unamtambua nani pichani?” Yule Polisi akampa picha yule Mama, Mama Ashura akaipokea picha japo kwa wasiwasi lakini alipoiangalia ile picha alishtuka sana, akameza funda la mate.

“Hapana’’akajibu lakini kwa hofu sana kiasi kwamba yule polisi akahisi pengine kuna jambo analificha. Kilichomshtua Mama Ashura ni kuniona Mimi kwenye ile picha ya ndoa ambayo Mjomba Kambona aliwapatia polisi

“Na huyu Kijana hapa?” akauliza Polisi, Mama Ashura akamtazama yule Kijana. Akaachia tabasamu la hofu kisha akajibu

“Ni Salehe, anaishi pale” akaonesha na kidole kabisa. Majibu haya yakamuacha yule polisi kinywa wazi, basi akarudi hadi nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Hakuna ushahidi wa anachosema Mjomba Kambona. Lakini Mjomba akawaaambia

“Nina namba ya huyu Mzee alikua anawasiliana na Mama yake Saida, hii namba nimepewa na Mama Saida. Jina ni hilo la Mwinyimkuu” akasema Mjomba japo kwa sauti ya kupoa, ikabidi Polisi waipige ile namba.

Ikapokelewa na Mtu mwingine kabisa tena Mwanamke akimuuliza yule Polisi Nani wewe? Yalikua kama maigizo ya Filamu lakini lilikua tukio la kweli, nyakati zote hizo Mzee Mwinyimkuu alikua akitabasamu akiwa anamtazama Mjomba Kambona.

“Mnaona anavyo nitazama, huyu anajua kila kitu” akasema Mjomba lakini hakuwa na ushahidi, maneno yake yalikua ni sawa na kuupaka upepo rangi. Muda wote Mzee katili alikua akitabasamu kwa mpango fulani ulio kichwani pake

Polisi walikosa ushahidi, ikaonekana kuwa Mjomba Kambona aliyakosea maelezo yake. Kibaya zaidi hata picha aliyowaonesha Polisi kuwa ndiye aliyeniowa ilikanwa kwa kuoneshwa Salehe mwingine na kilichotia nguvu kukosekana ushahidi ni maneno ya Mama Ashura. Angefanyaje Mjomba wangu zaidi ya kutoa kitambaa na kujifuta jasho ila moyoni aliamini Mzee Mwinyimkuu alikua anajua wapi nilipo, pia hapakua na ushahidi mwingine sababu Mzee Mwinyimkuu hakuhudhuria ndoa yangu

Polisi wakamwambia Mjomba Kambona

“Tutaendelea na Uchunguzi, kwasasa wewe liachie jeshi la Polisi. Tutakupa taarifa ya Uchunguzi juu ya Saida pia huyo Kaka yake” haikua kauli yenye matumaini, ilimvunja moyo sana Mjomba Kambona. Akamwambia Mzee Mwinyimkuu

“Saida hawezi kutoweka kirahisi, lipo unalolijua. Siondoki Rukwa hadi nihakikishe nampata Mpwa wangu” alisema hivyo kisha aliongozana na Polisi kuondoka, Salehe feki na Mzee Mwinyimkuu wakatazamana kisha wakawa wanawatazama namna Polisi na Mjomba Kambona walivyokuwa wanaondoka.

Wala hawakufika mbali, kabla hata hawajapanda kwenye gari ya Polisi. Mjomba Kambona alianguka na kufariki papo hapo akitokwa na Mapovu mdomoni. Licha ya jitihada za jeshi la polisi kumkimbiza Hospitali lakini alikua tayari amefariki

Taarifa ikarudi Dar-es-salaam kuwa Mtu waliyemtuma kuja kututafuta Mimi na Kaka Hamidu alikua tayari ameshafariki. Yalikua ni majonzi juu ya Majonzi, taarifa hii ilipomfikia Baba yangu alifariki pia kwa presha. Bundi aliizingira familia yangu, misiba miwili ndani ya siku moja, Mzee Mwinyimkuu akashinda tena kwa kishindo kikubwa sana.

**

Nilihesabu siku ambazo nilikua ndani ya ile nyumba ya mateso, zilitimia siku saba ngumu. Nilikonda nikawa kama Mtoto mdogo, niliishiwa nguvu. Kilichokuwa kimebakia kwangu ilikua ni kufa tu. Kila nilipoamka nilijikuta nimeshaondolewa kidole kimoja, pumua yangu ikawa ya

shida sana. Nikakosa uwezo wa kuwatambua Watu kirahisi, yule Bodaboda aliendelea kuniletea chakula kila siku lakini pia sauti ya Mwanaume mmoja kugumia ilikua ni sauti ya Kila siku

Lilikua ni jambo la kawaida sana yeye kupaza sauti, sikuwahi kufahamu alikua akipitia mateso gani, ila dakika za mwisho niligundua kuwa naye alikua akipelekewa chakula na huyu huyu Bodaboda anayeniletea Mimi chakula.

Sikuweza kusimama tena, vidonda vilianza kutoa funza sababu sikuwa na dawa yoyote isitoshe joto la mle ndani liliniathiri kwa kiasi kikubwa, Mwenzenu niliwahi kufika Jehannam nikiwa Hai.

Basi siku moja yule Bodaboda alikuja, siku yenyewe palikua na mvua kubwa. Aliingia akiwa ameloa sana anatetemeka kwa Baridi, japo nilikua katika nyakati za mwisho kabisa za uhai wangu lakini niliweza kugundua kuwa Baridi lilikua tatizo kubwa kwake. Alikua akiniandalia chakula huku akitetemeka nikagundua anasumbuliwa na tatizo linalo sababishwa na Baridi.

Akajikaza, akaniwekea chakula. Alipaswa kunilisha sababu Mimi nilikua siwezi tena hata kushika kijiko, nilikonda mno hadi mishipa ya Damu ilikua ikionekana. Akajitahidi kuniinua ili kunikalisha kitako niweze kuegemea ukuta anilishe vizuri, siku hii nilipanga kuacha kula ili nife mapema maana mateso yalinizidi kabisa, Jamani naposema nilikonda basi ujue nilikonda nikawa na kilo chache sana halafu kichwa kikawa kikubwa.

Nilitamani kumuuliza ana shida gani, huyu Mtu hakuwahi kunitesa wala hakuwahi kunisemea jambo baya isipokua alikua hajibu maswali yangu yote niliyokuwa namuuliza.

Hali yake ilianza kuwa mbaya, akashindwa hata kunishikilia akaanguka chini na kuanza kugala gala kwa maumivu Makali sana, mlango ulikuwa wazi hakuufunga sababu alipoingia alikua tayari ana hiyo hali ya Maumivu, niliona ni nafasi ya kutoroka lakini sikuwa na akiba yoyote ya nguvu iliyobakia

Nikatamani kuendelea kuishi ghafla tu, namna pekee ya kuendelea kuwa hai ni kutoroka. Huko nje mvua ilikua ikinyesha na kusababisha kelele kubwa sana kwenye Bati. Sikuwa na nguvu ya kusimama, nikaona ni bora nijiburuze nione kama naweza kufika nje

Yule Bodaboda alipoona naanza kujiburuza akajua nataka kumtoroka, akili yake ikatamani anizuie lakini mwili ulimsaliti, nguvu zilimwisha akiwa sakafuni anapumua kwa shida sana. Nikaendelea kujivuta taratibu huku nikiwa ninasali Mungu niliyemkatia tamaa azidi kunipa nguvu, unajua kwanini niliamini naweza kuondoka pale?

Kwasababu hapakua na mtu mwingine aliyekuwa anakuja isipokua yeye, hivyo hakuna tena wa kunizuia, halafu niliwaza kufika chumba ambacho yule Mwanaume anagumia ili kama yeye ana nguvu tusaidiane kutoroka.

Nilijiburuza kama nyoka hadi nilipotoka nje ya chumba kile, palikua na funguo kwenye kitasa. Nikapata akili ya dharura kuwa huwenda funguo ile inaweza nisaidia kufungua milango mingine

maana ilikua na funguo tatu zilizowekwa sehemu moja, naipataje Funguo ni lazima nisimame niichomoe

Kivumbi kilianzia hapo, nilikonda Mimi kiasi kwamba upepo unaweza nipeperusha, Malaika Mtoa roho alikua amenisimamia akiniuliza nasimama au achukue roho yangu, sijui nguvu zilitoka wapi nikasimama kwa kuyumba huku nikitetemeka. Nikachomoa funguo, ile nataka kupiga hatua nikaanguka

Basi nikagugumia kwa maumivu, nilihitaji kufanya haraka maana kama yule Bodaboda atapata nguvu basi sitaweza tena kuondoka, nikamkumbuka Mama na Baba yangu, nikamkumbuka Kaka Hamidu. Ghafla nguvu zikaamka

Nikajikaza na kuanza kujiburuza sakafuni kama nyoka vile, kwa mwendo huo huo nilijikuta nikikiacha chumba kwa mbali kidogo, sikuufunga ule mlango wa chumba nilichomuacha Bodaboda.

Basi nilipofika kama chumba cha tano hivi nikasikia Mtu akiugonga mlango kwa nguvu huku akisema

“Njoo unitoe humu Mshenzi wewe, mtauwa wangapi. Siku ikifika mtakufa kama Kuku” alisema kwa hisia sana lakini hakujuwa kuwa Mimi nilikua tayari nipo mlangoni. Mlango ulikua umefungwa, korido lilikuwa refu halafu vyumba vilikua mbali mbali. Nilijitahidi sana kusimama nifungue mlango lakini nilikua nakosa nguvu, nilijaribu kama mara tatu lakini niliishia kuanguka

Wakati nikiwa nimeanguka nikageuka nyuma, ndipo nilipomuona yule Bodaboda akijikongoja kwa maumivu kuja nilipo, alikua amelishikilia tumbo lake. Hapo sasa yule Malaika mtoa roho nikamuona kama anachukua koleo kwa ajili ya kuichukua roho yangu.

Sauti ya yule Mwanaume ilizidi kusema, kibaya zaidi Mimi ndiye mwenye funguo halafu sauti yangu ilikua haitoki. Nikasema kama sisimami basi siondoki. Yule Bodaboda akawa anazidi kuja upande wangu kwa kasi akionekana kuanza kupiga hatua za nguvu. Nikamtaja Mungu nikasema

“Mungu nipe nguvu niishinde hii vita” nikajivuta haraka nikasimama nikiwa ninayumba, nikaanza kusaka tundu la kuweka funguo maana nguvu yenye ilikua sifuri, nikawa najitahidi huku nikiwa natetemeka. Mara naingiza mara nakosea, huku yule Bodaboda akizidi kunisogelea, hata nilipopaatia nilikua nimeingiza funguo isiyo yake.

Akawa karibu zaidi kiasi kwamba akipiga hatua tatu anakuwa amenifikia na kunizuia kuufungua mlango, nikapapasia kwa bahati nzuri nikapatia funguo nikavuta nguvu za mwisho nikatekenya kitasa lakini tayari Bodaboda alikua ameshanivaa na kuniangusha chini, Bahati nzuri ule mlango ulikua tayari umeshafunguka

Akatoka mwanaume mmoja na kuanza kumkita mateke yule Bodaboda hadi akamtupilia mbali huko akiwa hoi sana anatokwa na damu mdomoni, eneo la Korido lilikua linawaka taa isipokua

vyumbani tu. Sikuamini macho yangu Mtu ambaye nilikuja kumuona na kumtambua japo nilimuona mara moja tu

Alikua ni yule Mwanaume niliyemuazimaga simu kule Buchani, Ndio! Ni Abuu, masikini naye alikua mateka wa Mzee Mwinyimkuu baada ya kujulikana ananifuatilia Mimi, kwa muda mfupi naye alikua amepungua sana japo alikua na nguvu.

Hakuniuliza chochote zaidi ya kuninyanyua na kuweka mkono wangu kwapani kwake tukawa tunaelekea nje, mvua bado ilikua inanyesha. Tulipokua tunakaribia kutoka kabisa tukamuona Mtu anakuja Mbio, tena akikimbia kwenye mvua, ikatubidi tujifiche nyuma ya Mlango wa kutokea

Yule Mtu alipofika, breki ya kwanza ilikua vyumbani kisha akamrudia yule Bodaboda aliyekuwa anagala gala. Akamuuliza kwa hasira

“Umefanya nini Mpuuzi wewe?” aliuliza kwa sauti ambayo niliitambua, ilikua ni sauti ya Mzee Mwinyimkuu. Nilishtuka na kupata nguvu, nilipokumbuka kuwa yeye ndiye mtesi wangu basi mkojo ulinibana. Ghafla tu nikajiona ni Binadamu ninayehitaji kujitetea

“Nenda, hatuwezi kuondoka wote. Kaiambie Dunia kuhusu huyu Mzee, kama nitarudi tutakutana na kama nitafia hapa basi Roho yangu itakua salama” alisema Abuu, roho iliniuma. Sikua na uwezo wa kuzungumza. Mdomo wangu wa juu na chini nilihisi kama vimeungana sababu nilikua na vidonda mdomoni hivyo kukaa kimya ndiyo yalikua maisha yangu.

Nikaitikia kwa kutumia kichwa kisha nikasimama kama Mzimu, Mungu akaamua kunikumbuka. Akanipa nguvu na ujasiri, alichotaka Abuu ni kumzuia Mzee Mwinyimkuu. Wakati naanza safari Mzee Mwinyimkuu akaja mbio nahisi alikua anaanza kutusaka, sijui alijuaje kuwa tunatoroka. Huyu Mzee alikua Mchawi haswa, aliponikaribia tayari Abuu alimdaka Mzee Mwinyimkuu wakaanza kupalangana, muda huo nami nikaanza kujivuta kuondoka pale taratibu hadi nikaingia kwenye mvua.

Ulikua mchana lakini anga lilikua na wingu la kutosha kiasi kwamba palikua na giza fulani isitoshe palikua Porini. Nilipopigwa na mvua nikapata nguvu ya kuanza kuchanganya Miguu yangu vizuri. Nikaanza kukimbia huku nikiyumba kama mlevi

Sijui nilikimbia umbali gani lakini nilikimbia bila kuangalia nyuma, nilikimbia sana hadi nilichoka kabisa nikaanguka na kupoteza fahamu zangu.

Nilirudisha fahamu na kuanza kujitambua nikiwa naburuzwa kwa kasi sana, watu walikua kama vile wamenizunguka. Walikua na mavazi ya kufanana, nilikua kwenye kitanda kiendacho kwa kasi mno, nikawasikia wakisema

“Apelekwe ICU Haraka sana, kazi ianze mara moja” niligundua nilikua Hospitalini, wale wauguzi walionekana kunikatia tamaa sababu nilikua na hali mbaya sana. Lakini mimi

mwenyewe nilijiona ni mzima wa Afya zote, mahali nilipokuwepo palikua ni hatari zaidi ya Kuzimu.

Chozi lilinibubujika nikafumba macho yangu huku nikimshukuru Mungu. Madaktari walifanya kazi yao kwa wiki tatu kuhakikisha najitambua zaidi, wakaniweka kwenye uangalizi maalum kwa kipindi chote hicho hadi nilipokumbuka yaliyonisibu.

Nikawaandikia jina Langu, mahali nilipotoka maana nilikua siwezi kuzungumza tena, Hospitali ikasambaza jina na taarifa zangu ndipo Mama yangu alipokuja Mbeya akiongozana na Ndugu wengine kunitambua. Mama alilia sana, sikuwahi kumuona Mama yangu akilia namna ile, yale Maisha yaliniathiri sana kisaikolojia. Nikapoteza uwezo wa kuzungumza kabisa. Taarifa ya Kifo cha Baba ilinihuzunisha mno, ikanitoa chozi.

Polisi walipokuja niliandika maelezo yangu, ilikua baada ya wiki sita. Mwezi mmoja na siku kadhaa, afya yangu ilianza kukaa sawa lakini sikuwa na Uwezo wa kuzungumza chochote isipokua kuandika. Polisi walinichukua ili nikawapeleke mahali nilipoteswa yaani nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu

Mimi na Mama tulienda, palikua ni pale pale kwa Mzee Mwinyimkuu. Namba ya nyumba ilikua ni ile ile, mazingira yale yale, chozi lilinibubujika sana hadi Mama akashindwa kujizuia.

Nilikua natembezwa kwenye kiti cha Walemavu maana bado miguu ilikua haipo sawa pia sikua na vidole nilikua najiuguza. Nikampa ishara Mama yangu kuwa anipeleke kwanza nyumba jirani, pale kwa muuza chapati, nilimkuta Mwanamke mwingine kabisa akitengeneza chapati, nikaandika kwenye karatasi

“Mama Ashura yupo wapi?” nilikua na ujumbe wa Mtoto wake Ashura nilitaka kwanza nimpe ujumbe, wakati huo polisi walikua wameizingira nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. Mama akamsomea yule Mwanamke, lakini cha ajabu eti akadai yeye ndiye Mama Ashura, nilishtuka alafu kingine kilichonipa mshituko ni kumuona Ashura mwenyewe, alikua ni Ashura yule yule niliyemuona Nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu

Haya mambo yalinifanya nianze kuonekana akili yangu bado haiko sawa, nikajitahidi kuwaambia kwa maandishi lakini niliishia kupewa pole tu, kisha nikapelekwa kwa Mzee Mwinyimkuu. Nako nikakutana na stori mpya kabisa

Kwanza ile nyumba si ya Mzee Mwinyimkuu, hawamfahamu. Wao wanaishi hapo Kwa Miaka mingi, nilitokwa na Mchozi, nyumba ile ile mazingira yale yale lakini stori tofauti. Nikaomba niingizwe ndani, nikapelekwa kwenye chumba nilichokuwa nalala

Nikakuta magunia ya vyakula, tena kilikua chumba chenye makorokoro mengi sana na hakikuonekana kua chumba cha kulala Mtu. Mama akaniambia

“Saida, najua umeteseka sana huku lakini hukumbuki chochote tena. Siku ukikumbuka nakuahidi tutarudi, yule Kijana na Baba yake watalipa” Kauli ya Mama yangu ilinimaliza akili yangu,

nilifikia hatua nikakubali kuwa akili yangu haipo sawa, inawezekanaje kila kitu kibadilike kwa haraka vile. Hakuna aliyeniamini

Lakini sasa wakati natoka nikajikuta nikipeleka macho yangu jikoni, nikaiona ile sufuria kubwa ambayo kwa mara ya kwanza nilipika mchicha mwingi, nikashtuka alafu nikauona Mchicha mwingi ukiwa kwenye Beseni. Kilichonishtua ni kwamba nilimuona Msichana wa umri wangu akiutengeneza.

Nilijikuta nikipiga yowe kali sana. Hali ya afya yangu ikawa sio nzuri nikarudishwa tena Hospitali. Tokea siku ile nilikua Msichana ninayekaa kimya hadi leo hii nawasimulia hiki kisa, sikumpata Mzee MwinyiMkuu wala Salehe, lakini sitakubali. Siku moja nitarudi Rukwa ili walipe kwa maumivu na mateso makali ninayoyapitia hadi sasa.

Kwasasa nimerudishwa kwetu Dar-es-salaam, niko Magomeni. Maisha yangu yamekuwa ya Ukimya sana, Sijazungumza tena tokea siku ile nilipozungumza kwa mara ya mwisho Rukwa, sijaandika chochote na wala sitaki kusema chochote kile ila kupitia mkasa huu nataka ujifunze.

Kamwe kwenye Maisha yako usiolewe au kuowa Mtu usiye mfahamu, Dunia ni Kichaka cha Mateso. Wasichana wengi wanayapitia mateso niliyoyapitia, wengi wanauawa, wengi wanapata ugonjwa wa akili. Hata wanaume wapo waliopoteza kila kitu, Siku nikifungua kinywa changu nitawasimulia mengi, kwasasa naishia hapa, naweka kalamu yangu chini.

AHSANTE……….MWISHO
Funzo kuu hili 🙌🏼
 
Ilipoishia “Wala hakuongea chochote akaanza kuniandalia chakula nile, nilikua nahema kwa shida sana.

“Kunywa Maji” alisema, alikua haniangalii usoni, nilikua na kiu ya maji lakini kiu kubwa ilikua ni kumuuliza Nauawa lini, nilimuuliza

“Mnanimalizia lini nikapumzike?” Kiukweli sikuwa na afya nzuri, ndani ya siku chache nilikonda. Yule Bodaboda akanitazama kisha akaniambia

“Kifo ni siri ya Mungu, hakuna anayeijuwa kesho itakuwaje” alisema kisha akanipa maji, sikuwa na nguvu ya kushika kikombe akaninywesha. Jinsi alivyonihudumia alionesha anahitaji niwe hai. Endelea

SEHEMU YA NANE

Niliyafakamia yale maji kwanza hadi yalinipalia, halafu nikahema. Akanitolea vidonge vya kunituliza maumivu. Sikusita kumeza kiukweli maana nilikua na maumivu makali sana kisha nilimshika mkono nikamuuliza

“Ningekuwa mdogo wako ungenifanyia hivi, unajua najisikiaje Kaka?’’ Chozi lilikua linanibubujika bila kuacha, akaniondoa mkono wangu kwa kutumia mkono wake mwingine kisha akasimama, akaniambia

“Kula upate nguvu” hakuzungumza tena, alisimama kisha alipiga hatua lakini alipofika mlangoni alisimama. Kama kuna kitu alitaka kuniambia lakini alighaili, hakujibu swali langu aliondoka na kuufunga mlango kwa funguo, unajua hata kama angeuacha wazi sikuwa na nguvu ya kukimbia kwa namna nilivyokua sina nguvu.

Nilisikia akiondoka, nililia sana Mimi. Hakuna siku inapita bila kudondosha chozi langu, nilimpoteza Kaka Hamidu na nilijiona ni mkosaji, nilijilaumu sababu bila kuolewa na Salehe basi Kaka Hamidu angekuwa hai hadi sasa. Kidogo zile dawa zilipunguza maumivu ya mwili lakini siyo maumivu ya Moyo wangu

Haikuchukua hata dakika nyingi nilisikia yowe la Mwanaume mmoja, yowe lile lilisikika moja kwa moja kutoka kwenye ile nyumba niliyohifadhiwa Mimi. Moyo ulinilipuka, niliamini ilikua ni nyumba ya Mateso makali zaidi hata nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Nilisimama hata nguvu sikujuwa ilitokea wapi

Nilisogea mlangoni ili kuisikia zaidi ile sauti, ndiyo! Ilitoka ndani ya moja ya vyumba vya ile nyumba, nilitamani kupaza sauti ila sikujua alikua akifanywa nini. Nilijiuliza

“Nani yupo ndani ya hii nyumba, anamfanya nini huyu anayepiga yowe” Ilikua ni sawa na kujitekenya kisha kucheka mwenyewe, jibu lingetokea wapi ikiwa hata mimi mwenyewe sijui nipo wapi

Yule Mwanaume baada ya kupiga yowe alianza kusema

“Msaada,Nani yupo ananisikia?” aliendelea kusema hivi, nikapata picha huwenda hata yeye mwenyewe hajui amefikaje na Nani amemleta ndani ya hii nyumba. Kupitia dirishani nilianza kuona jua namna lilivyokuwa likifanya safari ya kwenda kupumzika baada ya kuipiga ardhi kwa siku nzima.

Namna nyumba hii ilivyo ilionekana kujengwa kwa ajili ya kazi ya kuhifadhi Binadamu, hata dirisha lake lilikua kama la Mahabusu, lilikua dogo lanye nondo,hapakuwa na taa ndani ya chumba kiasi kwamba giza litakapoingia basi patakuwa giza tupu. Nilijikuta nikikaa mwenyewe bila hata kuambiwa, kwa namna ilivyo hata ukipiga kelele vipi huwezi kupata Msaada wowote.

Kwanza sikujuwa Mtu yule alikua ni Nani, sauti yake haikufanana na ya Kaka Hamidu. Wala si ya Mtu niliyehisi kuwa niliwahi zungumza naye.

**

Usiku ulipoingia ndiyo nililiona joto la jiwe, niliandamwa na ndoto za ajabu hadi niliamka, siyo Mimi tu hata yule Mwanaume alikua akigugumia nahisi naye alikua kwenye hali kama yangu. Niliamka na kukaa kitako nikaegemea ukuta

Nikiwa hapo nilianza kuona nuru ya mwanga, ikianza taratibu hadi ikaenea chumba chote, hapa nilikua na uhakika kuwa haikuwa ndoto tena bali ni tukio halisi. Nilimuona tena yule Mtoto mdogo anayetisha, safari hii alinionesha sura yake, nilikua kwenye Mshangao wa hali ya juu sana

“Umeshindwa kutoka hapa, umeshindwa kujaribu kufanya chochote. Wewe ni Mtu wa aina gani, unataka kila Mtu afe kama Kaka yako Hamidu” Ooh! Jamani nilishtuka, kama ningekua nina presha kwa haya yote ningekuwa tayari nimepotea kwenye uso wa Dunia, namna alivyokua anaongea alionesha alikua na tumaini na Mimi kwenye jambo fulani hasa la kuokoa uhai wa wengine lakini Mimi mwenyewe nilikua nimeshajikatia tamaa. Japo nilijawa na woga lakini nilimuuliza

“Wewe ni Nani, umetokea wapi?” nilipomuuliza alidondosha chozi la damu, alikua Mtoto wa ajabu sana

“Mimi ni Ashura Mtoto wa Mama Muuza chapati. Nenda kamwambie Mama yangu kuwa bado naishi kwenye nyumba ya Mzee Mwinyimkuu, Mimi sijafa” alisema kwa kupaza sauti kali ambayo ilinifanya nishindwe kuhimili zile kelele, pale pale nilijikuta nikiishiwa nguvu na kupoteza fahamu. Kitu pekee kilichobakia kwenye akili yangu ni ,kumbukumbu juu ya yule Mama anayeishi nyumba jirani na Mzee Mwinyimkuu, Mama aliyekuwa akiniuzia Chapati

Ndiyo‼ yeye ni Mama Ashura, nakumbuka alinitajia jina hili lakini sikuwahi kumuuliza huyo Ashura yupo wapi, huyu Mtoto wa ajabu alijitambulisha kwangu kama Ashura na alinitaka nimwambie Mama yake kuwa anaishi ndani ya nyumba ya Mzee Mwinyimkuu.

***

Baba yangu aliendelea kuumwa, Mama alikua anamuuguza huku akinitafuta Mimi kwa simu lakini aliendelea kutonipata, zilipita wiki mbili bila kupata mawasiliano yoyote yale. Salehe hakupatikana, hata Mzee Mwinyimkuu hakupatikana, Kaka Hamidu naye ilikua kama ndiyo

kichocheo kipya cha hofu kwa Familia yangu. Mara ya mwisho aliwaeleza anakuja kuonana na Mimi lakini baada ya hapo hawakujua kilichomfika na kupelekea kutopatikana kwenye simu kwa wiki mbili.

Vikafanyika vikao vya kututafuta Mimi na Kaka Hamidu maana hawakujua naishi Rukwa sehemu gani na pia Kaka Hamidu alikutwa na nini. Ni Mimi pekee ndiye niliyekuwa najua Kua Kaka Hamidu alikua ameuawa.

Familia ikamtuma Mjomba wetu aliyeitwa Kambona, alikua Mtu mzima na mwenye busara zake.

Akasafiri kutoka Dar-es-salaam hadi Rukwa akiwa na picha yangu, akaanza kunitafuta bila mafanikio kwa zaidi ya siku kumi. Mwishowe akaenda kituo cha Polisi maana sasa hakuna aliyekua na amani bila kujua tupo wapi, wote waliamini wakinipata Mimi watajua mahali alipo Kaka Hamidu maana mara ya mwisho aliwaambia anakuja kwangu. Polisi wakaanza kunitafuta kila kona ya Rukwa lakini hakuna aliyeweza kujua niko wapi, lakini kupitia jina la Mwinyimkuu Ambalo Salehe alilitaja alipokua ananichumbia, ikawawezesha kufika hadi nyumbani kwa huyu Mzee.

Hapa ndipo mahali ambapo nilikuwepo kabla ya kuhamishwa, nyumba hii ndimo alimouawa Kaka Hamidu tena kikatili sana na Mzee Mwinyimkuu. Walipofika walimkuta tena wala hakuwa na wasiwasi kabisa, najua alitumia akili sana kunihamisha vinginevyo polisi wangenikuta mle

“Wewe ndiye Mwinyimkuu?” aliuliza polisi baada ya salamu fupi

“Mnasemaje?” aliwauliza, alikua haogopi chochote wala Mtu yeyote yule, jeuri na katili mno “Saida anaishi hapa?” akauliza Polisi mmoja.

“Yeye ni Nani?” akawauliza

“Unajibu kwa dharau kiasi hicho Mzee, Saida ni Mpwa wangu Mimi. Ameolewa na Kijana anaitwa Salehe, upelelezi umeonesha kuwa ni Kijana wako huyo Salehe halafu unauliza ni Nani?” akaingilia kati mjomba Kambona na kumshika shati Mzee Mwinyimkuu, Polisi wakaokoa

“Unanivunjia heshiam si ndiyo?” akauliza Mzee Mwinyimkuu kwa hasira

“Siyo heshima tu, ntaivunja hata hii nyumba kama hutonipatia Saida wangu” Mjomba Kambona hakupoa kabisa, alijawa na hasira sana.

“Huyo Salehe unamfahamu?” Polisi wakamuuliza Mjomba Kambona

“Ndiyo, nimeozesha mwenyewe. Picha si hii hapa ya ndoa” akatoa picha, ile picha akapewa Mzee Mwinyimkuu.

“Umemtambua mtajwa pichani?” akauliza Polisi mmoja, Mzee Mwinyimkuu akaangua kicheko kisha akaita kwa sauti

“Salehe, hebu njoo uone maajabu ya Dunia” akaitikia Mtu kutokea ndani na kuwafanya Polisi na Mjomba Kambona wakae mkao wa kula kumuona Salehe. Ikachukua kama sekunde kadhaa tu Kijana mmoja akatoka ndani, Kijana aliyekuja hakufanana na Salehe wa kwenye picha.

“Unamfahamu Saida?” akauliza Mzee Mwinyimkuu akimuuliza huyo Kijana aliyemtambulisha kama Salehe, kiukweli hakuwa yule Salehe aliyeniowa kabisa yaani sura tofauti.

“Hapana, kuna nini?” akauliza huyo Salehe, kiukweli Mjomba Kambona alinywea. Lakini Polisi mmoja akasema

“Ongozana na Mimi Kijana” akamshika mkono Salehe na kwenda naye nje. Lengo la Polisi ni kutaka utambuzi kwa Majirani maana Upelelezi wao uliwaambia Salehe wa kwemye picha anapatikana kwa Mzee Mwinyimkuu. Wakafika hadi nyumbani kwa Mama Ashura maana ndipo palikua na Watu nje

Walipomuona Yule Kijana akiwa na Polisi vijana walikimbia hadi yule Polisi akashangaa, hata Mama Ashura naye alikua anataka kukimbia ila Polisi akamzuia Mama Ashura na Kumwambia asikimbie ana maswali kadhaa anataka kumuuliza, ndipo Mama Ashura akabakia lakini kwa hofu sana

“Unamtambua nani pichani?” Yule Polisi akampa picha yule Mama, Mama Ashura akaipokea picha japo kwa wasiwasi lakini alipoiangalia ile picha alishtuka sana, akameza funda la mate.

“Hapana’’akajibu lakini kwa hofu sana kiasi kwamba yule polisi akahisi pengine kuna jambo analificha. Kilichomshtua Mama Ashura ni kuniona Mimi kwenye ile picha ya ndoa ambayo Mjomba Kambona aliwapatia polisi

“Na huyu Kijana hapa?” akauliza Polisi, Mama Ashura akamtazama yule Kijana. Akaachia tabasamu la hofu kisha akajibu

“Ni Salehe, anaishi pale” akaonesha na kidole kabisa. Majibu haya yakamuacha yule polisi kinywa wazi, basi akarudi hadi nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu. Hakuna ushahidi wa anachosema Mjomba Kambona. Lakini Mjomba akawaaambia

“Nina namba ya huyu Mzee alikua anawasiliana na Mama yake Saida, hii namba nimepewa na Mama Saida. Jina ni hilo la Mwinyimkuu” akasema Mjomba japo kwa sauti ya kupoa, ikabidi Polisi waipige ile namba.

Ikapokelewa na Mtu mwingine kabisa tena Mwanamke akimuuliza yule Polisi Nani wewe? Yalikua kama maigizo ya Filamu lakini lilikua tukio la kweli, nyakati zote hizo Mzee Mwinyimkuu alikua akitabasamu akiwa anamtazama Mjomba Kambona.

“Mnaona anavyo nitazama, huyu anajua kila kitu” akasema Mjomba lakini hakuwa na ushahidi, maneno yake yalikua ni sawa na kuupaka upepo rangi. Muda wote Mzee katili alikua akitabasamu kwa mpango fulani ulio kichwani pake

Polisi walikosa ushahidi, ikaonekana kuwa Mjomba Kambona aliyakosea maelezo yake. Kibaya zaidi hata picha aliyowaonesha Polisi kuwa ndiye aliyeniowa ilikanwa kwa kuoneshwa Salehe mwingine na kilichotia nguvu kukosekana ushahidi ni maneno ya Mama Ashura. Angefanyaje Mjomba wangu zaidi ya kutoa kitambaa na kujifuta jasho ila moyoni aliamini Mzee Mwinyimkuu alikua anajua wapi nilipo, pia hapakua na ushahidi mwingine sababu Mzee Mwinyimkuu hakuhudhuria ndoa yangu

Polisi wakamwambia Mjomba Kambona

“Tutaendelea na Uchunguzi, kwasasa wewe liachie jeshi la Polisi. Tutakupa taarifa ya Uchunguzi juu ya Saida pia huyo Kaka yake” haikua kauli yenye matumaini, ilimvunja moyo sana Mjomba Kambona. Akamwambia Mzee Mwinyimkuu

“Saida hawezi kutoweka kirahisi, lipo unalolijua. Siondoki Rukwa hadi nihakikishe nampata Mpwa wangu” alisema hivyo kisha aliongozana na Polisi kuondoka, Salehe feki na Mzee Mwinyimkuu wakatazamana kisha wakawa wanawatazama namna Polisi na Mjomba Kambona walivyokuwa wanaondoka.

Wala hawakufika mbali, kabla hata hawajapanda kwenye gari ya Polisi. Mjomba Kambona alianguka na kufariki papo hapo akitokwa na Mapovu mdomoni. Licha ya jitihada za jeshi la polisi kumkimbiza Hospitali lakini alikua tayari amefariki

Taarifa ikarudi Dar-es-salaam kuwa Mtu waliyemtuma kuja kututafuta Mimi na Kaka Hamidu alikua tayari ameshafariki. Yalikua ni majonzi juu ya Majonzi, taarifa hii ilipomfikia Baba yangu alifariki pia kwa presha. Bundi aliizingira familia yangu, misiba miwili ndani ya siku moja, Mzee Mwinyimkuu akashinda tena kwa kishindo kikubwa sana.

**

Nilihesabu siku ambazo nilikua ndani ya ile nyumba ya mateso, zilitimia siku saba ngumu. Nilikonda nikawa kama Mtoto mdogo, niliishiwa nguvu. Kilichokuwa kimebakia kwangu ilikua ni kufa tu. Kila nilipoamka nilijikuta nimeshaondolewa kidole kimoja, pumua yangu ikawa ya

shida sana. Nikakosa uwezo wa kuwatambua Watu kirahisi, yule Bodaboda aliendelea kuniletea chakula kila siku lakini pia sauti ya Mwanaume mmoja kugumia ilikua ni sauti ya Kila siku

Lilikua ni jambo la kawaida sana yeye kupaza sauti, sikuwahi kufahamu alikua akipitia mateso gani, ila dakika za mwisho niligundua kuwa naye alikua akipelekewa chakula na huyu huyu Bodaboda anayeniletea Mimi chakula.

Sikuweza kusimama tena, vidonda vilianza kutoa funza sababu sikuwa na dawa yoyote isitoshe joto la mle ndani liliniathiri kwa kiasi kikubwa, Mwenzenu niliwahi kufika Jehannam nikiwa Hai.

Basi siku moja yule Bodaboda alikuja, siku yenyewe palikua na mvua kubwa. Aliingia akiwa ameloa sana anatetemeka kwa Baridi, japo nilikua katika nyakati za mwisho kabisa za uhai wangu lakini niliweza kugundua kuwa Baridi lilikua tatizo kubwa kwake. Alikua akiniandalia chakula huku akitetemeka nikagundua anasumbuliwa na tatizo linalo sababishwa na Baridi.

Akajikaza, akaniwekea chakula. Alipaswa kunilisha sababu Mimi nilikua siwezi tena hata kushika kijiko, nilikonda mno hadi mishipa ya Damu ilikua ikionekana. Akajitahidi kuniinua ili kunikalisha kitako niweze kuegemea ukuta anilishe vizuri, siku hii nilipanga kuacha kula ili nife mapema maana mateso yalinizidi kabisa, Jamani naposema nilikonda basi ujue nilikonda nikawa na kilo chache sana halafu kichwa kikawa kikubwa.

Nilitamani kumuuliza ana shida gani, huyu Mtu hakuwahi kunitesa wala hakuwahi kunisemea jambo baya isipokua alikua hajibu maswali yangu yote niliyokuwa namuuliza.

Hali yake ilianza kuwa mbaya, akashindwa hata kunishikilia akaanguka chini na kuanza kugala gala kwa maumivu Makali sana, mlango ulikuwa wazi hakuufunga sababu alipoingia alikua tayari ana hiyo hali ya Maumivu, niliona ni nafasi ya kutoroka lakini sikuwa na akiba yoyote ya nguvu iliyobakia

Nikatamani kuendelea kuishi ghafla tu, namna pekee ya kuendelea kuwa hai ni kutoroka. Huko nje mvua ilikua ikinyesha na kusababisha kelele kubwa sana kwenye Bati. Sikuwa na nguvu ya kusimama, nikaona ni bora nijiburuze nione kama naweza kufika nje

Yule Bodaboda alipoona naanza kujiburuza akajua nataka kumtoroka, akili yake ikatamani anizuie lakini mwili ulimsaliti, nguvu zilimwisha akiwa sakafuni anapumua kwa shida sana. Nikaendelea kujivuta taratibu huku nikiwa ninasali Mungu niliyemkatia tamaa azidi kunipa nguvu, unajua kwanini niliamini naweza kuondoka pale?

Kwasababu hapakua na mtu mwingine aliyekuwa anakuja isipokua yeye, hivyo hakuna tena wa kunizuia, halafu niliwaza kufika chumba ambacho yule Mwanaume anagumia ili kama yeye ana nguvu tusaidiane kutoroka.

Nilijiburuza kama nyoka hadi nilipotoka nje ya chumba kile, palikua na funguo kwenye kitasa. Nikapata akili ya dharura kuwa huwenda funguo ile inaweza nisaidia kufungua milango mingine

maana ilikua na funguo tatu zilizowekwa sehemu moja, naipataje Funguo ni lazima nisimame niichomoe

Kivumbi kilianzia hapo, nilikonda Mimi kiasi kwamba upepo unaweza nipeperusha, Malaika Mtoa roho alikua amenisimamia akiniuliza nasimama au achukue roho yangu, sijui nguvu zilitoka wapi nikasimama kwa kuyumba huku nikitetemeka. Nikachomoa funguo, ile nataka kupiga hatua nikaanguka

Basi nikagugumia kwa maumivu, nilihitaji kufanya haraka maana kama yule Bodaboda atapata nguvu basi sitaweza tena kuondoka, nikamkumbuka Mama na Baba yangu, nikamkumbuka Kaka Hamidu. Ghafla nguvu zikaamka

Nikajikaza na kuanza kujiburuza sakafuni kama nyoka vile, kwa mwendo huo huo nilijikuta nikikiacha chumba kwa mbali kidogo, sikuufunga ule mlango wa chumba nilichomuacha Bodaboda.

Basi nilipofika kama chumba cha tano hivi nikasikia Mtu akiugonga mlango kwa nguvu huku akisema

“Njoo unitoe humu Mshenzi wewe, mtauwa wangapi. Siku ikifika mtakufa kama Kuku” alisema kwa hisia sana lakini hakujuwa kuwa Mimi nilikua tayari nipo mlangoni. Mlango ulikua umefungwa, korido lilikuwa refu halafu vyumba vilikua mbali mbali. Nilijitahidi sana kusimama nifungue mlango lakini nilikua nakosa nguvu, nilijaribu kama mara tatu lakini niliishia kuanguka

Wakati nikiwa nimeanguka nikageuka nyuma, ndipo nilipomuona yule Bodaboda akijikongoja kwa maumivu kuja nilipo, alikua amelishikilia tumbo lake. Hapo sasa yule Malaika mtoa roho nikamuona kama anachukua koleo kwa ajili ya kuichukua roho yangu.

Sauti ya yule Mwanaume ilizidi kusema, kibaya zaidi Mimi ndiye mwenye funguo halafu sauti yangu ilikua haitoki. Nikasema kama sisimami basi siondoki. Yule Bodaboda akawa anazidi kuja upande wangu kwa kasi akionekana kuanza kupiga hatua za nguvu. Nikamtaja Mungu nikasema

“Mungu nipe nguvu niishinde hii vita” nikajivuta haraka nikasimama nikiwa ninayumba, nikaanza kusaka tundu la kuweka funguo maana nguvu yenye ilikua sifuri, nikawa najitahidi huku nikiwa natetemeka. Mara naingiza mara nakosea, huku yule Bodaboda akizidi kunisogelea, hata nilipopaatia nilikua nimeingiza funguo isiyo yake.

Akawa karibu zaidi kiasi kwamba akipiga hatua tatu anakuwa amenifikia na kunizuia kuufungua mlango, nikapapasia kwa bahati nzuri nikapatia funguo nikavuta nguvu za mwisho nikatekenya kitasa lakini tayari Bodaboda alikua ameshanivaa na kuniangusha chini, Bahati nzuri ule mlango ulikua tayari umeshafunguka

Akatoka mwanaume mmoja na kuanza kumkita mateke yule Bodaboda hadi akamtupilia mbali huko akiwa hoi sana anatokwa na damu mdomoni, eneo la Korido lilikua linawaka taa isipokua

vyumbani tu. Sikuamini macho yangu Mtu ambaye nilikuja kumuona na kumtambua japo nilimuona mara moja tu

Alikua ni yule Mwanaume niliyemuazimaga simu kule Buchani, Ndio! Ni Abuu, masikini naye alikua mateka wa Mzee Mwinyimkuu baada ya kujulikana ananifuatilia Mimi, kwa muda mfupi naye alikua amepungua sana japo alikua na nguvu.

Hakuniuliza chochote zaidi ya kuninyanyua na kuweka mkono wangu kwapani kwake tukawa tunaelekea nje, mvua bado ilikua inanyesha. Tulipokua tunakaribia kutoka kabisa tukamuona Mtu anakuja Mbio, tena akikimbia kwenye mvua, ikatubidi tujifiche nyuma ya Mlango wa kutokea

Yule Mtu alipofika, breki ya kwanza ilikua vyumbani kisha akamrudia yule Bodaboda aliyekuwa anagala gala. Akamuuliza kwa hasira

“Umefanya nini Mpuuzi wewe?” aliuliza kwa sauti ambayo niliitambua, ilikua ni sauti ya Mzee Mwinyimkuu. Nilishtuka na kupata nguvu, nilipokumbuka kuwa yeye ndiye mtesi wangu basi mkojo ulinibana. Ghafla tu nikajiona ni Binadamu ninayehitaji kujitetea

“Nenda, hatuwezi kuondoka wote. Kaiambie Dunia kuhusu huyu Mzee, kama nitarudi tutakutana na kama nitafia hapa basi Roho yangu itakua salama” alisema Abuu, roho iliniuma. Sikua na uwezo wa kuzungumza. Mdomo wangu wa juu na chini nilihisi kama vimeungana sababu nilikua na vidonda mdomoni hivyo kukaa kimya ndiyo yalikua maisha yangu.

Nikaitikia kwa kutumia kichwa kisha nikasimama kama Mzimu, Mungu akaamua kunikumbuka. Akanipa nguvu na ujasiri, alichotaka Abuu ni kumzuia Mzee Mwinyimkuu. Wakati naanza safari Mzee Mwinyimkuu akaja mbio nahisi alikua anaanza kutusaka, sijui alijuaje kuwa tunatoroka. Huyu Mzee alikua Mchawi haswa, aliponikaribia tayari Abuu alimdaka Mzee Mwinyimkuu wakaanza kupalangana, muda huo nami nikaanza kujivuta kuondoka pale taratibu hadi nikaingia kwenye mvua.

Ulikua mchana lakini anga lilikua na wingu la kutosha kiasi kwamba palikua na giza fulani isitoshe palikua Porini. Nilipopigwa na mvua nikapata nguvu ya kuanza kuchanganya Miguu yangu vizuri. Nikaanza kukimbia huku nikiyumba kama mlevi

Sijui nilikimbia umbali gani lakini nilikimbia bila kuangalia nyuma, nilikimbia sana hadi nilichoka kabisa nikaanguka na kupoteza fahamu zangu.

Nilirudisha fahamu na kuanza kujitambua nikiwa naburuzwa kwa kasi sana, watu walikua kama vile wamenizunguka. Walikua na mavazi ya kufanana, nilikua kwenye kitanda kiendacho kwa kasi mno, nikawasikia wakisema

“Apelekwe ICU Haraka sana, kazi ianze mara moja” niligundua nilikua Hospitalini, wale wauguzi walionekana kunikatia tamaa sababu nilikua na hali mbaya sana. Lakini mimi

mwenyewe nilijiona ni mzima wa Afya zote, mahali nilipokuwepo palikua ni hatari zaidi ya Kuzimu.

Chozi lilinibubujika nikafumba macho yangu huku nikimshukuru Mungu. Madaktari walifanya kazi yao kwa wiki tatu kuhakikisha najitambua zaidi, wakaniweka kwenye uangalizi maalum kwa kipindi chote hicho hadi nilipokumbuka yaliyonisibu.

Nikawaandikia jina Langu, mahali nilipotoka maana nilikua siwezi kuzungumza tena, Hospitali ikasambaza jina na taarifa zangu ndipo Mama yangu alipokuja Mbeya akiongozana na Ndugu wengine kunitambua. Mama alilia sana, sikuwahi kumuona Mama yangu akilia namna ile, yale Maisha yaliniathiri sana kisaikolojia. Nikapoteza uwezo wa kuzungumza kabisa. Taarifa ya Kifo cha Baba ilinihuzunisha mno, ikanitoa chozi.

Polisi walipokuja niliandika maelezo yangu, ilikua baada ya wiki sita. Mwezi mmoja na siku kadhaa, afya yangu ilianza kukaa sawa lakini sikuwa na Uwezo wa kuzungumza chochote isipokua kuandika. Polisi walinichukua ili nikawapeleke mahali nilipoteswa yaani nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu

Mimi na Mama tulienda, palikua ni pale pale kwa Mzee Mwinyimkuu. Namba ya nyumba ilikua ni ile ile, mazingira yale yale, chozi lilinibubujika sana hadi Mama akashindwa kujizuia.

Nilikua natembezwa kwenye kiti cha Walemavu maana bado miguu ilikua haipo sawa pia sikua na vidole nilikua najiuguza. Nikampa ishara Mama yangu kuwa anipeleke kwanza nyumba jirani, pale kwa muuza chapati, nilimkuta Mwanamke mwingine kabisa akitengeneza chapati, nikaandika kwenye karatasi

“Mama Ashura yupo wapi?” nilikua na ujumbe wa Mtoto wake Ashura nilitaka kwanza nimpe ujumbe, wakati huo polisi walikua wameizingira nyumba ya Mzee Mwinyimkuu. Mama akamsomea yule Mwanamke, lakini cha ajabu eti akadai yeye ndiye Mama Ashura, nilishtuka alafu kingine kilichonipa mshituko ni kumuona Ashura mwenyewe, alikua ni Ashura yule yule niliyemuona Nyumbani kwa Mzee Mwinyimkuu

Haya mambo yalinifanya nianze kuonekana akili yangu bado haiko sawa, nikajitahidi kuwaambia kwa maandishi lakini niliishia kupewa pole tu, kisha nikapelekwa kwa Mzee Mwinyimkuu. Nako nikakutana na stori mpya kabisa

Kwanza ile nyumba si ya Mzee Mwinyimkuu, hawamfahamu. Wao wanaishi hapo Kwa Miaka mingi, nilitokwa na Mchozi, nyumba ile ile mazingira yale yale lakini stori tofauti. Nikaomba niingizwe ndani, nikapelekwa kwenye chumba nilichokuwa nalala

Nikakuta magunia ya vyakula, tena kilikua chumba chenye makorokoro mengi sana na hakikuonekana kua chumba cha kulala Mtu. Mama akaniambia

“Saida, najua umeteseka sana huku lakini hukumbuki chochote tena. Siku ukikumbuka nakuahidi tutarudi, yule Kijana na Baba yake watalipa” Kauli ya Mama yangu ilinimaliza akili yangu,

nilifikia hatua nikakubali kuwa akili yangu haipo sawa, inawezekanaje kila kitu kibadilike kwa haraka vile. Hakuna aliyeniamini

Lakini sasa wakati natoka nikajikuta nikipeleka macho yangu jikoni, nikaiona ile sufuria kubwa ambayo kwa mara ya kwanza nilipika mchicha mwingi, nikashtuka alafu nikauona Mchicha mwingi ukiwa kwenye Beseni. Kilichonishtua ni kwamba nilimuona Msichana wa umri wangu akiutengeneza.

Nilijikuta nikipiga yowe kali sana. Hali ya afya yangu ikawa sio nzuri nikarudishwa tena Hospitali. Tokea siku ile nilikua Msichana ninayekaa kimya hadi leo hii nawasimulia hiki kisa, sikumpata Mzee MwinyiMkuu wala Salehe, lakini sitakubali. Siku moja nitarudi Rukwa ili walipe kwa maumivu na mateso makali ninayoyapitia hadi sasa.

Kwasasa nimerudishwa kwetu Dar-es-salaam, niko Magomeni. Maisha yangu yamekuwa ya Ukimya sana, Sijazungumza tena tokea siku ile nilipozungumza kwa mara ya mwisho Rukwa, sijaandika chochote na wala sitaki kusema chochote kile ila kupitia mkasa huu nataka ujifunze.

Kamwe kwenye Maisha yako usiolewe au kuowa Mtu usiye mfahamu, Dunia ni Kichaka cha Mateso. Wasichana wengi wanayapitia mateso niliyoyapitia, wengi wanauawa, wengi wanapata ugonjwa wa akili. Hata wanaume wapo waliopoteza kila kitu, Siku nikifungua kinywa changu nitawasimulia mengi, kwasasa naishia hapa, naweka kalamu yangu chini.

AHSANTE……….MWISHO
Hatimaye nimemaliza
 
Sijui kwako ndoa ina maana gani lakini kwangu Mimi ndoa ilinipotezea Muda wangu, iliniacha na Maumivu na kilema cha Maisha yangu.

Sikuwahi kuwaza chochote kuhusu ndoa wala kuitamani, lakini siku moja nilikua natoka sokoni Mabibo naelekea nyumbani Magomeni Usalama, niliposhuka kwenye daladala kwa bahati mbaya niliteleza na kuanguka wakati navuka barabara. Mfuko wenye vitu nilivyonunua sokoni uliangukia pembeni.

Nilihisi aibu sana siku ile na kibaya zaidi mvua ilikua imenyesha majira ya asubuhi, lilijaa tope lililoniharibia Baibui langu. Eneo nililoangukia palikua na kijiwe cha Bodaboda. Kama uwajuavyo walianza kushangilia anguko langu kitu kilichozidi kunipa hasira lakini sikuwa na la kufanya zaidi ya kujiokotanisha pale.

“Pole sana Dada” niliisikia sauti hii nikiwa nasimama, aliyenipa pole alinipatia na mfuko wangu akiwa ameokotanisha vitu vyangu. Alikua kijana mzuri mtanashati sana, nilijikuta nikiwa na kigugumizi kumjibu

“Unaelekea wapi?”

“Nyuma ya sheli, usijali” nilisema nikiwa najipangusa tope kutoka kwenye Baibui langu jeusi, akanipa mkono wake

“Naitwa Salehe Mwinyimkuu” Alijitambulisha kwangu, nilimtazama kwa sekunde kadhaa kisha nilimjibu

“Naitwa Saida”

“Nimefurahi kukufahamu, wacha nikusogeze” alisema, kwa msaada alionipa isingelikuwa hisani kukataa alichokiomba. Taratibu tuliikanyaga ardhi kuelekea karibu na nyumbani kwetu. Kwa muda mchache nilihisi kumjua kidogo, niligundua ni mpole, mwemye hekima na busara tele licha ya kuniambia ana Miaka 27 tu.

“Mimi nina Miaka 23” nilijitanbulisha kwake huku nikianza kunogewa na mazungumzo yake. Tuliongea mengi hadi kubadilishana namba za simu kitu ambacho sikuwahi kukifanya kwa Mtu nisiyemjua.

Tulizidi kuwasiliana kwa zaidi ya mwezi mzima huku tukiwa marafiki wa kawaida tu lakini baadaye Salehe alinitongoza.

Nisiwe mwongo wala mnafiki hata kabla ya kunitongoza nilianza kumpenda hivyo kunitongoza alikua anatimiza wajibu wake kama Mwanaume kwani nisingeliweza kumwambia Nampenda isitoshe Mimi nilikua Bikra kwa wakati ule.

Tulianza mahusiano ya Kimapenzi lakini nilimwambia Salehe kuwa Mimi nimelelewa kwenye familia ya Dini sana, Baba yangu ni msaidizi wa Shekh Mkuu wa Msikiti wa Magomeni hivyo kama ananipenda kweli basi awaone wazazi wangu kwanza. Sijui tuseme alikua na kiu sana au alikua anahitaji Mke sana maana alilifanya hilo siku tatu tu baada ya kumwambia

Baba yangu alifurahi sana, Mama pia alifurahi zaidi akaniambia

“Mwanangu ndoa ni Nusu ya Dini, sisi Wazazi wako tunakutakia kila lililo jema, Mungu akuongoze” Daima Mama yangu alikua Mtu wa karibu sana kwangu, alisimama na Mimi kwenye kila jambo hata ambalo Baba yangu alipingana na Mimi.

Salehe hakutaka kuchelewesha alilipa Mahali siku iliyofuata.

“Wewe Kijana ni Mtu wa wapi?” Baba alimuuliza Salehe wakiwa katika mazungumzo ya kawaida, kama Mzazi ni lazima ahakikishe usalama wa Binti yake

“Kwetu Rukwa lakini nipo Hapa Dar Likizo” alisema Salehe

“Ooh! Unajishughulisha na nini?”

“Nimeajiliwa, Mwalimu wa Shule ya Msingi Rukwa Mjini”

“Utamtunza Binti yangu?”

Kwanza Salehe alicheka kidogo kisha akamwambia Baba

“Nisipomtunza Mke wangu nitamtunza Nani, wanasema Mbuzi unayemlisha ndiye utakaye mkamua maziwa” Basi Baba na Salehe wakaishia kuangua vicheko, ilileta raha sana.

Ndugu wa Salehe walifika tena waliazimia kuwa ndoa ipite kabla likizo ya Salehe haijaisha ili tuondoke wote kuelekea Rukwa, sikuwahi kufikiria kuwa siku moja nitaolewa na kwenda mbali kama Rukwa. Kidogo nilipata huzuni, nilimzoea Mama yangu

“Usijali, hata Mimi niliwaacha Wazazi wangu Morogoro nikaja kuishi na Baba yako Saida. Umri ukifika hakuna la kukuzuia kuanzisha Familia yako” Mama yangu hakuacha kunitia Moyo. Baba aliachia tabasamu maana tulikuwa wote sebleni

“Ngoja niwaache muongee maongezi yenu ya kike” alisema Baba akaelekea zake Msikitini, zilipita siku kadhaa hadi siku ya ndoa ilipowadia. Ndoa ilipita salama, Siku ya pili tulianza safari ya kuelekea Rukwa Mimi na Mume wangu Salehe.

Bado nilikua Bikra wala hakunigusa usiku wa kwanza wa ndoa yetu hotelini kabla ya Kuanza safari, kwakua nami nikikua mgeni wala sikudai chochote kile. Tulifika Rukwa Usiku sana tena nikiwa ninasinzia, tulichukua Taxi hadi nyumbani kwa Salehe

“Karibu nyumbani Mke wangu, jisikie uko nyumbani kabisa na hapa ndipo tutakapoishi” alisema tukiwa tunashuka kwenye taxi, tulisimama mbele ya nyumba moja iliyo giza sana, sikushangaa sababu mwenye nyumba hakuwepo kwa muda mrefu. Nilijiegemeza kwenye bega la Salehe nikamwambia

“Mume wangu, ulipo nipo na nitaendelea kuwepo siku zote” lile Taxi liliondoka, kazi ya kuhamishia mabegi ndani ilianza. Salehe alikua ametangulia nami nilibakia nyuma nikikokota begi. Sijui ni mawazo yangu au nilisikia kitu halisi kabisa, nilisikia sauti za Watoto wakiomba Msaada

“Subhannah‼” nilishtuka, sikuisikia tena ile sauti maana mwanzo ilitokea ndani ya ile nyumba ambayo tulikua tukielekea. Mapigo ya moyo yalinienda mbio, niliposikiliza vizuri wala sikuzisikia tena nikajua ni fikra zangu tu. Basi niliendeelea kuvuta begi hadi ndani, taa zikawashwa

Palikua kimya sana, uzuri sikua na njaa wala hamu ya kula zaidi ya Kulala kutokana na Uchovu wa safari. Nilisimama kusuburia Salehe anioneshe chumba chetu, akaufunga mlango kisha akaniongoza hadi chumbani, nilipofika nilijitupa Kitandani na kujilaza kama pono bila kujali kuwa kitandani palikua vumbi tupu.

Nililala Usingizi wa nusu kifo hadi mapambazuko, sauti ya jogoo kuwika niliisikia ikiniamsha na kuniambia ni muda muafaka wa kuanza majukumu ya nyumbani. Macho yalijawa na Ukungu usio kifani, nilijinyoosha kama Kinda la ndege halafu nikajikuta nikipigwa na Butwaa zito sana ambalo kiukweli nilishangazwa mno na nilichokiona

“Nipo wapi hapa?” Nilijiuliza swali hili, niliipapasa akili yangu inikumbushe jambo lakini haikua tayari kufanya hivyo, Salehe hakuwepo Kitandani. Moyo ulinienda hali Jojo, nilinyanyuka taratibu kutoka kitandani.

Nitakueleza kwanini nilipigwa na Butwaa la ajabu, kwanza harufu ya Udi wenye harufu mbaya ilizagaa kote ndani, pili nilisikia sauti ya Mtu akitwanga na kwa hakika alikua akitwangia ndani halafu sauti ya Mtoto Mchanga anayelia nilizidi kuisikia. Taratibu nilitaka kujuwa nipo wapi haswa maana tayari nilianza kupata hofu fulani

Nilipiga hatua za taratibu hadi mlango wa kutokea chumbani, ile sauti ilitoweka na palikua kimya sana. Moyo wangu haukutulia kabisa licha ya ukimya wa ghafla niliousikia, jua lilikua tayari limeshatoka

Nyumba ilikua safi sana. Ilikua na korido ndefu yenye vyumba kadhaa japo kwa wakati huo sikuhesabu kutokana na hali niliyokua nikiihisi. Basi Mimi Saida nilijiuliza

“Ah ni mawazo gani haya Jamani, Ewee Allah niepushie Mbali” nilisema kisha nilirudi Chumbani kutafuta simu yangu nimpigie Salehe aniambie alipo si unajua maisha ya Ugeni yanavyoanza. Nilikumbuka mara ya mwisho simu niliiweka kwenye mkoba wangu

Sikuwa na shaka sana kuhusu simu yangu, niliikuta lakini kwa bahati mbaya ilikua imeisha chaji. Niliketi kitandani nikiwaza mambo kadhaa lakini niliona ni bora niweke simu chaji niwasiliane na Salehe

Nilipomaliza kuweka chaji na kuhakikisha simu yangu inaingia chaji nilipata nafasi ya kukiangalia kwa uzuri chumba, kilipangwa vizuri sana hadi nilijikuta nikitabasamu, nilijuwa ni Mume wangu Salehe alikua ameamka mapema na kuweka mazingira sawa. Nilijiona ni mwenye Bahati sana kuitwa Mke wa Salehe, nilikua na nguo zangu zilezile nilizokuja nazo hivyo wazo la kubadilisha nguo lilinijia lakini kabla ya kufanya hivyo nilisikia Mlango wa nje ukigongwa.

Sikujua naanzia wapi kuitikia wito huo, nilisogea hadi mlango wa chumba na kusikiliza vizuri. Mgongaji wa mlango alikua ni Mwanamke na sauti yake ilikua karibu sana hivyo kwa haraka niliamini anagonga mlango wa Nyumba ya Salehe. Hakuna aliyeitikia ile hodi hadi pale nilipoamuwa kumkaribisha nikiwa ndani tena kwa sauti ambayo aliisikia vizuri, nilijiangalia kama nilikua nipo sawa kutoka ndani kisha nilianza safari mara moja kutembea kwenye korido kuuelekea Mlangoni.

Niliufungua mlango wa kwanza kwa kutekenya kitasa tu kisha nikauelekea mlango wa Uwani ambao ndio mgongaji alikua hapo, nilipoufungua nilikutana na Mama Mmoja aliyebeba tenga la mboga mboga kichwani, alikua ameshakata tamaa alikua akiondoka nikamwita

“Mamaaa‼” alipogeuka alirudi hadi Mlangoni

Shikamoo Mama” nilimsalimia kwa adabu, ndivyo nilivyofundishwa kwetu kwa wazazi wangu, yule Mama alitabasamu kisha akaniuliza

“Hauchukui Mboga leo?” Nilitabasamu maana aliuliza kana kwamba alishawahi kuniuzia mboga ila nilielewa Lugha ya Kibiashara huwa hivyo mara zote

“Mimi ni mgeni hapa Mama, labda kesho nikiwa nimeyafahamu vizuri mazingira naweza kuchukua. Usiache kupitisha” nilisema kisha yule Mama aliondoka huku akiitikia

“Napita kila siku Mtaa huu, Wahiiii mboga mboga” alienda mbele zaidi kisha alitokomea machoni pangu. Kuzungumza na yule Mama ni kama kulinisahaulisha kuhusu Salehe lakini alipoondoka nilijiuliza

“Salehe ameenda wapi mbona hajaniaga?” Niliufunga mlango kisha nilirudi ndani, Nyumba ilikua kubwa ya Kisasa lakini ilikua kimya sana sikusikia hata sauti ya ndege kuruka. Uwani

palikua na sehemu ya kukaa nikaona ni bora nikae hapo kwanza nipate upepo, nilijikuta nikipitiwa na Usingizi wa ghafla tu.

Ndoto za hapa na pale zilinifuata usingizini na kunipa hekaheka hadi nikashtuka. Niliposhtuka nilikutana na sura mbili, moja ilikua ya Salehe na nyingine ni ya Mzee mmoja mweusi aliyevalia Baraghashia nyeupe na kanzu nyeupe. Macho yao yalikua kwangu

“Eeeh imekuaje umelala hapo Mke wangu?” aliniuliza Salehe, nilijitabasamisha kidogo kama Mtu anayezuga ili asinione kuwa mvivu

“Hewa ya hapa inavutia, kaupepo nikajikuta nasinzia tu”

“Sawa, huyu ni Baba yangu anaitwa Mzee MwinyiMkuu. Ni Baba yangu Mzazi” alisema Salehe, nilimsalimia yule Mzee kwa heshima sana hata naye alifurahia na kuona ni namna gani nina heshima.

“Marhaba Mkwe wangu mzuri, hakika Mwanangu hakukosea’’ akasema kwa Utani tukajikuta tukicheka kidogo

“Samahani, najua umenitafuta ila nilienda kumpokea Baba maana aliniambia nikirudi tu atakuja kwa ajili ya kukusalimia wewe Mke wangu” alijielezea Salehe, ni kweli Mzee MwinyiMkuu alikuja na begi dogo la Mgongoni lililochakaa sana.

Aaaah! Nimefurahi sana kumuona Baba yako Salehe, karibu Baba.” Nilisema kisha nilisimama na kulishika begi la Mzee MwinyiMkuu ambalo lilikua sakafuni, kabla sijaliinua yule Mzee alinishika mkono kwa nguvu sana hadi nilishtuka, nikamtazama Usoni alikua amenikazia sura yake

“Hili begi halishikwi na kila Mtu, Salehe unajua pa kulipeleka” alisema Mzee MwinyiMkuu, nilihemwa maana sikutegemea lakini hata kama ningelichukua ningelipeleka wapi wakati na Mimi ni Mgeni pale. Nilishusha pumzi, kilinishuka nikarudi kukaa, Salehe akaniambia

“Mzoee Baba yangu ana utani sana Saida, wacha nikaweke begi lake nakuja” Mara moja alipomaliza kusema alinyanyuka Salehe na kuelekea ndani, yule Mzee hakuacha kunitazama kwa jicho kali kama vile kuna kitu nimeharibu hadi nilianza kumwogopa, ikanilazimu kumwomba Msamaha

“Samahani Baba sikujua”

“Siku nyingine uwe unauliza, umeelewa?”

“Ndiyo Baba” Nilipomjibu alinikata jicho fulani la husda kisha akatoa mguno fulani wa kicheko cha dhihaka halafu akanyanyuka na kuiburuza kanzu yake akaingia zake ndani,nilishusha pumzi zote kama Mgonjwa wa Pumu. Niliusikia moyo wangu namna ulivyoamka nakuanza kudunda tena, hata koo ilianza kupitisha mate kwa kasi. Yaani sijui nikueleze vipi unielewe namna nilivyokua nimeshikwa na woga kupitiliza, sura ya yule Mzee niliyona imekaa kikatili sana

Wakati naendelea kujiuliza mara Mume wanu Salehe alirudi kutoka ndani, akaketi mahali alipokua ameketi Baba yake

“Baba yako ni Mkali sana Salehe hadi nimeogopa. Nimefanya kipi kibaya, kumsaidia Begi ni vibaya eti?” Nilimuuliza Mume wangu, yeye akanishika bega akaniambia

“Utamzoea, si unajuwa wazee wa zamani. Pengine hakutaka wewe ushike begi kwasababu zilizo kaa kitamaduni tu za Kizamani au kabila letu lakini ni mcheshi utamzoea kwa muda atakaokaa hapa.

“Ina maana atakuwa anaishi hapa na Sisi?”

“Ndiyo, ila muda mchache tu atakua ameondoka. Vipi umeshakula?” Basi kuzungumza na Salehe kulinifanya nisahau kilichotokea, tuliongea sana hadi Mchana tuliposikia adhana. Salehe akawa wa kwanza kunikumbusha kufanya Ibada, nilitabasamu nikashusha pumzi kidogo huku dimpozi zangu zikionekana
Kumbe ni Tamthilia
 
Back
Top Bottom