Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Sayansi haisemi inajua kila kitu

[emoji4]

Kuna mtu kakushurutisha au kakulazimisha kwa mabavu kuandika ulichoandika?

Siyo haisemi tu, sayansi haijui kila kitu na wala haitokuja kujua kila kitu kamwe, kuna mambo chungu mzima yatabakia kuwa ni fumbo kwa wanadamu mpaka mwisho wa dunia, hatuwezi kuuelewa ulimwengu kwa kuchukua maarifa yetu yote kwenye fani moja, na hata mchanganyiko wa fani zote pia bado haitatosheleza
20220511_155029.jpg
 
Mfano tafsiri na uelewaji wa mambo mengi yanategemea utashi wa mtu na mipaka atakayojiwekea. Hakuna hicho kitu kwenye vipimo vya kisayansi. Hatuwezi kupata maana tofauti kwenye seti moja ya data halafu wote tukawa sawa. Kitu ili kikubalike na kila mmoja lazima kipitie chujio la upinzani na matokeo yawe sawa kwa kila anayepima na kuona majibu.
Daah pole sana, inaonesha bado upo nyuma kisayansi tu kwa ujumla.

Tuhuma ulizotoa zipo katika kanuni za kikawaida zinazotumika kwa mambo ya kawaida na zinajitosheleza. Zipo chini ya Newtonian classical mechanics. Hapa ndio tutalazimishana umbali, muda na nafasi viwe sawa kwa kila atakayepima.

Lakini kakaa sayansi sasa imeendelea, hatufungwi na hizo kanuni tu. Kunakitu kinaitwa General/specific relativity mambo ya quantum mechanics. Huku bro hatuna yale mambo ya ukipima dakika mbili, basi kila mpimaji naye apime na aseme ni dakika mbili. Huku inaruhusiwa kabisa mtu kuuexperience ukweli wake kutokana na perception zake, na circumstance zake.

Mambo ya kiroho ni mambo advanced na ndio maana kila mmoja anaexperience kulingana na kiwango anachoweza kun'gamua katika hiyo infinity Truth. Uhusiano wa mtu na Mungu ni binafsi japo tunapokusanyika katika makundi makundi tunapata kusaidika zaidi maana; Chuma hunoa chuma.
 
Mungu yupo na ataendelea kuwepona anaepiga uwepo wa Mungu anamattzo ila Yesu na Mohammad hao hawapo na hao ndo utapeli unapoanzia na apo ndo ugomvi huanzia
Ahsante kwa kuunga mkono hoja kuu "Uwepo wa Mungu", ama kuhusu kukadhibisha uwepo wa hao walimu wawili wa hizi dini mbili kubwa kuliko zote ulimwenguni nashauri walau ungekuwa na andiko lenye kusupport madai yako kutoka katika vyanzo vya kihistoria vinavyoaminika, nimeandika neno "walau" kwa kusudi

La sivyo, wanafunzi wa hao walimu tunaweza tukakugeuzia kibao kwa hoja kwamba na wewe haupo wala hujawahi kuwepo, una uhakika gani kwamba wewe upo kweli na si fikra tu au wazo hai? Hujawahi kuwepo kweli, uwepo wako ni kama picha mnato mfano au picha kivuli inayochezeshwa kwenye game, au uwepo wako ni kama 'mirage' yaani mazingazinga "illusion" hujawahi kuwepo kweli, au uwepo wako ni kama robot tu na si mtu halisi, unaweza kututhibitishia uwepo wapo? Thibitisha

Kwani kabla ya hao uliowataja hakukuwa na ugomvi wala utapeli?
 
Essence ya kuamini na kuabudu iko na sababu. Tamaduni zina mchango mkubwa sana lakini pia baiolojia ya miili yetu. Chanzo mwilini kiko kwenye bongo zetu. Kuna kitabu kimeelezea vizuri na kwa urahisi hii pointi kinaitwa "human brain " cha dr. Rita Carter. Simple explanations za kuanzia. So utakuta kwa vile bongo zetu sote zimeundwa kuhitaji kuabudu vitu vya kuongoza maisha yetu kila sehemu duniani kuna hizi imani. Tofauti zinaibuka kulingana na mazingira au muingiliano wa tamaduni.
Nimekidownload, ntaendelea kukisomaga

Na kama ulivyosema inaonesha unaelewa kabisa kwamba; believing in a god is a sane idea. Any human of any culture with normal brain development is predisposed to believe in a certain form of a god. Muumba kwa sababu ya upendo wake aliweka hilo katika mwanadamu ili tujitambue na tumtafute yeye. That is evolution.

Sasa kutokana na ufupi wa akili zetu tukaendaaa hadi tukafikia mahala fulani, tukastack. Basi Muumba kwa sababu ya upendo wake kwetu tena akaona atusaidie kwa kutuongezea mafunuo mbalimbali na vitabu ili tumtambue vizuri zaidi. That is revelation.

Hata huu uzi unachojaribu kusema ni kimoja tu kwamba; wazo la Mungu ni wazo halali kabisa, wala sio kusema sijui ni yupi au yupoje. Hicho tu. Ngoja nitafute muda nione na hicho kitabu chasemaje.
 
Nimekidownload, ntaendelea kukisomaga

Na kama ulivyosema inaonesha unaelewa kabisa kwamba; believing in a god is a sane idea. Any human of any culture with normal brain development is predisposed to believe in a certain form of a god. Muumba kwa sababu ya upendo wake aliweka hilo katika mwanadamu ili tujitambue na tumtafute yeye. That is evolution.

Sasa kutokana na ufupi wa akili zetu tukaendaaa hadi tukafikia mahala fulani, tukastack. Basi Muumba kwa sababu ya upendo wake kwetu tena akaona atusaidie kwa kutuongezea mafunuo mbalimbali na vitabu ili tumtambue vizuri zaidi. That is revelation.

Hata huu uzi unachojaribu kusema ni kimoja tu kwamba; wazo la Mungu ni wazo halali kabisa, wala sio kusema sijui ni yupi au yupoje. Hicho tu. Ngoja nitafute muda nione na hicho kitabu chasemaje.
Hayo maelezo yake ya lini? Mbona kama yana ustawi mzuri, nimeyapenda

Ila ananitatiza, naona kama akijadiliana na wewe anakuwa na point kuliko akijadiliana na mimi [emoji3]

Au hii imekaaje?
 
Hayo maelezo yake ya lini? Mbona kama yana ustawi mzuri, nimeyapenda

Ila ananitatiza, naona kama akijadiliana na wewe anakuwa na point kuliko akijadiliana na mimi
emoji3.png


Au hii imekaaje?
😂😂😂 Alijibu post namba 209, sio moja kwa moja kivile ila najaribu kutumia lugha yake kumuonesha kwa uwazi zaidi mambo anayoyajua na kuyaamini tayari.

Alisema hivi [emphasis mine] "Essence ya kuamini na kuabudu iko na sababu. Tamaduni zina mchango mkubwa sana lakini pia baiolojia ya miili yetu. Chanzo mwilini kiko kwenye bongo zetu. Kuna kitabu kimeelezea vizuri na kwa urahisi hii pointi kinaitwa "human brain " cha dr. Rita Carter. Simple explanations za kuanzia. So utakuta kwa vile bongo zetu sote zimeundwa kuhitaji kuabudu vitu vya kuongoza maisha yetu kila sehemu duniani kuna hizi imani. Tofauti zinaibuka kulingana na mazingira au muingiliano wa tamaduni." - masdinero masproblemas

Naona jamaa ameendelea sana katika kujua the 'HOW' anahitaji sasa kuanza kuongezea na hints zinazopoint kwenye the 'WHY'. Baadaye aunganishe why na how maisha yawe matam zaidi😊
 
[emoji848]

Unajaribu kukimbia kivuli chako, ukifanikiwa nifahamishe nikutunze, maelezo yako ya awali yapo wazi, na hilo umelionyesha mara nyingi zaidi ulipokuwa ukijadiliana Uhakika Bro kuliko hata mimi "ulikuwa wamshangaa na kumuona mtu duni sana kuwa muumini na pia kuwa mwanabaiolojia", na kwenye maelezo yako ulijikita kadri uwezevyo kumthibitishia kwamba anachoamini haimpasi kuamini sababu eti ni mwanasayansi, sasa unachojaribu kukana ni nini? Kujua kugeuzageuza maana ya sentensi na maneno siyo kujua kujenga hoja
Ndio, sio sawa mtu kujitambulisha taaluma ya sayansi halafu aendelee kutoa hoja za kiroho. Ni kuchafua tawi husika. Bora atoe maoni yake binafsi na si kutaka kukuza uzito wa hoja kwa kuongezea sifa za taaluma anayodai kujikita. Kuanza kwa kujitambulisha mimi ni "fulani" ni kutaka kujipa mamlaka zaidi wakati hoja ni dhaifu. Jaribu kuelewa sio kurukia maneno tu.
 
Hey, hatupo kwenye siasa, jibu unachoulizwa 'taja', hili si darasa la siasa! hivi we jamaa una shida gani? yaani uulizwe ni yapi mapungufu ya fani ya takwimu, udai takwimu kama fani haina mapungufu bali watakwimu na wanaojihusisha na fani ya takwimu kama wanadamu ndo wana mapungufu, hii akili ndo huwa unaitumia kuvuka barabara?

Takwimu kama fani ina madhaifu au mapungufu yafuatayo:
  • Haielezi phenomenom ambazo ni qualitative
  • Haielezi stori nzima "takwimu hueleza mambo kwa muhtasari"
  • Takwimu ni fani isiyodili na figure moja kwa mfano: uzito wa mtu X
Kinachokushinda kueleza kama hivyo ni nini? Eti sayansi siyo jambo la kiimani, mara sijui muziki kama fani hauna madhaifu! Nani kakwambia hauna? Tuhamie kwenye music?

Najua fika kinachokufanya ukwepe kutaja udhaifu wa fani ya sayansi, endelea kuzunguka mbuyu hivyohovyo, la sivyo utaivua fani nguo na baadhi ya angle zitabaki tupu, kukwepakwepa hivyo ni salama kwa misingi yako batili
Kumbe we ni mtu wa kukariri... aliyekudanganya qualitative phenomenon haziwezi kuelezwa na takwimu ni nani? Unasikitisha. Everything can be quantified. Tusiende mbali, una mengi ya kujifunza.
 
Nijibu kwa kifupi tu kwamba, una shida kubwa mno ya uelewa, maelezo yako ya mwanzo yanakiri na kusadikisha ushahidi unaotolewa na watu wengi kuhusu uchawi halafu mwisho unakama kwa hoja inayopingana na hiyo ya mwanzo ya kukosekana kwa ushahidi, ulikuwa unatengeneza statement of the problems e? What if huyo mtu! Siyo wewe uliyesema "watu wengi", au ulisa

Eti uchawi haupo kwa sababu hauna athari kama unavyodhaniwa! Hili si suala la kudhani, Ebo! Wala siyo suala la kukosekana kwa athari, ni hali ambayo kwa 100% ipo na hatuhitaji sayansi ituthibitishie kuwepo au kutokuwepo kwake, sayansi haina uwezo huo, sayansi ina udhaifu mkubwa katika kushindwa kuyatambua/kuyaeleza/kuyakubali/kuyabaini baadhi ya mambo ambayo ni halisi 'reality' na kukimbilia kwenye hutimisho la kutokuwepo kwa hayo mambo! Na nilijua ni lazima utajificha humo ndo maana kwenye maelezo yangu ya mwanzo sikusita kueleza

Eti utapokeaji kitu bila uhakika nacho, unahitaji uhakika gani? Mambo mangapi kwenye sayansi tumefundishwa na tumeyapokea na hatuna uhakika nayo? Na siyo kuwa na uhakika nayo tu bali mengi hayapo kabisa, au yapo kama idea tu lakini hayatahibitishiki kwa kutumia milango ya fahamu wala majaribio, au hatuna uhakika nayo wala hatuna uhakika juu ya uwepo wa hayo. Ulishawahi kuhakiki uwepo wa Moles au Atoms? Ulihakikije? Wapi ulishawahi kuhakiki uwepo wa hewa au upepo? Ulihakikije? Ulishawahi kuiona hewa au una-experience tu? Wapi ulishawahi kuhakiki uwepo wa latitude na longitude? Uache unafiki, mambo kibao tumemezeshwa tu pasina uhakiki wowote na tumeyapokea kwa upofu pasina hata kuthubutu kufanya uchunguzi. Ushauri: Unapokuwa unajenga hoja yoyote kumbuka kuanzia kwenye sayansi, weka hilo akilini, kama zipo lakini

Eti huo ujinga! Ita hiyo phonemena vyovyote utakavyo, hilo halibadilishi chochote wala haliondoshi chochote
Unachekesha sana. 100% ulizipimaje? Yaani wewe ni mshirikina wa aina zote kumbe... Imani zimekujaa. Ndio maana nikasema tuko parallel. Mitazamo yako ya kale sana.
 
Hongera, hili umejibu vizuri kiasi. Sayansi kushindwa kutambua akili ilipo hakuifanya akili iwepo au isiwepo, na hili linagutusha kwamba si kila ambacho sayansi inashindwa kulitolea ufafanuzi hitimisho ni kutokuwepo kwake

Na hilo linagutusha zaidi kwamba kuna phenomenon ambazo ni superior kwa sayansi na akili ni moja wapo, kama sayansi imeweza kuelezea unobservable mystical phenomenon kama atoms na subatoms, inashindwaje kueleza akili ambayo ni innate unobservable qualitative phenomenon?

Ahsante sana, kwa mara ya kwanza umedhihirisha udhaifu wa sayansi hapo ulipoandika "Sayansi haisemi inajua kila kitu", ama kusuhu dini kujua kila kitu hilo sijui umelipatia wapi? Hamna dini inayofundisha hivyo, acha kulisha imani za watu maneno ya uongo

Sasa huo udhaifu wa sayansi ulioutaja hapo ndo phenomena kama JUJU "Uchawi" zinaingia ndani yake. Najua fika kwamba unajua udhaifu wa sayansi japo unajifanya kujificha chini ya kivuli cha dole gumba lako. Sayansi kushindwa kujua kila kitu hakuyafanyi mambo yasiyojulikana na sayansi yawepo au yasiwepo [emoji4]. Nachokupendea huwa unarukaruka wee halafu baadaye unajifunga mwenyewe

Niweke wazi katika maelezo yako yote uliyowahi kuandika, hichi kipengele umeonyesha ukomavu wa ufahamu, umekitendea haki kwa kiasi chake, doa chafu: kuchanganya maelezo kwa kutuhumu dini kujua kila kitu
Inabidi uelewe consciousness ni kitendo sio kitu fulani stationary... observation yake inafanyika mubashara. Mfano kuelewa nini kinakuza imani kichwani mwako inabidi ufungwe sensa ukiwa unaomba, au kama huwa unakemea, kutoa ushuhuda nk.. kila sehemu kichwan hubadilika kulingana na tukio unalofanya au kuwaza. Mambo mengi tayari yanajulikana na mengine mengi yatajulikana. Ramani yote itakamilika. Ni suala la muda na si kwamba imeshindikana. Again, mtazamo wako wa kuegemea beyond scientific knowledge ni wa kale. Badilika, uachane na hizo imani zote potofu.
 
Achilia tusiojua kusoma wala kuandika ambao kwa wewe unatuona hatuna akili, ni wanasayansi wangapi wakubwa kwa wadogo, wasasa na wakale wamezikosoa vibaya mno nadharia zake za evolution? Hao wanasayansi hawana akili? Wewe ndo una akili sana e? Unachojaribu kufunikafunika na kupakapaka mafuta hapo ni nini?

Huu utahira wa Darwin endelea kujadiliana na wanafunzi wa darasa la kwanza D, tena wale wasio na mtaala wa Montessori, japo hata wao watakuona dishi limeyumba
Hakuna mwanasayansi au mtu yoyote mwenye kujua kusoma na kuelewa atabisha kuhusu evolution. Hivi vitu vinavyotokea kila siku kudhihirisha kwamba viumbe vinabadilika kila wakati huyajui? Ina maana unaandika based on past experiences na sio dunia ya leo? Ibuka kutoka pango hilo ulilopo uungane na wenzio. Unless umeridhika na hizo imani zako za uongo. Eti mungu umtumainiae!
 
?

Ukubaki ukatae sisi haituhusu, wewe kuona jambo fulani ni upuuzi hakulifanyi hilo jambo kuwa ni upuuzi. Na huo ufahamu ulioupata kwenye quote ya Einstein ni wewe na akili zako za kukodisha tu, kwa sisi ambao tunamsoma na kumuelewa Einstein tunajua amemaanisha nini alipohusisha hayo mambo mawili 'uhusiano'
Unadhani ni mimi tu?[emoji1787] iko hivi, imani uliyonayo wewe hapo sio kila mtu anaifata. Kimsingi kama una dini moja au dhehebu unalofata sijali lolote lile, tofauti yako na watu wasiofata ujinga wowote ni ndogo mno. Umekataa imani zote duniani ukabaki na hiyo moja wakati wengine tumeenda mbele zaidi kukataa zote pamoja na hiyo moja yako. Imani yako ni ujinga kama zingine zote. Tua zigo hilo!

Einstein yawezekana alikuwa deist. Wewe hapo ni theist. Kwa namna kubwa deism ni position ngumu kuhoji zaidi ya kwako wewe theism na mungu wako unayemtumainia. Tusiende mbali sana, kama Einstein alikuwa na imani so what? Unataka wote tufate imani kwa sababu ya mtaalamu mmoja? Tumia akili na ujenge hoja yenye mantiki.
 
Hilo halijalishi! Eti "dhana", unataka kuthibitisha nini? Iwe ni dhana au ni yakini sisi hilo halituhusu, hayo ni mambo yanayoishi kwenye moyo na fikra za mtu sisi hatuwezi kuyajua, hoja ni kwamba "ALBERT EINSTEIN NI MWANASAYANSI NA ALIAMINI MUNGU YUPO". Sasa je ni Mungu yupi na mwenye sifa zipi? Mjadala wetu haukuwa sifa za Mungu, mada ilikuwa "kuamini au kutoamini uwepo wa Mungu kwa wanasayansi". Kwa kifupi tu ni kwamba mjadala wetu wa awali umeishia hapo na imejitosheleza, yafuatayo ni nyongeza tu

Najua umeuliza hivyo kwa sababu umesoma maelezo machache ambayo Einstein alinukuliwa aliposema anaamini Mungu wa mwanafalsafa Spinoza. Kwa upeo wako finyu utakuwa umesoma sifa chache za huyo Mungu kama makala nyingi zilivyonukuu na umebweteka badala ya kutafuta marejeo halisi ya Spinoza alipojaribu kueleza sifa za Mungu wake. Nikufumbue macho kwamba sifa za Mungu wa Spinoza zinazolandana mno na sifa za Mungu wa Abrahamic Religions kuliko kutofautiana kwake, yaani karibu 65% - 85% ya sifa za Mungu wake alizoeleza zinamsadifu Mungu wa Abrahamu au Mungu wa wengi katika wanadamu

Halafu pia, hivi kuna sehemu au siku uliwahi kuniuliza Mungu wangu ana sifa zipi au ni Mungu gani? Kilichokufanya usiniulize ni nini? Mbona uliendelea tu kujadili uwepo au kutokuwepo kwake? Ni wazi kwamba una utambuzi usiohitajia kuniuliza kujua Mungu wangu ni wa aina gani na ana sifa gani? Ulipoandika "baada ya kuabudu uchukue telescope/microscope umchungulie umuone Mungu" ulikusudia Mungu gani? Ng'ombe au Mwamba? Kwani Miungu hivyo haionekani kwa macho ya nyama hadi utumie hadubini? Ni wazi kwamba ulijua mimi kama theist ni Mungu gani ninayemkusudia na ana sifa zipi kuu

Kwa upeo wako unaona ni jambo linalowezekana wanasayansi/wanafalsafa wote ambao ni theists wakaamini Mungu mwenye sifa zinazofanana kwa 100%? Sasa tunaposema wanasayansi 'theists' wanaamini uwepo wa Mungu huwa tunamaanisha nini? Huwa tunazingatia kufanana kwa 100% kwa sifa za Uungu kwa kila mmoja wao? Au huwa tunakusudia Mungu wa aina gani? Hoja nyingine hata siyo za kuibua, ungekausha tu

Na huenda hujanielewa, ngoja nikukokoteze tena!

Kwani sifa za Mungu aliyeaminiwa kuwepo au kuzungumziwa na Plato au Socrates ndo sifa za Mungu wa Eliyya au Zakaria ?

Je, sifa za Mungu aliyeaminiwa na kuzungumziwa na Faraday au Pasteur ndo sifa za Mungu wa Yesu au Muhammad?

Kwani hata Abrahamic Religions kila dini inayounda hilo kundi inapoelezea sifa za Mungu wao huwa zinafanana kwa 100%?

Ingia ndani kidogo, yaani katika ngazi ya madhehebu ya kila dini, je kila dhehebu linavyoeleza sifa za Mungu wao ndivyo mapote mengine ya dini hiyo yanavyoeleza pasina kutofautiana kukubwa au kudogo?

Shuka katika ngazi ya waumini wa dhehebu moja la kila dini, je kila muumini anayejiegemeza katika dhehebu A au B sifa za Mungu anayemuamini anavyozieleza zinafanana zote na sifa za Mungu wa muumini mwenzake wa dhehebu hilohilo?

Katika kujiuliza hayo maswali bila shaka kuna mambo utakuwa umejifunza ikiwemo hili: ufahamu hutofautiana hata kwa watoto waliotoka kwenye mfuko mmoja wa uzazi, ni mambo ya kawaida watu kutofautiana uelewa kutokana na kutofautiana upeo na daraja la ubobezi wa fani yeyote

Na haswa kwenye hilo kinachozingatiwa ni dhamira ya mlengwa kwa Mungu kwa kubainisha japo sifa zake kuu chache, kukosea au kupatia kumuelezea ni matokeo ya ufahamu tu, na wala hilo haliondoshi kusudi la Mungu wala uwepo wake. Hivi kwani Einstein hata katika sayansi ni vingapi amepatia na vingapi amekosea? Sasa kama yapo hayo kinachokushangaza kwenye hili ni nini na ukizingatia filosofia wala thiolojia si fani zake. Nanukuu maelezo yako "Tafsiri na uelewaji wa mambo mengi yanategemea utashi wa mtu na mipaka atakayojiwekea"
Unaongea uongo sana. Tufanye umeshinda. Maneno yako hayawezi kuwa karibu zaidi na uzishi. Nanyanyua mikono juu.
 
Nimekidownload, ntaendelea kukisomaga

Na kama ulivyosema inaonesha unaelewa kabisa kwamba; believing in a god is a sane idea. Any human of any culture with normal brain development is predisposed to believe in a certain form of a god. Muumba kwa sababu ya upendo wake aliweka hilo katika mwanadamu ili tujitambue na tumtafute yeye. That is evolution.

Sasa kutokana na ufupi wa akili zetu tukaendaaa hadi tukafikia mahala fulani, tukastack. Basi Muumba kwa sababu ya upendo wake kwetu tena akaona atusaidie kwa kutuongezea mafunuo mbalimbali na vitabu ili tumtambue vizuri zaidi. That is revelation.

Hata huu uzi unachojaribu kusema ni kimoja tu kwamba; wazo la Mungu ni wazo halali kabisa, wala sio kusema sijui ni yupi au yupoje. Hicho tu. Ngoja nitafute muda nione na hicho kitabu chasemaje.
"...kwa sababu ya upendo wake aliweka..." seriously?
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Alijibu post namba 209, sio moja kwa moja kivile ila najaribu kutumia lugha yake kumuonesha kwa uwazi zaidi mambo anayoyajua na kuyaamini tayari.

Alisema hivi [emphasis mine] "Essence ya kuamini na kuabudu iko na sababu. Tamaduni zina mchango mkubwa sana lakini pia baiolojia ya miili yetu. Chanzo mwilini kiko kwenye bongo zetu. Kuna kitabu kimeelezea vizuri na kwa urahisi hii pointi kinaitwa "human brain " cha dr. Rita Carter. Simple explanations za kuanzia. So utakuta kwa vile bongo zetu sote zimeundwa kuhitaji kuabudu vitu vya kuongoza maisha yetu kila sehemu duniani kuna hizi imani. Tofauti zinaibuka kulingana na mazingira au muingiliano wa tamaduni." - masdinero masproblemas

Naona jamaa ameendelea sana katika kujua the 'HOW' anahitaji sasa kuanza kuongezea na hints zinazopoint kwenye the 'WHY'. Baadaye aunganishe why na how maisha yawe matam zaidi[emoji4]
Kwa kuongezea *zimeundwa kupitia evolution (sio mungu)
 
Hayo maelezo yake ya lini? Mbona kama yana ustawi mzuri, nimeyapenda

Ila ananitatiza, naona kama akijadiliana na wewe anakuwa na point kuliko akijadiliana na mimi [emoji3]

Au hii imekaaje?
Ukiwa na misamiati hovyo na maswali ya ajabu unategemeaje maongezi ya maana? Mimi sio mwalimu kukuweka sawa na maneno yako yasiyo na weledi.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Alijibu post namba 209, sio moja kwa moja kivile ila najaribu kutumia lugha yake kumuonesha kwa uwazi zaidi mambo anayoyajua na kuyaamini tayari.

Alisema hivi [emphasis mine] "Essence ya kuamini na kuabudu iko na sababu. Tamaduni zina mchango mkubwa sana lakini pia baiolojia ya miili yetu. Chanzo mwilini kiko kwenye bongo zetu. Kuna kitabu kimeelezea vizuri na kwa urahisi hii pointi kinaitwa "human brain " cha dr. Rita Carter. Simple explanations za kuanzia. So utakuta kwa vile bongo zetu sote zimeundwa kuhitaji kuabudu vitu vya kuongoza maisha yetu kila sehemu duniani kuna hizi imani. Tofauti zinaibuka kulingana na mazingira au muingiliano wa tamaduni." - masdinero masproblemas

Naona jamaa ameendelea sana katika kujua the 'HOW' anahitaji sasa kuanza kuongezea na hints zinazopoint kwenye the 'WHY'. Baadaye aunganishe why na how maisha yawe matam zaidi[emoji4]

"Zimeundwa kuhitaji kuabudu" Zimeundwa na nini au na nani? Na kwa nini ziwe na hiyo quality ya kuhitaji kuabudu? Kwa nini zisiwe zimeundwa huru 'free' - kinyume na kuabudu?

Yupo vema kumbe, ni dots chache tu ambazo akifanikiwa kuziunganisha basi kajinasua kwenye mabano, safi
 
Back
Top Bottom