Mimi si Mwanasiasa, ila kwenye hili la Tozo hapana

Mimi si Mwanasiasa, ila kwenye hili la Tozo hapana

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,030
Reaction score
20,391
Wakuu najua uzima upo wa kutosha sema mtakuwa na stress za Tozo tu nyie. Baada ya kuwasalimu ngoja kidogo na mimi nitie neno.

Binafsi mimi si Mwanasiasa wala sijawahi kushabikia chama ila kwenye hili ngoja na mimi nilopoke kidogo.

Awamu hii ya sita ambayo inaongozwa na mama shupavu kwango kama sijaelewa maana uzoefu wangu unakinzana na niliyo yaona awamu ya tano.

- Awamu ya tano hapakua na ongezeko la tozo za Miamala, ila awamu hii tutaimba ule wimbo pendwa wa chama tawala Wacha waisome namba.. hapa si chama pinzani bali sote.

Pia kwenye hili naona chama kilichopo kimeamua kutunyonga kwenye ulipaji wa Pango japo wanasema eti unalipia Zaidi ya elfu mbili Unapata Umeme, lakini ukilipa chini ya 5,000 kupata umeme sahau.

Kumbuka haya yote ni awamu hii, pia nikiangalia mama yeye hasemi sana kuhusu haya wapo mawaziri wake yeye busy na kusafiri.

NB: Tulio pinga awamu ya 5 na kuanza kushabikia awamu hii msifikili imewasahau nawacheki tu.
Sina mengi ila tutaisoma namba kiukweli na Yajayo yanafurahisha mko tayari wananzengo?
 
Tutaelewana tu!! Walioimba na walioimbiwa kale ka wimbo ka 'acha waisome namba' wote tuko sawa.
 
Unaweza kufafanua hapo nilipo-bold?!
Mkuu ipo hivi.

Tanesco walisema ili kupata umeme unatakiwa kulipia Zaidi ya 2,000 ili 1,000 ulipie pango kwa mwezi wa saba na 1,000 nyingine tena italipia pango kwa mwezi huu wa nane.

Hivyo ukitaka kupata umeme unalipa labda 3,000 ili wakikata 2,000 yao utabakiwa na 1,000 na hiyo ndo itatumika kununua Umeme.
Lakini mimi na majira pamoja na wadau wa karibu hata ukilipia Umeme wa 4,000 inagoma mpaka ulipe 5,000 au zaidi.
 
Back
Top Bottom