Minazi ni miti iliyo hatarini kupotea, dalili zinaonekana

Minazi ni miti iliyo hatarini kupotea, dalili zinaonekana

Nimependa hii mada, nilikuwa nataka kujua mavuno na masoko, eka moja ya minazi inazaa nazi kiasi gani (average), kila baada ya muda gani..
na masoko ya nazi yakoje, na, je, mazao mengi yanaathiriwa sokoni na teknolojia,mfano nazi za azam, vipi kuhusu zao hili..? asante Sky Eclat
Pia nimekuwa interested ila nakosa taarifa za kutosha.
 
..kuna uzi mmoja niliweka contacts za kituo cha utafiti cha serikali cha zao la minazi.

..ofisi zao ziko Mikocheni Dsm na wana vitalu vya miche viko Bagamoyo na Mkuranga.
Nilikuwa nasearch hapa kuhusu mada ya 🥥 nadhani nilishausoma ule wenye hizo taarifa nitarudi kule nione, umaskini ni kikwazo sana kwangu mkuu nataka kufanya kitu kitakachohakikishia kizazi changu kipato cha kuwasaidia, sitaki wapitie yale ninayoyapitia hivi sasa.
 
Sorry nje ya mada .
Nina mpango wa kulima migomba heka 5.kwangu Mimi Naona zao la migomba linawai kumtoa mtu.manake mwaka mmoja mavuno tayali.ntapanda mwaka huu mwezi wa 9.
Ni wazo mwakani ntajalibu Hilo zao pia
Boss tupe mrejesho
 
Habari boss mrejesho wa minazi maana nataka kuingia miguu yote
Bado mzee, ile 25 niliyopanda ni ya kienyeji, kuzaa ni ndani ya miaka 7.
Kuna mingine hii ya muda inazaa, takribani minazi 70+,shida tu ni wezi, ingekuwa si wezi, basi nazi 2000 kila baada ya miezi mi3 ni suala la kawaida ila wezi wananikomesha mzee.
 
View attachment 1767152
Asili ya miti au zao hili ni Asia, Waarabu na wafanyabiashara walileta zao hili Tanzania miaka ya 1600-700. Minazi ya asili hi chukua miaka 10 tangu kupanda mpaka kuvuna au kuangua Nazi. Mti wa mnazi hustaamili ukame na una maisha ya miaka 100 tangu kupandwa.

Kilimo cha minazi kiliwafaa Waarabu waliomua kuweka makazi katika Pwani za Afrika. Minazi hupaswa kufyekewa na uvunjaji ni kila baada ya miezi mitatu. Iliwawezesha wenye mashamba kufanya shughuli nyingine wakiwa wanasubiri Mavuno.

Wingi wa minazi ulisaidia watu kusuka viungo vilivyoezekea nyumba. Matapa yalitumika kulalia kuanzia kwenye vitanda hata kwenye misiba. Vifuu vya nazi vilitengeneza pawa , vifungo, shanga na hereni.

Minazi mingi iliyopandwa na wahenga imeshapita umri wa uhai (life span) na hapa katikati hakukuwa na jitihada nyingi za kupanda minazi mipya. Matokeo yake ni uhaba wa makuti ya kutengenezea viungo na matapa.

Kama kiungo cha kupikia nazi zina soko kubwa na uhaba wake unasababisha bei kuwa kubwa sokoni. Wenye mapenzi mema na hili zao tuanze kampeni ya kupanda minazi
Hayo madude si ndio mwarabu aliyaleta hayo?
 
View attachment 1767152
Asili ya miti au zao hili ni Asia, Waarabu na wafanyabiashara walileta zao hili Tanzania miaka ya 1600-700. Minazi ya asili hi chukua miaka 10 tangu kupanda mpaka kuvuna au kuangua Nazi. Mti wa mnazi hustaamili ukame na una maisha ya miaka 100 tangu kupandwa.

Kilimo cha minazi kiliwafaa Waarabu waliomua kuweka makazi katika Pwani za Afrika. Minazi hupaswa kufyekewa na uvunjaji ni kila baada ya miezi mitatu. Iliwawezesha wenye mashamba kufanya shughuli nyingine wakiwa wanasubiri Mavuno.

Wingi wa minazi ulisaidia watu kusuka viungo vilivyoezekea nyumba. Matapa yalitumika kulalia kuanzia kwenye vitanda hata kwenye misiba. Vifuu vya nazi vilitengeneza pawa , vifungo, shanga na hereni.

Minazi mingi iliyopandwa na wahenga imeshapita umri wa uhai (life span) na hapa katikati hakukuwa na jitihada nyingi za kupanda minazi mipya. Matokeo yake ni uhaba wa makuti ya kutengenezea viungo na matapa.

Kama kiungo cha kupikia nazi zina soko kubwa na uhaba wake unasababisha bei kuwa kubwa sokoni. Wenye mapenzi mema na hili zao tuanze kampeni ya kupanda minazi
Andiko bora kabisa hili na limenihamasisha kufufua shamba langu la minazi huko Pwani.
 
Government intervantion is inescapable for this bro. Hata uwe na innovation kiasi gani without government intervantion you will stuck.
Upo sahihi. Cha muhimu ni kuweka mikakati na kuihusisha Serikali ili mafanikio yapatikane.
 
..kweli.

..lakini " hed ek " inakuja kwenye kuchagua kati ya mbegu za asili au kisasa.

..kwasababu kisasa wanasema inazaa baada ya miaka 4 na asili inazaa baada ya miaka 7.

..vilevile wanasema kisasa inazaa nazi nyingi kuliko minazi ya asili, ila haihimili magonjwa.
Miaka saba siyo mingi mkuu cha msingi hatujachelewa. Tukapande minazi tuondokane na umasikini.
 
Sky Eclat , makaveli10 ,

..kati ya minazi, miembe, michungwa, ipi inaingiza kipato kikubwa zaidi?
Nitakuwa mnafiki mie nina minazi tu. michungwa, kijana wa shamba alileta uhuni, akaifyeka na kutengeneza mkaa.

Sijui hiyo miembe ni ya kisasa ama lah..
Ninachojua nazi unavuna kila baada ya miezi mi3 hivi, yaani unapovuna hutoi zoote, unatoa makole yale yenye nazi kavu, unaacha nyingine, baada ya miezi mi3 unashusha tena.
 
Back
Top Bottom