Mirathi ya nyumba iliyojengwa na mjane yazua balaa; ukoo wa mume na ukoo wa mke wanaigombania

Mirathi ya nyumba iliyojengwa na mjane yazua balaa; ukoo wa mume na ukoo wa mke wanaigombania

Kiwanja kilikua cha mume lakin kwa msingi huo wana haki na jasho la ndugu yao
Mume alifariki kitambo mirathi ikagawanywa mama akachukua chake kwa maana hiyo kiwanja kilikiwa Mali hali ya mke .Na ikumbukwe ndoa ya Kikristo kifo kinaimaliza,maana hiyo hakuwa mke wa mtu Tena baada ya kifo mumewe.Sasa ndugu wa mume Mali inawahusuje hapo.
 
Upande wa huyo mama wanazingua. Mke kama aliolewa na mahari ilishatolewa, baada ya kufiwa na mumewe hakuolewa maana yake ni kwamba kila kitu hapo ni halali ya ukoo wa mume.

Hao wapogoro waache ujinga.
Hapana ndoa huvunjwa na kifo huyo alikuwa single wakati kifo kinamchukua
 
Ndoa imekufa sio kila mpogolo wa morogora atazikwa huko.

Mbona huyo Tarimo wa juzi kazikwa mbeya yule aliyekufa Ukraine.

Huyu mliomzika bagamoyo mbona bado mnataka na Mali za marehemu na hamjamzikq huko Moshi?

Acheni utapeli mnauwana wenywe Vibinti vidogo vikatili ..huko machame wana sura za kijangili demu ana ngeu za uso kama jambazi .

Ngoja utaona sheria itakavyoamua ndio utajua nani tapeli
 
Haijalishi kazikwa wapi. Ukweli ni kuwa alikuwa single na no longer wife wa late husband.
Kweli kabisa chief.Hebu wajiulize huyu mjane angeamua kuuza baada ya kifo Cha mwanae walikuwa na nguvu ya kumzuia hao ndugu wa mume.Kama hapana amini Mali za ndugu Yao mwanaume ziliisha baada ya kugawiwa mjane baada ya mwanae kufa.Ndugu wa mume wajitafakar
 
Habari wadau.

Kama mnavyojua suala la mirathi linavyotolewa macho hapa Tanzania.

Jirani kwetu kuna mama amefariki na kuacha nyumba nzuri tu na hajaacha mtoto hata mmoja.

Historia ya huyu mama ( kabila mpogoro) mwaka 1991 aliolewa kwa ndoa ya kanisani na mume wake ( kabila mchaga)

Baada ya kufunga ndoa walinunua kiwanja na mume wake na kuzaa mtoto mmoja wa kiume.

Mwaka 1994 mume wa huyu mama alifariki na kumuacha mke na mtoto mmoja wakiwa hai.

Taratibu za mirathi ya mume wake zilifanyika baada ya msiba. Mama na huyo mwanae wakapewa hiko kiwanja maeneo ya tegeta kikiwa kitupu hakijaanzwa ujenzi wowote.

Maisha yakaendelea. Mama huyu hakuolewa tena . Aliendelea kuishi na mwanae kwa kupanga nyumba ya NHC keko. Na mdogo mdogo akaanza ujenzi wa nyumba katika kiwanja walichoachiwa na mumewe.

Alijenga nyumba nzuri tu ya kisasa. Na zingine ndogo ndogo pembeni za kupangisha. Maana kiwanja kilikuwa kikubwa sana ( maana enzi wananunua tegeta ilikuwa pori ardhi haina thamani miaka ya 90 muuzaji anakuuzia bonge la kiwanja kwa bei ndogoo..)

Baada ya kumaliza ujenzi yeye na mwanae waliendelea kuishi nyumba ya NHC na kule tegeta walipojenga wakapangisha wapangaji kadhaa.

Mwaka 2015 mama alipata msiba mwingine wa kufiwa na mtoto wake huyo mmoja kwa ajali ya gari na hii ikamfanya mama kubaki peke yake bila mtoto wala mume.

Mama akaendelea kuishi mwenyewe mpaka na yeye mama alipofariki mwaka huu mwanzoni.

Mwili wa mama ulisafirishwa kwenda moshi kuzikwa walipozikwa mume wake na mwanae.

Shida imekuja kwenye nyumba zilizojengwa na huyo mama. Ukoo wa mume unasema ni mali zao. Na ukoo wa mke nao unasema ni mali zao maana zimejengwa kipindi mume wa huyo mama ameshafariki.

Wataalamu wa mirathi Kesi kama hii upande upi kati ya ukoo wa mume na ukoo wa mume una haki ya kurithi hizo mali za huyu mama.

Wazazi wa huyu mama wote wameshafariki pia.
wewe kwa akili yako ndogo huyo mama alioa au aliolewa.?
 
Tofautisha single na mjane.
Yaani wasomi WA siku hizi hata Akili ya kuchambua mambo hamna.
Mjane/single wote hawana waume na wanaweza kuolewa tena. Jikite kwenye hoja na si kuanza kuleta dharau.
 
Sio Utapeli.
Kama MKE kazikwa upande wa mume, tafsiri yake bado ni Mali ya Ukoo wa mumewe.

Kama Ndoa ilivunjika au ilivunjwa, sio sababu ya kuzika MKE upande wa mumewe.

Hao Ndugu wa Mke ndio wanashida.
Sema ni vile Watu hawaelewi haya Mambo.
Mwanamke akishaolewa anakuwa hayupo Chini ya umiliki WA ukoo wake tena, anaenda kwenye umiliki wa ukoo WA mwanaume.

Ni vile kizazi cha sasa kimeshavurugwa
1.Kuzika marehemu siyo kigezo au sababu ya kuwa na uhalali wa kisheria wa kurithi mali za marehemu uliyemzika.
2.Sheria ya Mirathi inawatambua warithi halali ni (i) Mjane (ii) Watoto wa Marehemu (iii) Wazazi wa Marehemu.
Endapo kama wote hawa hawapo, basi, ndugu zake wa karibu ndio wanaofuata kuwa warithi halali. Ndugu hao ni kama vile dada zake wa damu, kaka zake wa damu, n.k.
3. Kwa kuwa mume wa huyo mama marehemu alitangulia kufa, kisheria hali hiyo inajulikana kama "kaukimbia urithi" kwenye mali/ardhi inayomilikiwa kwa umiliki wa maslahi ya pamoja yasiyogawanyika (joint occupation or matrimonial property ownership), hivyo, ndugu wa huyo mume hawana haki yoyote ile kwenye hizo mali/nyumba kwani ndugu yao alijitoa mapema kwenye umiliki wa hiyo nyumba na kisha umiliki huo wote kuhamia kwa mkewe na mtoto waliobaki hai.
4. Ndugu wa huyo mama wanapaswa kufungua kesi ya mirathi ya usimamizi wa mali za huyo mama na wamteue msimamizi wa mirathi, hao ndugu wa mume wa marehemu endapo kama watakuwa na pingamizi lolote basi watawasilisha huko Mahakamani, na kwa vyovyote vile pingamizi hilo lazima litakosa mashiko na litatupiliwa mbali na Mahakama.
5.Mwisho.
Mali na nyumba zote za huyo mjane ni urithi halali kwa ndugu zake, ndugu wa mumewe hawana haki ya kurithi mali hizo.
 
Nendeni mkaolewe na hao wenye tamaa ya mali ,siku wanaume zenu wakifa ndo mtaona kila rangi kuna watu hawana utu kisa ya mali.
 
Kesi si kesi, kifo si taraka ndiyo sababu mpogoro alizikwa Moshi, mke alirithi mali za mumewe na zake hivyo upande wa mke hauna chao kwani walikwishalipwa chao(mahali).
 
Habari wadau.

Kama mnavyojua suala la mirathi linavyotolewa macho hapa Tanzania.

Jirani kwetu kuna mama amefariki na kuacha nyumba nzuri tu na hajaacha mtoto hata mmoja.

Historia ya huyu mama ( kabila mpogoro) mwaka 1991 aliolewa kwa ndoa ya kanisani na mume wake ( kabila mchaga)

Baada ya kufunga ndoa walinunua kiwanja na mume wake na kuzaa mtoto mmoja wa kiume.

Mwaka 1994 mume wa huyu mama alifariki na kumuacha mke na mtoto mmoja wakiwa hai.

Taratibu za mirathi ya mume wake zilifanyika baada ya msiba. Mama na huyo mwanae wakapewa hiko kiwanja maeneo ya tegeta kikiwa kitupu hakijaanzwa ujenzi wowote.

Maisha yakaendelea. Mama huyu hakuolewa tena . Aliendelea kuishi na mwanae kwa kupanga nyumba ya NHC keko. Na mdogo mdogo akaanza ujenzi wa nyumba katika kiwanja walichoachiwa na mumewe.

Alijenga nyumba nzuri tu ya kisasa. Na zingine ndogo ndogo pembeni za kupangisha. Maana kiwanja kilikuwa kikubwa sana ( maana enzi wananunua tegeta ilikuwa pori ardhi haina thamani miaka ya 90 muuzaji anakuuzia bonge la kiwanja kwa bei ndogoo..)

Baada ya kumaliza ujenzi yeye na mwanae waliendelea kuishi nyumba ya NHC na kule tegeta walipojenga wakapangisha wapangaji kadhaa.

Mwaka 2015 mama alipata msiba mwingine wa kufiwa na mtoto wake huyo mmoja kwa ajali ya gari na hii ikamfanya mama kubaki peke yake bila mtoto wala mume.

Mama akaendelea kuishi mwenyewe mpaka na yeye mama alipofariki mwaka huu mwanzoni.

Mwili wa mama ulisafirishwa kwenda moshi kuzikwa walipozikwa mume wake na mwanae.

Shida imekuja kwenye nyumba zilizojengwa na huyo mama. Ukoo wa mume unasema ni mali zao. Na ukoo wa mke nao unasema ni mali zao maana zimejengwa kipindi mume wa huyo mama ameshafariki.

Wataalamu wa mirathi Kesi kama hii upande upi kati ya ukoo wa mume na ukoo wa mume una haki ya kurithi hizo mali za huyu mama.

Wazazi wa huyu mama wote wameshafariki pia.


Umasikini kitu kibaya sana
Sasa wewe baba yangu, kaka yangu, mjomba wangu unaendaje kugombea Mali ukweni nilikoolewa mimi lakini?
 
Back
Top Bottom