Misafara ya viongozi inachosha, inatesa na kurudisha nyuma maendeleo, IGP Sirro peleka Traffic Sweden kujifunza misafara ya wenzetu, Time is Money!

Miaka hiyo ya tisini na 97,98 wakati ICTR iko juu haswa na moto........... Nakumbuka akawa anapita askari mmoja wa ICTR alivalia kiraia na hakuwa raia wa Tanzania................ Mara paaah askari wa Tanzania akamvaa ondoka kaa pembeni. Yeeye akamuulisha how and why akamjibu Rais mstaafu Mwal. Nyerere anapita akamjibu kwani inahusiana vipi na movement yangu... nimejaza njia nzima ama.............

Huko Sweden kuna budget yake? na je wataelewa?
 
Mkuu misafala ni tawala zote, Rais akitoka ni msafala,Mi nashauri inunuliwe helicopter nzuri na ya Kisasa isaidie kuokoa Muda.
Leo nilikuwa Mwenge kwa saa 1 nzima gari ilikuwa mbele kabisaa tumekaa sana kusubiri msafala upite.
 
Iwe ilani ya CCM kuwa serikali hsipaswi kuwapotezea muda wananchi wake walipa kodi.
 

Soon watahamia dodoma tuvumilie tu foleni zitaisha.Wasipoweka foleni watatambulika vipi kuwa ni viongozi
 
Wasiwasi wangu ni juu ya haya magari ya Ambulance yanayobeba wagonjwa kuwakimbiza hospitali ! Hivi kama yanapita kwenye barabara ambayo kuna msafara wa Rais unakuja huwa yanasimamishwa au yanaruhusiwa kupita?
Au Rais kwanza mgonjwa baadaye?
 
Kwanza nikupongeze kwa kuona umuhimu wa kutuma hii kitu, katika Hisabati Kuna kitu kinaitwa Standardisation, yaani kukileta kitu karibu na kingine ili visiachane Sana, na ndio maana kwa kimombo huita " Measure of central tendency". Nchi uliyotufanananisha nayo imbali Sana na sisi kiasi kwamba sijui Kama inawezekana ingawa nakuunga mkono kwa kusafiri huleta mafunzo mengi Kama wasemavyo waswahili kuwa Mguu mtembezi haukosi mwiba. Mimi ningeshauri tuanze na kuondoka upendeleo wa migawanyo inayofanyika kwenye makutano makubwa Kama vile Uhasibu, Tazara, Keko, Kamata n.k, Mimi kupitia funzo tulililopata Ubungo ningetamani Serikali Sehemu hizo nilizotaja hapo juu ziwekwe Round About kubwa Kama ya Ubungo ili kuepusha foleni Kama ilivyopungua Ubungo, Pia Askari wetu wa usalama barabarani wajikite kwenye kuhakikisha usalama unakuwepo wakati wa Mzunguko na waepukane na mawazo kwamba saa hizi wanaotokea upande Fulani Ni muhimu zaidi kuliko wengine hii huleta usumbufu Sana hasa nyakati za asubuhi na jioni, Pia wakati mwingine waweza mwona Askari anaingia Kati anavuta Magari ya upande mmoja muda mrefu mpaka unajiuliza sisi wa upande wa huku tumefanya kosa gani, ukitaka kuliona hili pita Kilwa road asubuhi/ jioni ukitokea Mjini/ Mbagala Mutawalia.
 
Kwa wenzetu viongozi wengi wao wanapita kihalali.

Nani anahofu ya ulinzi wa magari na misafara mirefu na isiyo jali kazi za raia wake?

Wanashindana kwa nguvu na uonevu na sio kwa hoja ndio vyanzo vya woga na uhitaji wa kuwekwa mtu kati eti 'for security purposes'.

Wanaambiwa wakafanye kazi huku wanawasimamisha kwenye misafara mirefu isiyo na tija.
 
Watu wanalinda ugali mkuu, timing inaweza ikaenda vibaya ugali wa mtu ukamwagika.
 
Huwezi kuifananisha Sweden na Tanzania kwenye Mambo ya ustaarab. Kule wanajielewa lakini huku kwetu madereva wa vyombo vya Moto wengi vichwa vigumu, sababu nadhani Ni umasikini na ujinga. Madereva wetu kipisha kingora Ni wazito Sana na mwengine anaweza kuona barabara ni nyeupe akaingia bila kujiuliza.

Paragraph ya nne, umemuonea tu. Mbona Mzee kikwete alikua anasafiri Sana lakini Mambo yalikua Ni haya haya. Nadhani ni chuki binafsi.
 
Wanaboa Sana hao watu,wawe wanasafiri usiku kutoka na kuingia mjini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…