Kuna moja aliandika: 'Kudua na Kugosha chedi nini'...sikujua ni nini ila lilinikaa kichwani. Siku moja nikasikia binti mmoja akiongea kikwao katamka neno chedi, alipomaliza maongezi nikamuuliza..'kudua na kugosha chedi nini'? Akajibu, bora kudua napata raha pia..
Aisee, kumbe nawe ulishaiona..kama siyo kipare basi kisambaa...ngoja waje wenyewe watatuambiagari ya kawe - buguruni cjajua maana yake had leo
Hahahaha,duhh,sijui kama matajiri wanajua majina ya magari yao
Unataka kali?@Zanzibar Spices.Hii hapa, 'KANIITIE MKEO'.
Hahaha nimeipenda MTALAKA HATONGOZWImkuu niko hapa mto wami na nimefika hapa kwa kazi maalumu ya kukuongezea umri na hapa magari ni mengi sana ya kila aina na hapa yanapita taratibu sana kwa hiyo usijali wewe subiria na ujiandae na mbavu kuna hilo limeandikwa [MOTO HAULAMBWI] lingine limeandikwa[MTALAKA HATONGOZWI] lingine hilo linakuja limeandikwa [SUMU HAIONJWI] lingine hilo limeandikwa [TOROKA UJE] lingine hiloo limeandikwa [GUSA UNASWE] lingine hiloo limeandikwa [CHEZEA MSHAHARA USICHEZEE KAZI] lingine hiloo [MTAJI WA MASIKINI NI NGUVU ZAKE MWENYEWE] lingine hiloo [MBWA HATUMWI MACHINJONI] lingine hiloo [ PESA SABUNI YA ROHO] samahani magari ni mengi na kila moja limeandikwa ila tatizo haka kamchina kangu kioo kimechakaa sana kuandika ninachukua muda mrefu sana na kimeshaanza kuonyesha battery iko low.