Misemo inayoandikwa kwenye vyombo vya usafiri, we acha tu!

mkuu niko hapa mto wami na nimefika hapa kwa kazi maalumu ya kukuongezea umri na hapa magari ni mengi sana ya kila aina na hapa yanapita taratibu sana kwa hiyo usijali wewe subiria na ujiandae na mbavu kuna hilo limeandikwa [MOTO HAULAMBWI] lingine limeandikwa[MTALAKA HATONGOZWI] lingine hilo linakuja limeandikwa [SUMU HAIONJWI] lingine hilo limeandikwa [TOROKA UJE] lingine hiloo limeandikwa [GUSA UNASWE] lingine hiloo limeandikwa [CHEZEA MSHAHARA USICHEZEE KAZI] lingine hiloo [MTAJI WA MASIKINI NI NGUVU ZAKE MWENYEWE] lingine hiloo [MBWA HATUMWI MACHINJONI] lingine hiloo [ PESA SABUNI YA ROHO] samahani magari ni mengi na kila moja limeandikwa ila tatizo haka kamchina kangu kioo kimechakaa sana kuandika ninachukua muda mrefu sana na kimeshaanza kuonyesha battery iko low.
 

gari ya kawe - buguruni cjajua maana yake had leo
 
I like JF nimecheka sana.. ngoja nirudi kumtumikia mwajiri tena,.....
 
Hivi na daladala za kizungu huwa zina hizi misemo?

''Boti haina msaada, kipofu haelekezi njia''!
 
Hahaha nimeipenda MTALAKA HATONGOZWI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…