Mishahara kuchelewa, kipimo kingine cha uwezo wa Rais Samia

Mishahara kuchelewa, kipimo kingine cha uwezo wa Rais Samia

KILA Mwisho wa mwaka huwa hivi kuwa na subira tu
June mwaka Jana tulipata tarehe 20 June 2020. Coz bajeti inaishia but July tulichelewa kwa kuwa mwezi mpya wa fedha kwa mwaka 2020. June 2021 ilibiidi tupate fasta coz hela ipo [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Upumbavu wako ndio unakufanya uwe mtumwa wa mishahara

Wekeza kula mazao ya mshahara sio kula mshahara

NB "Kuna marekebisho makubwa ya madaraja na kulipa baadhi ya malimbikizo hivyo mvumilie mpaka jumatatu"
Wewe umewekeza wapi mkuu?
 
Suala la kuchelewesha mishahara halina uhusiano wowote na kiwango cha mishahara inayolipwa. Mwajiri hulipa mshahara kwa kadri ya uwezo wake, lakini ulipwe kwa wakati. Fluctuation ya namna yoyote ile katika tarehe za kulipa mshahara hudhihirisha either huna cha kulipa au huna nidhamu/unapuuza tu wafanyakazi wako.
Tutolee kelele hapa na vimalalamiko vyako vya kishamba.
 
Bosi hanuniwi? Pale tu

Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.

Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
Tutolee kelele hapa na vimalalamiko vyako vya kishamba.
 
24 unalalamika? kuna taasisi qamezoea kupitishwa hadi tarehe 2.

lakin kama pia unaona ni ishu. tafuta biashara kuliko kukaa unasubiria mshahara wa serikal.. halad ulichelewa unalalamika.
boss hanuniwi
Ushauri mzuri, lakini sidhani kama atakuelewa. Kajijaza ujinga na vihoja vyepesi na vya kishamba.
 
Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.

Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
Kwa kua watu hawauwawi hovyo na hawapotei hovyo kama awamu iliyopita huo mshahara kuchelewa sio neno

Halafu awamu iliopita iliacha deni kubwa sana kwahiyo hata siku tukiambiwa "mwezi huu hautokua na mshahara" poa tu

Ila nyie WASUKUMA mlijua kututesa
 
Umenena vema,na watumishi wafunge mashule,mahospital na tra waache kukusanya kodi twende tukajenge reli ya kisasa
Tra, mahospitali na mashule havitafungwa, isipokuwa watapewa posho ndogo saana halafu lilefungu kubwa la mafedha yanayotolewa kulipa mishahara yapelekwe kwenye ujenzi wa miradi itakayoweza kuzalisha ajira mpya zaidi ya million 20. Angalia nimabilion mangapi yanayotolewa kila mwezi kwakulipa watumishi. Tujibane ndani ya miaka mitatu tuone kama hatutakuwa na neema kubwaa baadae.
 
Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.

Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
Usiku usiku tayari
 
Natarajia kilio nchi nzima mishahara kutobadilika mwezi huu, yangu macho na masikio kuhusu madaraja mapya. Kwn mpk sasa waliopata wanasema kitu ni kile kile.
 
Mtoa mada acha utoto jifunze kuwa na plan B acha kulalamika kama Mwana Wa Israeli safarini walilalamika kwa Kila kitu. Jipange chapa kazi
 
Kwa kua watu hawauwawi hovyo na hawapotei hovyo kama awamu iliyopita huo mshahara kuchelewa sio neno

Halafu awamu iliopita iliacha deni kubwa sana kwahiyo hata siku tukiambiwa "mwezi huu hautokua na mshahara" poa tu

Ila nyie WASUKUMA mlijua kututesa
Hao watu waliyokuwa wanapotea hovyo ni watu wa aina gani na sababu ni zipi?
 
Kinachowasumbua ni wivu plus uchawi.
Mtu kuulizia haki zake eti anajidhalilisha!!!
Kuna mwana jf alijifanya ni afisa wa B.O.T kumbe ni mganga njaa anatia huruma.
Wa tz bana hapa Kuna watu wamekuponda wakijifanya jiajiri wakati na wao choka mbaya wameajiriwa Kama wewe..hii ndo tz life mtandao.
 
Leo tarehe 24 mishahara bado haijalipwa. Ieleweke kwamba vitu kama hivi ndivyo vitakavyopima uwezo wa Rais Samia kama anastahili awamu ya pili au la.

Nachelea kusema kwamba kwa mwezi kama huu (mwisho wa mwaka wa fedha) kufika tarehe 24 mishahara haijalipwa si dalili njema huko tuendako.
unawaza mshahara tu, fanya kazi kwa ufanisi Kwanza
 
Wacha ichelewe, kama ilikuwa inawahi sababu ya kupora kwenye akaunti za wafanyabiashara, na ichelewe maana ndio uhalisia!
 
Back
Top Bottom