Vipi hakuna bajeti ya Ukimwi kwa ajili ya msafara wa Raisi?
Sio tu hatujui mshahara wake,hata kodi halipi wakati obama analipa
Jamani kuna mtu anayejua mshahara wa raisi wa Tanzania ni kiasi gani? Kuna mtu kaniambia ni $200,000 na kitu kwa mwaka...sikuamini lakini akanihakikishia kuwa taarifa zake ni za uhakika. Bado ninasita kuamini ingawaje sina taarifa zozote na sijawahi kuona mahala popote pale kuhusu mshahara wa raisi.
Na mshahara wa makamu wa raisi..?
Waziri mkuu..?
Spika wa bunge..?
Mkuu wa majeshi ya ulinzi, polisi,magereza..?
Jaji mkuu..?
Kama kuna mtu anayejua...ni wapi tunaweza kupata taarifa hizi?
nakumbuka kuna wakati mwalimu alijipunguza mshahara kutoka shilingi 4000 hadi 2000 kwa mwezi! Tukijadili kinadharia hivi kuna ubaya gani hii mishahara (na mingine inayolipwa kwa kodi ya wananchi)ikiwa wazi? Au kuna faida gani ikiwa wazi?
we unalipwa sh. ngapi??? SAMAHANI KAMA HUTO JALISwali zuri sana na nadhani Ikulu watakapo kamilisha site yao ni vizuri wakiziweka habari hizi wazi kwa wananchi kuziona... Waajiriwa wote wateuliwa na rais ni vizuri tukifahamu mishahara yao!
Hizi taarifa kwa Tz kuzipata hata uzitafute mchana na usiku kamwe hutozipata