Misiba bado ina nguvu sana Afrika

Misiba bado ina nguvu sana Afrika

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Unaweza kucheza na vyote lakini sio msiba.. Misiba Afrika ni kama mila na desturi.. Ni utamaduni wenye nguvu bado

Kuna muunganiko wa ajabu na wenye nguvu sana kwenye mila na desturi za Kiafrika na wageni wanautamani lakini hawawezi tena maana walishaharibu
Nadhani ndio chimbuko la Ubhuntu kwamba sisi ni wamoja langu lako na lako langu!

Matunda ya huu muunganiko ni haya (japo sasa unakufa kwa baadhi ya vipengele)
1. Kikipikwa chakula mpishi ataambiwa aongeze kidogo kunaweza kuwa na mgeni

2. Mgeni akifika bila taarifa na chakula kilishapikwa atakaribishwa hicho hicho

Kusaidiana na kushiriana kazi za kijamii kama ujenzi, kilimo, harusi , jando nk...

Kwenye ujenzi na kilimo mhusika halipi hela mbali huandaa chakula na vinywaji kwa washiriki Kwenye sherehe mbali mbali waalikwa kila mtu huleta alichonacho kwa hiari na bila kupangiwa

Usithubutu kwa namna yoyote ile kukosa shughuli mbali tatu mfululizo. Utatengwa na Jamii yote Kuna baadhi ya matukio unaweza kuyaruka lakini makinika sana kwenye ugonjwa na misiba..

Wana msemo wao kama tulifurahi pamoja bali hata kwenye kulia tulie pamoja
Wagonjwa was Afrika walikuwa hawana shida .. Maana Jamii inayomzunguka itampa support ya kila kitu

Matukio ya misiba ndio sensitive zaidi.. Utakavyofanya kwenye misiba ya wengine ndivyo watakavyofanya kwenye misiba inayokuhusu

Kama Kazi yako ilikuwa kutoka rambirambi tuu nao watafanya hivyo hivyo kwako

Kama ulikuwa huli kwenye misiba yao, siku likikufika watafanya kila kitu ila hawatakula hata kama umeandaa biriani na nyama choma Kama hukuwepo siku ya msiba mpaka mazishi ukirudi nenda kahani.. Huo ndio upendo..LAKINI kamwe usiondoke siku msiba umeshatokea.. Ahirisha mambo yako nenda kaonekane, kaa kidogo kisha omba udhuru ondoka

Kuna wachache watakaokusema vibaya lakini wengi kwenye hao wachache watakutetea na kukusema vizuri
Bado utamaduni wa kuzikana una nguvu sana Africa!
Usiende mpirani kisha urudi kutoa pole.. Kwa kuona haya wanaweza kukupokea lakini moyoni wana kisasi nawe!

Hicho kisasi kitatungwa mimba
Hiyo mimba italelewa na kuzaliwa mtoto

Mtoto kisasi akikua na kukomaa kifuatacho ni malipizi..!
Good morning Tanganyika❤❤❤
626614ea-21f5-4c21-a226-a698b068f837.jpeg
 
Unaweza kucheza na vyote lakini sio msiba.. Misiba Afrika ni kama mila na desturi.. Ni utamaduni wenye nguvu bado

Kuna muunganiko wa ajabu na wenye nguvu sana kwenye mila na desturi za Kiafrika na wageni wanautamani lakini hawawezi tena maana walishaharibu
Nadhani ndio chimbuko la Ubhuntu kwamba sisi ni wamoja langu lako na lako langu!
Matunda ya huu muunganiko ni haya (japo sasa unakufa kwa baadhi ya vipengele)
1. Kikipikwa chakula mpishi ataambiwa aongeze kidogo kunaweza kuwa na mgeni
2. Mgeni akifika bila taarifa na chakula kilishapikwa atakaribishwa hicho hicho
.Kusaidiana na kushiriana kazi za kijamii kama ujenzi, kilimo, harusi , jando nk...
Kwenye ujenzi na kilimo mhusika halipi hela mbali huandaa chakula na vinywaji kwa washiriki
Kwenye sherehe mbali mbali waalikwa kila mtu huleta alichonacho kwa hiari na bila kupangiwa

Usithubutu kwa namna yoyote ile kukosa shughuli mbali tatu mfululizo. Utatengwa na Jamii yote
Kuna baadhi ya matukio unaweza kuyaruka lakini makinika sana kwenye ugonjwa na misiba.. Wana msemo wao kama tulifurahi pamoja bali hata kwenye kulia tulie pamoja
Wagonjwa was Afrika walikuwa hawana shida .. Maana Jamii inayomzunguka itampa support ya kila kitu

Matukio ya misiba ndio sensitive zaidi.. Utakavyofanya kwenye misiba ya wengine ndivyo watakavyofanya kwenye misiba inayokuhusu

Kama Kazi yako ilikuwa kutoka rambirambi tuu nao watafanya hivyo hivyo kwako
Kama ulikuwa huli kwenye misiba yao, siku likikufika watafanya kila kitu ila hawatakula hata kama umeandaa biriani na nyama choma
Kama hukuwepo siku ya msiba mpaka mazishi ukirudi nenda kahani.. Huo ndio upendo..LAKINI kamwe usiondoke siku msiba umeshatokea.. Ahirisha mambo yako nenda kaonekane, kaa kidogo kisha omba udhuru ondoka

Kuna wachache watakaokusema vibaya lakini wengi kwenye hao wachache watakutetea na kukusema vizuri
Bado utamaduni wa kuzikana una nguvu sana Africa!
Usiende mpirani kisha urudi kutoa pole.. Kwa kuona haya wanaweza kukupokea lakini moyoni wana kisasi nawe!

Hicho kisasi kitatungwa mimba
Hiyo mimba italelewa na kuzaliwa mtoto
Mtoto kisasi akikua na kukomaa kifuatacho ni malipizi..!
Good morning Tanganyika❤❤❤View attachment 3157251
😁lakini nilipata mualiko kwenye kikao cha kikoba muhimu cha wale mabeberu wakuu wanaotugaia maokoto. Mnisamehe waungwana napenda kuwapa pole sana natumai mazishi yalienda salama.
 
😁lakini nilipata mualiko kwenye kikao cha kikoba muhimu cha wale mabeberu wakuu wanaotugaia maokoto. Mnisamehe waungwana napenda kuwapa pole sana natumai mazishi yalienda salama.
Kwani ilikuwa lazima uende wewe? Kwamba bila wewe shughuli haifanyiki au hainogi? Wachunguze washauri wako vizuri.. Kumbuka. Kikulacho...!?
 
Unaweza kucheza na vyote lakini sio msiba.. Misiba Afrika ni kama mila na desturi.. Ni utamaduni wenye nguvu bado

Kuna muunganiko wa ajabu na wenye nguvu sana kwenye mila na desturi za Kiafrika na wageni wanautamani lakini hawawezi tena maana walishaharibu
Nadhani ndio chimbuko la Ubhuntu kwamba sisi ni wamoja langu lako na lako langu!
Matunda ya huu muunganiko ni haya (japo sasa unakufa kwa baadhi ya vipengele)
1. Kikipikwa chakula mpishi ataambiwa aongeze kidogo kunaweza kuwa na mgeni
2. Mgeni akifika bila taarifa na chakula kilishapikwa atakaribishwa hicho hicho
.Kusaidiana na kushiriana kazi za kijamii kama ujenzi, kilimo, harusi , jando nk...
Kwenye ujenzi na kilimo mhusika halipi hela mbali huandaa chakula na vinywaji kwa washiriki
Kwenye sherehe mbali mbali waalikwa kila mtu huleta alichonacho kwa hiari na bila kupangiwa

Usithubutu kwa namna yoyote ile kukosa shughuli mbali tatu mfululizo. Utatengwa na Jamii yote
Kuna baadhi ya matukio unaweza kuyaruka lakini makinika sana kwenye ugonjwa na misiba.. Wana msemo wao kama tulifurahi pamoja bali hata kwenye kulia tulie pamoja
Wagonjwa was Afrika walikuwa hawana shida .. Maana Jamii inayomzunguka itampa support ya kila kitu

Matukio ya misiba ndio sensitive zaidi.. Utakavyofanya kwenye misiba ya wengine ndivyo watakavyofanya kwenye misiba inayokuhusu

Kama Kazi yako ilikuwa kutoka rambirambi tuu nao watafanya hivyo hivyo kwako
Kama ulikuwa huli kwenye misiba yao, siku likikufika watafanya kila kitu ila hawatakula hata kama umeandaa biriani na nyama choma
Kama hukuwepo siku ya msiba mpaka mazishi ukirudi nenda kahani.. Huo ndio upendo..LAKINI kamwe usiondoke siku msiba umeshatokea.. Ahirisha mambo yako nenda kaonekane, kaa kidogo kisha omba udhuru ondoka

Kuna wachache watakaokusema vibaya lakini wengi kwenye hao wachache watakutetea na kukusema vizuri
Bado utamaduni wa kuzikana una nguvu sana Africa!
Usiende mpirani kisha urudi kutoa pole.. Kwa kuona haya wanaweza kukupokea lakini moyoni wana kisasi nawe!

Hicho kisasi kitatungwa mimba
Hiyo mimba italelewa na kuzaliwa mtoto
Mtoto kisasi akikua na kukomaa kifuatacho ni malipizi..!
Good morning Tanganyika❤❤❤View attachment 3157251
Good morning kaka
 
Usithubutu kwa namna yoyote ile kukosa shughuli mbali tatu mfululizo. Utatengwa na Jamii yote Kuna baadhi ya matukio unaweza kuyaruka lakini makinika sana kwenye ugonjwa na misiba..
Slowly this is dying out. Inaweza ikachukua muda, lakini inakuja: Kwa vipi?
1. Kuna makampuni ya kuzika yananzishwa. Hutahitaji watu kuja msibani. Ndugu wa karibu ndio watakuwa kwenye msiba na maziko yanafanywa na ndugu hao hao, technical staff wakiwa kampuni za mazishi i.e kuchimba Kaburi, kufukia and all that is necessary for that business! (Western World wako hapa, hakuna mkusanyiko wa mtaa/kijiji etc kwenye mazishi).
Wengi wangependa kufanya kama hapo No.1 lkini fedha bado kikwazo....... lakini everybody is inclined to that route...it is a matter of time!

(ni kama ushoga, tunaupiga vita sana tena sana, but our kizazi hiki cha bongo fleva, wako inclined to that! Wasanii wanachexa UCHI kwenye stage na sasa jamii inaanza kuwakubali as "NORMAL" muziki)
 
Kwani ilikuwa lazima uende wewe? Kwamba bila wewe shughuli haifanyiki au hainogi? Wachunguze washauri wako vizuri.. Kumbuka. Kikulacho...!?
Lakini chadema waliendelea na siasa zao wakati watu wapo msibani
 
Unaweza kucheza na vyote lakini sio msiba.. Misiba Afrika ni kama mila na desturi.. Ni utamaduni wenye nguvu bado

Kuna muunganiko wa ajabu na wenye nguvu sana kwenye mila na desturi za Kiafrika na wageni wanautamani lakini hawawezi tena maana walishaharibu
Nadhani ndio chimbuko la Ubhuntu kwamba sisi ni wamoja langu lako na lako langu!

Matunda ya huu muunganiko ni haya (japo sasa unakufa kwa baadhi ya vipengele)
1. Kikipikwa chakula mpishi ataambiwa aongeze kidogo kunaweza kuwa na mgeni

2. Mgeni akifika bila taarifa na chakula kilishapikwa atakaribishwa hicho hicho

Kusaidiana na kushiriana kazi za kijamii kama ujenzi, kilimo, harusi , jando nk...

Kwenye ujenzi na kilimo mhusika halipi hela mbali huandaa chakula na vinywaji kwa washiriki Kwenye sherehe mbali mbali waalikwa kila mtu huleta alichonacho kwa hiari na bila kupangiwa

Usithubutu kwa namna yoyote ile kukosa shughuli mbali tatu mfululizo. Utatengwa na Jamii yote Kuna baadhi ya matukio unaweza kuyaruka lakini makinika sana kwenye ugonjwa na misiba..

Wana msemo wao kama tulifurahi pamoja bali hata kwenye kulia tulie pamoja
Wagonjwa was Afrika walikuwa hawana shida .. Maana Jamii inayomzunguka itampa support ya kila kitu

Matukio ya misiba ndio sensitive zaidi.. Utakavyofanya kwenye misiba ya wengine ndivyo watakavyofanya kwenye misiba inayokuhusu

Kama Kazi yako ilikuwa kutoka rambirambi tuu nao watafanya hivyo hivyo kwako

Kama ulikuwa huli kwenye misiba yao, siku likikufika watafanya kila kitu ila hawatakula hata kama umeandaa biriani na nyama choma Kama hukuwepo siku ya msiba mpaka mazishi ukirudi nenda kahani.. Huo ndio upendo..LAKINI kamwe usiondoke siku msiba umeshatokea.. Ahirisha mambo yako nenda kaonekane, kaa kidogo kisha omba udhuru ondoka

Kuna wachache watakaokusema vibaya lakini wengi kwenye hao wachache watakutetea na kukusema vizuri
Bado utamaduni wa kuzikana una nguvu sana Africa!
Usiende mpirani kisha urudi kutoa pole.. Kwa kuona haya wanaweza kukupokea lakini moyoni wana kisasi nawe!

Hicho kisasi kitatungwa mimba
Hiyo mimba italelewa na kuzaliwa mtoto

Mtoto kisasi akikua na kukomaa kifuatacho ni malipizi..!
Good morning Tanganyika❤❤❤View attachment 3157251

MSIBA KTK MFUMO WA KIISLAMU
Mazishi katika Uislamu hufuata taratibu maalumu ambazo zimewekwa na sheria za Kiislamu (Sharia). Hapa ni muhtasari wa hatua za kuendesha mazishi kwa mujibu wa Uislamu:


---

1. Utunzaji wa Mwili wa Marehemu

Kuthibitisha kifo: Hakikisha kwamba marehemu amefariki kwa hakika.

Kuwafahamisha Waislamu wengine: Taarifa ya kifo hutolewa ili Waislamu wa karibu wajiandae kushiriki mazishi.

Kuhifadhi mwili: Mwili wa marehemu unatakiwa kushughulikiwa kwa heshima. Inapaswa kufunikwa mara moja.



---

2. Uoshaji wa Mwili (Ghusl Mayyit)

Nani anaosha?: Mwili wa marehemu huoshwa na watu wa karibu, kama familia, kwa kuzingatia jinsia ya marehemu (wanawake kwa wanawake, wanaume kwa wanaume). Mwanandoa anaweza kumuosha mwenzi wake.

Mchakato:

1. Mwili huoshwa kwa maji safi na yenye joto.


2. Uoshaji hufanywa mara tatu au zaidi kama inahitajika, kuanzia sehemu za siri (chini ya kifuniko), mikono, uso, na mwili wote.


3. Maji yenye manukato (kama sidr au camphor) hutumika mwishoni.





---

3. Kufunika Mwili (Kafan)

Mwili hufunikwa kwa sanda nyeupe (kafan), ambayo ni vipande vya vitambaa safi.

Idadi ya vipande:

Wanaume: Vipande vitatu vya sanda.

Wanawake: Vipande vitano vya sanda (vikiongeza vazi la kifua na kilemba).




---

4. Swala ya Janaza

Swala ya Janaza ni ibada ya sala inayoswaliwa kwa ajili ya marehemu.

Mahali: Hufanyika msikitini, nyumbani, au uwanja wa wazi karibu na kaburi.

Mkusanyiko: Kadri ya uwezo, watu wengi wanahimizwa kushiriki.

Mchakato:

1. Imamu husimama mbele ya mwili wa marehemu.


2. Swala ni ya rakaa moja na haina rukuu wala kusujudu. Inajumuisha Takbira nne:

Takbira ya kwanza: Kusoma Surah Al-Fatiha.

Takbira ya pili: Kumwombea rehema Mtume Muhammad (Durood).

Takbira ya tatu: Dua ya kumuombea marehemu.

Takbira ya nne: Dua fupi kwa Waislamu wote.






---

5. Mazishi (Defna)

Kuchimba kaburi: Kaburi linapaswa kuwa la kutosha kwa mwili kufukiwa bila kuonekana.

Kuzika:

1. Mwili wa marehemu huwekwa kaburini kwa upande wa kulia, kuelekea Qibla.


2. Dua fupi husomwa wakati wa kuweka mwili kaburini.


3. Kaburi hufukiwa kwa udongo.



Kuepuka tamaduni zisizo za Kiislamu: Hakuna kuweka mapambo au sanamu juu ya kaburi.



---

6. Dua na Sadaka

Waislamu huombwa kumwombea marehemu msamaha na huruma kwa Mwenyezi Mungu.

Inahimizwa kutoa sadaka kwa niaba ya marehemu ili thawabu ziendelee kumfikia.



---

Mazishi ya Kiislamu ni rahisi na yanazingatia heshima na uadilifu kwa marehemu, huku yakifuata maagizo ya Qur’an na Sunnah za Mtume Muhammad (SAW).
 
Nlishawahi shuhudia jamaa alikuwa akienda msibani alikuwa na yabia ya kutokula chakula kilicho andaliwa huku akisema mm nimekula vingi sana Sina kitu ambacho sijala siku anafariki kilipikwa chakula kingi mno watu wakazika halafu waondoka huku wakisema tumekula vingi sana kwo hiyo n kweli broo waafrika tuna Tania ya kulipiza visasi shirikinna wenzio kwa Kila jambo Ili nawe washiriki kwenye mambo yako
 
Back
Top Bottom