Misiba mingi ya Wakristo ina gharama kubwa kuliko wengine

Misiba mingi ya Wakristo ina gharama kubwa kuliko wengine

Makaburi yenyewe ni gharama tupu, wauza majeneza wanatengeneza majeneza ya gharama tofauti kila uchao. Zamani ilikuwa mbao tu zinarandwa linaundwa sanduku mtu anazikwa nalo. Wakaanza kupaka vanishi, wakapandisha bei. Sasa hivi wanaweka hadi vidani na marembo ya kila aina. Ni bajeti yako tu upate la gharama gani. Kwenye misosi nako ni gharama tupu. Ukipika ugali maharage watu hawali wanataka upike vyakula vya kifahari. Angalau wali mweupe watakula kwa shingo upande. Ukubwa wa msiba huendana na gharama za mazishi
 
Usiniquote vibaya mkuu.
Nimesema ya kikristo kwasababu kwa asilimia kubwa ndiyo huwa na mchakato mrefu! Tofauti na dini nyingine ambao wao mazishi hayahitaji hata jeneza. Samahani kama utakuwa umeelewa tofauti
Kwani shida kwako ipi,kila mbuzi hula urefu wa kamba yake.
 
Zama za leo ni tofauti kabisa na zama za mababu zetu. Ukisoma vitabu vya dini utagundua kuwa mazishi hayakuhitaji hata majeneza. Mfano Lazaro inaonesha alizikwa tu na sanda pasi na jeneza.

Leo hii watu wanashindana hadi kwenye gharama za majeneza. Hivi kwanini basi majeneza yote yasiwe yenye ubora unaolingana ili kuondoa hii tofauti?

Mtu akipata msiba anawaza namna gani aufanye msiba huo uwe wa kifahari! Na wakati mwingine marehemu alikosa msaada wa tiba bora; na huenda ndio hasa chanzo cha kifo chake!
Hapana, ni kwa sababu wana uwezo wa kubeba hizo gharama. Vinginevyo haina maana yoyote kuingia gharama kibao wakati mtu keshakufa
 
Na hata wakila, chakula kikiwa na kasoro wanalalamika.
Ndio binadamu sisi tulivyo.
nilihudhuria msiba fulani, wali ulikuwa na mchanga mwingi balaa, sikuumaliza nilimpa mtu mwingine ale, niliishia kulalamikia wapishi
 
Michakato gani ya kikikristo inataka pesa nyingi.


Mfano, Mimi kwetu misiba ni ya Jamii nzima, kila mfiwa kwa uwezo wake. Kazi ya viongozi wa dini ni kusoma ibada ya mazishi tu na nyimbo za kusindikiza mwili.


Nimekuja Uchaggani, Kuna shida kubwa: MC analipwa, wachimba kaburi wanalipwa, padre analipwa.

Bado hujakodi muziki, viti wapishi na hema.


Sasa hapo utasingizia ukiristo au tamaduni binafsi za watu fulani??
halafu huko moshi mkitoka kuzika mnakuta mmeandaliwa misosi na vinywaji kama vyote. Mbege mapipa kadha, bia na soda za kumwaga, watu wanakaa mkao fulani wa kunywa mbege tani yako
 
Michango ya msiba ni mikubwa na unalazimishwa kutoa.
Watu wengi leo hii wakupatwa na msiba wanawaza namna ya kuufanya uwe wa kifahari. Wanashona sare, wanaandaa ukumbi nk.

Mbaya zaidi usipotoa mchango unatengwa! Sasa swali langu ni je kuna umuhimu wa hayo yote?
siku hizi wana print mpaka mabango makubwa yenye picha ya marehemu na ujumbe fulani wa nukuu ya biblia
 
Alifariki baba mzazi wa nabii na mtume mmoja mwenye mbwembe nyingi maarufu na mwenye kupenda kujisifia yeye kuliko kumsifia Mungu, huo msiba uliacha gumzo mtaani kwa vyakula vya kifahari utadhani ni harusi fulani hivi ukumbini. Malizia kwenye jeneza lilikuwa la gharama kubwa wakati wengine wanazikwa na jeneza la saiprasi tu tena halijarandwa wala kupigwa vanishi
 
halafu huko moshi mkitoka kuzika mnakuta mmeandaliwa misosi na vinywaji kama vyote. Mbege mapipa kadha, bia na soda za kumwaga, watu wanakaa mkao fulani wa kunywa mbege tani yako
Bufee lazima liwepo. Na Kama huna kitu hata padre hakanyagi utazikwa Kama Mzoga na walevi tu
 
Zama za leo ni tofauti kabisa na zama za mababu zetu. Ukisoma vitabu vya dini utagundua kuwa mazishi hayakuhitaji hata majeneza. Mfano Lazaro inaonesha alizikwa tu na sanda pasi na jeneza.

Leo hii watu wanashindana hadi kwenye gharama za majeneza. Hivi kwanini basi majeneza yote yasiwe yenye ubora unaolingana ili kuondoa hii tofauti?

Mtu akipata msiba anawaza namna gani aufanye msiba huo uwe wa kifahari! Na wakati mwingine marehemu alikosa msaada wa tiba bora; na huenda ndio hasa chanzo cha kifo chake!
Wenzako wanapenda na fasheni,harusi ya millioni hamsini,ila miezi miwili washaachana
 
Bufee lazima liwepo. Na Kama huna kitu hata padre hakanyagi utazikwa Kama Mzoga na walevi tu
misiba imekuwa kama sherehe fulani hivi. Anyway ishakuwa kama utamaduni uliozoeleka. Unakuta watu wamejaa kumbe wengine wanapata wasaa wa kupata mlo tofauti kwa siku
 
Back
Top Bottom