Misingi, itikadi za dini na mabomu ya kujitoa mhanga

Misingi, itikadi za dini na mabomu ya kujitoa mhanga

Inaonesha imani zao za dini wazungu hazina athari kwenye maisha yao na tamaduni zao na ndiyo maana wanaendana nazo bila tabu yeyote,hivyo inaonekana uislamu ndio tishio la tamaduni zao wazungu walizozizoea.


Tatizo la vijana ama waumini wengi wa kiislam ni wepesi sana wa kukopi vitu bila hata kufikiri. Mtume Mohammed alikuwa anayafanya haya karne ya 6, analazimisha watu wamuite 'Mtume' na wakikataa anawaua kisha anabaka wake zao. Na sasa vijana wa kiislam wanayafanya yale yale, wakiona mtu aendani na Imani yao wanajilipua mabomu ili kuwaua.
 
Nimeipenda hiyo Idar-al-islam, ambayo ndiyo imezaa jina la Daresalaam.
Maana yake - maskani ya uislam.

Dola ya Kiislam haitofanikiwa kusimama, kama itataka kueneza Uislamu kwa nguvu.
Baadhi ya makundi ya Kigaidi kama ISS yanajipambanua wazi wazi kabisa katika kuonesha nia ya kueneza Uislamu kwa vita na kuwaua wasioamini.
Uislamu kama utaenezwa kwa Upendo na amani basi unaweza kujitanua na kuweza kujenga himaya au dola kubwa duniani katika kipindi kijacho.
Matendo ya Vurugu na Vita yanaleta matokeo hasi kwenye jamii iliyostaarabika na kuishia kudhoofisha imani husika.
😂😂😂😂 umenifanya nicheke hapo kwenye "uislamu unaweza kujitanua na kuweza kujenga himaya au dola kubwa duniani katika kipindi kijacho" hivi unajua dini yenye wafuasi wengi duniani na dini inayokuwa kwa ksi zaidi duniani? Hebu fuatilia inaonekana haujui unacho kiandika 😂😂
 
Upo wrong mkuu,Jihad ipo ya (nafsi) ambayo ni kupambana na nafsi yako juu ya kutofanya mambo ya maasi.Pia ipo jihad ya vita(kital).
Nizungumzie jihad ya vita ambayo ndio msingi wa mada yako, hii jihad ikikuja miaka takriban 13 baada ya mtume kupewa utume,vita ya Badr ndo ilikuwa ya kwanza kupiganwa baina ya waislam na wasiokuwa waislam.Ndani ya miaka 13 waislam walitaabika kwa kuteswa na kuuliwa na makafiri wa Mecca ndipo ikipokuja ruhusa kuwa sasa waislam wajitetee kwa kupambana na adui yao.
Jihad haikuja kuwalazimisha watu kuwa waislam bali ilikuja kuutetea na kuulinda usilam,dini haienezwi kwa nguvu inaenezwa kwa hoja zisizo na mashaka.
Upanga au jihad ulikuja ku-defend uislam baada ya kuonewa sana na kwa kipindi kirefu.
Quran inasema ktk surat Albaqara kuwa hakuna kulazimishana ktk dini sasa ww umetoa wapi kwamba jihad ipo kulazimisha watu waingie ktk uislam?
Well said
 
Tatizo watu wanachagua pa kuamini na wanataka waelewe kama akili yao inavyojitaka ielewe. Hata ulete tani na tani za ushahidi kamwe hawatokuelewa. Kwa nini? Kwa sababu wameshajichagulia mahala pa kuamini na akili yao inataka ielewe kama inavyojitaka ielewe.

Uislam ni dini yenye misingi yake, nguzo zake na taratibu zake. Na kama unataka kuuhoji uislam basi uhoji kutokana na uislam wenyewe na wala si kwa kupitia muislam. Kwa sababu mfumo na anayeufuta mfumo ni njia moja ila wapita njia ni tofauti.

Uislam haujaimiza kujieneza kwa kutumia mapambano ya kumwaga damu au kwa njia yoyote ile ya vurugu. Kwa nini? Kwa sababu uislam wenyewe unasema " Laa ik' raha fii ddin" hakuna kulazimishana katika dini. Na hii ni aya katika suratul Baqarah. Nafahamu katika Qur'an zipo aya za vita. Swali la kujiuliza kwa nini zipo aya za vita. Ukitaka kulijua hili lazima urudi katika historia ya uislam kipindi cha Muhammad. Kwa nini? Kwa sababu Qur'an imeshuka kutokana na matukio na katika historia tunapata matukio husika.

Uislam haukuanzisha vita, isipokuwa wao walianzishiwa vita. Walinyimwa Uhuru wa kuabudu, walipokonywa Mali zao zote walizomiliki, walitengwa na jamii na wakawa wanauliwa kisa tu ni Muislam. Iliwalazimu mpaka kuhamia mji mwengine. Na licha ya hayo njiani wakawa wanawindwa kama wanyama na wakawa wanauliwa. Wakaanzisha makazi katika mji waliyoufikia nao ni Madinah. Wakafuatwa huko huko wakawa wanaendelea kufanyiwa dhulma. Na Maswahaba wakimuuliza mtume Muhammad s.a.w, mtume anawajibu kwa kuwaambia msiwadhuru waacheni lakini bado walikuwa ni wenye kuonewa. Na baada ya hapo ndipo zikashuka aya zinazoruhusu wapigane " wameruhusuwa kuzichapa wale wanaodhulumiwa; na mpambane nao mithili ya wao wanavyopambana na ninyi. Na wakaambiwa wasiwapige watoto, wanawake na wazee na wala wasiharibu vyanzo ambavyo vina manufaa kwa binadamu wote; Kwani Mungu hawapendi wanochupa mipaka".

Sasa fananisha wanayoyafanya Isis, al Qaeda, Boko haram na Alsha bbab. Tujiulize wanapigana kwa misingi ip?

Aya na hadithi za vita zimebaki ni ," Defensive " tu kama nchi zilivyojiwekea mipaka yake kwamba ukivuka tu mipaka yake basi umeingia kwenye vita na hiyo nchi, kadhalika na uislam vilevile. Sihofii watu kuja na tofauti na haya, kwa sababu wameshachagua mahala pa kuamini na akili yao inavyotaka ielewe kama inavyojitaka ielewe. Na hayo makundi yote ya kigaida yameondolewa na wanawazuoni wa kislam kwamba si waislam.
Umemaliza kila kitu mkuu ila bado kuna vichwa vigumu
 
Tatizo la vijana ama waumini wengi wa kiislam ni wepesi sana wa kukopi vitu bila hata kufikiri. Mtume Mohammed alikuwa anayafanya haya karne ya 6, analazimisha watu wamuite 'Mtume' na wakikataa anawaua kisha anabaka wake zao. Na sasa vijana wa kiislam wanayafanya yale yale, wakiona mtu aendani na Imani yao wanajilipua mabomu ili kuwaua.
Ungeweka na ushahidi wapi mtume alilazimisha mtu kuingia kwenye uislamu na wapi alibaka wake zao?
 
Nimeipenda hiyo Idar-al-islam, ambayo ndiyo imezaa jina la Daresalaam.
Maana yake - maskani ya uislam.

Dola ya Kiislam haitofanikiwa kusimama, kama itataka kueneza Uislamu kwa nguvu.
Baadhi ya makundi ya Kigaidi kama ISS yanajipambanua wazi wazi kabisa katika kuonesha nia ya kueneza Uislamu kwa vita na kuwaua wasioamini.
Uislamu kama utaenezwa kwa Upendo na amani basi unaweza kujitanua na kuweza kujenga himaya au dola kubwa duniani katika kipindi kijacho.
Matendo ya Vurugu na Vita yanaleta matokeo hasi kwenye jamii iliyostaarabika na kuishia kudhoofisha imani husika.
Bandari salama ni nini?
 
Killing is part and percel of their religion..
Angalizo: Sijataja dini ya mtu
 
Mwandishi huko alikocopy na wewe mwenyewe wala dunia nzima hata hao wamarekani wameshindwa kutoa definition ya ugaidi. Gaidi ni nani? Ugaidi ni nini? Dunia hii ya leo ukiwa unatetea haki yako unakuwa listed ni gaidi. Kama ulikua hujui....Nelson Mandela ameshawahi kuwekwa kwenye list ya magaidi kwa matendo yake yale ya kupiga ubaguzi wa rangi na kutetea uhuru.

Tukichambua ugaidi kwa matendo.....basi George Bush, Obama, Tony Blair, Emmanuel Macron et al wote ni magaidi. Anti Balaka ni magaidi, na wale wanaoshambulia wenzao Rohingya Myanmar nao ni magaidi.

Ulichokiandika hapo ni kuhusianisha Uislam na Ugaidi na hiyo ni western propaganda. Magaidi wapo dunia nzima. Na Uislam sio ugaidi.

Kuna kitu hukijua katika ulimwengu wa leo. Usiandike usivyovijua.
 
Mie nimependa hiyo definition Mpya ya ugaidi.

Mie awali nilijua ugaidi ni kuua Mtu Au kuhujumu mali bila ya Haki Kumbe ipo specific.
Hiyo sio definition ya ugaidi. Mpaka hakuna definition ya ugaidi. Hakuna.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] umenifanya nicheke hapo kwenye "uislamu unaweza kujitanua na kuweza kujenga himaya au dola kubwa duniani katika kipindi kijacho" hivi unajua dini yenye wafuasi wengi duniani na dini inayokuwa kwa ksi zaidi duniani? Hebu fuatilia inaonekana haujui unacho kiandika [emoji23][emoji23]
Najua
Kati ya watu wa duniani.
33% ni Wakristo ambao idadi yao ni karibu Bilioni 2.3
Hapo 50% ni RC.
21% ni Waslamu ambao ni idadi ya 1.5 billion people.
Wahindi wako 13% ya population ya dunia.
Sasa kikichokufanya hadi ucheke ni kitu gani ?
Funguka mkuu.
 
Kwao yana make Sense sana ndio maana wapo tayari kufa kwa ajiri ya kuyafikia maslahi yao,
tatizo mbinu wanayotumia ina madhara kwa watu walengwa na wasio walengwa.
Jingine huwa hawaweki wazi madai yao, kwani yangejulikana kijamii yangeweza kushughurikiwa kijamii pia.
Kama hawako wazi ndio ujue wana ajenda zao na wala hawapo pale kidini.
 
Kuna tofauti kati ya kuweka sheria na kufata sheria unazoweka mwenyewe..Mtu anayesema anatetea wanyonge ndo huyo huyo ambaye anaweza kuwa mnyanyasaji mkuu.
Uislamu una sheria zake na si hayo mangorongonjo hapo juu wala si hayo ambayo magaidi wanayafanya [kama ni kweli wanafanya mnayosema],ukidhulumiwa ilhali unayo njia sahihi ya kuzuia hiyo dhulma na ukakaa kimya hata wewe uliyedhulumiwa upo makosani.mtu akikuvamia nyumbani kwako kukudhuru basi ni wajibu wako kupambana nae hata akipatwa na baya gani lililotokana na uvamizi wake huna hatia...
 
Yako matukio mengi sana mabaya ambayo hayo makundi yanawafanyia Wakristo.
Kule Afrika ya kati waliwaua Wakristo kwa makusudi kabisa mpaka baadhi ya Wakristo wakaunda kikundi chao cha Antibaraka ili kujilinda na dhulma dhidi yao, kikundi hicho kilifanya mauaji ya kutisha kwa lengo la kulipa kisasi. Matokeo yake nchi ikakosa Amani kwa kipindi kirefu.
Hayo makundi adui yao namba moja ni Wakristo, namba mbili ni watu wa imani nyingine, namba tatu ni Waislamu wasiowaunga mkono.
Ndio maana kila mahali yanapoanzishwa na kudumu ni pale penye makazi ya waislamu, maana baadhi yao wanashiriki kuyaanzisha na kuyafadhiri, na asilimia kubwa ya watu wa makundi hayo ni waislamu.
Ni lazima tuelezane ukweli kwa nia ya Kujenga jamii yenye Amani.
Ndiyo maana nikasema unatumia hisia mkuu,et kwamba magaidi adui wao wa kwanza ni wakristo! Inaonesha mkuu nawe una chuki za kidini,watu wanabutua mabomu kwenye mikusanyiko ya watu wenye imani tofauti halafu wewe unakuja kusema adui yao mkuu wakristo.

Yani umeshindwa kusema kila mpenda amani ni adui wa hao magaidi matokeo unaanza kugawa watu kiimani kwamba et adui wao ni mkristo,imani zengine na waislamu wenye kuwapinga.
 
Tatizo la vijana ama waumini wengi wa kiislam ni wepesi sana wa kukopi vitu bila hata kufikiri. Mtume Mohammed alikuwa anayafanya haya karne ya 6, analazimisha watu wamuite 'Mtume' na wakikataa anawaua kisha anabaka wake zao. Na sasa vijana wa kiislam wanayafanya yale yale, wakiona mtu aendani na Imani yao wanajilipua mabomu ili kuwaua.
Hayo mambo yameanza kwenye biblia kasome visa vya mitume kwenye biblia utakutana na mambo kama hayo yamefanywa na mitume.
 
Hii mada unatakiwa uitazame kwa umakini wake hasa ktk misingi ya imani inayoujenga uislam au ukristo. Huwa najiuliza hawa wanaoitwa magaidi wanatumia kitabu gani nikakuta ni kurani hiyohiyo labda wanapishana tafsiri au mmoja wao ameamua kuwa passive ili aendane na jamii ya kisasa inayomzunguka.
Hapa ninapoandika hii post natizama documentary ya TO THE BELIEVERS inayoelezea shekhe Maulana Abdul Aziz na misikiti yake ya Red Mosques. Siyo movie ni documentary na mahojiano aliyoyafanya ukipata muda uitazame unaweza pata kitu ktk mada hii
 
Mbona marekani hashighulikii haya makundi??
Mkuu nyumba ya pili wakila dagaa siyo lazima na wewe ule dagaa. Hatuwezi kuilazimisha nchi yyte kuingilia ugomvi bila ridhaa yake. Vita inahitaji vyanzo vingi vya mapato kuendesha.
 
Kuna mungu mmoja hivi,yeye anapenda kuona watu wakikata wenzao viungo Kwa sababu ya mabomu ya kujitoa mhanga.
Pia amewaaidia watu wake kuwa ukijilipua basi peponi unapewa vimwana bikila wanajaa basi la Abood,Sasa wanajilipua kama hawana akili vile.
 
Mkuu unakumbuka shambulio la kigaidi pale Garissa nchini Kenya? Magaidi waliruhusu waislamu wakaondoka wao wakaanza kuua wakristo sasa tutofautisheje ugaidi na uislamu? Alafu waislamu hamuwezi kujenga hoja kumshawishi Mkiristo asilimu mpaka mtumie nguvu na pesa. Unaposema waislamu walionewa mpaka ikashuka haya yakujitetea au kulinda uislamu kwa panga je aya iyo ukomo wake lini? Nijibu kwa umakini.
MKUU tukio la gharisa likifanya jamaa angu mmoja wa miaka mingi tukakosana. Mimi nilipost article ktk group la wasap ilielezea tukio lilivyotokea. Habari hiyo ilikuwa inaelezwa na almanusura wa kiislam amabye hakupendezwa na lile tukio la gharisa. Jamaa akanifuata Inbox kuwa kwanini na post vile. Nikamwambia thts what happened aisee alijisikia vibaya sana yaani pamoja ni msomi mzuri, muislam mzuri lakini hakupata amani kuona taarifa ile inawafikia au watu wajue kilichotokea.
Kumbuka huyu hakupenda lakini je anaweza ku argue aya kwa aya na wanaofanya hayo na kuwa prove wrong...sidhani kama anaweza. Since then hatukuwa kama zamani ktk urafiki
 
Back
Top Bottom