UKWELI NA UPOTOSHWAJI JUU YA JIHAD
Mnamo tarehe 11, Septemba, 2001, watu wachache waliteka nyara ndege ne za kiraia na kuzitumia kama silaa kuzua hofu ndani ya Marekani, hususan kwenye yale majengo mawili ya kituo cha Biashara cha Ulimwengu. Wafanyakazi wote na abiria katika ndege hizo, na vile vile takriban raia wapatao elfu tatu walipoteza maisha yao katika mashambulizi yake.
Sera za mambo ya nje za Marekani kuhusiana na nchi za Kiislam hazithibitishi uhalali wa kwamba raia wa Marekani waliokuwa ndani ya ndege zile na yale majengo ya Kituo cha Biashara cha Dunia wauawe. Hivi sivyo Uislam unavyofundisha. Hebu yaangalie yale maelekezo ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) katika wakati wa vita: Yeye kwa uwazi kabisa alikataza mauaji ya wazee, watoto na wanawake.1 Wale ambao walipoteza maisha yao katika yale majumba marefu ya kituo cha Biashara cha Dunia na ndani y a ndege zile wote walikuwa ni raia, na wachache wao walikuwa ni Waislam.
Viongozi wote wa Kiislam ndani ya Marekani, Canada, na Duniani kote kwa uwazi kabisa walishutumu utekaji nyara ule ambao ulitendwa huko Marekani kama ni kitendo cha kigaidi ambacho hakikubaliki katika Uislam.
Shutuma hizo ziliegemea kwenye thamani ya kidunia ya utukufu wa maisha ya mwanadamu. Qur’an Tukufu inasimulia kisa cha mauaji ya kwanza katika historia, kile cha watoto wawili wa Adam (a.s.) ambamo Qabil (Cain) alimuua ndugu yake, Habil (Abel). Hili liko katika Sura ya 5 ya Qur’an Tukufu, aya ya 27 hadi 31.
Mwishoni mwa kisa hiki, Mwenyezi Mungu anasema:
“………………yeyote atakayemuua mtu ambaye hakuua, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewaua watu wote, na mwenye kumwacha mtu hai ni kama amewaacha watu wote hai……….” (5:32)
Ni dhahiri kutokana na aya hii kwamba (1) isipokuwa kama mtu ameshitakiwa na kuthibitika kuwa amemuua mtu, yeye hawezi kuuawa – na (2) kwamba kumuua mtu asiye na hatia ni sawa na kuua watu wote.
Hivyo ni Vipi Kuhusu Jihadi?
Moja ya mambo yaliyo kinyume ya zama hizi ni kwamba ingawa njia za mawasiliano zimeendelea kwa kiasi kikubwa mno, watu bado wana matatizo katika mawasiliano yenye maana ya makusudi kabisa na mazungumzo na tamaduni nyingine na dini mbali mbali. Kuna upotovu wa taarifa mwingi na kutoeleweka kwa imani ya Kiislam.
Watu wengi binafsi, wale wa kawaida na wataalam pia wamejaribu kuiunganisha tarehe 9/11 na dhana ya Jihadi katika Uislam. Katika moja ya mazungumzo ya maonyesho ya redio ya Toronto, mara baada ya Septembea kumi na moja, nilimsikia mpiga simu mmoja akasema kwamba kile kilichotokea siku ile kilikuwa kwa 10% ni ugaidi na 90% ni Uislam. Kiongozi mmoja wa kikristo mwenye siasa kali huko Marekani alisema katika onyesho lake la kwamba “Yumkini (inawezekana) Muhammad alikuwa gaidi.”
Hivyo ni muhimu kuzungumza Kuhusu Jihadi katika Uislam.
a) Uislam ni Dini ya Amani
Uislam kimsingi ni dini ya amani. Jina lake “Islam” linatokana na neno la kiarabu “Silm” ambalo lina maana mili: moja ni “kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu” na ya pili ni “amani”. Maana zote zinaingiliana.
Wakati wowote Waislam wanapokutana, wanatumia maamkizi ya amani “as-salaam alaykum – amani iwe juu yako,” na huyo mtu mwingine anajibu kwa kusema “alaykums-salaam – juu yako iwe amani.”
ISLAM
SILM
1. Kujisalimisha kwa Allah
2. amani (kwa wanadamu wenzio)
Sala za kila siku zinaanza na kumsifu Allah kama “Rehema na Mwenye fadhila” na zinaishia na salam za amani kwa wote.
b) Dhana ya Jihad
Dhana ya Jihadi inahitaji kueleweka vizuri. Watu wengi katika vyombo vya habari wanayachukulia maneno ya Qur’ani nje ya muktadha wake. Na kwa hiyo hebu tuone ni nini maana ya Jihadi?
Hili neno “Jihad” halina maana ya “vita takatifu.” Huu ni utoaji wa ki- magharibi wa dhana pana katika mafundisho ya Kiislam. Muulize mtaalam yoyote yule wa lugha ya kiarabu na atakwambia kwamba “Jihad” haina maana ya “vita takatifu.” Maneno, au usemi huu wa “vita takatifu” umekuja kutokana na dhana ya Kikristo ya “vita ya haki,” na umetumika hovyo hovyo kama lahaja ya Kiislam tangu zile siku za Krusedi.
Hivyo basi, Jihadi ina maana gani?
Katika lugha ya kiarabu, neno Jihadi kwa maana halisi ni kujitahidi na kufanya kazi kwa bidii sana kwenye jambo fulani. Katika Istilahi za Kiislam, linabakia na maana halisi hizo katika vipimo viwili tofauti, ambavyo vinaelezewa kwa “Jihadi kubwa” na “Jihadi ndogo.”
Jihadi kubwa – inajulikana kama mashindano ya kiroho, mashindano kati ya nguvu mbili ndani yetu: nafsi na mwili. Moyo unapambana na matamanio ya kimwili. Mapambano haya ya kiroho ni Jihadi inyoendelea ndani ya kila mmoja wetu. Uislam unawatarajia wafuasi wake kutoa kipaumbele kwenye nafsi na dhamira juu ya mwili na tamaa zake.
Kule kufunga katika mwezi wa Ramadhani ni mfano wa mafunzo ya kila mwaka kwa ajili ya Jihadi hii.
Jihadi ndogo ni yale mapambano ya silaha. Hata hivyo, hii haina maana ya moja kwa moja kwamba ni matumizi ya kufanya vurugu za kidhalimu zisizo na haki. Hii Jihadi ndogo inaweza kugawanywa kwa namna mbili: Uchokozi na ulinzi. Uchokozi na uvamizi dhidi ya watu wowote wale hauruhusiwi katika Uislam; kwa hali yoyote ile, ulinzi ni haki kamili ya kila mtu na kila Taifa.
JIHÃD
(Mapambano)
KUBWA NDOGO
(ya kiroho) (Mapambano ya silaha)
Ulinzi Uchokozo
Uislam umeruhusu hii Jihad ndogo kwa ajili tu ya kuwalinda Waislam na ardhi zao, na kudumisha amani katika jumuiya za Kiislam.
Jihadi Ndani ya Qur’ani Tukufu
a) Aya za mwanzo
Hebu sasa tuende kwenye baadhi ya aya kutoka kwenye Qur’ani Tukufu.
Vita vya kwanza alivyopigana Mtume na wafuasi wake vilikuwa ni vita vya kujihami kiulinzi. Vinajulikana kama vita vya Badr, sehemu ambayo iko karibu na mji wa Madina (ule mji wa Mtume huko Arabuni). Hivi vilikuwa ni vita ambavyo Mtume alitoka na wafuasi wake kukabiliana na majeshi ya adui ambayo yamekuja kutokea Makkah ambako kulikuwa bado kunadhibitiwa na makafiri.
Aya ya kwanza ya Jihadi ndogo, mapambano ya silaha, ambayo ilishuka kwa wakati huo, imo kwenye Sura ya 22 ya Qur’an Tukufu, aya ya 39-40. inaelezea wazi kabisa lengo la hii Jihadi ndogo:
“Imeruhusiwa (kupigana) kwa wale ambao wanapigwa, kwa sababu wamedhulumiwa, na kwa hakika Mwenyezi Mungu anao uwezo wa kuwasaidia, wale ambao wametolewa majumbani mwao bila sabau ya haki………”
Halafutena ikizungumzia kuhusu wale makafiri wa Makkah ambao walipigana vita baada ya vita dhidi ya Mtume na wafuasi wake huko Madina, Qur’ani Tukufu katika sura ya 2, aya ya 190 inasema:
“Na wapigeni vita katika njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanakupigeni vita, wala msiruke mipaka, hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wanaoruka mipaka.”
Katika aya hii, mazungumzo ni kuhusu kutoa majibu kwenye vita kwa kujilinda na kujihami wenyewe, hakuna kauli ya kuanzisha uchokozi hata kidogo. Hata katika mtindo wa mapambano ya kujihami, Mwenyezi Mungu Mtukufu bado anawaonya Waislam kwamba wasije “wakavuka” mipaka inayostahiki.
Uislam unawafundisha Waislam wawe wenye nguvu ili kuweza kujilinda wenyewe, lakini hivyo haina maana kwamba wao wawe wachokozi au madhalimu. Katika Sura ya 8, aya ya 60-61 ya
Qur’an Tukufu, Mwenyezi Mungu ametoa mwongozo huu wa jumla kwa uwazi kabisa pale ambapo anazungumza na Waislam kwa namna ifuatayo:
“Na waandalieni nguvu kiasi mnavyoweza, na kwa farasi ambao wamefunzwa (kwa maandalizi hayo) ili muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu, na maadui zenu, na wengine wasiokuwa wao, msiowajua, bali Mwenyezi Mungu anawajua.”
Baada ya kutoa maelekezo hayo ya Jumla na mwongozo wa kuwa wenye nguvu na waliojiandaa tayari kwa kujilinda wao wenyewe, aya inaendelea kusema:
“Na kama wakiaelekea (hao maadui) kwenye amani, nawe pia ielekee na umtegemee Mwenyezi Mungu……..”
Kwa ufupi, Uislam unawataka Waislam kuwa na nguvu ili kwamba watu wengine wasije wakawaonea; lakini pia wanapaswa kunyoosha mkono wa amani hata kuelekea kwa maadu zao kama kuna kuwepo na mwelekeo wa amani kwa upande wa adui.
b) Tatizo la Maandiko na Muktadha wake
Baadhi ya waandishi na wazungumzaji wanazinukuu aya za Qur’an Tukufu nje ya muktadha wake na kujaribu kuulaumu Uislamu kwa kueneza vurugu na ugaidi. Wanachukua maandishi na wanayatumia nje ya “muktadha” wake.
Ni sawasawa kabisa na mtu anayetafuta ndani ya Biblia na kuchukua maneno au sentensi zifuatazo ili kuthibitisha kwamba Biblia inaendeleza vurugu:
“Chukua viongozi wote wa watu hawa na uwauwe.” (Hesabu 25:7)
“Sasa wauwe watoto wa kiume wote. Na muue kila mwanamke ambaye amelala na mwanaume, lakini muacheni kila msichana ambaye hajalala na mwanaume kamwe.” (Numbers 31:17-18)
“Muue kila mwanaume na kila mwanamke ambaye sio bikira.” (Waamuzi – 21:11)
Hakuna mtu mwenye akili timamu atakayekubali uwasilisho wa “nje ya muktadha” kama huo wa mistari ya Biblia. Hata hivyo, bado tunawaona wainjilisti na wahubiri wengi wa Kikristo wakifanya hivyo hivyo hasa kwenye Qur’an bila hata kusita kokote kule.
Hivyo hebu tuangalie baadhi ya mifano ya kuchukua “maneno” ya Qur’an Tukufu nje ya “muktadha” wake.
Mfano wa kwanza
Sura ya 2 aya ya 191 inanukuliwa kama ifuatavyo:
“Waueni popote mtakapowakuta.”
Ili kuuelewa muktadha kamili wa aya hii, soma kuanzia aya ya 190 hadi 193 kwa pamoja zote:
“Na wapigeni vita katika njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanakupigeni vita, wala msiruke mipaka, hakika Mwenyezi Mungu hawapendi warukao mipaka. Na wauweni popote muwakutapo, na muwatoe popote pale walipowatoeni, na fitna ni mbaya zaidi kuliko kuua. Wala msipigane nao katika Msikiti Mtukufu mpaka wao wawapigeni ndani yake. Na ikiwa watakupigeni basi nanyi pia wapigeni, kama hiyo ndio malipo kwa makafiri. Lakini watakapokoma, basi (waacheni) hakika Mwenyezi Munguni mwingi wa kusamehe, mwenye kurehemu. Na wapigeni mpaka pasiwepo na mateso, na dini iwe ni ya Mwenyezi Mungu peke yake, watakapokoma basi pasiwepo na uadui ila dhidi ya madhalimu.”
Muktadha huu unafafanua kwamba ile aya ya 191 inawaruhusu Waislamu wa Madina kujihami wenyewe kiulinzi dhidi ya uchokozi na uvamizi wa makafiri wa Makkah. Kwa hakika haisemi kwamba waende wakipita duniani kote ili kumuua kila kafiri watakayemkuta!
Mfano wa pili
Sura ya 4, aya ya 74 ambayo inadhaniwa kwamba inahimiza umwagaji damu:
“Basi wapigane katika njia ya Mwenyezi Mungu wale wanaouza maisha (yao) ya dunia kwa akhera. Na anayepigana katika njia ya Mwenyezi Mungu akauawa au akashinda, basi hivi karibuni tutampa malipo makubwa.”
Wale wanaoinukuu aya hii, kwa manufaa yao, kwa urahisi tu wanaiacha ile aya inayofuatia ya 75 ambayo inaelezea lengo na uhalali wa hii Jihadi ndogo.
“Na mna nini, hampigani katika njia ya Mwenyezi Mungu, na wale wanaoonewa katika wanaume na wanawake na watoto ambao husema: Mola wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu, na utujaalie mlinzi kutoka kwako, na utujaalie msaidizi kutoka kwako…………”
Aya hii dhahiri kabisa inawahimiza Waislam kusimama kwa ajili wanaume, wanawake na watoto wanaonewa.
Hivi dini za kimungu zisiwatetee wanaume, wanawake na watoto wanaoonewa?
Mfano wa tatu
Sura ya 9, aya ya 12: “Basi wauweni viongozi wa ukafiri.”
Hii ni sehemu tu ya fungu zima la maneno ambamo Mwenyezi Mungu anazungumzia kuhusu Waislam huko Madina na mkataba wao wa makubaliano ya kusimamisha mapigano na makafiri wa Makkah. Tazama aya ya 12 -14:
“Na kama wakivunja viapo vyao baada ya kuahidi kwao na wakatukana dini yenu, basi wauweni viongozi wa ukafiri kwani viapo vyao havina maana ili wapate kujizuia. Je, hamtapigana na watu waliovunja viapo vyao na wakafunga nia ya kumfukuza Mtume, nao ndio waliokuanzeni mara ya kwanza? Je mnawaogopa? Basi Mwenyezi Mungu anastahiki zaidi mumuogope, ikiwa nyinyi mmeamini. Peganeni nao, Mwenyezi Mungu atawaadhibu kwa mikono yenu, na awahuzunishe na akunusuruni juu yao na avipoze vifua vya waumini aondoe ghadhabu ya nyoyo zao, na Mwenyezi Mungu humkubalia toba ampendaye, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hekima.”
Muktadha huu kwa uwazi kabisa unatoa haki ya kujihami kwa Waislam, bali kwa hali yoyote ile, hautangazi uchokozi.
Mfano wa Nne
Sura ya 9, aya ya 36: “Na nyote piganeni na washirikina.” Kwa kweli, msitari huu ni sehemu ya aya nzima ambamo Mwenyezi Mungu anazungumzia kuhusu utakatifu wa miezi minne kati ya miezi yote kumi na mbili, ambamo kupigana kumekatazwa. Kisha inasema:
“Na piganeni na washirikina kwa pamoja kama wao wote wanavyopigana nanyi, na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanao muogopa.”
Wale wanaopenda kuzichukua aya za Qur’an Tukufu nje ya muktadha wake kwa faida yao wanaiacha ile sehemu “kama wao wote wanavyopigana nanyi.” Kama unavyoona, aya hii pia inatoa majibu kwa ule uchokozi ulioanzishwa na washirikina dhidi ya Waslamu; haizungumzii juu ya kuanza vita.
c) Hitimisho
Kutokana na mifano hii, ni dhahiri kabisa kwamba Uislam hauzungumzii juu ya Jihadi ndogo kwa ajili ya uchokozi; bali inawaruhusu Waislam kujilinda kivitendo maisha yao, mali zao na ardhi zao dhidi ya uchokozi wowote ule, na pia kupigana kwa ajili ya kukomesha udhalimu dhidi ya wanaume, wanawake na watoto wanaoonewa.
Zile aya kuhusu waabudu masanamu wa Makkah zenyewe ni makhsusi sana na zilizohusika kwa kipindi kile tu. Hebu tuangalie tena ile sura ya 22, aya ya 39 hadi 40:
“Imeruhusiwa kupigana kwa wale wanaopigwa kwa sababu wamedhulumiwa, na kwa hakika Mwenyezi Mungu anao uwezo wa kuwasaidia. Ambao wametolewa majumbani mwamo pasipo haki ila kwa sababu wanasema Mola wetu ni Mwenyezi Mungu. Na kama Mwenyezi Mungu asingeliwakinga watu baadhi yao kwa wengine, bila shaka yangelivunjwa mahekalu na makanisa, masinagogi na misikiti ambamo jina la Mwenyezi Mungu hutajwa kwa wingi. Na bila shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anayemsaidia Yeye. Hakika MwenyeziMungu ni Mwenye nguvu Mtukufu.”
Uislamu unashughulika na jamii ya mwanadamu yenye uhalisia na sio ya kidhanifu. Katika maneno ya Dr. Sayyed Hussain Nasr, “Waislam wanayaona maadili ya Kikristo ni adhimu sana kwa wanadamu wa kawaida kuweza kuyafuata; inaelekea kwamba ile amri ya sheria ya kugeuza shavu la pili ilikuwa ikilengwa kwa watakatifu tu. Wakristo kwa karne nyingi hawakuonyesha kujizuia katika vita kuliko watu wasiokuwa Wakristo. Wazo lililohubiriwa na utaratibu uliofuatwa vimekuwa wakati mwingi havihusiani.” 2
Tumalizie na Sura ya 109 ya Qur’an Tukufu
:
“Sema: Enyi makafiri! mimi siabudu mnachokiabudu, wala ninyi hamuabudu ninayemuabudu. Wala sitaabudu mnachoabudu. Wala ninyi hamtaabudu ninayemuabudu. Ninyi mna dini yenu nami nina dini yangu.”
Matumizi mabaya ya “Jihãdi”
Kwa sababu tu kwamba neno “Jihad” linatumiwa vibaya na baadhi ya Waislamu kwa ajili ya ajenda zao za kisiasa, Waislamu hawapasi kuitelekeza dhana hii tukufu ya Imani ya dini yao. Wakati wa kuzungumzia kuhusu Jihadi, mimi nimewasikia Waislam wengi wakielezea ile Jihadi kubwa (ya kiroho) tu na kukwepa kuzungumzia hii Jihadi ndogo kwa maana ya mapambano ya silaha (kijeshi) juu ya kujihami. Sisi kama Waislam, tunasimama imara mafundisho yetu na hatuhitaji kuomba samahani kwa ajili ya hilo hata kama nyoyo au nafsi zilipotoka zitateka nyara Istilahi za Imani yetu kwa ajili ya manufaa yao ya kisiasa.
Sio watu kama Bin Laden tu ambao wanateka na kutumia vibaya Istilahi tukufu za Kiislam; tumeona vile vile hata serikali ya Marekani ikitetea hii dhana ya Jihadi ndogo pale ilipokubaliana na maslahi yake binafsi ya siasa za kidunia.
Wakati wa ukaliaji kivamizi wa Urusi huko Afghanistan katika miaka ya themanini (1980’s), Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa lilitumia mamilioni ya dola kwa ajili ya kuwagawia wanafunzi wa Afghanistani vitabu vya kiada vilivyojazwa mapicha ya vurugu na mafundisho ya “Upenda Mapambano wa Kiislamu.” Vikiwa vimechapishwa katika lugha zinazotawala za ki Afghan za Dari na Pashtu. Vitabu hivi vya kiada viliendelezwa katika miaka ya mwanzoni ya 1980 chini ya msaada juu ya ukimwi (Aids) kwa Chuo Kikuu cha Nebraska – Omaha na Kituo chake cha Mafunzo yaAfghanistan. Shirika hilo lilitumia Dola 51 milioni katika program ya elimu ya Chuo hicho ndani ya Afghanistan kuanzia 1984-1994.
Vitabu vya kwanza, ambavyo vilijazwa habari za Jihadi na kuonyesha michoro ya mabunduki, risasi, askari jeshi na mitego ya mabomu, vimetumika tangu wakati huo kama kiini cha mtaala wa mfumo wa shule wa Afghanistan. Tofauti na watoto wote duniani kote kulikobakia, ambao vitabu vyao vya kiada vya hisabati vina mapicha ya matunda ya tufaha na machungwa, watoto wa Afghanistan walifundishwa kuhesabu kwa michoro inayoonyesha vifaru, makombora na mabomu ya kutegwa ardhini.
Na kwa hiyo pale ilipofaa maslahi yake ya kimkakati, wa hila, Marekani iliendeleza utamaduni wa Jihadi miongoni mwa watoto wa Afghanistan kwenye miaka ya themanini na Raisi Reagan aliwahi hata kuwakaribisha “Mujahidina” wa Afghanistani huko White House. (Hata Taleban walitumia hivyo vitabu vilivyotolewa na Marekani, ingawa chama hicho chenye siasa kali kulikwaruza na kufuta nyuso za binadamu katika kuendana na mfumo wao msingi halisi.) Kwa sasa kwamba ule utamaduni wa vurugu umekuja kuisumbua Marekani, utawala wa Marekani uko kinyume kabisana wazo la Jihadi na unawategemea Waislam kuiacha dhana hiyo kabisa kabisa.
Waislam hawawezi kutegemea kubadili mawazo yao juu ya dhana hii tukufu ya Jihadi, kwa sababu tu kwamba baadhi ya Waislam wapotovu au mamlaka kadhaa za kidunia wanaitumia vibaya Jihadi kama neno. Waislam wanapaswa kushutumu vikali.
Matumizi mabaya ya Jihadi na kwa kujiamini kabisa waithibitishe na kuitamka kwa dhati dhana hii ya Jihadi kama inavyoelezwa na Qur’an Tukufu na mifano mitukufu ya Mtume Muhammad (s.a.w.).
Vyombo vya habari na kuwapiga chapa Waislam
Kwa kuzingatia haya tuliyoyasema hapo juu, hakuna uhalali wa kuhusisha tukio la Septemba 11 na ile dhana ya Jihadi ndogo katika Uislam.
Hata hivyo, tumesikitishwa sana kuona kwamba vitengo Fulani vya vyombo vya habari, hususan vipindi vya mazungumzo ya maonyesho vya radio bado vinazidi kuchochea chuki dhidi ya
Waislamu, Waarabu na ile imani Tukufu ya kuamini Mungu mmoja ya Uislam. Hii ni licha ya ukweli kwamba Waislamu kiulimwengu walikishutumu kile kitendo cha kigaidi cha Septemba kumi na moja ambamo yalipotea maisha ya watu wasio na hatia.
Kuwalenga Waislam au Waarabu kulikoegemea kwenye hatia kwa ushiriki ni makosa kabisa. Huu undumilakuwili katika vyombo vya habari kwa kweli unatisha. Hebu fikiria japo kwa muda:
Wakati bomu lilipolipuka mnamo siku za mwanzoni za mwezi wa Septemba 2001 huko Ireland ya Kaskazini karibu na shule ya katoliki katika eneo jirani la Protestante, hakuna hata mtu mmoja aliyeilaumu jamii nzima ya Waprotestanti kama “magaidi na wauaji”. Wakati wanaharakati wa IRA walipofanya vitendo vya ugaidi huko Ireland ya Kaskazini au Uingereza, hakuna hata mtu mmoja katika vyombo vya habari va Magharibi ambaye aliipachika Imani ya Katoliki jina kama “Dini ya Ugaidi.”
Pale Dr. Goldstein Mloweziwa Kiyahudi huko Israeli, alipoingia kwenye msikiti wa huko Habron miaka michache iliyopita na akawapiga risasi wafanya ibada wa Kipalestina, hakuna mtu aliyesema kwamba Wayahudi wote ni “magaidi.” Wakati Wa-Serbia walipowaua Waislam kikatili huko Bosnia, vyombo vya habari kamwe havikulilaumu Kanisa la Orthodox kwa jambo hilo ingawa baadhi ya Wahubiri wa Kanisa hilo walikuwa wakiwabariki wanamgambo wa Serbia kabla wao hawajaingia katika kuwaua wafungwa wa Kiislam.
Hata hivyo bado tunaona kwamba wakati Waarabu au Waislamu wachache wanapofanya vitendo vya kuogofya, Waislam wote na Waarabu wote wanapewa jina la “magaidi na wauaji” moja kwa moja. Kama Waislam, tunaviomba vyombo vya habari kutenda haki na sio jingine lolote.
Vyombo vya habari vinapaswa kutambua kwamba wale wateka nyara ambao walitumia ndege zile kama silaha hawakuteka nyara tu zile ndege na kuua maelfu ya watu wasio na hatia huko
Marekani; vile vile wamewaonea na kuwaathiri Waislam bilioni moja na ambao sasa wamepewa au kupachikwa jina kama “wauaji na magaidi.”
JIHADI WIKIPEDIA
Jihadi ni neno lenye asili ya Kiarabu (جهاد jihād) na lenye maana ya kujitahidi kwa ajili ya Allah katika dini ya Uislamu.
Mtu anayehusika katika jihadi huitwa "mujahid". Jihadi ni wajibu wa kidini kwa Waislamu.
Jihadi katika Qurani
Katika Qurani neno jihadi liko mara 41, mara nyingi katika usemi "jihadi kwenye njia ya Mungu (الجهاد في سبيل الله al-jihad fi sabil Allah)". . Katika Qurani "jihadi" huwa hasa na maana ya kijeshi lakini si wazi kama maana hiyo ilikuwa mapigano dhidi ya wenye imani tofauti kwa jumla au vita vya kujihami tu.
Jihadi katika mafundisho ya wataalamu wa shari'a
Katika mafundisho wa wataalamu Waislamu wa karne za kwanza baada ya Muhammad jihadi ilikuwa na shabaha ya kupanua eneo chini ya utawala wa Uislamu na utetezi wake, hadi Uislamu ungekuwa dini tawala.
Hii haikuwa na shabaha ya kuwalazimisha wote wasiokuwa Waislamu kupokea dini hiyo. Katika mafundisho ya wataalamu wa kale, wale walioitwa "Wapagani" walipaswa kushambuliwa hadi wakubali Uislamu au wauawe. Lakini watu wa "ahl al-kitab" (wenye misahafu) yaani Wakristo, Wayahudi na Wasabayi walipewa nafasi ya kukubali kipaumbele cha Waislamu na kuishi chini ya utawala wa Waislamu katika hali ya dhimma.
Katika mwendo wa upanuzi wa utawala wa Kiislamu nafasi ya dhimma iliongezwa pia kwa dini nyingine kama Uzoroastro na Uhindu ingawa hao wana miungu mingi sana.
Mwishoni karibu kila jumuiya ya kidini ilipewa nafasi ya kukubali hali ya dhimma.
Jihadi kati ya Waislamu wa leo
Leo hii ina maana tatu kati ya Waislamu hasa
kutetea imani ya Kiislamu pamoja na kulinda umma ya Waislamu, pia kutetea Waislamu wanaoshambuliwa.
kushindana na udhaifu wa nafsi na kujitahidi kuwa mtu mwema.
jitihada za kuboresha umma ya Waislamu.
Waislamu kadhaa wanaitumia pia kwa maana ya kueneza Uislamu kwa njia ya silaha na matishio. Hapa kuna hata vikundi kama Al Qaida na Boko Haram wanaotumia mbinu za ugaidi kwa jihadi jinsi wanavyoielewa. Ingawa idadi yao si kubwa kati ya Waislamu kwa jumla, watu wengi nje ya Uislamu wanaelewa neno hasa kwa maana inayotangazwa na hao.
TUMSOME PIA MWANA ZUONI
DR ZAKIR NAIK UFAFANUZI JUU YA JIHAD
Jihad
In a lecture given in University of the Gambia, Zakir strongly condemned the atrocities around the world in the name of Jihad, where innocent people lost their lives, saying "Jihad is misunderstood by both Muslims and non-Muslims, Jihad means to strive and struggle to make society better, the best form of Jihad is to strive and struggle against non-Muslims, using the teachings of the Quran; to the Prophet Peace Be Upon Him and the Almighty Allah, Islam means peace." According to Naik, the killing of any innocent person, either Muslim or not is prohibited by Islam, while condemning the double-standard, played by the western powers and media who describes Muslims as extremists and fundamentalists. He said in unequivocal term that, even in Islamic Jihad, there are laid down rules and regulations as when and how to kill a person, which he noted, totally contradicts what is currently happening around the world, by some groups who claim to fight for Jihad.
In another lecture given in Al-Khawaneej, Dubai, Naik stated that the most mistranslated and misunderstood word about Islam by non-Muslims and even some Muslims is "Jihad", which, he said, has nothing to do with the phrase "holy war" that is never actually used in the Quran or sunnah and was first used by the crusaders who killed millions in the name of Christianity. He added the word "Jihad" actually means to strive or struggle against one's own evil inclinations, to make the society better, in self-defense on a battlefield, and against oppression.
September 11 attacks and Osama bin Laden
In a lecture delivered on 31 July 2008 on Peace TV, Naik commented on the attacks of 11 September: "it is a blatant, open secret that this attack on the Twin Towers was done by George Bush himself".He also said that "even a fool will know" that the 9/11 attacks were "an inside job" orchestrated by US President George W. Bush.
His opinions on 9/11 have been denounced by the United States and he has been denied entry into the United Kingdom and Canada for speaking engagements.
His views and statements on terrorism have been often criticised in the media. Speaking of Osama bin Laden, when Naik was asked whether the former was a terrorist, he stated that he did not have an opinion since had not met him, nor interrogated him, and is neither a friend nor an enemy. He believes in checking up information before passing it on to another person. However, Naik went on to say "If he is fighting enemies of Islam, I am for him. I don't know him personally. If he is terrorizing America, the biggest terrorist, I am with him. Every Muslim should be a terrorist. The thing is that if he is terrorizing a terrorist, he is following Islam."
Terrorism, killings and suicide bombing
Later in 2010, Naik said that he had been quoted out of context regarding the remarks on terrorism. "As far as terrorist is concerned", he said, "I tell the Muslims that every Muslim should be a terrorist.... What is the meaning of the word terrorist? Terrorist by definition means a person who terrorises. So in this context every Muslim should be a terrorist to each and every anti-social element. I'm aware that terrorist is more commonly used for a person who terrorises innocent human beings. So in this context no Muslim should ever terrorise a single innocent human being."
Naik stated that Hitler, "who was not a Muslim, is the biggest terrorist in the world as he incinerated 46 million [sic.] Jews."
When asked about his views on killings, Naik said "the Quran says so - if anyone kills an innocent human being, Muslim or non-Muslim, it is as though he has killed the whole humanity, So how can any Muslim kill innocent human being?". It was only permissible, he said, to kill a person who "has killed someone else ... or created corruption in the land." He also criticized the media for "picking up verses of the Quran or hadiths and quoting them out of context to mislabel Islam as a religion that promotes violence and killing". He said that "critics of Islam quotes Verse 5/9 which reads: 'Wherever you find a non-Muslim, kill him' out of context to malign Islam though it was an order in a battlefield, and Islam always promotes peace as better option during war."
In a press conference via skype, when Naik was asked his opinion on suicide bombings he replied affirmatively saying it was permitted in Islam and said "it is haram if innocent people are being killed. But, if suicide bombing is used as a tactic of war, then it may be permitted. For example, in World War II, Japan used suicide bombing as a tactic of war."
Najibullah Zazi
Najibullah Zazi, the Afghan-American linked to Al-Qaeda who was found guilty in the 2009 New York City Subway and United Kingdom plot was an "admirer" of Naik's sermons. When Time hinted that his preachings could have inspired Najibullah Zazi's terrorist activities, Naik insisted: "I have always condemned terrorism, because according to the glorious Koran, if you kill one innocent person, then you have killed the whole of humanity."
ISIS
Naik called Islamic State of Iraq and Syria the "anti-Islamic State of Iraq and Syria" and said that, the enemies of Islam are promoting ISIS. He also added that, "the Quran says so - if anyone kills an innocent human being, Muslim or non-Muslim, it is as though he has killed the whole humanity. So how can any Muslim kill innocent human being? .. We should not say ISIS, we should say AISIS. Because they are anti-Islamic. I request all the muslims of the world, as well as the muslim media, please don't help the enemies of Islam in attacking Islam." He further added that, "If you verify you will know that I am totally against terrorism. I am totally against killing innocent human being." He expressed his view on the move by the United States government to launch an attack on the ISIS in Syria and Iraq that, he strongly condemns the act by the Islamic State group, but he is also not equally supporting the move by the Americans to launch the attack. In another lecture in Dubai, he stated, It is, therefore not correct to say ISIS or Islamic State has killed Syrian or Iraqi innocents. He said, "We should say anti-Islamic state kills them as Quran affirms that whoever kills an innocent person is as if he kills all humanity, and he who saves a single person - disregard his religion, is like saving all humanity."
Orlando shooting
Zakir criticized the media for "linking Islam" with the Orlando attack. He accused the media of a "double-standard strategy" saying, "the same (double-standard strategy) is happening with a man related by nothing to Islam but by his name who killed over 50 gays in Orlando."
WENYE CHUKI NA UISLAMU NI WENGI NA HAWAJAANZA WAO MANA WAPINGAJI WA MUNGU WAPO TANGU ZAMA ZA NUHU NA HAYA YANAHITAJI UJUZI NA UCHAMBUZI WA MAMBO MAANA KUNA WATU WAPO
NYUMA YA PAAZIA.....TERRORISM NI
BIASHARA KUBWA YUPO MNUFAIKAJI.
HIVI NI VITA NA PROPAGANDA JUU YA DINI YA HAKI YA MWENYEZI MUNGU...HIVI PUNDE WATAIPATA YAKINI
NA ALLLAH ANAJUA ZAIDI