Uchaguzi 2020 Misururu ya Wadhamini wa Tundu Lissu Tarime haijapata kutokea, huyu mtu ana nini lakini?

Uchaguzi 2020 Misururu ya Wadhamini wa Tundu Lissu Tarime haijapata kutokea, huyu mtu ana nini lakini?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hali ndio kama mnavyoona ndugu zangu

Subpost 2 - Wadhamini wakiwa kwenye mstari kumdhamini mhe Rais Tundu -lissu -Tar ( 359 X 640 ).jpg
Subpost 1 - Wadhamini wakiwa kwenye mstari kumdhamini mhe Rais Tundu -lissu -Tar ( 359 X 640 ).jpg


Sina cha kuongeza , wale mnaotaka nyama zaidi endeleeni kula mtori , nyama mtazikuta chini
 
Upinzani hauwezi kufa kwa bunduki au kukamata viongoz wao, upinzani ni siasa Safi inayojibu matamanio ya wananchi pasipo vitisho,visasi wala matusi na fitina mbalimbali. Kweny siasa Chama tawala ni Chama pinzani dhidi ya Chama pinzani and vice versa!!Hawa wote ili wawini kukubalika wanahitaji siasa Safi na uongozi bora!

Kama kuna Chama kinadhani kitapata wafuasi ama kitaongeza wafuasi Bila siasa Safi kisahau iko siku kitakufa kifo cha mbwa!

Tunahtaji siasa itakayojali utu wetu na haki zetu na si kutupa haki yetu huku utu wetu ukifichwa kwenye viloba hapana!!

Mungu bariki Tanzania mpya itakayojali utu na zetu!!
 
Ni halali kabisa, Tundu ni mwanasiasa mwenye ushawishi mzuri sema mshindani wake Kutokea CCm yeye ni mwanasiasa mwenye ushawishi mkubwa mara 10 zaidi yake

Tundu atashindanaaa!! Lakini hatoshinda, ni Nani Kati ya Lowasa na huyo Lisu ayekuwa ni mwanasiasa mwenye ushawishi zaidi ya mwingine?

Lakini lowasa licha ya kuwa ni mwanasiasa nguli Kwa Magufuli alisalimu amri

Kwa sasa, Tz hii hakuna kama Magufuli
 
Picha kama hiyo mimi naisoma hivi:

Naona waTanzania watulivu kabisa wanaotafuta haki yao ya msingi ya kuwachagua viongozi wao wanaopenda wawaongoze miaka mitano.

Watu hawa watakwenda kupiga kura kutimiza adhma yao hiyo, kwa utulivu bili ya rabsha zozote.

Halafu baada ya hapo, kura hizo kundi la watu wanaamua hazina thamani yoyote, na wala hazihesabiki katika kumpata kiongozi atakayetangazwa.

Ninaishia hapo katika mtiririko huo wa mawazo yangu.

Hapana. Kabla hujanirukia kwa jazba, sijaandika kwamba waTanzania wengine wapo kwenye mistari mingine, nao wametulia kama hawa. Wao pia wanastahiri heshima yao na kama ndio watakuwa wengi kwa kura zao za haki, basi wana haki ya kupata mtu wanayemtaka, nasi sote ambao hatukumpa kura zetu tutaheshimu maamuzi hayo bila ya shari kama ni matokeo ya haki.
 
Back
Top Bottom