Mita mpya za maji ni kama king’amuzi, maji yakiisha inaji-lock

Mita mpya za maji ni kama king’amuzi, maji yakiisha inaji-lock

Katibu mkuu Wizara ya Maji mhandisi Antony Sanga amesema utofauti wa mita hizo na mita zingine ni kuwa unaweza ukamgawia jirani uniti za maji kama unavyohamisha salio kwenye simu na akaendelea kupata huduma, vilevile kama unahama nyumba uliyokua ukiishi na kuna uniti zako zimebaki kwenye mita unaweza ukahama nazo pia. KONGOLE SANA
Hii system niliikuta Mbeya, Mwanjelwa na Soweto.
IMG_20201219_180016.jpg
 
Wasoma Mita waliopo kazini kwa Sasa wataekekea wapi?
kusoma mita ni kazi ya kikoloni ktk zama hizi za kidigitali.
sasa wafundishwe namna ya kuzisoma kwenye computer sio manual tena.
tena sasa watakuwa wamepunguziwa kazi ya kuzurura, watatulia ofisini.
tuko ktk zama za sayansi na tecknologia.
 
Hili ndilo litakuwa mwarobaini wa tatizo la kubambikiana Bills! Unatumia maji ya 3000 unapewa bill ya 12000.
Extrovert mzee wa kicheko, nakupa angalizo yasije kutokea yale ya tanesco mfumo uka buma siku iyo hamtakoga😅😅😅😅
 
Nahisi, itakuwa na betri, solar na kakompyuta kadogo ndani kwa ndani. Ni nzuri kwakweli! Ndiyo maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Hata Tanesco ilikuwa unaletewa postpaid, baadae luku za nje, na sasa hivi unaingiza umeme kwa rimoti tu ukiwa ndani!
 
Mbona hizo Iringa mjini zimefungwa kitambo,ni mwaka wa pili sasa.
 
Katibu mkuu Wizara ya Maji mhandisi Antony Sanga amesema utofauti wa mita hizo na mita zingine ni kuwa unaweza ukamgawia jirani uniti za maji kama unavyohamisha salio kwenye simu na akaendelea kupata huduma, vilevile kama unahama nyumba uliyokua ukiishi na kuna uniti zako zimebaki kwenye mita unaweza ukahama nazo pia. KONGOLE SANA
Kivip,wale wa kushea mita moja weng je,wahama nayo vp
 

Serikali kupitia Wizara ya Maji kuanzia mwezi Julai inatarajia kuanza kufunga mita za maji za malipo ya kabla[PRE PAID WATER METERS] ambazo zitakuwa na mfumo wa King’amuzi unaweza ukanunua ukiwa sehemu yoyote duniani

Katibu mkuu Wizara ya Maji mhandisi Antony Sanga amesema utofauti wa mita hizo na mita zingine ni kuwa unaweza ukamgawia jirani uniti za maji kama unavyohamisha salio kwenye simu na akaendelea kupata huduma, vilevile kama unahama nyumba uliyokua ukiishi na kuna uniti zako zimebaki kwenye mita unaweza ukahama nazo pia.
Safi sana! Yahooooo! Nipo Arusha, kilio changu siku zote ni ubambikiwaji wa bill! Familia yangu ni ta watu wanne (mimi, mke wangu, Mjukuu na binti wa kazi), bili inakuja Tsh. 89,500 kwa mwezi! Utadhani nina kiwanda. Cha kusikitisha huduma yao kwa mteja ni ya hovyo sijapata ona nchi hii. Ukienda lalamika wana printi bili za nyuma a kisha kukutumia SMS za vitisho kwenye simu. Hawataki kujua chanzo cha tatizo ni nini! Sasa nimeamua siwalipi waje wachukue mita yao!
 
Siku network ikigoma ndio wenye vyoo vya ndani mtazungumza
 

Serikali kupitia Wizara ya Maji kuanzia mwezi Julai inatarajia kuanza kufunga mita za maji za malipo ya kabla[PRE PAID WATER METERS] ambazo zitakuwa na mfumo wa King’amuzi unaweza ukanunua ukiwa sehemu yoyote duniani

Katibu mkuu Wizara ya Maji mhandisi Antony Sanga amesema utofauti wa mita hizo na mita zingine ni kuwa unaweza ukamgawia jirani uniti za maji kama unavyohamisha salio kwenye simu na akaendelea kupata huduma, vilevile kama unahama nyumba uliyokua ukiishi na kuna uniti zako zimebaki kwenye mita unaweza ukahama nazo pia.
Da asavali zile bili za kutubambikia ndio zitakuwa mwisho wake na wenzangu mimi wale vishoka wa kuchezea na kurekebisha mita ili apate chochote hatima yao ndio imefikia ukingoni,sijui walioajiriwa kazi ya kusoma mita watafanya kazi gani sasa kwa maana walikuwa wanakaa tuvijiweni wakituandikia bili za uongo na hata walikuwa hawasomi mita.
 
Back
Top Bottom