Mitandao ya simu ipige faida ya internet kwa mara ya mwisho. Elon Musk kuleta internet ya Starlink Tanzania

Ndiyo watanunua mzigo kwa musk wakuuzie wewe.
Hapana. Sasa hivi hapa Tanzania kuna baadhi ya kampuni wanatumia starlink. Niambie wananunua kutoka kwenye mtandao gani wa simu kama siyo wanalipa moja kwa moja kwa Elon Musk?
 
labda iwe propaganda, ila kama yupo serious yatamkuta yale yaliyomkuta TROY REID
 
Mimi nataka alete ushindani mkuu
 
Elon ametoa hiyo habari na atazidi kuipromote ili vibopa wa hisa wakatie mzigo

Mchizi ana cheza mind game sana yule

Hata hizo safari zake za kwenda mars, kila siku anakuambia anatest mitambo
Mara hadi mwaka gani

Ata akifanikisha, gharama yake haitakua kama sasa kifurushi cha week buku jero

Ccm tuliichagua wenyewe, tuache kusumbua watu
 
Yule ana akili lakin anapenda kick sana na mambo sio marahis kama watu wanavyochukulia
 
Hata safari za mars as long hamna ozone layer kwenye hizo sayari nyingine zitakua za gharama kubwa sana na hata mtu akienda hatakaa Zaid ya lisaa itabid ageuze chap kwa haraka
 
Hapana. Sasa hivi hapa Tanzania kuna baadhi ya kampuni wanatumia starlink. Niambie wananunua kutoka kwenye mtandao gani wa simu kama siyo wanalipa moja kwa moja kwa Elon Musk?
Musk kuuza kwa individual sizani aisee na ndiyo maana hapo mwenyewe umesema “baadhi ya kampuni” naamini itakuwa B2B
 
Yule ana akili lakin anapenda kick sana na mambo sio marahis kama watu wanavyochukulia
Jamaa ni genius, na level za quality zake
Kwa nchi za kiafrika. Hatuziwezi

Mfano hayo magari ya umeme. Hayashikiki mzee

Tutaendesha hizi hizi ist
 
Hata safari za mars as long hamna ozone layer kwenye hizo sayari nyingine zitakua za gharama kubwa sana na hata mtu akienda hatakaa Zaid ya lisaa itabid ageuze chap kwa haraka
Huwezi kukaa mars week nzima ukatoboa.

Idea zake ni theoretical sana, life in mars.
Eti duniani kuna siku haitakua salama
Jamaa anacheza na akili zetu
 
Huwezi kukaa mars week nzima ukatoboa.

Idea zake ni theoretical sana, life in mars.
Eti duniani kuna siku haitakua salama
Jamaa anacheza na akili zetu
Ni ngumu sababu kubwa ni solar radiation, hakuna oxygen na gravitational force ni ndogo sana means mtu atatembea kwa shida sana

Solar radiation ni sababu kubwa ya kwanza unajua ukifikiria jinsi ozone layer ilivyoumbwa kwa sis tunaomuamin tunasema alikua fundi sana Ile layer ni ya ajabu Sana mfano ikiondoka Leo dunian viumbe wote tunakufa immediately
 
Sina uhakika sana kuhusu gharama lkn nnachokuhakikishia ni kwamba StarLink sio mpinzani wa hii internet ya simu moja moja (ambayo wengi ndo wanatumia) bali ni mpinzani wa hizi aina mpya za huduma ya internet kama vile TTCL Fibre, supakasi etc... ambazo zinamuhitaji mtu awe na router. Na hizo hutumika mara nyingi ofisini au kwa wenye familia kubwa zinazohitaji matumizi makubwa ya internet kama vile hawa wachina au wahindi waliopo huku kikazi

Kwa mtumiaji wa kawaida StarLink sio option kabisa kwa sababu Kit yake inakuja na kitu kama Dish fln hv dogo dogo pamoja na router yake. Hii haina tofauti na mambo ya ADSL ya TTCL, au kdg Home Internet ya Tigo. Yaani mm na simu yangu moja au mbili eti ninunue dish niwe natembea nalo wakati nikiwa na lain kila kitu ni poa tu.
 
hili la starlink tushalizungumzia sana starlink sasa hivi ipo kwenye majaribio nchi kadhaa za Africa kama Nigeria na Msumbiji

ada ya mwezi ni $99 (around 240,000) kwa kifurushi cha kawaida na premium ni dola 500 ambayo roughly ni 1.2m

hio ni satelite internet ambayo ina speed mbovu tu hasa latency, inauzwa laki 2 na 40 kwa mwezi, huwezi cheza games vizuri na vitu vingi ambavyo una live stream havitakua vizuri

fiber, 4g na 5g zote zina speed nzuri kuliko starlink, TTCL kuanzia 55,000, voda 5G kuanzia 120,000, zuku kuanzia 69,000 etc ni much better.

starlink waachie watu wa vijijini mkuu wenye pesa, haitaondoa mtandao wowote ule wa Tanzania.
 
Ndo maana nilimwambia muanzisha uzi aache ushabiki mambo sio marahisi kama anavyodhani
 
Tarajien magonjwa mengi ya saratani na vifo vya ghafla, bila kusahau kuongezeka kwa vizaz vya watoto walemavu.

Satellite inapofanya mawasiliano kutoka ilipo mpka kukufikia ulipo, kuna nishati ya electromagnetic waves inayosafiri kwa kasi ambayo ili upate signal zake inabidi na device yako iwe na strong radio/ waves receiver ili kupata mawasiliano yasiyo na mikwamo kwamo.

Pia itahitajika nguvu kubwa ya nishati ktk device yako ili iweze kudumu na chaji kwa muda mrefu ikipambania kukamata hayo mawimbi.

Radiation hizo huwa na waves length tofaut tofaut kulingana na uhitaji wa matumiz, mfano ili mtandao uwe strong bila kukwama itahitajika energy kubwa ya uzalishaji wa mawimbi hayo kwa kasi na frequency kubwa ili kukufikia mhitaji, kama mujuavyo, mawimbi hayo huwa na athari kwa mwili wa binadamu, kuanzia akili, genetic effect kiujumla uhai wako uko hatarin.

Tuombe wabuni njia ambazo ni salama, hata hizi simu tunapotumia zina athari kutokana na upokeaji wa mawimbi hayo kutoka ktk minara/mitambo, na mujue kuwa jinsi unavyoongeza kasi ya mtandao 3g/4g/5g ndivyo kasi na nguvu huwa attracted kwa device yako na wew mtumiaji tegemea athari japo hazitokuwa za ghafla, mfano kupungua nguvu za kiumbe kama device yako huifadhiwa mifuko ya suluali ambapo , mawimbi hayo huweza kukupiga na kuathiri uzazi wako, pia ugumba utegemee

Jinsi × ray inavyofanya kazi, nuclear radiation zinavyofanya kazi ndivyo hivyo Radio waves za mawasiliano hufanya kazi, ni vile hizi hazina nguvu sana, lkn madhara yapo makubwa.

Serikal zinapokubali technologies ziwe zinatoa na side effects za hizo technologies bila kusahau ways za kujikinga maana hizi nchi zetu masikin raia ni wabishi wa kujali afya zao.
 
Mjadala umefungwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…