Mitego ya Rais ya kununua Magoli iwakamate wajinga wa hili Taifa tu. Mimi siwezi kamatwa kamwe

Mitego ya Rais ya kununua Magoli iwakamate wajinga wa hili Taifa tu. Mimi siwezi kamatwa kamwe

Kwa kweli ni ujinga wa hali ya juu kufurahia utapanyaji wa fedha kwenye starehe zisizo na tija wakati mambo muhimu kabisa, yanayohitaji sana pesa yashindwa kupata fedha.

Nina mfano unaoishi ambao sitausahau maishani, tuliwapeleka watu waliokuwa kwenye hali mbaya sana baada ya kupata ajali ya agari, na mmoja alifariki, lakini majeruhi wale baada ya kuwafikisha hospitali ya wilaya walikaa kwa masaa 7 bila ya huduma ya daktari kwa sababu hospitali nzima ina madaktari watatu tu walioajiriwa, na mmoja ni daktari mfawidhi, anashughulika zaidi na masuala ya utawala, mmoja yupo likizo, na aliyebakia azunguke wodini kuwahudumia wagonjwa wote. Tulipolalamika kwa huduma dhaifu, patron wa hospitali alitujibu kwa hasira kuwa, 'msitusumbue, hata mngekuwa ninyi msingeweza. Rais wenu anagawa hovyo pesa kwenye magoli lakini sisi hapa tumeandika barua za kuomba kuajiri madaktari na wauguzi mpaka tumechoka. Jibu kila mara ni kuwa Serikali haina pesa. LAKINI hela ya kununulia magoli na kusafiri na wasanii nje ya nchi ipo nyingi sana'. Tulipatwa na simanzi kubwa. Ikabidi tuliokuwepo pale hospitali tuchangishane pesa haraka ili majeruhi wale wakimbizwe hospitali ya rufaa. Maana tuliambiwa ambulance ipo ila hela ya mafuta hakuna, hela ya dereva na nurse hakuna.

Hapo ndipo ilipofikia nchi hii!! Mambo ya kijinga yanafanywa ni muhimu, na mambo ya muhimu yamepuuzwa kabisa. Inakera sana. Watawala wanatafuta sifa za kijinga kabisa!!
Mama anapiga Kampeni za 2025, ile ni mitego kaweka Ulimbo ili akamate wajinga?
 
FIFA wanatuma Tanzania shilingi bilioni moja kila baada ya miaka miwili, unajua zinatumikaje hizo pesa?.

Akija Rais mwingine tutajua mbele ya safari ataamua kufanya vipi kuhusu michezo.

JPM alikuwa anagawa maburungutu ya pesa kwa wapita njia huko mitaani, ulishawahi kuhoji juu ya tabia yake hiyo kipindi kile akiwa bado yupo hai?.

Acheni nongwa za kitoto hizi.
Hadi hapo mkuu bado tu haujaona hoja yangu? Napinga hilo suala la kugawa pesa iwe kwa simba na yanga au kwa kuwapa tu raia ni sawa na mtu kukupa samaki badala akupe nyavu ukavue mwenyewe.

Kama angekuwa mwenye kugawa hizo pesa ni raia wa kawaida tu anatoa pesa zake binafsi basi wala nisingeongea ila tunamzungumzia kiongozi mkuu wa nchi hapa, anachofanya ni kujinufaisha yeye kisiasa hana nia ya dhati kusaidia soka letu.

Halafu unavyosema akija Rais mwengine atajua afanye nini kuhusu michezo utadhani anachofanya Samia kununua magoli ya simba na yanga inasaidia michezo Bongo.
 
Huko kwa wahitaji mbalimbali peleka pendekezo kwa Waziri Ridhiwani Kikwete ndio mhusika mkuu, kwenye michezo kuna Mwana FA hawa ni mawaziri wawili wenye bajeti mbili tofauti.
Hata kwenye michezo kuna uhitaji pia kama yangefanyiwa kazi hayo mahitaji ingekuwa limefanyika jambo la msingi sana kuliko kununua magoli ya simba na yanga, hizi ni siasa kwenye michezo tu hazina msaada wowote kwenye soka la bongo.
 
Hata kwenye michezo kuna uhitaji pia kama yangefanyiwa kazi hayo mahitaji ingekuwa limefanyika jambo la msingi sana kuliko kununua magoli ya simba na yanga, hizi ni siasa kwenye michezo tu hazina msaada wowote kwenye soka la bongo.
CCM ni Chama cha siasa kina umri wa miaka 47 usishangae kwa wao kufikiria kufanya siasa kila unapotokea mwanya wa kufanya hivyo ndio lengo la kwanza la uwepo wao.

Motisha unafaa sana kuwafikia hao kina Yanga na Simba wameifikisha CCM hapa ilipofikia.

Na michezo imekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 10 ya JPM na SSH, timu ya wanawake chini ya miaka 17 kwa mara ya kwanza imeshiriki michuano ya kombe la dunia, ni kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1961, mengi yanafanyika lakini hatukumbuki kuyaona kwani akili zetu ni za kukosoa tu, hazifikirii mema yanayofanyika huko kwenye michezo.
 
Hadi hapo mkuu bado tu haujaona hoja yangu? Napinga hilo suala la kugawa pesa iwe kwa simba na yanga au kwa kuwapa tu raia ni sawa na mtu kukupa samaki badala akupe nyavu ukavue mwenyewe.

Kama angekuwa mwenye kugawa hizo pesa ni raia wa kawaida tu anatoa pesa zake binafsi basi wala nisingeongea ila tunamzungumzia kiongozi mkuu wa nchi hapa, anachofanya ni kujinufaisha yeye kisiasa hana nia ya dhati kusaidia soka letu.

Halafu unavyosema akija Rais mwengine atajua afanye nini kuhusu michezo utadhani anachofanya Samia kununua magoli ya simba na yanga inasaidia michezo Bongo.
Kugawiwa pesa wavuvi wa samaki zipo sera nenda katika wizara ya mifugo na uvuvi uwe na mipango yenye kueleweka ya uvuvi uone kama wizara haitakuwezesha juu ya upatikanaji wa nyavu na mafunzo sahihi ya uvuvi.

Tatizo lako unaitwisha michezo lawama za sera za wizara nyingine ukisahau kuwa michezo na utamaduni ni wizara yenye mahitaji yake yanayojitegemea sawa na hizo wizara nyingine.

Una uhakika gani kuwa hana ni ya kusaidia michezo yetu wakati aliwapa Yanga ndege ya kwenda na kurudii kule Algeria mwaka juzi wakati walipokwenda kucheza na USM Algiers mechi ya fainali ya kombe la shirikisho?., Tatizo lako unalalamika wakati huna hata data za kisasa za kinachoendelea nchini mwako!.

Michezo ni tasnia pana sana zaidi ya haya magoli yanayonunuliwa kwa shilingi milioni tano kila moja.
 
CCM ni Chama cha siasa kina umri wa miaka 47 usishangae kwa wao kufikiria kufanya siasa kila unapotokea mwanya wa kufanya hivyo ndio lengo la kwanza la uwepo wao.

Motisha unafaa sana kuwafikia hao kina Yanga na Simba wameifikisha CCM hapa ilipofikia.

Na michezo imekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 10 ya JPM na SSH, timu ya wanawake chini ya miaka 17 kwa mara ya kwanza imeshiriki michuano ya kombe la dunia, ni kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1961, mengi yanafanyika lakini hatukumbuki kuyaona kwani akili zetu ni za kukosoa tu, hazifikirii mema yanayofanyika huko kwenye michezo.
Mkuu hapa tunajadili suala la Rais kugawa pesa simba na yanga kwa kununua magoli, sasa hayo ya kwamba tunakosoa tu hatufikirii mema sijui yanatoka wapi?
 
Mkuu hapa tunajadili suala la Rais kugawa pesa simba na yanga kwa kununua magoli, sasa hayo ya kwamba tunakosoa tu hatufikirii mema sijui yanatoka wapi?
JPM alikuwa anagawa pesa huko njiani misafara yake ikisimama na akaanza kuongea na raia na watu waliona poa tu Samia kaamua kuwapa motisha Yanga na Simba wanapocheza mechi za kimataifa.

Milioni tano kwa goli moja ni pesa kidogo sana kulinganisha na mabilioni yanayokusanywa kila siku na TRA.
 
Back
Top Bottom