Mitume walikuwa wanaomba kuombewa na wafuasi kipindi wanafanya huduma. Kwanini mwingine anaombewa hata baada ya kufa?

Mitume walikuwa wanaomba kuombewa na wafuasi kipindi wanafanya huduma. Kwanini mwingine anaombewa hata baada ya kufa?

Mnamtakia Aman mfu marehemu?

Hizo kumtakia Aman zinamsaidia nn?

Kama alikufa katika dhambi ,asubiri Moto wa jehanum
Kwenye Uislamu wema hauishi hata mtu akifa , kama alisomesha watu utanufaika mpaka wale watu waishe wote, huku ni rahaa tupuu, Mtume Mohamadi kafundisha watu tutamtakia imani mpaka waislamu wote waishe
 
Kama umesoma Ile habari vizuri utagundua Isaka alikuwa anampenda Esau zaidi ya Yakobo. Ndio maana mama akaamua kusaidia kumdanganya kwasababu yeye alikuwa anampenda Yakobo.

Baraka za Mungu zinamfikia mtu aliye na haki. Tena Mungu alimchukia Esau kwa kuuza haki yake kwa mlo mmoja.

Mungu makemeo yake tayari yapo kwenye neno, hahitaji kuja leo specifically amkemee mtu. Ukisoma neno utapata maelekezo na makemeo.
Maswali yangu umeyaona? narudia hili moja labda unaweza elewa , kwanini Mungu aliendelea kumbariki Yakobo pamoja na kutumia njia za uongo? inakuwaje ubatili ulete jambo jema? aya jibu
 
Dhehebu pekee linalo kiri kuwa Allah hana mshirika , hakuzaa wala hakuzaliwa, Mohamadi ni mtume wa Mungu na Issa bin Maryamu ni nabii tu wala sio Mungu, hili ndio dhehebu la kufata, swali jingine?
Litaje Hilo dhehebu katika Shia ,Sunni na hayo mengine 70+
 
Kwenye Uislamu wema hauishi hata mtu akifa , kama alisomesha watu utanufaika mpaka wale watu waishe wote, huku ni rahaa tupuu, Mtume Mohamadi kafundisha watu tutamtakia imani mpaka waislamu wote waishe
Huo wema unamsaidia nn ikiwa hakutubu?

Anapata nn marehemu ?
 
Hakika mkuu, huu ni ukweli unaodumu milele. Imeandikwa mtu anakufa mara moja na baada ya hapo ni hukumu.
Kuna wale wanakufa halafu wanafufuliwa na akina gwajima na bushiri, wale siku wanakufa mara ngapi?
Au wao hili andiko haliwahusu?
 
Litaje Hilo dhehebu katika Shia ,Sunni na hayo mengine 70+
Wote hao wanakubali kuwa Allah hana mshirika hakuzaa wala hakuzaliwa, Mohamadi ni nabii wa Mungu, Isa bin maryamu ni nabii sio Mungu, hivyo yote hayo yako sawa , swali jingine?
 
Unamsaidia sana maana tunaendelea kufundisha na kumuombea dua, hivyo thawabu tunazo pata na yeye anapata
ACHA kudanganywa ukifa hujatubu na kuungama ,imeisha hiyo

Yaan ufanye upuuz duniani utegemee ukifa uombewe Aman na rehema ? Yaan uende mbinguni kwa lift?

Haya mafundisho Ni ya mashetan ,muasisi Ni Roman Catholic , wao wanaita purgatory

NDIO maana ukichunguza kwa jicho la 3

Utagundua Uislamu ULIANZISHWA na Roman Catholic
 
Wote hao wanakubali kuwa Allah hana mshirika hakuzaa wala hakuzaliwa, Mohamadi ni nabii wa Mungu, Isa bin maryamu ni nabii sio Mungu, hivyo yote hayo yako sawa , swali jingine?
Kama wanakubaliana kipi kinachowafanya watofautiane ?

Na hiyo uliyotaja sio mising ya uislamu

Hizo Ni sababu zako binafs
 
Maswali yangu umeyaona? narudia hili moja labda unaweza elewa , kwanini Mungu aliendelea kumbariki Yakobo pamoja na kutumia njia za uongo? inakuwaje ubatili ulete jambo jema? aya jibu
Haki ya mzaliwa wa kwanza aliipata kihalali hivyo ndio maana akapata na baraka zake.
 
Mtume Paulo aliyaomba makanisa ya Rumi, Efeso na lile la Korintho yamuombee ili injili iweze kufika mbali zaidi kwa kinywa chake.

Alipomaliza huduma aliaga katika barua kwa Timotheo kwamba ameilinda imani na kwamba anaenda zake kwenye taji aliyowekewa.

Mtume Petro naye alikumbusha kuombea huduma na alipomaliza aliwaambia waumini kwamba wakati umefika kwake kuondoka tena itakuwa kutundikwa juu ya msalaba kichwa kikiwa chini na miguu juu.

Hawa wote wawili walikuwa na furaha na kuondoka duniani kwa uhakika na ushindi. Walikuwa wakiwasisitiza waumini wafuate mfano wao.

Sasa nashangaa kuna nabii eti ni wa mwisho na ndio mkuu kwa wote lakini mpaka sasa anaombewa akiwa amefariki.

Alikwama wapi na nini kimemfanya yeye asiwe na uhakika wa kuingia mbinguni mpaka aendelee kuombewa?
Yasio kuhusu achana nayo broo we elewa ivyo ivyo na sisi acha tumuombee huyo wetu kwani we unaumia
 
Kama wanakubaliana kipi kinachowafanya watofautiane ?

Na hiyo uliyotaja sio mising ya uislamu

Hizo Ni sababu zako binafs
1. Wote wanakubali kuwa Allah ni Mungu
2.wote wanakubali mohamadi ni nabii
3.wote wanakubali kuwa Isa bin Maryamu ni nabii sio Mungu
Hayo mengine yote sio tatizo kutofautiana, sasa watu wanatofautiana kwenye mwezi muandamo hivi ni vitu vidogo ambavyo haviwezi mtoa mtu katika Uislam
 
Kuna wale wanakufa halafu wanafufuliwa na akina gwajima na bushiri, wale siku wanakufa mara ngapi?
Au wao hili andiko haliwahusu?
Sina uhakika na hao unaowataja kwasababu sijafuatilia kwa karibu kujua details zao.

Ila mtumishi yoyote wa kweli wa Mungu anaweza kumuombea aliyekufa ili afufuke ikiwa ndio mapenzi ya Mungu hasa ikiwa huyo mtu hajakamilisha kusudi lake na shetani amehusika kukatisha maisha yake.
 
Ukiwa huna uhakika na unachoandika ni BORA KUTOANZISHA UZI....

kwenye Uislam ukisikia anatajwa Mola Mlezi utasikia kwa mfano Allah Subhanah Wataala, akitajwa Mtume utasikia Rehema na Amani ziwe juu yake, wakitajwa mitume wote waliobakia aliwemo mtume wa Allah Issah utakisikia Alayh Salam, wakitajwa maswahaba utasikia Radhiallah Anhu, Waja wema waliotangulia Rahmahullah au waliopo HAI utasikia hafidhallah

Kwa hiyo siyo kweli UNACHOKISEMA KUWA KWENYE UISLAM MTUME ANAOMBEWA MSAMAHA.....

MOLA MLEZI ameweka utaratibu wa kumtukuza YEYE kila anapotajwa au unapotaja jina la Mola Mlezi, kuwatakia salama na amani Waja wema waliotangulia kwa maana waliishi na kumridhisha YEYE na YEYE amewaridhia na wanaombewa mpaka na malaika...


KINYUME CHAKE kwa kila aliyeishi kwa UJABARI NA KUMUASI MOLA MLEZI KAMA FIRAUNI na wote wanaomfuatia basi utasikia yakitamkwa MKASIRIKO YA MOLA MLEZI NA KUWEKWA MBALI NA REHEMA ZAKE baada ya majina yao!!!!

Kwa aliye hai ataombewa UONGOFU ila akifa mwanadamu kati uasi basi hadi Malaika watamwombea Makasiriko ya Mola Mlezi....

HUJAWAHI ONA MTU ANAFARIKI NA WATU WANAFURAHI KUWA WATAPUMZIKA KUTOKANA NA MAUDHI AU DHULMA ZAKE???? Au MWINGINE ANAFARIKI KILA YUALIA KUTOKANA NA WEMA WAKE KWA WATU???

Basi jua vivyo hivyo kwa wanadamu na Mailaka kumwombea aliyefariki au hata aliye HAI...
Swadakta kabsa
 
ACHA kudanganywa ukifa hujatubu na kuungama ,imeisha hiyo

Yaan ufanye upuuz duniani utegemee ukifa uombewe Aman na rehema ? Yaan uende mbinguni kwa lift?

Haya mafundisho Ni ya mashetan ,muasisi Ni Roman Catholic , wao wanaita purgatory

NDIO maana ukichunguza kwa jicho la 3

Utagundua Uislamu ULIANZISHWA na Roman Catholic
Maombezi sio jambo la kukurupuka, ni matokeo ya kazi nzuri uliofanya duniani, kama mtoto dini ulikuwa unaacha kumuelekeza sasa atakuombea vip dua? ukiona watu wanaomba dua ujue ni matokeo ya kazi nzuri za hao watu walipokuwa duniani, kama mimi namuombea sheikh wangu kwa kunipa elimu hii murua kabisa, ukiona vyaelea vimeundwa
 
Haki ya mzaliwa wa kwanza aliipata kihalali hivyo ndio maana akapata na baraka zake.
Uhalali uko wapi kijana wakati mtoa baraka kadanganywa ? au hujui mzee Isiaka alilalamika kudanganywa, yaani wewe haki iwe yako halafu utumie uongo kuipata uko serious kweli!!!
 
Uhalali uko wapi kijana wakati mtoa baraka kadanganywa ? au hujui mzee Isiaka alilalamika kudanganywa, yaani wewe haki iwe yako halafu utumie uongo kuipata uko serious kweli!!!
Kijana baraka inatoka kwa Mungu, Isaka alikuwa channel tu ya kupitishia ndio maana hakuwa na namna ya kumbariki Esau baada ya Yakobo kuchukua nafasi. Isaka hakulalamika popote, alishangaa tu na nadhani hakuwa na taarifa kwamba Esau alishauza haki yake.
 
Kijana baraka inatoka kwa Mungu, Isaka alikuwa channel tu ya kupitishia ndio maana hakuwa na namna ya kumbariki Esau baada ya Yakobo kuchukua nafasi. Isaka hakulalamika popote, alishangaa tu na nadhani hakuwa na taarifa kwamba Esau alishauza haki yake.
Baraka inatoka kwa Mungu kupitia baba mzazi, sasa baba mzazi tayari alishadanganywa na akatoa baraka kwa kudanganywa, maana yake process nzima imejaa ubatili na baraka zimejaa ubatili, vip Mungu atie mkono wake kwenye ubatili wa namna hii?
 
Uduni wa wachangiaji ni ishara kuwa mleta mada umefeli kwenye lengo lako.......watu wamekausha tu wanaendelea na mambo mengine. Kajipange tena!
Rudi hapa kwenye komenti yako. Watu wamechoka kuombea wafu.
 
Back
Top Bottom